Mbona Mwarabu amemdharau sana mwanamke kiasi hiki? Tatizo ni nini?

hannibali

JF-Expert Member
Jul 7, 2020
468
427
Habari za muda huu wanaJF na poleni na majukumu ya kutafuta tonge. Niende moja kwa moja kwenye mada husika.

Hivi kwanini Mwarabu amemdharau sana mwanamke? Imenifanya nifikirie kwa undani zaidi baada ya jana kuona footage ikimuonesha Mwarabu akimtoa mwanamke kwenye mgahawa ambao eti inasemekana ni sehemu ya jamii ya kiume. Sasa the way alivyokuwa anamtoa utafikiri kama si kiumbe cha kawaida, ilinipasa kujiuliza mara mbili mbili.

Ivi wanawake si mama zetu kabisa na wamechangia kwa namna moja ama nyingine katika malezi yetu. Sasa kwanini anatengwa kama mtu kutoka sayari nyingine? Hii kitu ipo katika jamii nyingi za Kiarabu na sio hicho tu kuna vitu vingi ambavyo mwanamke anakatazwa kufanya kama vile:

• Haruhusiwi kuendesha magari
• Haruhusiwi kufanya kazi za jeshi na intelijensia
• Wanawake hawawezi kufungua akaunti benki bila ruhusa maalumu kutoka kwa mwanaume.
• Wanawake wanalazimika kuwa na ridhaa ya kiongozi wa kiume mfano katika familia ili kupata pasi ya kusafiria au kuondoka nchini.
• Kwenye maeneo mengine ya maisha mfano masomo, kazi na hata kwenye kupata baadhi ya huduma za kiafya mwanamke hapati kipaumbele sawa na mwanaume

Tatizo ni nini hasa mpaka kukawa na tabaka kubwa namna hii kati ya mwanamke na mwanaume? Ni mfumo au kitu gani? Mwanamke ana nini ambacho ni cha ajabu kiasi hicho? Au wanaona kama ni kiumbe hakistahili kuwepo?

Wanazengo wanaoelewa zaidi leo tuje kuwekana sawa hapa.
 
Mwanamke kuna tamaduni za kupuuzwa zinamchukulia kama chombo/kifaa. Yaani anaonekana yupo basi tu kwa zawadi au huruma za mwanaume. Haki yake kubwa ilikuwa ni kuvumilia na kunyenyekea.

Sasa hao baadhi ya Waarabu wenye mazoea kama hayo wanapungua kadri ya uelewa unavyoongezeka. Mfano Qatar na U.A.E wana afadhali kuliko ilivyo kwa Saudi Arabia ambako crown prince wao naye alionekana anataka modernization lakini kumbe sio.

Kule UK, wao badala ya kutetea mwanamke wameanza kumnyanyasa mwanaume.
 
Wanaume wa kale walishagundua mwanamke ana akili kuliko mwanaume so walianzisha tamaduni za kumfanya mwanamke ajione ni duni siku zote na ukishajiona duni huwezi kujiamini hata kama una akili kiasi gani.

Ndio maana kuna baadhi ya wanaume wanawaogopa wanawake wenye elimu kubwa na wenye fedha maana wanajiamini.
 
angalau kidogo ukristo, lakini kule kwingine wamezidi sana
Hapana. Wote ni wamoja. Unaona kuna unafuu katika ukristu kwa sababu wakristu wamekengeuka, na mambo mengine ya kwenye kitabu chao wanayatilia shaka na kuamua kuachana nayo, la sivyo wote wangekuwa sawa.

Hadhi ya mwanamke katika jamii, utumwa n.k. ni mambo ambayo ukristu umeamua kuachana nayo japo biblia inayaongelea kama ndio desturi (ya wakati huo)
 
Umesahau kuwa mwanamke hauruhusiwi kutaja majina yake halisi mbele za watu bila idhini ya mme wake ( ukiwa hospital au sehemu watakayo hitaji majina yako inatakiwa utaje majina ya mme wako ama usiseme kabisa )
 
Wanawake sijui walikwama wapi kwa kweli.
Nyakati za Yesu hata kwenye sensa wanawake hawakuwa wanahesabiwa Kama watu.
Hata Marekani hajapita hata karne moja tangu waruhusiwe kupiga kura.
Yote hiyo ni ubaguzi! Sasa huwa najiuliza ubaguzi mpaka kwenye vitabu vya dini! Wanawake na watoto kutokuhesabiwa kwani wao siyo watu jamani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom