Mbona wakati wa sasa watu wa PCM, PCB, CBG wanafaulu sana kidato cha sita kuliko enzi zetu au kizazi hiki ubongo wao mzuri zaidi?

Kama we in mdau wa elimu jibu utakuwa nalo, ukweli ni kwamba vijana wa siku hizi ni hovyo sana(siyo wote), sijajua vizuri lengo LA serikali ni nini haswa, mbali ya kwamba uwezo wao ni mdogo sana kuliko kawaida lakini wanazidi kufanya vizuri kuliko miaka yote. Mfano matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa juzi ndo yametia simanzi, watoto wetu wamefanya vizuri kuliko uwezo wao, hatukatai yote mema, lakini inatisha kuona kijana tayari amefanya vizuri kidato cha 6 lakini bado hana uwezo wa kuchanganua mambo madogo hata ya kawaida, mfn hai kuna mzazi ananiambia binti yake amepata 2 ya point 10, lakini anajua fika Huyo binti yake hakuwa na uwezo wa kupata alama hiyo...huu ni mfano halisi. Ila yote tunashukuru acha maisha yaendelee.
 
Daah! Kweli kabisa,Yaani enzi hizo ukipata "E" mbili kidume University unaenda na Mkopo 100%.Unakuta masela wamepiga E moja na SS za kuendea Diploma.Now days Vijana wanafaulu sana au wanafaulishwa.
Mbinu za kufundishia Sasa nzuri,mwanafinzi Hana stress wazazi Wana uwezo wanampa mahitaji yote,vitabu viko vya kutosha hawategemei Mwalimu tu ,uhusiano was walimu na wanafunzi mzuri Sio Kama zamani baba aliniambia walikuwa wakimwona Mwalimu anapita kijijini walikuwa wanakimbia kujificha porini
 
Kama we in mdau wa elimu jibu utakuwa nalo, ukweli ni kwamba vijana wa siku hizi ni hovyo sana(siyo wote), sijajua vizuri lengo LA serikali ni nini haswa, mbali ya kwamba uwezo wao ni mdogo sana kuliko kawaida lakini wanazidi kufanya vizuri kuliko miaka yote. Mfano matokeo ya kidato cha sita yaliyotangazwa juzi ndo yametia simanzi, watoto wetu wamefanya vizuri kuliko uwezo wao, hatukatai yote mema, lakini inatisha kuona kijana tayari amefanya vizuri kidato cha 6 lakini bado hana uwezo wa kuchanganua mambo madogo hata ya kawaida, mfn hai kuna mzazi ananiambia binti yake amepata 2 ya point 10, lakini anajua fika Huyo binti yake hakuwa na uwezo wa kupata alama hiyo...huu ni mfano halisi. Ila yote tunashukuru acha maisha yaendelee.
Ndio Maana zamani walikuwa wakifeli Sana sababu walikuwa wakijaza mbo.mengi kichwani unakuta anajua mambo.mengi makubwa na madogo Hawa wa Sasa wanajikita kwenye masomo hawajazi vichwa mambo mengi.Halafu wa sasa umri pia hauruhusu kujaza Mambo mengi kichwani.Mtoto anamaliza kidato Cha sita ana miaka 17 unataka ajue mengi ya Nini? Zamani miaka hiyo mtu Bado Yuko Shule ya msingi anajua kuchunga mifugo,kulima,kuwinda,kwenda kuuza mazao sokoni,nk mimambo kibao kichwani atafaulu wapi?
 
Miaka ya nyuma mtu akifaulu amefaulu kweli na kichwani yupo vizuri, uzuri aina ya walimu inajulisha nini kinaendelea kwa sasa na hata mitihani imekua dhaifu sana, serikali boresheni mazingira ya walimu zama zinabadilika kuishi kiujamaa na walimu ni dhambi
Mitihani ya Sasa hivi dhaifu unaota wewe.Biology ya zamani ya form two Sasa hivi mtoto anaisoma darasa la sita.Kama umesoma msingi zamani kakae na mtoto wa msingi Sasa hivi mpeane hesabu uone Kama utakatiza na elimu yako ya zamani
 
Hiz kombi wanachukua wenye ufaulu mzuri. Ukiwafatilia vizuri wanakuwa wamefaulu vizuri toka shule ya msingi, na form 4. Ni tofaut na hizi za art ambazo wengi huchukua baada ya kuwa na ufaulu mdogo apo nyuma.
 
Nimetazama matokeo nikagundua tofauti ya miaka yetu n'a sasa.. Nimeona vijana wa kidato cha sita PCM.. PCB... CBG wakifauli kuliko miaka ya 2011 kurudi nyuma
Naona watoto wa sasa wana akili, kipindi chetu nakumbuka naenda kusoma PCM naulizwa umeona nani kafaulu hapa mtaani??
Hivyo labda watoto wa sasa wana akili ama mitihani imekua rahisi
 
Mitihani ya Sasa hivi dhaifu unaota wewe.Biology ya zamani ya form two Sasa hivi mtoto anaisoma darasa la sita.Kama umesoma msingi zamani kakae na mtoto wa msingi Sasa hivi mpeane hesabu uone Kama utakatiza na elimu yako ya zamani

Ningekujibu ila ulivyoniambia naota nimekupuuza
 
Naona watoto wa sasa wana akili, kipindi chetu nakumbuka naenda kusoma PCM naulizwa umeona nani kafaulu hapa mtaani??
Hivyo labda watoto wa sasa wana akili ama mitihani imekua rahisi
Vyakula Sasa hivi viko vingi wanakula Hadi vya kujenga akili Sio vya kujenga mwili the zamani watu walikuwa wanakula ili washibe tu Sasa hivi Watoto wanakula balanced diet inachangia wao kuwa na uwezo mkubwa wa akili tofauti na zamani ambapo watu walikuwa na uwezo mkubwa wa kuhimili matatizo Sio wa akili
 
Daah! Kweli kabisa,Yaani enzi hizo ukipata "E" mbili kidume University unaenda na Mkopo 100%.Unakuta masela wamepiga E moja na SS za kuendea Diploma.Now days Vijana wanafaulu sana au wanafaulishwa.
Wanafaulishwa mkuu, hata level ya chini hujiulizi zamani shule ya msingi shule nzima walikua wanafaulu watoto 3 mwishk 5!!!! Siku hizi imekua kinyume chake 3 au 5 ndo wanafeli tu.
 
Nimetazama matokeo nikagundua tofauti ya miaka yetu n'a sasa.. Nimeona vijana wa kidato cha sita PCM.. PCB... CBG wakifauli kuliko miaka ya 2011 kurudi nyuma
Kwanza zamani hakukuwa na tuition, pili materials ya kusoma yalikuwa changamoto lakini kwa sasa kuna material ya kila aina mfano kina Mgote Ally abdall Ngaiza na mengineyo. lakini kubwa kuliko zamani mlikuwa mnasomea sifa, yani kitu hakipo kwenye syllabus lakini utakuta mtu anakomaa nacho kuonesha utabe kwa wenzake. Kwa sasa unasoma kilicho kwenye syllabus then SAA 5 mapema tuu unaenda zako kulala mpaka kesho saa 11 mnawahi mchakamchaka.
 
Nimetazama matokeo nikagundua tofauti ya miaka yetu n'a sasa.. Nimeona vijana wa kidato cha sita PCM.. PCB... CBG wakifauli kuliko miaka ya 2011 kurudi nyuma
Kwanza zamani hakukuwa na tuition, pili materials ya kusoma yalikuwa changamoto lakini kwa sasa kuna material ya kila aina mfano kina Mgote Ally abdall Ngaiza na mengineyo. lakini kubwa kuliko zamani mlikuwa mnasomea sifa, yani kitu hakipo kwenye syllabus lakini utakuta mtu anakomaa nacho kuonesha utabe kwa wenzake. Kwa sasa unasoma kilicho kwenye syllabus then SAA 5 mapema tuu unaenda zako kulala mpaka kesho saa 11 mnawahi mchakamchaka.
 
mkuu mambo yanabadilika sana

Enzi zenu hamkuwa na graduates vipanga wa COET UDSM wanaofundisha physics na Chemistry sekondari baada ya kukosa ajira .

Enzi zenu mlikuwa hamuelewi bali kukariri sasa mtoto toka nursery anasoma English medium hadi Feza utamuweza?

Enzi zenu kulikuwa hakuna Google hakuna YouTube
 
Nyie watu wa zamani si mlisoma na jamaa mmoja hivi PhD holder aliyesema Ghadafi alikuwa rais wa Kuwait, baada ya kuona katoa boko akabadilisha na kusema ni wa Iraq. Huwa napiga story na wazee wengi tu na wanapenda kusifia enzi zao lakini uwezo wao ni wa kawaida tu kama vijana wa saizi tu. Kila zama zina watu wenye akili nyingi, za kawaida na wasio nazo kabisa.

Usijaji ufaulu kwa kuangalia idadi maana zamani wanafunzi walikua wachache na idadi ya shule ilikua ndogo pia.
 
Siasa tu hizi zinaendelea kwa sasa, ngoja mzee baba ang'atuke uone hali itakua mbaya kuliko zamani.. Siku hizi disturbances zimekua nyingi zaidi, social media, more freedom kwa watoto na ufundishaji wa bora liende wa walimu vyote vinachangia kudhoofisha ufaulu wa wanafunzi.
 
Tatizo wazazi wetu walishindwa kuwekeza kwenye elimu sababu ya vipato vyao vilikuwa vidogo kutokana na sera ya ujamaa wakati huo, wazazi wa sasa wanawekeza kwenye elimu kuliko zamani. Halikadhalika sera ya ujamaa ilitaifisha shule binafsi, ambazo sasa hivi ziko juu kuliko zile za umma. Chochote kitakacho sababisha hizi shule zisiwepo kitarudisha nyuma sekta ya elimu
 
Mkuu ulichoongea hakina uhalisia you tube hizi hizi zilizojaza Amber ruty na ushilawadu mwingi, yani sisi tu watu wazima kutumia mitandao kwa faida bado kuna tatizo sembuse vijana, clip kibao mitandaoni watoto wanakata viuno, tatizo kubwa sana sasa hivi ni maadili ya wazazi kushuka, zamani mtoto kujua baba amegombana na mama ni ishi, ila sasa hivi mtoto anajua hadi michepuko ya mzazi, sasa tunafundishana nini kimaadili
You miss my point
 
Kwenye internet inategemea unatafuta nini maana inankila kitu, wewe inawezekana unahangaika na akina umber Ruti lakini wengine wanatafuta vitu vyenye manufaa zaidi, internet ina kila aina ya information unayotaka ukitaka utajiri utapata, ukitaka Malaya utapata, ukitaka neno la Mungu utapata, tatizo ni wewe sio internet

Sasa kwa maadili yetu hapa Tanzania hiyo hali ipoje Mpaka sasa
 
Sasa kwa maadili yetu hapa Tanzania hiyo hali ipoje Mpaka sasa
Mkuu maadili ya mtoto yanachangiwa na wazazi wapo vijana wengi Wana maadili mazuri Tu Kwa sababu wamelelewa vizuri, usisubili dunia imfundishe mtoto wako atakutana na mengi na maadili yatakuwa mabaya,mwongoze kijana wako apate uelewa
 
Back
Top Bottom