Mbio za Watuhumiwa "UFISADI" Kwenda Mahakamani Zimeishia Wapi?

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Hivi kweli hizi mbio na matamshi makali makali kwenye vyombo vya habari kwa hao watuhimiwa kuwa wangewafikisha watoa tuhuma mahakamani zimeishia wapi... au hisia zetu kuwa hiyo ilikuwa mikwara mbuzi zimekuwa kweli?...

Posted Date: 11/17/2007

Mbio za watuhumiwa wa ufisadi kwenda mahakamani, zimeishia wapi?

Na Ramadhan Semtawa

KUITWA fisadi kama si fisadi huwa inaumiza roho kweli, kiasi ambacho, kama ni tuhuma za uongo, mtu huweza kupata kesi kwa kuua anayemtuhumu.

Hii inaumiza zaidi kwa mtu aliyepewa dhamana ya kuongoza idara yoyote katika ofisi ya umma, ambayo huendeshwa kwa kodi inayotozwa kwa sehemu kubwa kutoka kwa wavuja jasho wa nchi hii yaani wakulima na wafanyakazi.

Nasema kodi za wakulima na wafanyakazi, ndiyo! najua matajiri wengi ambao ni wafanyabiashara katika nchi hii hawalipi kodi na hawa ni wahujumu wakubwa wa uchumi wa nchi, lakini hii si mada yangu.

Hapa najadili na kuangalia heshima ya madaraka ya umma katika siku hizi na zama zile wakati wa serikali ya chama cha Tanganyika African National Union (TANU), ambacho hadi leo bado kinabaki kuwa msingi wa maadili ya uongozi wa umma.

Heshima ya madaraka ya umma imesisitizwa sana katika moja ya ahadi kumi za Mwana TANU, kwamba "Cheo ni Dhamana", kwa mantiki hiyo, aliyepewa dhamana hiyo hakutakiwa kuitumia kwa maslahi binafsi.

Iliwezesha kuwepo heshima ya madaraka ya umma na kuzingatiwa kwa maadili ya kazi, ikiwa ni pamoja na mapambano dhidi ya ufisadi.

Ufisadi katika awamu ya kwanza chini ya serikali ya TANU, ulipigwa vita kwa nguvu zote, hivyo mtu aliyetuhumiwa au kubainika na rushwa au kuhujumu uchumi alijihisi kama mhaini na aliomba ardhi ipasuke.

Nchi hii ilikwenda vizuri, waliokuwa wakifanya ufisadi ambao ni pamoja na kuhujumu uchumi, walihofu kweli na kila mmoja alikuwa akitaka kulinda heshima yake katika jamii na nafasi ya madaraka aliyonayo.

Hii imenisukuma kujadili hawa ambao walitajwa na wapinzani kwamba ni mafisadi, baadhi yao walikaa kimya lakini wengine wakatamka kwenda mahakamani kujisafisha.

Binafsi, nilijawa na hamu kuona wapi watuhumihawa hawa wangefungua kesi zao na lini hasa ili kujisafisha na tuhuma hizi.

Kwa maana, hawa ni watu ambao heshima zao katika nchi zimechafuka, Watanzania wengi wanawaona ni watu waliohujumu uchumi tu kutokana na tuhuma hizo za ufisadi wa mabilioni ya fedha za umma.

Kibaya zaidi hata watoto au ndugu zao ambao wana upeo, hawawezi kujisikia vizuri katika mkusanyiko na wenzao wanaposikia baba zao wanaitwa mafisadi na pia si heshima kwa mtu anayeongoza ofisi ya serikali kuitwa fisadi.

Hii ni dhambi na aibu kubwa , kutuhumiwa kufanya ufisadi kwa nchi masikini kama Tanzania ni dhambi kubwa ambayo lazima mtu athibitishie umma undani wa tuhuma kwa kutumia vyombo vya sheria.

Kwa maana tuhuma za kuhujumu uchumi kwa kutumia madaraka ya umma katika nchi kama hii yenye watoto wanaokufa kwa malaria kila kukicha na akina mama na dada zetu wanaojifungulia vichakani vijijini, ni dhambi kubwa.

Hii inatosha kwa mtuhumiwa wa ufisadi kwenda haraka mahakamani ili umma ujue kama kweli ni fisadi au si fisadi.

Ndiyo maana niliposikia akina Gray Mgonja Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Patric Rutabanzibwa, Katibu Mkuu Wizara ya Maji na Nazir Karamagi, Waziri wa Nishati na Madini, wanakwenda mahakamani nilifurahi.

