Mbona hivi?

MgonjwaUkimwi

JF-Expert Member
Mar 10, 2006
1,336
875
Mbona hivi? Jamaa aliyekatika kidole kwenye ajali anapiga kelele masaa kadhaa, aliyekatika shingo yuko kimyaaaa!!

Mbona hivi? Mtu akikaa uchi bila kukusudia na huku akiwakodolea macho wanaomwangalia kwa mshangao, wanaomwangalia wanasemezana kwamba ni malaya, wakati akikaa uchi kwa makusudi huku akisoma gazeti, wapita njia watamsaidia wakizani kakosea!!

Mbona hivi? Majuu wahuni uvalia suluari zao magotini wakati watu wenye heshima zao bongo uvalia tumboni/kwapani!! wahuni wa bongo watavalia wapi, na wenye heshima zao majuu watavalia wapi??

Mbona hivi? Mwalimu anayelipwa anaandikia ubaoni, mwanafunzi hasiye na kazi anaandikia daftarini

Mbona hivi? Kunguni au mbu hawajaenda japo shule na inawachukuwa robo sekunde kugundua mshipa wa damu, dokta mwenye madgree ya kugundua mishipa atachukuwa masaa kadhaaa huku akiomba wasaidizi wake waje!!

Mbona hivi? Pilau ni wali husiohitaji mboga na mchuzi, kachumbari na mchuzi wake vimefikaje mezani?

Mbona hivi? Mtu kajikwaa na kuanguka barabarani, yuko bize kuangalia nani amemuona wakati anaanguka, badala ya kuangalia wapi yawezekana kaumia!

Mbona hivi? Hakuna kikaratasi cha onyo kutoka wizara ya ustawi wa jamii kwa wavaaji sketi na gauni kinachosema "vazi hili kamwe halitakustiri na halitaendana na maadili ya jamii pale mvaaji unapokaa chini na kutawanya miguu mbele ya kadamnasi"
 
Naona weekend ya Thanxgiving ipo mwendo mdundo/maneno semaga, maposo ponsoloto. Haya kaka, hayo ni mambo ya known knowns/known unknows/unknown knowns.........kaazi kweli kweli.!!!!
Umenikumbusha mambo ya uswahilini, choo cha nje mlango gunia. Balaa ni ile siku yenye kiupepo cha taratibu kiasi kwamba gunia linakuwa linapeperushwa kishkaji bila mjisaidiaji kujua!!! inakuwa "mbona hivi" pale watu wanapoona mali za watu kwa bei ya dezo na hakuna atayethubutu kumstua muhusika juu yalojiri ili apate kubuni miondo mbinu mipya, ya kujisaidia kwenye choo cha mlango gunia!!!.
 
Mbona hivi? Jamaa aliyekatika kidole kwenye ajali anapiga kelele masaa kadhaa, aliyekatika shingo yuko kimyaaaa!!

Mbona hivi? Mtu akikaa uchi bila kukusudia na huku akiwakodolea macho wanaomwangalia kwa mshangao, wanaomwangalia wanasemezana kwamba ni malaya, wakati akikaa uchi kwa makusudi huku akisoma gazeti, wapita njia watamsaidia wakizani kakosea!!

Mbona hivi? Majuu wahuni uvalia suluari zao magotini wakati watu wenye heshima zao bongo uvalia tumboni/kwapani!! wahuni wa bongo watavalia wapi, na wenye heshima zao majuu watavalia wapi??

Mbona hivi? Mwalimu anayelipwa anaandikia ubaoni, mwanafunzi hasiye na kazi anaandikia daftarini

Mbona hivi? Kunguni au mbu hawajaenda japo shule na inawachukuwa robo sekunde kugundua mshipa wa damu, dokta mwenye madgree ya kugundua mishipa atachukuwa masaa kadhaaa huku akiomba wasaidizi wake waje!!

Mbona hivi? Pilau ni wali husiohitaji mboga na mchuzi, kachumbari na mchuzi wake vimefikaje mezani?

Mbona hivi? Mtu kajikwaa na kuanguka barabarani, yuko bize kuangalia nani amemuona wakati anaanguka, badala ya kuangalia wapi yawezekana kaumia!

Mbona hivi? Hakuna kikaratasi cha onyo kutoka wizara ya ustawi wa jamii kwa wavaaji sketi na gauni kinachosema "vazi hili kamwe halitakustiri na halitaendana na maadili ya jamii pale mvaaji unapokaa chini na kutawanya miguu mbele ya kadamnasi"

Mkuu MgonjwaUkimwi

MgonjwaUkimwi unashitakiwa na jamii kwa ksababisha mbavu za wasomaji kuvunjika vunjika kwa maadishi yako ndani ya JF kitendo ulichokifanya siku na mahali pasipojulikana. Kuna wagonjwa kibao wako MOI na kuna hatari wakafanyiwa upasuaji wa vichwa badala ya mbavu. Hukumu nitatoa mara mgonjwa wa mwisho atakapopata nafuuuuu.

Hongera Mkuu kwa ubunifu mzuri.
 
Mbona hivi? 1+1 = 2, lakini 0+0 = 0. Pambafu! Taifa stars wakipoteza mechi ya ugenini na nyumbani, yaani 0+0, tutasema hawajapoteza mechi? Si watakuwa wamepoteza mechi mbili, yani 0+0 = 2?
 
Mbona hivi?Ulaya mbwa akijisaidia bosi wake anaokota kinyesi, Africa bosi akijisaidia mbwa wake anaokota kinyesi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom