Mbinu za wapinzani kufanya siasa awamu hii

phillipinne

New Member
Jun 27, 2016
4
7
Siasa katika nchi za mfumo wa vyama vingi hutoa fursa kwa wanasiasa na wananchi kuwa na chama zaidi ya kimoja yani chama tawala na chama/vyama vya upinzani kama ilivyo katika nchi yetu.
Ni ukweli ulio wazi kufanya siasa za upinzani na kukuza upinzani katika nchi za kiafrika ikiwemo Tanzania sio jambo jepesi kutokana na ukakasi toka dola za serikali namna zinavyotumiwa na vyama tawala.
Hata hivyo navipongeza vyama vya upinzani hapa nchini kwa hatua vilivyofikia kwa sasa katika maendeleo Yao ya kisiasa, hata hivyo bado vyama hivi vinahitaji kukuwa zaidi na kuwa imara zaidi hatimae kuaminiwa kuongoza dola na mamlaka zote za nchi kwa mjibu wa katiba yetu.
Hivyo basi vyama hivi lazima viwe na mbinu madhubuti kuhakikisha ukuaji wao kama ifatavyo;


1. Kuwa na sera mama na itikadi zao,ni mda mwafaka sasa vyama vyetu kuweka wazi sera mama zao na kueleweka kwa wananchi kwani sera mama ndo huwa wakati mwingine hutofautisha chama kimoja na kingine. Mfano sera juu ya ulinzi wa nchi,sera za kimataifa na hata uchumi.
Pia itikadi ya chama hujengeka ndani ya nyoyo za wanachama wao hivyo kuwafanya kuwa kama waumini wa chama chama chao.

2. Kutengeneza uongozi wa chama kuwa na taswira ya kitaifa hii ni pamoja na kuwa na viongozi wenye kwendana na utamaduni na mtazamo wa nchi kiujumla. Uongozi wenye taswira ya familia au kabsa sio mda mwafaka katika kipindi hiki na kuendelea.

3.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom