buswelu moja
JF-Expert Member
- Aug 24, 2014
- 226
- 147
MAHAKAMA ya hakimu mkazi Arusha inatarajia kutoa hukumu ya kesi iliyofunguliwa na mkuu wa wilaya mstaafu nchini,Dahn Makanga dhidi ya mfanyabiashara ,Mathew Mollel ambaye ni mkazi wa jijini Arusha .
Hukumu ya kesi hiyo inatarajiwa kutolewa mnamo Novemba 14 mwaka huu na hakimu mkazi wa mahakama hiyo,Gwantwa Mwankuga baada ya upande wa mashtaka na utetezi kufunga ushahidi wao.
Katika kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi kumi na upande wa utetezi ulikuwa na shahidi mmoja .
Awali,Mollel kupitia kwa wakili wake Ephraim Koisenge aliieleza mahakama hiyo kwamba alikuwa na mashahidi wawili.
Katika kesi hiyo Mollel anadaiwa mnamo mwaka 2014 akiwa jijini Arusha alighushi mukhtasari wa serikali ya mtaa wa Levolosi.
Ushahidi wa upande wa utetezi mahakamani unaonyesha kwamba Mollel aliuziwa eneo hilo na Makanga kiundugu eneo ambalo linadaiwa kughushiwa mukhtasari .
Mollel,katika utetezi wake anadai ya kwamba Makanga akiwa mkuu wa wilaya ya Kasulu alimvamia nyumbani kwake akiwa na askari wa jeshi la polisi wakitafuta hatimiliki ya kiwanja nambari 231 kitalu DD eneo la Mianzini jijini Arusha.
Katika ushahidi wake mahakamani hapo Mollel anakanusha madai ya kughushi mukhtasari wa serikali ya mtaa wa Levolosi kwa kuwa mukhtasari anaoutambua ni ule uliopitishwa na wajumbe wa serikali ya mtaa wa Levolosi chini ya katibu wa kikao hicho ambaye ni marehemu ,Sara Kara na mwenyekiti wake,Haruna Fundikira.
updates;- wanajukwaa hukumu ni siku ya jumanne ya wiki ijayo ripota wenu wa nguvu nitakuwa mahakamani kuwapa kila kitu live bila chenga stay tuned
Mwisho.
Hukumu ya kesi hiyo inatarajiwa kutolewa mnamo Novemba 14 mwaka huu na hakimu mkazi wa mahakama hiyo,Gwantwa Mwankuga baada ya upande wa mashtaka na utetezi kufunga ushahidi wao.
Katika kesi hiyo upande wa mashtaka ulikuwa na mashahidi kumi na upande wa utetezi ulikuwa na shahidi mmoja .
Awali,Mollel kupitia kwa wakili wake Ephraim Koisenge aliieleza mahakama hiyo kwamba alikuwa na mashahidi wawili.
Katika kesi hiyo Mollel anadaiwa mnamo mwaka 2014 akiwa jijini Arusha alighushi mukhtasari wa serikali ya mtaa wa Levolosi.
Ushahidi wa upande wa utetezi mahakamani unaonyesha kwamba Mollel aliuziwa eneo hilo na Makanga kiundugu eneo ambalo linadaiwa kughushiwa mukhtasari .
Mollel,katika utetezi wake anadai ya kwamba Makanga akiwa mkuu wa wilaya ya Kasulu alimvamia nyumbani kwake akiwa na askari wa jeshi la polisi wakitafuta hatimiliki ya kiwanja nambari 231 kitalu DD eneo la Mianzini jijini Arusha.
Katika ushahidi wake mahakamani hapo Mollel anakanusha madai ya kughushi mukhtasari wa serikali ya mtaa wa Levolosi kwa kuwa mukhtasari anaoutambua ni ule uliopitishwa na wajumbe wa serikali ya mtaa wa Levolosi chini ya katibu wa kikao hicho ambaye ni marehemu ,Sara Kara na mwenyekiti wake,Haruna Fundikira.
updates;- wanajukwaa hukumu ni siku ya jumanne ya wiki ijayo ripota wenu wa nguvu nitakuwa mahakamani kuwapa kila kitu live bila chenga stay tuned
Mwisho.