Mbona sasa hivi matangazo ya kampuni za BETTING yameshamiri sana?

mpasta

JF-Expert Member
Jan 17, 2011
917
1,997
Hivi karibuni kila redio unayosikiliza hasa hizi za FM KITAA ukiitoa TBC basi lazima ukutane na matangazo ya kupigia debe kamari mpaka inakera. Kwenye simu nako kila wakati zinatumwa meseji za kuhamasisha watu wajiunge na ubashiri...

Hivi kama Taifa tumeshajiandaa na madhara yanayokuja na yajayo kutokana na BETTING???. Tunajua uhalifu kiasi gani utaongezeka, familia ngapi zitavunjika, matatizo mangapi ya afya ya akili inayotokana na msongo wa mawazo yatatokea???N.K...Ndio uatakuta sasa kazini Baba zima na midevu yake ana MIKEKA yake ya KUBET, Vyuo vikuu ndio useme Madenti wana BETT kwa kutumia Bumu hawa si ndio watakuja kuugua "Gambling Disorder" kesho na kesho kutwa wamekuwa MAWAZIRI wetu wa nchi pesa za bajeti ya wizara wanaenda KUBETT kwenye MACASSINO
Asubuhi nilikuwa nasoma PAPER moja ya Utafiti imetoka tarehe 24/01/2022 yenye kichwa cha habari "GAMBLING RELATED SUICIDES IN EAST AFRICAN COMMUNITY", humo nimekuta wenzetu KENYA kujiua kutokana na madhara ya BETTING wanaongoza, wakifuatiwa na UGANDA kisha ndio sisi TZ, tena mbaya zaidi hao waliojiua wengi wao walikuwa wana elimu ya Chuo Kikuu na wameajiriwa.

Chambilecho "Mwenzako akinyolewa wewe tia maji", sheria ya michezo ya kubahatisha inasema wazi

"Mtu yeyote atakaye ruhusu mtoto chini ya miaka 18 kushiriki, kuingia au kukaa karibu na eneo la Mchezo wa Kubahatisha, anahesabika kafanya kosa na anastahili kulipia faini ya shilingi 500,000/- au kifungo kisichopungua miezi mitatu au vyote kwa pamoja”
Nani anafuatilia utekelezaji huo?Mbona huku mitaani tunawaona watoto wa Sekondari chini ya umri wa miaka 18 wapo kwenye Slot mashine za MCHINA??.
Nguvu ya kukusanya kodi ya michezo ya Kubet bora iendane na nguvu za kudhibiti madhara vinginevyo tutakuja kubwa na Taifa la ajabu sana, sasa vijana mtaani BETTING ndio imekuwa chanzo cha mapato hapo ndio Shida inapoanzia....
 
Kila ukifungulia Redio karibia kila stesheni ni kamari tu, kucheze kubahatisha na mapesa kutolewa, watu wanapokea mamilioni, matv, na mambo kede kede kwa kuchangiana kucheza kamari buku buku kwenye maredio.

Hapo bado kamari za kwenye mitandao ya simu, na kwenye mipira, wazee wa mikeka, na wazee wa makasino, kwezi Tanzania pesa ipo. Mfano kuna redio kila baada ya nusu saa, au lisaa yanatoka mamilioni, sasa unashangaa wanaojichangisha huko hewani mpaka mshindi achukue laki 5 mpaka 10M ni wangapi?

Kuna mmoja akanishangaza kuwa ana line tatu, zote alikua anazichezea kuona ipi itashinda au ipi yenye bahati, kweli tuna pesa.

Kuna mwana JF yoyote aliewahi kushinda kweye hizi za redio za kila baada ya nusu saa atupe mrejesho?

Mwaka flani nilifanya kazi kama customer care agent kampuni flani ya simu, kulikua na kamari flani ya kushindania magari, nadhani lilifanyika miezi kadhaa.

Siku niko kwenye majukumu yangu ya kupokea simu akapiga mteja analalamika kacheza miezi yote hashindi, kuchek kweli kacheza inakaribia 3M, nikamshauri akomae siku yake inakuja, ila nilimuhurumia.

Sasa hivi ni kwenye maredio imeshika kasi, ni mipesa tu inatolewa, alafu tunalalamika tozo.

Ngoja tuendelee kukamuliwa mpaka maji tuite mma.
 
Kuna mmoja leo kashinda kacheza mara 170. Sasa mfano mtu kama huyo anatega mingo radio 5 kubwa ili ashinde si laki sita kabisa hiyo inapotea.

Mimi naona wangeregulate upande wa matangazo yawe kwenye intaneti tu maana hayawafikii watoto kwa urahisi.

Hii ya kutwa kutangaza kwenye maredio na mativi wanaharibu watoto maana wao wanaamini kila wanachoona kwa tv ni sahihi.
 
Wakubahatika wanabahatika, imagine unacheza mara 50 ama 200 halafu unashinda 2 million na TV simatphone huoni hiyo ni bingo?
 
Wamiliki wa radio wamejiongeza. Matangazo ya radio pekee hayawezi kuendesha vituo vya radio. Na siku hizi hata matamasha ya,muziki hayalipi. Jamaa wameona fursa kwa,wajinga wajinga wengi ivo wanawakamua buku buku ili waweze lipwa mishahara yao
 
Bora huko kwenu kuna Kmari hii ninayosikiliza kila baada ya nusu saa wana vipindi vya kuisifu serikali ya awamu ya sita na miradi yake hewa
 
Kamari ni kupoteza mwelekeo tu , ulishawahi kuona mtu kaendelea kwa kubet? fanyeni kazio vijana acheni kuitajirisha kina klusaga na daimondi wakati nyie wenyewe hata chakula cha mchana hamna uhakika nacho
 
Wamiliki wa radio wamejiongeza. Matangazo ya radio pekee hayawezi kuendesha vituo vya radio. Na siku hizi hata matamasha ya,muziki hayalipi. Jamaa wameona fursa kwa,wajinga wajinga wengi ivo wanawakamua buku buku ili waweze lipwa mishahara yao
Wa
kamari ni kupoteza mwelekeo tu , ulishawahi kuona mtu kaendelea kwa kubet? fanyeni kazio vijana acheni kuitajirisha kina klusaga na daimondi wakati nyie wenyewe hata chakula cha mchana hamna uhakika nacho
Ngoja wapigwe
 
Wakubahatika wanabahatika, imagine unacheza mara 50 ama 200 halafu unashinda 2 million na TV simatphone huoni hiyo ni bingo?
Concept ya kamari zote duniani ni kwamba katika kila watu 1000 mnaoliwa vihela vyenu ni chini ya watu 10 tuuu watakaopata/kushinda. Kwa maneno mengine hii maana yake ni kwamba nyie watu 990 fedha zenu zitatumika kulipa wale watu 10 na kinachobaki choootee ni faida ya mcheza kamari. Sasa serikali haiwezi kuwagusa kwa sababu wewe uliyeshinda say laki tano (za wale wenzako 990) hutapata hiyo laki tano maana itakatwa kodi ya serikali. Pili yule mchezeshaji kamari na yeye atalipa kodi serikalini kulingana na kipato ambacho nyie watu 1000 mmemchangia.. Hii kitu kuna nchi nimesikia kama India ni marufuku kabisa.
 
Kamari ni kupoteza mwelekeo tu , ulishawahi kuona mtu kaendelea kwa kubet? fanyeni kazio vijana acheni kuitajirisha kina klusaga na daimondi wakati nyie wenyewe hata chakula cha mchana hamna uhakika nacho
Kabisa... Huyu jamaa huko Kenya alikuwa na haya ya kusema kuhusu kamari kwa rais mtarsjiwa...
 
Kabisa... Huyu jamaa huko Kenya alikuwa na haya ya kusema kuhusu kamari kwa rais mtarsjiwa...
Hiii hapa...
Screenshot_20220908-171306.jpg
Screenshot_20220908-171318.jpg
 
Back
Top Bottom