FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,872
- 109,169
Kuna siku zingine Ikulu ilihamia Chato, usisahau hilo.Jk aliwashtua watu wakati alipoonyesha wapwani hawakupendelea mji mkuu kuhamia dodoma. Awamu yake ya urais swala la kuhamia dodoma halikuwekwa kabisa kwenye ajenda.
Sasa tuna rais mwanamama mpwani. Tangu ameshika urais inaonekana kama tumerudi dar kwani kila kitu yuko hapa dar. Amehutubia wazee wa dar juzi, amepokea hati za mabalozi dar juzi jumatano anaapisha wakuu wa mikoa dar. Mwenda zake shughuli dodoma zilifanyika ikibidi kwenye mahema. Sasa hii trend ya kurudi dar mbona inapata kasi sasa wakati hadi sheria ishasema dodoma ndio mji mkuu.
Tunamuomba mama samia awe na moyo na ujasiri kusimamia sera na utendaji kama magufuli. Wananchi walimpigia kura magufuli kwa wingi watafarijika sana kuona misimamo yake inaendelezwa.