Rais Samia: Nimepigiwa sana kelele kuhusu Katiba, ila kwa sasa tusahau kwanza

Mnyerede

JF-Expert Member
Dec 29, 2016
210
226
WanaJukwaa,

Rais Samia wakati akiwaapisha Mawaziri amesema kuwa amepigiwa sana kelele kuhusu katiba mpya, ila kwa sasa anaomba tusahau kwanza.

Swali ni je kuna uwezekano mama akarudisha mchakato wa katiba au ndio hapa kazi tu?

Haki huinua taifa.


Pia ni zaidi ya mara mbili mama huwa anakosea, anapohutubia na kusema Bunge la Katiba badala ya kusema Bunge la bajeti, sasa je mzimu wa Katiba Mpya bado unamsumbua hasa baada ya leo kusema kuwa anapata ' push' nyingi kuhusu Katiba Mpya lakini kwa hilo wasahau kidogo.

Nini maoni yako?
 
Huu mzimu hautamuacha salama hata kidogo! Maana alishiriki kwenye mchakato wake kuanzia mwanzo mpaka kwenye hatua ulipofikia. Kimsingi hana cha kupoteza, lakini pia hana hulka kama zile za bosi wake hayati! Hivyo kama vipi, aumalizie tu.
 
Wana JF

Raisi Samia wakati akiwaapisha mawaziri amesema kuwa amepigiwa sana kelele kuhusu katiba mpya, ila kwa sasa anaomba tusahau kwanza. Swali ni je kuna uwezekano mama akarudisha mchakato wa katiba au ndio hapa kazi tu?

Haki huinua taifa.
 
Wanajukwaa ni zaidi ya mara mbili mama huwa anakosea, anapohutubia na kusema Bunge la Katiba badala ya kusema Bunge la bajeti, sasa je mzimu wa Katiba Mpya bado unamsumbua hasa baada ya leo kusema kuwa anapata ' push' nyingi kuhusu Katiba Mpya lakini kwa hilo wasahau kidogo.

Nini maoni yako?

We unaonaje, mana mwenyewe kashasema katiba msahau kidogo, kitugani kigumu hapo mkuu.
 
Back
Top Bottom