Mbinu zinazotumiwa na Matapeli kwenye M-Pesa,Tigo Pesa Airtel M n.k

Nikiwa kama wakala wa E-money (Miamala ya pesa) nimeshuhudia mambo mengi sana ambayo nafikiri kwa kuyasimulia naweza nikawasaidia watu wengi sana especially mawakala wa hizi Mpesa,Tigopesa, AirtelMoney nk kuepuka utapeli ambao hufanywa na watu wenye nia mbaya. Natambua kwa wakala anayefanya kazi kwa kutegemea kamisheni let say ya laki 3 kwa mwezi unapotapeliwa let say laki 7 inauma sana na inaweza kukurudisha nyuma kimaendeleo. Zifuataza ni mbinu ambazo hutumiwa na matapeli kwenye hizi miamala.

Mbinu 1: Wakala unapokea ujumbe wa kupokea pesa mfano, "...imethibitishwa umepokea kiasi cha Tsh xxx kutoka kwa xxxx salio lako ni xxx" Wakati unashangaa nani katuma hiyo pesa (Kutoa) mara unapokea simu mara nyingi hujitambulisha kwamba wanatokea Mpesa, Tigopesa etc watakuuliza kama kuna pesa umeipokea imetumwa kimakosa na mtu hivyo wanaomba uirudishe, mara nyingi huwa wanajitahidi kukuwekea pressure sana wa vitisho vya kuifungia laini yako ili usipate wazo la kuangalia salio, Ukifanya kosa ukawasikiliza ukaituma hiyo pesa IMEKULA KWAKO.
Mara nyingi njia hii hufanyika kwa ushirikiano na wafanyakazi wa mitandao husikaambao husaidia kujua kiasi cha salio ulilonalo kwenye simu yako. Na katika hili tigopesa wanafanya sana.

Solution: Hakikisha unamhudumia mtu unayemuona mbele yako, Kama mtu akikosea kutuma pesa mtandao husika baada ya kukupigia simu wataikata iyo pesa na kuirudisha kwa mhusika na sio kukwambia wewe wakala uirudishe. Na hakikisha messeji yoyote ya muamala unayopokea kwenye simu yake imetoka M-Pesa, TigoPesa nk na sio kwenye namba flani ya simu.

Mbinu 2: Mtu anakuja anakuja anakupa simu yake anakuomba umtolee pesa, unamuuliza shilingi ngapi anakwambia hana ukakika, anakuomba umuangalizie salio, ukiuliza salio inakuomba password, unamuomba akupe password anakuomba simu ili aweke password alafu anakaa nayo akisubiri meseji ya salio iingie then anakupa iyo msg ya salio. Labda unaona msg "Imethibitishwa salio lako ni 590,000..." atakwambia umtolee labda lakin5 na Mara nyingi unapokuwa unafanya hayo huyo mtu anakuwa ana hali flani ya haraka sana na anakuwa anakuharakisha au ukute hiyo simu yake inaita mara kwa mara hivyo kukukatisha mara kwa mara kutoa pesa. Mara anatokea mtu either ana bodaboda au gari nje, Basi huyu mteja wako anakuulizaa, Kaka /dada ushatoa? unamjibu "bado, kuna watu wanakupigia hapa wananikatisha katisha sana" atakwambia, "Samahani dada/kaka naomba wakati unaendelea kutoa nipe hiyo hela nimpe huyu jamaa hapa nje ananisubiri kuna mgonjwa hapo tunampeleka hospitali" Kwakuwa unaona una simu yake ambayo umeona msg ina salio la kutosha na kweli umeona kuna mtu anamsubiri nje UKIMPA TU HIYO HELA UMELIWA, Anaondoka na simu atakuachia, ukiweka password aliyokupa itagoma, unakuta ka simu kwenyewe ni ka itel kapya ka 20,000.

Solution: Mbinu hii imewatapeli watu wengi sana pesa, hakikisha USIMPE MTEJA PESA KABLA HUJAPATA MSG YA KUCONFIRM KWENYE SIMU YAKO YA UWAKALA, NA PIA USIMPE MTU PESA KWA KUANGALIA MSG ALIYOIPATA YEYE KWENYE SIMU YAKE. Mteja anapokuja kwako kutoa hela akikuomba umtolee, akishakupa simu USIIMRUDISHIE MPAKA UMALIZE KUFANYA MUAMALA (Usimpe aweke password alafu akurudishie mwambie akutajie password na kama hataki mwambie atoe mwenyewe). Ukimpa simu aweke password ndo hutumia huo mwanya kuweka msg ya kuonyesha wana salio kwenye simu yao, Mpe mteja pesa pale tu unapopata confirmation kwenye simu yako.

Mbinu ziko nyingi ila hizi ndo hutumika zaidi na zingine wataongeza wadau.
nyongeza usimruhusu mteja akupe hela uzihesabu then umrudishie kisha akazuga zuga akakurudishia tena umwekeee hapa hakikisha unahesabu tena pesa alizokupa.usimwamini mteja hata kidogo.mimi pia nina ofisi ya uwakala na nmb bahati mbaya hilo tukio limenitokea mwenyewe.nimeibiwa laki kwa mtindo huo.nikwamba utapomtumia salio palepale anahamisha na line anatupa.tuwe makini hizi biashara zenyewe hazina faida kivileee
 
Hao ndo kuwapiga wapate akili.
Ukipiga hata laki nne halafu kamishen inakuja 80.... Ndo akili itafungua....(utani Mkuu)
ujue walio pewa jukumu la kuwaelimisha mawakala wanakaa ofisini

Ila wapige hela wanajifanya kuitisha semina kwa mawakala lengo sio kufundisha ila nikupiga hela za kampuni


Elimu ya mara kwa mara kwa mawakala ni mhimu kuliko hata wahusika wanavyo lichukulia
 
Nilitumia sim banking kuweka hela kwny akaunti yangu ya tigopesa ilikuwa usiku kama saa 4 hela nilikuwa nataka nilipie vifaa asbh.


Hela ikaingia msg haikuja lkn nilivyocheki salio kwny tigopesa ilionyesha ipo...asubuhi nmeamka niende kwa wakala nitoe hamna hata senti kupiga simu tigo naambiwa sijui nmetuma hela kwa Mtu anaitwa bakari maulid na namba haipatikani.

Kwenda polisi nikaandikiwa maelezo halaf file liende kwa mtu anayedili na mambo ya mtandao sijui nn.

Nikaona isiwe tabu nimwachie Mungu tu.
Hii pia imemtokea Dada yangu last week. Sema ni hela mbuzi. Siku ya kwanza wamechukua thirty, na ndo ulikuwa hiyo hiyo kwa tigopesa yake. Kesho yake wakampiga tena 15 baada ya kuweka hiyo hiyo 15. Halafu text ya tigopesa ikaingia umetuma pesa kwenda namba XXX. Kuwapigia tigo wakajibu eti hii kitu haiwezekani labda we mwenyewe umetuma. Siku ya tatu ikaja tena text kuwa muamala haujafanikiwa. Kumbe jamaa alikuwa kwenye system anataka kujitumia tena pesa. Kweli Tigo ndo wanaongoza kwa wizi Huu. Wanafanyakazi wao wengi hawapo loyal!
 
Hii pia imemtokea Dada yangu last week. Sema ni hela mbuzi. Siku ya kwanza wamechukua thirty, na ndo ulikuwa hiyo hiyo kwa tigopesa yake. Kesho yake wakampiga tena 15 baada ya kuweka hiyo hiyo 15. Halafu text ya tigopesa ikaingia umetuma pesa kwenda namba XXX. Kuwapigia tigo wakajibu eti hii kitu haiwezekani labda we mwenyewe umetuma. Siku ya tatu ikaja tena text kuwa muamala haujafanikiwa. Kumbe jamaa alikuwa kwenye system anataka kujitumia tena pesa. Kweli Tigo ndo wanaongoza kwa wizi Huu. Wanafanyakazi wao wengi hawapo loyal!
Hawa tigo wana baadhi ya mambo wanashindwa kuyafanyia marekebisho kwa Wateja hasa inapo tokea umekosea hela bahati mbaya
 
Halafu njia nyingine jamaa anakupigia. Halafu anakuwa very smart, hana haraka. Anakupigia anakwambia yeye ni wakala wako mkuu. Kuna pesa wamekutumia hebu angalia salio. Kwanza anakwambia umtajie namba yako nyingine akupigie huko ili simu yenye line ya wakala iwe free. Ukishamtajia namba Zako anakupigia huko then anakwambia kuna salio limetumwa kwako na kukutaka ucheck salio. Ukichek unakuta salio ni lile lile lako. Then anakwambia bado halijaingia. Ndo anaanza kukupa process za kufuata ili salio jipya liingie. Hapo anakutajia namba kibao hata huwez gundua kwa haraka kuwa ni namba zake. Ukibugi tu unajikuta umehamisha salio lako lote kwake na inakuwa ishakula upande wako. Walishanipigia Mara mbili ila zote nilipangua. Mara ya kwanza nilishtukia mchezo hatua za mwisho nkakata simu. Second time wakapiga tena nkawatukana tu wakakata simu yao
 
Halafu njia nyingine jamaa anakupigia. Halafu anakuwa very smart, hana haraka. Anakupigia anakwambia yeye ni wakala wako mkuu. Kuna pesa wamekutumia hebu angalia salio. Kwanza anakwambia umtajie namba yako nyingine akupigie huko ili simu yenye line ya wakala iwe free. Ukishamtajia namba Zako anakupigia huko then anakwambia kuna salio limetumwa kwako na kukutaka ucheck salio. Ukichek unakuta salio ni lile lile lako. Then anakwambia bado halijaingia. Ndo anaanza kukupa process za kufuata ili salio jipya liingie. Hapo anakutajia namba kibao hata huwez gundua kwa haraka kuwa ni namba zake. Ukibugi tu unajikuta umehamisha salio lako lote kwake na inakuwa ishakula upande wako. Walishanipigia Mara mbili ila zote nilipangua. Mara ya kwanza nilishtukia mchezo hatua za mwisho nkakata simu. Second time wakapiga tena nkawatukana tu wakakata simu yao
Duuuh mzee hongera unaonekana uko makini kwelikweli aisee
 
Nilitumia sim banking kuweka hela kwny akaunti yangu ya tigopesa ilikuwa usiku kama saa 4 hela nilikuwa nataka nilipie vifaa asbh.


Hela ikaingia msg haikuja lkn nilivyocheki salio kwny tigopesa ilionyesha ipo...asubuhi nmeamka niende kwa wakala nitoe hamna hata senti kupiga simu tigo naambiwa sijui nmetuma hela kwa Mtu anaitwa bakari maulid na namba haipatikani.

Kwenda polisi nikaandikiwa maelezo halaf file liende kwa mtu anayedili na mambo ya mtandao sijui nn.

Nikaona isiwe tabu nimwachie Mungu tu.
baba angu naye kaibiwa hvyo kama ww laki 2 kwenye voda....alitumiwa hela kwenda kutoa akaambiwa hela ulimtumia mtu flan flan siku flan na mdaa..kupiga simu voda ndo akaelekezwa hvyo akasema ye hajafanya transaction yoyote tokea apate hyo pesa
Wakamwambia aripoti police

aliona ata akienda police haisaidi chochote utapewa tu rb ukae nayo tu bure..mwisho wa siku alikumbuka alimpa wale wanaosajili line simu yake. Tukajua ndo hao hao wamemwibia

So na ww pesa yako haiwezi potea hiv hiv kama hujafanya muamala huenda simu yako alishika mtu hawa matapel wakipata tu mwanya wa kushika simu yako umeliwa
 
Halafu njia nyingine jamaa anakupigia. Halafu anakuwa very smart, hana haraka. Anakupigia anakwambia yeye ni wakala wako mkuu. Kuna pesa wamekutumia hebu angalia salio. Kwanza anakwambia umtajie namba yako nyingine akupigie huko ili simu yenye line ya wakala iwe free. Ukishamtajia namba Zako anakupigia huko then anakwambia kuna salio limetumwa kwako na kukutaka ucheck salio. Ukichek unakuta salio ni lile lile lako. Then anakwambia bado halijaingia. Ndo anaanza kukupa process za kufuata ili salio jipya liingie. Hapo anakutajia namba kibao hata huwez gundua kwa haraka kuwa ni namba zake. Ukibugi tu unajikuta umehamisha salio lako lote kwake na inakuwa ishakula upande wako. Walishanipigia Mara mbili ila zote nilipangua. Mara ya kwanza nilishtukia mchezo hatua za mwisho nkakata simu. Second time wakapiga tena nkawatukana tu wakakata simu yao
Hawa watu wapo smart sana usipokua makini unaliwa huyo wako wanafanana na hawa hawa wanaopiga umeshinda kiasi flan naona wameiboresha kihivyo baada ya kusanukiwa
 
baba angu naye kaibiwa hvyo kama ww laki 2 kwenye voda....alitumiwa hela kwenda kutoa akaambiwa hela ulimtumia mtu flan flan siku flan na mdaa..kupiga simu voda ndo akaelekezwa hvyo akasema ye hajafanya transaction yoyote tokea apate hyo pesa
Wakamwambia aripoti police

aliona ata akienda police haisaidi chochote utapewa tu rb ukae nayo tu bure..mwisho wa siku alikumbuka alimpa wale wanaosajili line simu yake. Tukajua ndo hao hao wamemwibia

So na ww pesa yako haiwezi potea hiv hiv kama hujafanya muamala huenda simu yako alishika mtu hawa matapel wakipata tu mwanya wa kushika simu yako umeliwa
Mimi tokea siku hiyo situmii tena simbanking na hela nikiweka kwny simu namtumia mtu hapohapo haikai hata dakika 2
 
Njia nyingine ni hii inayotumiwa sana na mawakala ambao sio waaminifu hasa kwa wateja wakiume:-

Unaenda kwa wakala kuweka pesa kwenye acount ya simu yako na wakala anaikariri namba yako ya simu kisha anampatia tapeli wa kike ambae anakutumia pesa kiasi flani na baada ya kutuma tu anakupigia simu kuwa katuma pesa kimakosa hivyo anaomba kwa unyenyekevu sana umrudishie! Kwa udhaifu wa wanaume wengi utarudisha pesa huku ukiwa tayari umeshaanza matamanio na same tyme anapiga simu mtandao husika ili kuiblock ile pesa ambayo alikutumia na hewani humpati tena!
 
Hivi kwa mfano ninarundika pesa zangu Kwene M-Pawa yani M-PESA inakuwa zero balance muda wote wanaweza niiibia hao watumishi wa voda wasio waaminifu????
 
baba angu naye kaibiwa hvyo kama ww laki 2 kwenye voda....alitumiwa hela kwenda kutoa akaambiwa hela ulimtumia mtu flan flan siku flan na mdaa..kupiga simu voda ndo akaelekezwa hvyo akasema ye hajafanya transaction yoyote tokea apate hyo pesa
Wakamwambia aripoti police

aliona ata akienda police haisaidi chochote utapewa tu rb ukae nayo tu bure..mwisho wa siku alikumbuka alimpa wale wanaosajili line simu yake. Tukajua ndo hao hao wamemwibia

So na ww pesa yako haiwezi potea hiv hiv kama hujafanya muamala huenda simu yako alishika mtu hawa matapel wakipata tu mwanya wa kushika simu yako umeliwa
Mmoja aliniambia et anaomba simu yangu anisajiri na kifurushi cha chuo, nikampa simu lakn baada ya hapo lain yangu ikafungiwa, nikaja kugundua alitaka kufanya muhamara kwa kutumia miaka iliyoko kwenye kitambulisho changu kama password.
 
Mmoja aliniambia et anaomba simu yangu anisajiri na kifurushi cha chuo, nikampa simu lakn baada ya hapo lain yangu ikafungiwa, nikaja kugundua alitaka kufanya muhamara kwa kutumia miaka iliyoko kwenye kitambulisho changu kama password.
Hahahaa aisee ndo hvyo usikubali kuwapa sim wana mbinu zao uyo anaonekana hakua mzoefu
Mana ata huyo mzee wangu aliambiwa hvyo hvyo wamuungie vifurushi vya chuo
 
Utapeli nilioupata jana,Walinipigia simu wakisema wametoka kitengo cha Bonus cha voda,nimeshinda Laki mbili na simu ya Techno,wakataka kujua mara ya mwisho niliweka shs ngap mpesa? Nikawaambia hivi naongea na nyie nna balance la mia tano,rusheni hiyo laki mbili basi nije voda shop kuchukua techno,mbona walikata simu.
 
Utapeli nilioupata jana,Walinipigia simu wakisema wametoka kitengo cha Bonus cha voda,nimeshinda Laki mbili na simu ya Techno,wakataka kujua mara ya mwisho niliweka shs ngap mpesa? Nikawaambia hivi naongea na nyie nna balance la mia tano,rusheni hiyo laki mbili basi nije voda shop kuchukua techno,mbona walikata simu.

uliwaweza kweli matapeli wakubwaaa
 
Back
Top Bottom