CHASHA FARMING
JF-Expert Member
- Jun 4, 2011
- 7,789
- 8,914
mkuu@chasha kuku wangu aliatamia mayai 12 lakini cha kushangazaza alitotoa kifaranga 1 tu je ni makosa gani yaliyofanyika hapo? au ni kawaida kutokea ivyo?
Pole sana mkuu, Kuna sababu kama mbili tatu hivi.
1. Mayai kutokuwa na mbegu- Hapa majogoo ni machache sana au ni wengi kiasi kwamba wanafukuzana tu na hakuna wanacho kifanya.
2. Mayai yalipitiliza muda wake wa kutakiwa kuatamiwa- Mara nyingi siku 7 ndo the best baada ya siku saba hatch bility huanza kupungua sana.
3. Mayai hayakuhifadhiwa vizuri-Hapa kuna ishu ya mayai kushikwa na maji, Mafuta, au kuwekwa sehemu yenye joto kubwa na kazalika
-Hakikisha mayai yanahifadhiwa vizuri kwenye tray sehemu iliyo chongoka iwe chini.
4. Kuku wako ni mzembe- Kuna kuku kwa kweli huwa hawana sifa za kuatamia mayai vizuri, utakuta kila mara yuko nje