Hii inatokana na tuhuma zinazowakabili kuwa kubwa ambazo mtazamo wangu ni za kuhujumu uchumi wa nchi kwani mamilioni wanayodaiwa kuhusika nayo katika upotevu au mikataba isiyokuwa na maslahi kwa nchi, ni mengi.

Kibaya zaidi, watu hawa ni bora wangekaa kimya kama baadhi ya wenzao lakini walijigamba kwenda mahakamani matokeo yake hadi leo hii haijulikani mbio zao zimeishia wapi?

Hii inatoa taswira mbaya kwa umma, umma unajenga hisia kwamba hizi tuhuma za ufisadi dhidi ya hawa wana wa nchi wanaotajwa, ni za kweli hivyo kuamsha hasira zao.

Umma huu umechoka, tayari umepigwa na umasikini huku maisha yakzidi kuwa magumu siku hadi siku, thamani ya fedha ikizidi kuporomoka ikilinganishwa na mfumuko wa bei za bidhaa.

Hakuna kitu kibaya katika maisha kama kundi kubwa la wananchi wakiwa katika hali ngumu, huku wakijenga hisia kwamba kundi dogo linanufaika kwa kuibia na kuhujumu uchumi wa nchi kwa kutumia madaraka ya umma.

Lazima watawala walioshika madaraka ya dola na watendaji wote wa ngazi tofauti katika mhimili yote ya dola ambayo inaendeshwa kwa kodi za umma, wajitambue, wajenge heshima ya ofisi za umma kwa kuhakikisha hazitumiki kinyume na ahadi ya 'Cheo ni Dhamana'!

Kwa maana kama hawa waliotuhumiwa na kuahidi kwenda mahakamani wangekuwa wamejengeka katika maadili ya uongozi na kutambua zile ahadi kumi za mwana TANU, basi tayari wangekuwa wamekwenda mahakamani.

Lakini masikini looh! nchi ina watu ambao wanaonekana kuwa wana 'system' lakini ni hawa ambao leo hii wanathibitisha kwamba walipinga Azimio la Arusha ndiyo wengine wanatuhumiwa kuitumia ofisi za umma kuhujumu uchumi wa nchi.

Umefika wakati, lazima tuwe na taifa la viongozi wa serikali ambao wakitaka kuhongwa watalia kwa kutoa machozi, taifa ambalo kila mtu katika nafasi yake atafanyakazi akijua anafanya kwa ajili ya nafsi yake.

Tubadili fikra na mtazamo kwamba, madaraka ya umma ni sehemu ya kuhujumu uchumi wa nchi kwa kujilimbikizia utajiri badala ya kutumikia nchi na kufuata maadili katika kusimamia dhamana hiyo.

Naamini haya ni mambo ambayo watuhumiwa hawa wa ufisadi waliotaka kwenda mahakamani walipaswa kukaa na kutafakari kwa kina, lakini hawakufanya au wanatumia unyonge wa Watanzania na kuona hakuna umuhimu wa kufanya hivyo.

Hawa wameutangazia umma wa Watanzania kwamba watakwenda mahakamani kujisafisha na tuhuma za ufisadi, sasa wanapaswa kukumbuka 'Ada ya Mja Hunena, Muungwana ni Vitendo'.


Je, mbio na azma hii imeishia wapi, je wamebaini kwamba wakienda mahakamani mengi yataibuka na kuzidi kuumbuka?

Sasa kama ni hivi, basi waitishe tena mikutano na waandishi wa habari kama mwanzo, kisha wautangazie umma kwamba wameachana na mpango wao wa kwenda mahakamani na watoe sababu.

Hii si hiari yao ni lazima kwa maana mabosi wao ni wananchi ambao ndiyo wanaoendesha serikali kwa kulipa kodi ambazo pia zinawalipa wao mishahara.

Kwenda mahakamani au kutokwenda halikupaswa kuwa jambo la hiari, lakini wanaweza kufanya hivi kutokana na upole huo wa Watanzania.

Lakini ukweli ni kwamba, matukio kama haya yangekuwa katika nchi ambazo wananchi wamejenga utamaduni wa kupinga uchafu wa viongozi wa serikali kwa njia za maandamano na migomo, hawa tayari wangekuwa wameng'olewa katika nafasi hizo.

Leo hii hawa wanaringia udhaifu huu, lakini umma huu siku moja utalipuka, moto wake utachoma na kuwasambaratisha wote wanaoihujumu nchi.

Tanzania ya mwaka 1970 si kama ya leo, ya leo haiwezi kuwa kama ya kesho au kesho kutwa, mabadiliko yanakuja taratibu, fikra za utaifa na uzalendo zinazoambatana na ujasiri wa umma kufanya maamuzi, zinakuwa siku hadi siku.

Wapo vijana wenye fikra za kimapinduzi wanazidi kuamka, wako ndani na nje ya nchi hii, wanajua mbivu na mbichi, hawawezi kukubali kuona nchi inatafunwa.

Sasa ni vema watuhumiwa wa ufisadi ambao wameazimia kwenda mahakamani wakafanya hivyo wenyewe kama walivyoutangazia umma , kwani kutokufanya hivyo ni kuzidi kucheza na akili za Watanzania na kuichafua serikali, mbio zao zimeishia wapi?


Source: Gazeti la Mwananchi.

SteveD.
 
Zimeishia pale pale kama za wale waliowataja zilipoishia...kwa maneno mengine, majina yametajwa na kitakachofuatia hakuna. CCM na Kikwete watachaguliwa tena kwa asilimia kubwa tu. Anayebisha na asubiri aone....hamna haja ya kuandikia mate wakati wino upo. 2010 sio mbali...
 
Zimeishia pale pale kama za wale waliowataja zilipoishia...kwa maneno mengine, majina yametajwa na kitakachofuatia hakuna. CCM na Kikwete watachaguliwa tena kwa asilimia kubwa tu. Anayebisha na asubiri aone....hamna haja ya kuandikia mate wakati wino upo. 2010 sio mbali...

Bado wanajipanga, wako busy kufunua vitabu vya sheria waone wapi watawaweka kona wapinzani. Wanasheria nao wanadai dau kubwa
 
Zimeishia pale pale kama za wale waliowataja zilipoishia...kwa maneno mengine, majina yametajwa na kitakachofuatia hakuna. CCM na Kikwete watachaguliwa tena kwa asilimia kubwa tu. Anayebisha na asubiri aone....hamna haja ya kuandikia mate wakati wino upo. 2010 sio mbali...

...inasikitisha, na uliyonena yana ukweli mwingi tu ndani yake. Ndipo hapo mtu anapothibitisha kuwa UTEKELEZAJI nchini mwetu katika kila nyanja ya maisha ya Mtanzania ndiyo wa kulaumu na ni chanzo cha maisha yetu kuwa duni kila leo hii...

Kwa maana kama watu wanaita waandishi wa habari kueleza kitu halafu wiki chache au miezi kadhaa ikipita, yote waliyosema yanakuwa yamesahaulika, huu miye nitauita "ugonjwa wa Mtanzania", sijui yapi yanayotajwa kwenye sera za kitaifa basi yanakumbukwa na kutekelezwa? maana nayo huitiwa vyombo vya habari yanapowajia vichwani viongozi wetu. Labda ndiyo maana wengine wanasema kuwa mwafrika ni mgumu kuelewa na mwepesi kusahau... hivi lini tutaanza kutekeleza vile tunavyovisema?!

SteveD.
 
Bado wanajipanga, wako busy kufunua vitabu vya sheria waone wapi watawaweka kona wapinzani. Wanasheria nao wanadai dau kubwa

UFUNUO, nadhani kwa upande wa wapinzani kuna wanasheria walijitokeza kuwa mawakili wa bure... na nimatumaini yangu wale waliotajwa 'mafisadi' kutokana na huo ufisadi nao basi wana wanasheria wao na hilo halitakuwa gharama kama madai ya wapinzani ni ya kweli, kama ni ya uongo basi gharama zinaweza kuwa za juu kweli kama usemavyo... lakini kwanini sasa walitoka mchaka mchaka kualika vyombo vya habari na kutishia kuwa wanasheria wao wanajipanga kwenda kuwawakilisha...

SteveD.
 
Hilo limethibitisha kwamba kweli ni mafisadi. lakini hata kama hawakwenda mahakamani inawezekana wanakosa raha mitaani maana kila wakionekana wananyooshewa vidole "fisadi yuleee kapita" au "fisadi yuleee anakuja" si haba. Dhamira zao pia zinawashtaki.
 
Hakuna atakaekwenda mahakamani kwani tumeshawapa mikakati ya kushika mmoja ni kuwambia wakienda mahakamani ni kupoteza fedha zao,hivyo waachwe wanaowanadi mafisadi waendelee na makelele,na zaidi ilivyokuwa hakuna madhara,kura zetu,wasimamizi wetu mitaji yetu,polisi wetu majeshi yetu sasa ya nini kushindana na wenye njaa.
 
Ni kweli mwiba hiyo ndiyo jeuri yao, lakini wanatakiwa kusoma historia maana kama wanakula wenyewe na kuyasahau hayo majeshi yao, polisi wao, watumishi wao iko siku hao watakuwa sumu yao.

Sisi tutaendelea kupiga kelele mpaka kieleweke
 
Lowassa: Tutajieni mafisadi




na Joseph Malembeka, Morogoro



WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, amekana serikali kuwatambua watu wanaotajwa kuwa vigogo wake, wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya na rushwa.
Kwa kuwa serikali haiwatambui watu hao, Lowassa amewataka watu, wakiwemo viongozi wa dini na katika sekta mbalimbali nchini, kuwataja vigogo hao ili serikali iwashughulikie.

"Nasema watajeni, na ninaahidi tutawashughulikia bila kujali cheo cha mtu au nafasi aliyonayo katika taifa hili na nje ya taifa," alisema Lowassa.

Alisema hayo jana alipokuwa akihutubia waumini na watu mbalimbali waliofika kwenye viwanja vya Kanisa ka Kiinjili la Kilutheri (KKKT) Bungo mjini hapa, katika sherehe za kumuweka wakfu Askofu wa kanisa hilo Dayosisi ya Morogoro, Jacob ole Mameo.

"Jamani kwa muda mrefu nimekuwa nasikia wanaokamatwa kwa dawa za kulevya na rushwa eti ni watu wadogo wadogo huku vigogo wakitazamwa, tatizo ni kuwa mnasema tu vigogo, vigogo hamuwataji," alisema Lowassa.

Waziri Mkuu aliwasihi waumini wa dini zote kuisaidia serikali katika vita dhidi ya rushwa na dawa za kulevya baada ya maelezo yaliyotolewa na Askofu Mameo, kuwa bila ushirikiano vita hiyo haitakwisha.

Katika hotuba hiyo, Lowassa, aliutaka uongozi wa Mkoa wa Morogoro kusimamia vema haki za wananchi katika migogoro ya ardhi inayowakabili kwa muda mrefu, ili kuepusha matatizo yayoweza kujitokeza.

"Mimi niendelee kuwaomba viongozi hasa wa dini kuisaidia serikali katika mapambano haya na matatizo ya ardhi ambayo ufumbuzi wake unahitaji busara kutoka kwenu," alifafanua.

Baada ya kusimikwa rasmi kuliongoza kanisa hilo, Askofu Mameo alisema dayosisi ya Morogoro imekuwa msitari wa mbele kuisaidia serikali kuboresha huduma za jamii zikiwemo elimu, maji na afya.

"Hadi sasa tangu ianzishwe, dayosisi hii tumefanikiwa kuboresha mambo mbalimbali ikiwemo kuchimba visima 22 vya maji safi kwenye wilaya, kata na vijiji," alisema Askofu Mameo.

Aidha, alisema kanisa hilo liko msitari wa mbele katika mapambno dhidi ya ujambazi, dawa za kulevya, rushwa na mimba kwa wanafunzi.

"Kuna usemi usemao kelele za chura hazimzuii ng'ombe kunywa maji mtoni, usemi huu hasa ni kichocheo cha watu kuendelea kushiriki katika vitendo hivyo bila woga… serikali iongeze nguvu," alisema askofu huyo.

Kuhusu migogoro ya ardhi mkoani hapa, alifafanua kuwa itakuwa chanzo cha kuvunja ndoto za maisha bora kwa kila Mtanzania, iwapo juhudi za makusudi hazitachukuliwa kunusuru tatizo hilo, lililoota mizizi katika jamii ya wakulima na wafugaji.

Naye Askofu Mkuu wa kanisa hilo nchini, Alex Malasusa, aliyemweka wakfu askofu huyo, alimhakikishia Waziri Mkuu kwamba, KKKT itaendelea kuwashauri wananchi katika masuala ya amani, maendeleo na kukuza uchumi.

Kusimikwa kwa askofu Mameo, kunafungua ukurasa mpya wa kanisa hilo kuwa askofu wa pili baada ya aliyekuwepo, Askofu Richard Kitale, kumaliza muda wake kwa mujibu wa katiba ya kanisa hilo

Haya jamani mazingaombwe mengine haya,hivi lowasa hakusikia jina lake au kwa sababu mkubwa hakosei
 
Huyu EL nayo anataka kuumbuliwa! Kama mafisadi, walitajwa! Na yeye yumo kwenye list of shame ya BoT. Sasa anazungmzia hii ya wauza unga, mbona listi ilitoka siku nyingi sana! Jamani mtu aliyo nayo aibandike hapa JF ili wapambe wake EL wampelekee taarifa kwamba washikaji zake wamo!!
Lakini ili kurahisisha yote si angemwomba mshikaji wake no.1 Mungwana?
 
Huyu EL nayo anataka kuumbuliwa! Kama mafisadi, walitajwa! Na yeye yumo kwenye list of shame ya BoT. Sasa anazungmzia hii ya wauza unga, mbona listi ilitoka siku nyingi sana! Jamani mtu aliyo nayo aibandike hapa JF ili wapambe wake EL wampelekee taarifa kwamba washikaji zake wamo!!
Lakini ili kurahisisha yote si angemwomba mshikaji wake no.1 Mungwana?

Hawa viongozi wetu hizi kauli zao zimepinda sana, na sijui washauri wao wanafanya nini ama viongozi wenyewe ndo ma 'out spoken'???

Sasa Jk anasema orodha anayo anawapa muda.. mara PM anaibuka kwamba tuleteeni hiyo orodha.. sasa manake hawawasiliani ama??

Nimechoshwa na mawenge wenge haya!!
 
Hawa viongozi wetu hizi kauli zao zimepinda sana, na sijui washauri wao wanafanya nini ama viongozi wenyewe ndo ma 'out spoken'???Sasa Jk anasema orodha anayo anawapa muda.. mara PM anaibuka kwamba tuleteeni hiyo orodha.. sasa manake hawawasiliani ama?? Nimechoshwa na mawenge wenge haya!!

Hawa ni wasanii walio madarakani.....sioni tofauti zao na wale wazecomedi akina Masanja mkandamizaji
 
Inahitajika mtu awe na kichwa cha mwendawazimu kufahamu jinsi serikali ya JK_EL inavyofanya kazi.

Labda huwa wanakutana vijiweni tu, hawana muda rasmi wa kukutana kwenye baraza la mawaziri na kujadili mambo ya msingi.

Kila mtu anafanya kazi kivyake ndo maana na yeye anataka kupelekewa hiyo list kivyake!
 
Ni kweli mwiba hiyo ndiyo jeuri yao, lakini wanatakiwa kusoma historia maana kama wanakula wenyewe na kuyasahau hayo majeshi yao, polisi wao, watumishi wao iko siku hao watakuwa sumu yao.

Sisi tutaendelea kupiga kelele mpaka kieleweke

Sure mkuu,

Walikuwa wanapima upepo wakaona umewaelemea.
They were only trying 2 buy time!

na wamefanikiwa sana kwani hivi sasa yameshaisha hamna kuzomea tena wala nini ni kidumu tu chama, hujaona wasomi wetu huko uganda?

Shame!
 
Lakini huu usanii wa viongozi kwenda majukwaani na kutoa hizi kauli eti wenye majina ya wauza unga au wala rushwa waniletee huu ni upumbavu wa hali ya juu na inaonyesha jinsi hizi blah blah za mikingamo za nchi yetu zilivyofikia pabaya na ndio maana tunaendelea kuwa maskini tuu kila siku,na nani kawaambia wao ndio polisi au mahakama ndio tuwapelekee hao watuhumiwa? yaani wao ndio polisi,mahakama na waziri mkuu? tutafika kweli? tunahitaji kuheshimu utawala wa sheria na vyombo vyake ndio maana kuna watu wanalipwa kufanya hizo kazi sio majungu majungu tuu ya hawa kina EL majukwaani ilimradi kupata umaarufu tuu.
 
Hii inatosha kuthibitisha ni namna gani viongozi wetu walivyo. Wao kung'aka vile ilikuwa tu ni bosheni ya kimtindo ili kufanya wananchi waone wanachafuliwa tu majina yao. Sasa kwa sababu hali ni almost shwari no need! utawasikia tena ikizuka kashfa nyingine. Ila very interesting mmoja wao (Vicent Mrisho) hajawahi kutamka lolote kuhusu tuhuma hizo. Na huyu mzee inaonyesha ni mafia kweli!!!!!!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom