plan z
JF-Expert Member
- Jun 10, 2019
- 1,381
- 1,414
Hi Guys!
Moja kwa moja kwenye mada. Niwaombe moods wasiedit majina, nikiyapa yaanze na herufi ndogo ni herufi ndogo hivyo hivyo, herufi kubwa ni herufi kubwa hivyohivyo.
Haya tuendelee, nimeona kuna thread humu imeelezewa kwa kina kweli kumbe inapotosha raia. Hivyo na mimi nimeona nichukue jukumu la kuja kuwaokoa raia wanaopotea kama maandiko yanavyosema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa kuwa na maarifa."
Kuna member ameanzisha thread kuhusu "mungu wa freemasonry" akimnadi kuwa ni mungu mkuu kuliko Mungu aliyezifanya mbingu na nchi, na alijaribu kumbadilishia Mungu wetu jina na kumwita alivyoona yeye lakini Mungu wetu wala haitwi hivyo.
Hiyo thread iliwasha taa ya hatari kwenye ufahamu wangu nikijua fika hizo ni mbinu kadhaa za ulimwengu wa giza kupotosha ukweli kuhusu Mungu wetu wa mbinguni.
Basi moja kwa moja nizibainishe mbinu hizo kama ifuatavyo, na kabla sijaanza kubainisha nieleze tu kwaufupi ni kwamba miungu mingi ilianza kile kipindi cha Mwanzo sura ya 6 na kuendelea, na asilimia kubwa ya miungu hiyo ni nafsi mbalimbali za wanadamu waliowahi kuishi duniani wakaamua kujitukuza na kuabudiwa badala ya Mungu aliyezifanya mbingu na nchi na kuabudiwa. Kuna mungu mmoja pia alianzia kwenye hiyohiyo Mwanzo sita nafsi yake imejigawa huko na huko kila mahali ila na yeye ni nafsi iliyojitukuza vilevile na amebudiwa na umati mkubwa haswa.
Sitajibu maswali kwa sababu sitaki kushindanisha imani. Unachotakiwa kukifanya ni "take it or leave it"
MBINU ZINAZOTUMIWA.
1. WANAKUAMINISHA KWAMBA mungu WAO NDIYE mungu MKUU NA MUUMBAJI
Hii ni mbinu wanayoitumia na hapa wanaweka maneo mengi mazuri yatakayokuvutia uone kuna ukweli ndani yake kumbe siyo. Ulimwengu wa giza hawana jipya, utendaji kazi wao umeiga mbinu ambazo utendaji kazi wa Mungu wa kweli unatumia, hivyo mtu pasipo kufikiri anaweza akaona mbona kama kuna ukweli ndani yake kumbe ni uongo. Hata mitume na manabii wa uongo, wote ibada zao unaweza ukaona zinataka kufanana fanana vile na ukweli, ila wanatambulikana kwa matunda yao kama vile ambavyo imeandikwa "Mtawatambua kwa matunda yao", wengi ni waganga wa kienyeji wanatumia mizimu yao kuwatabiria watu kama ilivyotokea kipindi kile cha Mfalme Sauli alivyoona yamemshinda akaenda kwa mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, ndicho wanachokifanya hawa wa sasa, na wana miungu yao ila unaweza ukadhani ni ukweli kumbe uongo.
2. WANA yesu WAO WA UONGO NA KWA miungu MINGINE MARA NYINGI HUYO yesu WAO WA UONGO UTAKUTA YUKO MSALABANI ANATIA HURUMA KWELI, LAKINI KUMBE NI JANJA YAO.
Kama tunavyojua takribani zaidi ya miaka elfu mbili hivi iliyopita alikuja mtu aliyetikisa ulimwengu hasa ulimwengu wa giza, yaani YESU KRISTO. Matendo yake aliyotenda akiwa duniani yaliacha alama na hayasahauliki, kwani hadi leo umati mkubwa wa wanadamu huenda nchi ya Israeli kushuhudia kwa vitendo matendo yaliyotendwa na mwamba huyu aitwaye KRISTO YESU.
Sasa ulimwengu wa giza ukapiga hesabu tunafanyaje, maana matendo yake yalikuwa dhahiri. Wakaja na mbinu kwamba kila miungu wamtengeneze yesu wao wa uongo ili wanapoteka nafsi za wanadamu zikifikishwa huko zione aah kumbe tuko sehemu salama kumbe siyo, hii pia ni tatizo kutokana na watu wengi kutokuwa na kina katika imani na neno, nafsi inadanganyika kirahisi sana.
3. WANA MBINGU ZAO NA JEHANUM ZAO ZA UONGO.
Hii mbinu wamefanikiwa kidogo sana kuwaaminisha watu kwamba hakuna Jehanum, wengine wakidai hakuna mbingu.
Wanapotosha kwamba mahali panapoitwa toharani, eti kwamba mtu akifa na dhambi anaenda toharani kwa muda anateseka kulingana na dhambi zake kisha anaenda mbinguni. Huu ni uongo, na mbinu hii imefanya wanadamu wajisahau sana na kuishi maisha ya dhambi kisa eti kuna toharani halafu mbinguni.
Pia wengine wanajehanum zao wanaaminisha nafsi za wanadamu wasipotenda hizo kazi zao za giza kwa bidii wataingia huko, kuna wengine wanasema wamepelekwa mbinguni na jehanum ndo hao sasa wamedanganywa na wanakuja kudanganya watu.
Mbingu ipo na Jehanum ipo kwa siku za mwisho hakuna toharani. Wengine wanasema Mungu ni wa huruma eti hataweza kuwaangamisha umati mkubwa wa wanadamu Jehanum na kuhalalisha matendo ya dhambi, pasipo kujua kwamba Mungu akisema amesema, na Neno lake litatimia.
4. MAFUNDISHO YA KISHETANI.
Nyakati hizi ni nyakati za mwisho za hatari, watu wamejitenga na imani na kausikiliza mafundisho ya kishetani.
Mafundisho haya huwafanya watu wasiamini ukweli kuhusu Mungu wa kweli badala yake huwafanya waamini mafundisho ya uongo zaidi.
5. UJIO WA VIUMBE WA AJABU
Kuna viumbe wa ajabu hutokea na kuteka nafsi za wale watu waliokwenda kuwashangaa. Watu wakawaona kama viumbe wenye akili zaidi na wengine wakafikiri ndiyo miungu ya kweli kumbe siyo.
Nikipata nafasi ntakuja kuongeza mbinu zingine wanazozitumia.
Moja kwa moja kwenye mada. Niwaombe moods wasiedit majina, nikiyapa yaanze na herufi ndogo ni herufi ndogo hivyo hivyo, herufi kubwa ni herufi kubwa hivyohivyo.
Haya tuendelee, nimeona kuna thread humu imeelezewa kwa kina kweli kumbe inapotosha raia. Hivyo na mimi nimeona nichukue jukumu la kuja kuwaokoa raia wanaopotea kama maandiko yanavyosema "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa kuwa na maarifa."
Kuna member ameanzisha thread kuhusu "mungu wa freemasonry" akimnadi kuwa ni mungu mkuu kuliko Mungu aliyezifanya mbingu na nchi, na alijaribu kumbadilishia Mungu wetu jina na kumwita alivyoona yeye lakini Mungu wetu wala haitwi hivyo.
Hiyo thread iliwasha taa ya hatari kwenye ufahamu wangu nikijua fika hizo ni mbinu kadhaa za ulimwengu wa giza kupotosha ukweli kuhusu Mungu wetu wa mbinguni.
Basi moja kwa moja nizibainishe mbinu hizo kama ifuatavyo, na kabla sijaanza kubainisha nieleze tu kwaufupi ni kwamba miungu mingi ilianza kile kipindi cha Mwanzo sura ya 6 na kuendelea, na asilimia kubwa ya miungu hiyo ni nafsi mbalimbali za wanadamu waliowahi kuishi duniani wakaamua kujitukuza na kuabudiwa badala ya Mungu aliyezifanya mbingu na nchi na kuabudiwa. Kuna mungu mmoja pia alianzia kwenye hiyohiyo Mwanzo sita nafsi yake imejigawa huko na huko kila mahali ila na yeye ni nafsi iliyojitukuza vilevile na amebudiwa na umati mkubwa haswa.
Sitajibu maswali kwa sababu sitaki kushindanisha imani. Unachotakiwa kukifanya ni "take it or leave it"
MBINU ZINAZOTUMIWA.
1. WANAKUAMINISHA KWAMBA mungu WAO NDIYE mungu MKUU NA MUUMBAJI
Hii ni mbinu wanayoitumia na hapa wanaweka maneo mengi mazuri yatakayokuvutia uone kuna ukweli ndani yake kumbe siyo. Ulimwengu wa giza hawana jipya, utendaji kazi wao umeiga mbinu ambazo utendaji kazi wa Mungu wa kweli unatumia, hivyo mtu pasipo kufikiri anaweza akaona mbona kama kuna ukweli ndani yake kumbe ni uongo. Hata mitume na manabii wa uongo, wote ibada zao unaweza ukaona zinataka kufanana fanana vile na ukweli, ila wanatambulikana kwa matunda yao kama vile ambavyo imeandikwa "Mtawatambua kwa matunda yao", wengi ni waganga wa kienyeji wanatumia mizimu yao kuwatabiria watu kama ilivyotokea kipindi kile cha Mfalme Sauli alivyoona yamemshinda akaenda kwa mwanamke mwenye pepo wa utambuzi, ndicho wanachokifanya hawa wa sasa, na wana miungu yao ila unaweza ukadhani ni ukweli kumbe uongo.
2. WANA yesu WAO WA UONGO NA KWA miungu MINGINE MARA NYINGI HUYO yesu WAO WA UONGO UTAKUTA YUKO MSALABANI ANATIA HURUMA KWELI, LAKINI KUMBE NI JANJA YAO.
Kama tunavyojua takribani zaidi ya miaka elfu mbili hivi iliyopita alikuja mtu aliyetikisa ulimwengu hasa ulimwengu wa giza, yaani YESU KRISTO. Matendo yake aliyotenda akiwa duniani yaliacha alama na hayasahauliki, kwani hadi leo umati mkubwa wa wanadamu huenda nchi ya Israeli kushuhudia kwa vitendo matendo yaliyotendwa na mwamba huyu aitwaye KRISTO YESU.
Sasa ulimwengu wa giza ukapiga hesabu tunafanyaje, maana matendo yake yalikuwa dhahiri. Wakaja na mbinu kwamba kila miungu wamtengeneze yesu wao wa uongo ili wanapoteka nafsi za wanadamu zikifikishwa huko zione aah kumbe tuko sehemu salama kumbe siyo, hii pia ni tatizo kutokana na watu wengi kutokuwa na kina katika imani na neno, nafsi inadanganyika kirahisi sana.
3. WANA MBINGU ZAO NA JEHANUM ZAO ZA UONGO.
Hii mbinu wamefanikiwa kidogo sana kuwaaminisha watu kwamba hakuna Jehanum, wengine wakidai hakuna mbingu.
Wanapotosha kwamba mahali panapoitwa toharani, eti kwamba mtu akifa na dhambi anaenda toharani kwa muda anateseka kulingana na dhambi zake kisha anaenda mbinguni. Huu ni uongo, na mbinu hii imefanya wanadamu wajisahau sana na kuishi maisha ya dhambi kisa eti kuna toharani halafu mbinguni.
Pia wengine wanajehanum zao wanaaminisha nafsi za wanadamu wasipotenda hizo kazi zao za giza kwa bidii wataingia huko, kuna wengine wanasema wamepelekwa mbinguni na jehanum ndo hao sasa wamedanganywa na wanakuja kudanganya watu.
Mbingu ipo na Jehanum ipo kwa siku za mwisho hakuna toharani. Wengine wanasema Mungu ni wa huruma eti hataweza kuwaangamisha umati mkubwa wa wanadamu Jehanum na kuhalalisha matendo ya dhambi, pasipo kujua kwamba Mungu akisema amesema, na Neno lake litatimia.
4. MAFUNDISHO YA KISHETANI.
Nyakati hizi ni nyakati za mwisho za hatari, watu wamejitenga na imani na kausikiliza mafundisho ya kishetani.
Mafundisho haya huwafanya watu wasiamini ukweli kuhusu Mungu wa kweli badala yake huwafanya waamini mafundisho ya uongo zaidi.
5. UJIO WA VIUMBE WA AJABU
Kuna viumbe wa ajabu hutokea na kuteka nafsi za wale watu waliokwenda kuwashangaa. Watu wakawaona kama viumbe wenye akili zaidi na wengine wakafikiri ndiyo miungu ya kweli kumbe siyo.
Nikipata nafasi ntakuja kuongeza mbinu zingine wanazozitumia.