sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,014
TUELEWANE MAPEMA, MAMBO MUHIMU.
1.Mtoto wangu hachezi na watoto wa kihuni mitaan na akienda kijijini ni nje kidogo ya mji na ndiko nlipokulia, watoto anaocheza nao wengi walezi wao nawajua tunafahamiana, pia hakuna watoto wa mitaani huko kama mjini.
2. sifurahi kwamba mwanangu ni mjanja au very social tangu nianze utaratibu huu wa malezi, bali nafurahi kwa sababu anakua katika hali ya tabia njema huku akiwa na moyo wa kujifunza.
3. Kuna wengi wamekuja na mawazo yao kwamba nimsomeshe mtoto shule za milioni 40 ili ajifunze mengi zaidi, Nashukuru kwa mawazo yenu huo uwezo sina, nawatakia kila la kheri mje muwapeleke watoto wenu hizo shule
TURUDI KWENYE MAADA
Nilistuka mapema sana juu ya madhara ya kusomesha watoto hizi private, unakuta mtoto anatoka saa 11 jioni, akitoka hapo ni tuition, akitoka hapo ni homework na wengi hawatoki nje ni geti kali ni ndani tu hii inahirbu sana maisha ya mtoto.
Pia Malezi ya siku hizi pia yamechangia mno kuwafanya watoto wawe wamezubaa maana watoto wengi wanafugwa kama kuku ndani ya mageti (geti kali) huku wazazi wengi wakijidanganya kwamba wanapata furaha kamili kwa katuni na kunanunulia games.
Nakumbuka zamani tukitoka shule tulikua hatukai ndani kucheza games au kuangalia katuni, Tulikua na vikundi vya watoto mitaani tunacheza mpira, kuogelea na hata kujifunza kuto onewa hovyo hovyo, dada zetu walicheza rede, kupika, n.k
Hii michezo na maisha haya yalifanya tujue kuishi na jamii tofauti na siku hizi unakuta mtoto ana maarifa ya kucheza games, katuni na kukariri tu vya darasani. ukimpeleka huyu mtoto nje kuna uwezekano mkubwa wa yeye kuonewa na hata kuwa mpweke asiwe na marafiki maana hana elimu ya watu
Binafsi mtoto wangu wa kiume namsomesha english medium hizi, mara ya kwanza shule niliyompeleka walikua darasani 18 tu na wanatoka saa 11, kwa huu uchache nakumbuka alikuwa ana rafiki moja tu na muda mwingi ulikuwa ni kusoma hadi saa 11, wakitoka huja na school bus
nikaona huu upuuzi sasa, shule ndio ni muhimu ila sio kila kitu kwa mtoto wangu kuna maisha mengi mno anayopaswa kujifunza, Nikamwamishia shule ambayo wapo 48 darasani na wanatoka saa saba na nusu ila tu darasa la saba tu ndio wanatoka saa tisa. Yeye yupo darasa la tatu shuleni huwa yumo kumi bora na hii inatosha kwangu siamini sana mambo ya kuwa wa kwanza bali naamini matokeo yanayoridhisha
akitoka shuleni anakula, anafua nguo zake, Zamani hii kazi haikumhusu, nilimpiga geti kali
Nikaanzisha utaratibu kukiacha kidume huru nampeleka nje kidogo ya mjini kwa bibi yake ambako huhumuika na wenzake, mara nyingi huendA kuogelea nae, kuwinda nae, n.k Pia kajufunza kuchinja kuku na kusonga ugali wake.
Siku hizi kawa muongeaji mno nlivyomwanzishia huu utaratibu, Kawa mjanja, Shuleni kwao kageuka kuwa aina ile ya mwanafunzi darasani ambae kila mwanafunzi anataka kuwa rafiki yake na nadhani hii ni kwasababu huwa anawapa stori ama kuwafundisha wenzake vitu alivyofundishwa au alivyofanya huko kwa bibi yake,
Shule aliyopo ni yeye peke yake anaweza kuruka zile sarakasi za nyuma basi wenzake wanamkubali sana,
Nimeitwa shuleni kwa kesi za utundu utundu huu wa wavulana kama kupiga kelele na kutania wasichana, Binafsi ndivyo navyotaka awe mchangamfu na nikiri tu nilifurahi hizi kesi japo nilimkanya kwa shingo upande , Sitaki mtoto azubae zubae
Sijamlipia school bus kwa maksudi kabisa japo nina uwezo, nilishangaa aliponiambia wenzake pia shuleni wanapenda sana wawe wanatembea kama yeye pamoja na wenzake wawili ambao hawajalipiwa school bus
Michezo ambayo kuku wa kisasa wanaofungiwa ndani ambayo hawataijua
-Kutengeneza manati , kuwinda ndege porini , kombolela, Kidali poo, ufinyanzi n.k (michezo ya kitamaduni kwa mvulana wa kiafrika)
-Kujifunza kukabiliana na hatari, kuna kesi nliitwa shuleni yeye na rafiki yake walimchangia mwenzao muonezi wa darasa la juu, nisingefurahi kama ningeitwa anaonewa kupigwa
-kujifunza kugawana / kukarivisha - ukija na chakula ni vyema kujua pia marafiki zako wananjaa kuna watoto hawahuagi kukaribisha
-Kupuliza kimhwepelo
-kukimbiza kuku
-mpira wa chandimu
Elimu ya darasani ni muhimu sikatai, binafsi ndio imenipa ajira, lakini vijana wengi wapo mtaani wanalalamika wamesoma na hawana ajira na hakuna cha zaidi wanachoweza, hapa ndipo elimu za ziada zinapokuwa muhimu
Malezi sio kumfungia mtoto na kumbana sana ukiamini ndio njia ya kumlinda , LA HASHA!!
1.Mtoto wangu hachezi na watoto wa kihuni mitaan na akienda kijijini ni nje kidogo ya mji na ndiko nlipokulia, watoto anaocheza nao wengi walezi wao nawajua tunafahamiana, pia hakuna watoto wa mitaani huko kama mjini.
2. sifurahi kwamba mwanangu ni mjanja au very social tangu nianze utaratibu huu wa malezi, bali nafurahi kwa sababu anakua katika hali ya tabia njema huku akiwa na moyo wa kujifunza.
3. Kuna wengi wamekuja na mawazo yao kwamba nimsomeshe mtoto shule za milioni 40 ili ajifunze mengi zaidi, Nashukuru kwa mawazo yenu huo uwezo sina, nawatakia kila la kheri mje muwapeleke watoto wenu hizo shule
TURUDI KWENYE MAADA
Nilistuka mapema sana juu ya madhara ya kusomesha watoto hizi private, unakuta mtoto anatoka saa 11 jioni, akitoka hapo ni tuition, akitoka hapo ni homework na wengi hawatoki nje ni geti kali ni ndani tu hii inahirbu sana maisha ya mtoto.
Pia Malezi ya siku hizi pia yamechangia mno kuwafanya watoto wawe wamezubaa maana watoto wengi wanafugwa kama kuku ndani ya mageti (geti kali) huku wazazi wengi wakijidanganya kwamba wanapata furaha kamili kwa katuni na kunanunulia games.
Nakumbuka zamani tukitoka shule tulikua hatukai ndani kucheza games au kuangalia katuni, Tulikua na vikundi vya watoto mitaani tunacheza mpira, kuogelea na hata kujifunza kuto onewa hovyo hovyo, dada zetu walicheza rede, kupika, n.k
Hii michezo na maisha haya yalifanya tujue kuishi na jamii tofauti na siku hizi unakuta mtoto ana maarifa ya kucheza games, katuni na kukariri tu vya darasani. ukimpeleka huyu mtoto nje kuna uwezekano mkubwa wa yeye kuonewa na hata kuwa mpweke asiwe na marafiki maana hana elimu ya watu
Binafsi mtoto wangu wa kiume namsomesha english medium hizi, mara ya kwanza shule niliyompeleka walikua darasani 18 tu na wanatoka saa 11, kwa huu uchache nakumbuka alikuwa ana rafiki moja tu na muda mwingi ulikuwa ni kusoma hadi saa 11, wakitoka huja na school bus
nikaona huu upuuzi sasa, shule ndio ni muhimu ila sio kila kitu kwa mtoto wangu kuna maisha mengi mno anayopaswa kujifunza, Nikamwamishia shule ambayo wapo 48 darasani na wanatoka saa saba na nusu ila tu darasa la saba tu ndio wanatoka saa tisa. Yeye yupo darasa la tatu shuleni huwa yumo kumi bora na hii inatosha kwangu siamini sana mambo ya kuwa wa kwanza bali naamini matokeo yanayoridhisha
akitoka shuleni anakula, anafua nguo zake, Zamani hii kazi haikumhusu, nilimpiga geti kali
Nikaanzisha utaratibu kukiacha kidume huru nampeleka nje kidogo ya mjini kwa bibi yake ambako huhumuika na wenzake, mara nyingi huendA kuogelea nae, kuwinda nae, n.k Pia kajufunza kuchinja kuku na kusonga ugali wake.
Siku hizi kawa muongeaji mno nlivyomwanzishia huu utaratibu, Kawa mjanja, Shuleni kwao kageuka kuwa aina ile ya mwanafunzi darasani ambae kila mwanafunzi anataka kuwa rafiki yake na nadhani hii ni kwasababu huwa anawapa stori ama kuwafundisha wenzake vitu alivyofundishwa au alivyofanya huko kwa bibi yake,
Shule aliyopo ni yeye peke yake anaweza kuruka zile sarakasi za nyuma basi wenzake wanamkubali sana,
Nimeitwa shuleni kwa kesi za utundu utundu huu wa wavulana kama kupiga kelele na kutania wasichana, Binafsi ndivyo navyotaka awe mchangamfu na nikiri tu nilifurahi hizi kesi japo nilimkanya kwa shingo upande , Sitaki mtoto azubae zubae
Sijamlipia school bus kwa maksudi kabisa japo nina uwezo, nilishangaa aliponiambia wenzake pia shuleni wanapenda sana wawe wanatembea kama yeye pamoja na wenzake wawili ambao hawajalipiwa school bus
Michezo ambayo kuku wa kisasa wanaofungiwa ndani ambayo hawataijua
-Kutengeneza manati , kuwinda ndege porini , kombolela, Kidali poo, ufinyanzi n.k (michezo ya kitamaduni kwa mvulana wa kiafrika)
-Kujifunza kukabiliana na hatari, kuna kesi nliitwa shuleni yeye na rafiki yake walimchangia mwenzao muonezi wa darasa la juu, nisingefurahi kama ningeitwa anaonewa kupigwa
-kujifunza kugawana / kukarivisha - ukija na chakula ni vyema kujua pia marafiki zako wananjaa kuna watoto hawahuagi kukaribisha
-Kupuliza kimhwepelo
-kukimbiza kuku
-mpira wa chandimu
Elimu ya darasani ni muhimu sikatai, binafsi ndio imenipa ajira, lakini vijana wengi wapo mtaani wanalalamika wamesoma na hawana ajira na hakuna cha zaidi wanachoweza, hapa ndipo elimu za ziada zinapokuwa muhimu
Malezi sio kumfungia mtoto na kumbana sana ukiamini ndio njia ya kumlinda , LA HASHA!!