Mbona hayati Magufuli alijenga vituo vya afya bila kukamua wananchi tozo za miamala? Alitoa wapi pesa?

Ndio zile zilikuwa zinachukuliwa kwenye mabenki na zingine ndio kina Sabaya walikuwa wanazikusanya kimenomeno
Kwa hiyo ujue Kuna walioumizwa
 
"Sitishwi wala sitishiki." - JPM
Kauli ya kimamlaka.Kauli ya kijasiri.Kauli ya kuthubutu kufanya hata kama maadui wamekuzunguka.Na kweli hakutishika na nchi ikanyooka na kuanza kunawiri.
 
Hili swali lazima tujiulize wadau. Mbona hayati JPM alijenga vituo vya afya 460+ bila kutukamua tozo kama hizi?

Je, kama alipata hizo pesa na kujenga vituo, chanzo kilikuwa ni kipi?

Je, kuna haja ya kutumia ujenzi wa vituo vya afya, shule na barabara kama justification ya kodi kama hizi?

Je, hakuna chanzo kingine cha mapato.
Mbona Samoa anaajiri, anatoa nyongeza za mishahara na kuendeleza miradi - pesa anapata wapi?
 
Hili swali lazima tujiulize wadau. Mbona hayati JPM alijenga vituo vya afya 460+ bila kutukamua tozo kama hizi?

Je, kama alipata hizo pesa na kujenga vituo, chanzo kilikuwa ni kipi?

Je, kuna haja ya kutumia ujenzi wa vituo vya afya, shule na barabara kama justification ya kodi kama hizi?

Je, hakuna chanzo kingine cha mapato.
Waulize wafanyabiashara wa maduka ya kubadilisha fedha za kigeni hasa kule arusha watakuambia chanzo ni kipi
 
Hili swali lazima tujiulize wadau. Mbona hayati JPM alijenga vituo vya afya 460+ bila kutukamua tozo kama hizi?

Je, kama alipata hizo pesa na kujenga vituo, chanzo kilikuwa ni kipi?

Je, kuna haja ya kutumia ujenzi wa vituo vya afya, shule na barabara kama justification ya kodi kama hizi?

Je, hakuna chanzo kingine cha mapato.
Subiri tozo nyingine inakuja muda si mrefu maana Rais wa Tozo keshaahidi kudhaminj Mashindano ya CECFA kwa Wanawake
 
Hili swali lazima tujiulize wadau. Mbona hayati JPM alijenga vituo vya afya 460+ bila kutukamua tozo kama hizi?

Je, kama alipata hizo pesa na kujenga vituo, chanzo kilikuwa ni kipi?

Je, kuna haja ya kutumia ujenzi wa vituo vya afya, shule na barabara kama justification ya kodi kama hizi?

Je, hakuna chanzo kingine cha mapato.
Acha kumfananisha JPM na wacheza taarab.
 
Hili swali lazima tujiulize wadau. Mbona hayati JPM alijenga vituo vya afya 460+ bila kutukamua tozo kama hizi?

Je, kama alipata hizo pesa na kujenga vituo, chanzo kilikuwa ni kipi?

Je, kuna haja ya kutumia ujenzi wa vituo vya afya, shule na barabara kama justification ya kodi kama hizi?

Je, hakuna chanzo kingine cha mapato.
Brother Magu alitoza kodi mpaka wafanya biashara wakaijua maana ya kodi leo bidada kawalegezea wafanya biashara kodi na hata waliokuwa wakihakikisha kodi zinalipwa ipaswavyo wanapelekwa mahakamani..Bidada ni mmagharibi kweli kiasi kaingia mazima kumtoza kodi mama yangu masikini nikimtumia sh elfu ishirini ya paracetamol ambayo serikali haitoi bure..Kutoza kodi masikini ni kujifungulia milango ya ahera siyo vizuri.

Vyama vya upinzani hawawezi kujitokeza kulalamikia tozo wanazotozwa masikini bali kudai Katiba kwani wanajua katiba mpya wanayoidai ni chaka la wao kufikisha dhamira zao za kisiasa,, na hilo chaka linafyekwa kila siku Wapinzani kazi yao ni kuongopa tuu ati watanzania wanataka katiba mpya wakati ni wao na inaonyesha hawajui wananchi masikini wa Tanzania wanataka nini---kodi ya miamala hawaitaki ila CDM,ACT na wengineo wako kimya na wengine kushinda Ufipa street-kina Mbatia ili wapate ubunge ktk nchi ya kusadikika.

Kifo cha Brother ni pigo kubwa na nina uhakika Brother angekuwepo na tumewekewa vikwazo vya kiuchumi na vya aina yeyote asingefikia hatua ya kutoza kodi masikini kwani alimjua masikini ni nani,,,,Yametufika na Mungu tu ndiye ajuae
 
Hivi unajua madhara, maumivu, machungu na vifo vilivyosababishwa na taxforce kweli au ndo tuna bwabwaja ya Kiba?
 
Mikoani vilio vinatawala....hospitali za wilaya, achilia mbali vituo vya afya, wagonjwa wanalazimika kununua vifaa tiba na madawa kwenye maduka binafsi ya madawa. Kuna faida gani kupanua ujenzi wa vituo zaidi wakati vilivyopo havitoi huduma zinazotakiwa?
 
Tutamkumbuka mwamba yule wa Kanda ya ziwa
Kwa lipi?kuhutubia taifa kila siku?
Kwa taarifa tu hii ni bajeti ya JPM.
Bajeti ya serikali hukamilika mwezi February kila mwaka ( kuandaliwa)
Jamaa alikufa mwezi wa tatu. Sasa mama analaumiwa kwa lipi hapa.
JPM ndo alileta mpaka vikokotoo hapa.
Alidai kujenga Vituo vya afya nasi tukamshangilia. Wengi wetu ni mbumbumbu.
Hatujui kutofautisha kati ya kituo cha afya na jengo la kituo cha afya
Kinaitwaje kituo cha afya kama hakuna vifaa?
Tuliambiwa vimejengwa nchi nzima? Tukashangilia.
Hivi vinavyojengwa ni vipi tena?
 
Mikoani vilio vinatawala....hospitali za wilaya, achilia mbali vituo vya afya, wagonjwa wanalazimika kununua vifaa tiba na madawa kwenye maduka binafsi ya madawa. Kuna faida gani kupanua ujenzi wa vituo zaidi wakati vilivyopo havitoi huduma zinazotakiwa?
Usisahau JPM alituaminisha kwamba anafungua maduka ya MSD kila hospitali yapo wapi?
Kumtawala mtanzania ni simple sana
 
Hili swali lazima tujiulize wadau. Mbona hayati JPM alijenga vituo vya afya 460+ bila kutukamua tozo kama hizi?

Je, kama alipata hizo pesa na kujenga vituo, chanzo kilikuwa ni kipi?

Je, kuna haja ya kutumia ujenzi wa vituo vya afya, shule na barabara kama justification ya kodi kama hizi?

Je, hakuna chanzo kingine cha mapato.
Je ukiambiwa ndiye general Sir.baya alikuwa anafanikisha kwa namna moja au nyingi utasemaje?
 
Back
Top Bottom