Mbona Magufuli alipokuwa akikosoa ya Kikwete mlikaa kimya? Muacheni Rais Samia

Anna Nkya

Member
Oct 21, 2021
69
341
Halafu hii wala sio kwa vyama vya upinzani kama mnavyoweza kufikiri kwamba wao ndio wanampinga Rais Samia, hao watu wako CCM zaidi.

Ni hivi, leo Rais Samia kugusia wale vifaranga wa kutoka Kenya ambao enzi ya Magufuli walichomwa moto. Akasema "DHAMBI TUPU". Naona povu la kutosha hasa kwa watu wanaojiiita #TeamMagufuli.

Hii sio mara ya kwanza wao kutokwa povu. Wana povu la bandari ya Bagamoyo, wana povu la mabinti kurudi shule, walitokwa povu Mange Kimambi kusalamiana na Rais, wana povu Sabaya kufungwa, Kalemani kuondolewa na mipovu mingine mingi.

Hoja yao ni Rais kukosoa mfumo Serikali iliyopita.

WANAFIKI : Walikuwa wanashangilia hapa kila siku Magufuli akisema "Hii nchi imechezewa sana.... Tumepigwa..." na kauli nyingine nyingi za kutaka kuonesha Kikwete, Mkapa hata Mwinyi hawakufanya lolote. Mlishangilia sana hamkujali kuhusu Kikwete.

Magufuli alikuwa anaandika kitabu chake, he had his own principles ambazo hazikuwa sawa na Kikwete. It was right pengine to go against them.

Samia yes alikuwa Makamu wa Rais kwa Magufuli, but we all know how this country works. Rais ndo anaamua kila kitu, Makamu is just there jamani.

KAMA SAMIA KAAMUA KUYASEMA HADHARANI AMBAYO HAKUKUBALIANA NAYO ENZI YA MAGUFULI AACHWE. Tuambizane ukweli. Mbona akimsifu hamuongei? Hizo ni Double standards.

LET SAMIA BE SAMIA. KUCHOMA VIFARANGA NI DHAMBI
 
Tena walishangilia. Nonsense kabisa.
Na ushangiliaji wao ulikuwa mbaya sana. Walikuwa wanakera kama chenga za Morrison! Ila Mungu fundi sana! Yaani alimwondoa jamaa bila hata kuonesha kazuri hata kamoja!

Five years no salary increment, hakuwahi kuongea hata alivyowapoteza akina Ben Saa Nane halafu na wizi Chaguzi, 2019 na 2020! ROho mbaya sana huyo JPM!
 
Na ushangiliaji wao ulikuwa mbaya sana. Walikuwa wanakera kama chenga za Morrison! Ila Mungu fundi sana! Yaani alimwondoa jamaa bila hata kuonesha kazuri hata kamoja! Five years no salary increment, hakuwahi kuongea hata alivyowapoteza akina Ben Saa Nane halafu na wizi Chaguzi, 2019 na 2020! ROho mbaya sana huyo JPM!
Na bado hawajajifunza kitu.
 
Polepole ni mtu wa hatar sana kwa amani na utulivu wa taifa.

Ukosikiliza mahojiano yake na wasaf utagundua kabisa kwamba jamaa ni MUSIBA MPYA!

Haungi mkono kabisa serikali ya mama na yote yatokanayo!
 
Bado kidogo mtasema na kutajana tu roho ya mtu inawatesa sana, Magufuli ameshalala usingizi lkn bado mnateseka na kuumia tu.

Kuna watu sijawahi kuwaona hata wakitabasamu tu, chuki tupu, hamna Amani mioyoni mwenu.

Mimi nasubiri vita na timbwili litakaloibuka mtakapo salitiana na inakuja.

R.I.P. Magu
 
Polepole ni mtu wa hatar sana kwa amani na utulivu wa taifa.
Ukosikiliza mahojiano yake na wasaf utagundua kabisa kwamba jamaa ni MUSIBA MPYA!
Haungi mkono kabisa serikali ya mama na yote yatokanayo!
Na 2025 ndio atachukia zaidi maana anaoshwa mazima ili ajikite vizuri huko anapofanyia majungu yake,alijua bwana'ke ataishi milele sio!
 
Kama kuchoma vifaranga ni dhambi mkuu vipi kuchinja kuku au kuchinja mbuzi?
Tofautisha kufanya mapenzi na mke wa ndoa na kufanya mapenzi na hawala. Kuna kitu kinabadilika kwenye kufanya??? Kipi halali na kipi siyo na kwann wakati tendon ni lilelile?????
 
Serikali ina kazi moja tu: kusimamia sheria! Na ijulikane kuwa sheria ni msumeno. Ukiwa kiongozi wa serikali lakini ukawa husimamii sheria kwa kuogopa inavyokata, ujue kuwa huutendei haki uongozi wako.
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom