Mbinu nayotumia kumlea mwanangu anayesoma private awe mjanja, awe na furaha, asigeuke kuwa kuku wa kisasa

sky soldier

JF-Expert Member
Mar 30, 2020
5,408
19,014
TUELEWANE MAPEMA, MAMBO MUHIMU.

1.Mtoto wangu hachezi na watoto wa kihuni mitaan na akienda kijijini ni nje kidogo ya mji na ndiko nlipokulia, watoto anaocheza nao wengi walezi wao nawajua tunafahamiana, pia hakuna watoto wa mitaani huko kama mjini.

2. sifurahi kwamba mwanangu ni mjanja au very social tangu nianze utaratibu huu wa malezi, bali nafurahi kwa sababu anakua katika hali ya tabia njema huku akiwa na moyo wa kujifunza.

3. Kuna wengi wamekuja na mawazo yao kwamba nimsomeshe mtoto shule za milioni 40 ili ajifunze mengi zaidi, Nashukuru kwa mawazo yenu huo uwezo sina, nawatakia kila la kheri mje muwapeleke watoto wenu hizo shule


TURUDI KWENYE MAADA

Nilistuka mapema sana juu ya madhara ya kusomesha watoto hizi private, unakuta mtoto anatoka saa 11 jioni, akitoka hapo ni tuition, akitoka hapo ni homework na wengi hawatoki nje ni geti kali ni ndani tu hii inahirbu sana maisha ya mtoto.

Pia Malezi ya siku hizi pia yamechangia mno kuwafanya watoto wawe wamezubaa maana watoto wengi wanafugwa kama kuku ndani ya mageti (geti kali) huku wazazi wengi wakijidanganya kwamba wanapata furaha kamili kwa katuni na kunanunulia games.

Nakumbuka zamani tukitoka shule tulikua hatukai ndani kucheza games au kuangalia katuni, Tulikua na vikundi vya watoto mitaani tunacheza mpira, kuogelea na hata kujifunza kuto onewa hovyo hovyo, dada zetu walicheza rede, kupika, n.k

Hii michezo na maisha haya yalifanya tujue kuishi na jamii tofauti na siku hizi unakuta mtoto ana maarifa ya kucheza games, katuni na kukariri tu vya darasani. ukimpeleka huyu mtoto nje kuna uwezekano mkubwa wa yeye kuonewa na hata kuwa mpweke asiwe na marafiki maana hana elimu ya watu

Binafsi mtoto wangu wa kiume namsomesha english medium hizi, mara ya kwanza shule niliyompeleka walikua darasani 18 tu na wanatoka saa 11, kwa huu uchache nakumbuka alikuwa ana rafiki moja tu na muda mwingi ulikuwa ni kusoma hadi saa 11, wakitoka huja na school bus

nikaona huu upuuzi sasa, shule ndio ni muhimu ila sio kila kitu kwa mtoto wangu kuna maisha mengi mno anayopaswa kujifunza, Nikamwamishia shule ambayo wapo 48 darasani na wanatoka saa saba na nusu ila tu darasa la saba tu ndio wanatoka saa tisa. Yeye yupo darasa la tatu shuleni huwa yumo kumi bora na hii inatosha kwangu siamini sana mambo ya kuwa wa kwanza bali naamini matokeo yanayoridhisha

akitoka shuleni anakula, anafua nguo zake, Zamani hii kazi haikumhusu, nilimpiga geti kali

Nikaanzisha utaratibu kukiacha kidume huru nampeleka nje kidogo ya mjini kwa bibi yake ambako huhumuika na wenzake, mara nyingi huendA kuogelea nae, kuwinda nae, n.k Pia kajufunza kuchinja kuku na kusonga ugali wake.

Siku hizi kawa muongeaji mno nlivyomwanzishia huu utaratibu, Kawa mjanja, Shuleni kwao kageuka kuwa aina ile ya mwanafunzi darasani ambae kila mwanafunzi anataka kuwa rafiki yake na nadhani hii ni kwasababu huwa anawapa stori ama kuwafundisha wenzake vitu alivyofundishwa au alivyofanya huko kwa bibi yake,

Shule aliyopo ni yeye peke yake anaweza kuruka zile sarakasi za nyuma basi wenzake wanamkubali sana,

Nimeitwa shuleni kwa kesi za utundu utundu huu wa wavulana kama kupiga kelele na kutania wasichana, Binafsi ndivyo navyotaka awe mchangamfu na nikiri tu nilifurahi hizi kesi japo nilimkanya kwa shingo upande , Sitaki mtoto azubae zubae

Sijamlipia school bus kwa maksudi kabisa japo nina uwezo, nilishangaa aliponiambia wenzake pia shuleni wanapenda sana wawe wanatembea kama yeye pamoja na wenzake wawili ambao hawajalipiwa school bus :):)

Michezo ambayo kuku wa kisasa wanaofungiwa ndani ambayo hawataijua

-Kutengeneza manati , kuwinda ndege porini , kombolela, Kidali poo, ufinyanzi n.k (michezo ya kitamaduni kwa mvulana wa kiafrika)

-Kujifunza kukabiliana na hatari, kuna kesi nliitwa shuleni yeye na rafiki yake walimchangia mwenzao muonezi wa darasa la juu, nisingefurahi kama ningeitwa anaonewa kupigwa

-kujifunza kugawana / kukarivisha - ukija na chakula ni vyema kujua pia marafiki zako wananjaa kuna watoto hawahuagi kukaribisha

-Kupuliza kimhwepelo

-kukimbiza kuku

-mpira wa chandimu

Elimu ya darasani ni muhimu sikatai, binafsi ndio imenipa ajira, lakini vijana wengi wapo mtaani wanalalamika wamesoma na hawana ajira na hakuna cha zaidi wanachoweza, hapa ndipo elimu za ziada zinapokuwa muhimu

Malezi sio kumfungia mtoto na kumbana sana ukiamini ndio njia ya kumlinda , LA HASHA!!
 
Mkuu hayo ndo maisha.

Mfundishe kuheshimu watu wakubwa na wadogo asiwe na matusi.

Mfundishe kujitambua na kuwa muwazi kwako.

Mfundishe kuwa ipo siku hamtakuwa wote.

Mfuindishe kuwa yeyr kama yeye yupo hapa ili aje kuwa mtu wa pekee hivyo anatakiwa achague ana ndoto gani tokea hapo alipo.

Mfundishe kuwa maisha yanaanza anapojitambua na sio anapoajiriwa.

Mtengenezee mindset nzuri tokea utoto atakuja kuwa bonge la genius.

Hakikisha unafanya jae mijadala na kubishana nae kwa hoja ili awe na uwezo mkubwa wa kufikiri.

Mimi nafanya hayo kwa mdogo wangu sasahivi yuko kidato cha pili yuko vizuri anajuia anafanya nini ana time management nzuri,ana commitment nzuri huwezi amini kama ni kijana ambae anapitia kubaleghe.

Nilishamuambiaga kuwa dogo unapitia wakati wa kubaleghe,wakati mgumu sana kwenu nyie watoto ila tambua wakati huu ni wakati wa kujifunza subra na uvumilivu na kujishusha kwa sababu ni wakati ambao uinajiona wewe ndo wewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera ..
Lakini umesahau vitu vya msingi..
Aina ya shule..
Zipo shule zina jali Sana extra caricularr na social skills...
Pili umesahau kumpa mtoto vitabu vya ziada vingi vyenye story za kila aina..

Tatu kuwa makini na bibi ..
Wanaharibu saana watoto
 
Hongera ..
Lakini umesahau vitu vya msingi..
Aina ya shule..
Zipo shule zina jali Sana extra caricularr na social skills...
Pili umesahau kumpa mtoto vitabu vya ziada vingi vyenye story za kila aina..

Tatu kuwa makini na bibi ..
Wanaharibu saana watoto


Pole kwa tukio...
 
Hongera ..
Lakini umesahau vitu vya msingi..
Aina ya shule..
Zipo shule zina jali Sana extra caricularr na social skills...
Pili umesahau kumpa mtoto vitabu vya ziada vingi vyenye story za kila aina..

Tatu kuwa makini na bibi ..
Wanaharibu saana watoto
Mkuu naamini haya mambo ya social skills inabidi yawe kwa vitendo zaidi na ukiangalia kwa karibu sana watu wengi ambao hata wameishia darasa la nne wana social skills kubwa sana kwa sababu muda mwingi wanachangamana na jamii

Mtoto hata kama anafundishwa social skills kama yupo geti,akitoka shuleni anacheza games, hapo hamna kitu.

Mkuu huko ka bibi yake nakompeleka kuna stories mpaka basi, Nimeweka wazi kabisa huko shuleni anakosoma kama muongeaji sana kwasababu ana kabati la stories humo kichwani tofauti na wenzake wengi ambao kichwani kuna games na katuni tu.

Huyu bibi sidhani kuna tatizo, Kuna siku chalii alikuwa anadokoa jikoni naona bibi alimuongezea elimu ya vitengo kwa kumtia viboko vya mpera :) :)
 
......kulima, kuogelea mtoni, kuwinda, n.k anaenda huko kwa sababu hapa mjini watoto wengi ni mageti kali wapo ndani.
Unamuandaa mtoto kuwa Mpori pori!
Ni kumfanya aishi kwa furaha na kujifunza mengine ya ziada kuliko kufungiwa nyumbani maana nipo mjini mtaa ambao watoto wengi ni mageti kali,

Matokeo chanya aiyoonyesha saizi ni mchangamfu na kageuka kuwa mwanafunzi ambae wenzake wengi wanapenda kampani yake kwa sababu anajua vingi vya ziada nje wa 1+1x3-1 wanayofundishwa shuleni.

Shuleni namba zake ni 7 hadi 12 kari wa wanafunzi 48 na wastani wake huwa si chini ya 65, Sijawahi kuamini wala kumkaripia awe wa kwanza, Nimeidhika na haya matokeo
 
Hayo masiha ya geti kali skul bus and the like matokeo yake baada ya mda mtu anakuja anaanza kusema jamani nahisi mimi ni anti social siwezi kabisa kujichanganya na watu

Kumbe hii tabia saa nyingine ni ya kujitengenezea wenyewe
wazazi wanaona kuwafungia watoto wao na kuwabanabana wanapatia kumbe kwa kiasi kikubwa wanakosea
 
Mwana
Nilistuka mapema sana juu ya madhara ya kusomesha watoto hizi private, unakuta mtoto anatoka saa 10 jioni, akitoka hapo ni tuition, akitoka hapo ni homework na wengi hawatoki nje ni geti kali ni ndani tu hii inahirbu sana maisha ya mtoto.

Pia Malezi ya siku hizi pia yamechangia mno kuwafanya watoto wawe mazube maana watoto ni kuwafuga kama kuku ndani ya mageti (geti kali) huku wazazi wengi wakijidanganya kwamba wanapata furaha kamili kwa katuni na kunanunulia games.

Nakumbuka zamani tukitoka shule tulikua hatukai ndani ucheza games au kuangalia katuni, Tulikua na vikundi vya watoto mitaani tunacheza mpira, kuogelea na hata kujifunza kuto onewa hovyo hovyo, dada zetu walicheza rede, kupika, n.k Hii michezo na maisha haya yalifanya tujue kuishi na jamii tofauti na siku hizi unakuta litoto linachojua na games, katuni na what is water. ukimpeleka huyu mtoto nje kuna uwezekano mkubwa wa yeye kuonewa na hata kuwa mpweke asiwe na marafiki maana hajui ku interact na watu (Hili tatizo ni kubwa ulaya).

Binafsi mtoto wangu wa kiume namsomesha english medium hizi, mara ya kwanza shule niliyompeleka walikua darasani 18 tu na wanatoka saa kumi, kwa huu uchache nakumbuka alikuwa ana rafiki moja tu na muda mwingi ulikuwa ni kusoma hadi saa kumi.

nikaona huu upuuzi sasa, shule ndio ni muhimu ila sio kila kitu kwa mtoto wangu kuna maisha mengi mno anayopaswa kujifunza, Nikamwamishia shule ambayo wapo 48 darasani na wanatoka saa saba na nusu ila tu darasa la saba tu ndio wanatoka saa tisa. Yeye yupo darasa la tatu shuleni huwa yumo kumi bora na hii inatosha kwangu siamini sana mambo ya kuwa wa kwanza.

akitoka shuleni anakula, anafua nguo zake, Zamani nilikuwa nimempiga geti kali ila baada ya hapo nikaanzisha utaratibu anapelekwa nje kidogo ya mjini kwa bibi yake ambako hucheza na wenzake, kulima, kuogelea mtoni, kuwinda, n.k anaenda huko kwa sababu hapa mjini watoto wengi ni mageti kali wapo ndani.

Siku hizi kawa muongeaji mno nlivyomwanzishia huu utaratibu, Kawa mjanja, Shuleni kwao kageuka kuwa aina ile ya mwanafuzni darasani ambae kila mwanafunzi anataka kuwa rafiki yake na nadhani hii ni kwasababu huwa anawapa stori ama kuwafundisha wenzake vitu alivyofundishwa au alivyofanya huko kwa bibi yake,

Shule aliyopo ni yeye peke yake anaweza kuruka zile sarakasi za nyuma basi wenzake wanamkubali sana,

Nimeiwa shuleni kwa kesi za utundu utundu huu wa wavulana kama kupiga kelele na kutania wenzake (kesi 1 mwenzake kesi 2 wasichana) Binafsi ndivyo navyotaka awe mchangamfu na nikiri tu nilifurahi hizi kesi japo nilimkjanya kwa shingo upande, Sitaki mtoto azubae zubae

Sijamlipia school bus kwa maksudi kabisa japo nina uwezo, nilishangaa aliponiambia wenzake pia shuleni wanapenda sana wawe wanatembea kama yeye pamoja na wenzake wawili ambao hawajalipiwa school bus :):)

Ni hayo tu, Nawaonea huruma wazazi ambao huipa shule kipaumbele mno na kuwafungia watoto wao nyumbani, Matokeo yake mtoto anakuwa hana social skills, anakua anaonewa kirahisi, hafanyi mazoezi hata ya kuimarisha miguu kwasababu ya school bus, anakuwa yupo yupo tu kichwani anajua games na katuni tu.
ngu nilimpeleka shule ya masister iitwayo St Scolastica iko jirani na KM Ukonga. Alisoma day na kufanya vizuri sana darasa la saba. Sasa hivi yuko kidato cha tatu Morogoro, lakini kila ajapo likizo nimekuwa nikimwekea mazingira ya kujifunza WEB DEVELOPMENT na sasa amemaliza HTML, CSS3 na Javascript. Anasoma framework ili awe front end developer kabla ya kuendelea na back end. Kwa vile amependa sana na anaelewa mno kiasi cha kuanza kutengeneza portfolio yake, namwandaa kuja kusoma python na C++ baadaye.

Kufuatia kufungwa shule, hivi karibuni ataanza kutafuta kazi za mtandaoni ili atumie skills zake kujipatia kipato na kujijengea ujasiri wa kupambana sokoni.
 
Mwana

ngu nilimpeleka shule ya masister iitwayo St Scolastica iko jirani na KM Ukonga. Alisoma day na kufanya vizuri sana darasa la saba. Sasa hivi yuko kidato cha tatu Morogoro, lakini kila ajapo likizo nimekuwa nikimwekea mazingira ya kujifunza WEB DEVELOPMENT na sasa amemaliza HTML, CSS3 na Javascript. Anasoma framework ili awe front end developer kabla ya kuendelea na back end. Kwa vile amependa sana na anaelewa mno kiasi cha kuanza kutengeneza portfolio yake, namwandaa kuja kusoma python na C++ baadaye.

Kufuatia kufungwa shule, hivi karibuni ataanza kutafuta kazi za mtandaoni ili atumie skills zake kujipatia kipato na kujijengea ujasiri wa kupambana sokoni.
Tunafanana kidogo, mi mwanangu yupo grade 3, akiwa likizo namfunza Javascript for kids ambayo baada ya muda ataanza ku develop cartoons na baadae web. Big up.
 
Mwana

ngu nilimpeleka shule ya masister iitwayo St Scolastica iko jirani na KM Ukonga. Alisoma day na kufanya vizuri sana darasa la saba. Sasa hivi yuko kidato cha tatu Morogoro, lakini kila ajapo likizo nimekuwa nikimwekea mazingira ya kujifunza WEB DEVELOPMENT na sasa amemaliza HTML, CSS3 na Javascript. Anasoma framework ili awe front end developer kabla ya kuendelea na back end. Kwa vile amependa sana na anaelewa mno kiasi cha kuanza kutengeneza portfolio yake, namwandaa kuja kusoma python na C++ baadaye.

Kufuatia kufungwa shule, hivi karibuni ataanza kutafuta kazi za mtandaoni ili atumie skills zake kujipatia kipato na kujijengea ujasiri wa kupambana sokoni.
Tunafanana kidogo, mi mwanangu yupo grade 3, akiwa likizo namfunza Javascript for kids ambayo baada ya muda ataanza ku develop cartoons na baadae web. Big up.
Ntaka nikupe taarifa tu, Hakuna watu ambao wapo very socially awkard kama watu wanao deal mno na computers, kuanzia hackers, software developers, n.k hawa watu asilimia kubwa mno wapo socialy awkard na ninakupa homework ufanye research,

Muwe mnawatoa toa nje watoto wenu wasishinde ndani Hayo mambo ya kujifunza lugha za computer hizo mlizozitaja ama kukesha sana na pc yanaanzaga kutenegeneza uraibu flani hivi wa kuwa na pc muda mwingi na kujitenga na jamii, Ndio maana maisha ya programmers, online workers, gamers, internet trolls, web developers wengi yanakuaga ni lonely sana na kuanza kusingizia anti social na intrivert kumbe ni maisha wanayoishi


Nawashauri watoto wenu wafanye shughuli za nje ya nyumba kuliko kukaa kaa ndani, Hayo mambo ya java script, html, n.k naona tuwaachie wenzetu wazungu ambao ni wapweke mno rafiki zao ni mbwa, Ila kama utamfundisha hakikisha ana muda wa ku participate kwenye mambo ya social.

Huyu wangu saizi kawa muongeaji na mcheshi sana na pia anaruka sarakasi na bora iwe hivi kuliko awe introverted geek
 
Ntaka nikupe taarifa tu, Hakuna watu ambao wapo very socially awkard kama watu wanao deal mno na computers, kuanzia hackers, software developers, n.k hawa watu asilimia kubwa mno wapo socialy awkard na ninakupa homework ufanye research,

Muwe mnawatoa toa nje watoto wenu wasishinde ndani Hayo mambo ya kujifunza lugha za computer hizo mlizozitaja ama kukesha sana na pc yanaanzaga kutenegeneza uraibu flani hivi wa kuwa na pc muda mwingi na kujitenga na jamii, Ndio maana maisha ya programmers, online workers, gamers, internet trolls, web developers wengi yanakuaga ni lonely sana na kuanza kusingizia anti social na intrivert kumbe ni maisha wanayoishi


Nawashauri watoto wenu wafanye shughuli za nje ya nyumba kuliko kukaa kaa ndani, Hayo mambo ya java script, html, n.k naona tuwaachie wenzetu wazungu ambao ni wapweke mno rafiki zao ni mbwa, Ila kama utamfundisha hakikisha ana muda wa ku participate kwenye mambo ya social.

Huyu wangu saizi kawa muongeaji na mcheshi sana na pia anaruka sarakasi na bora iwe hivi kuliko awe introverted geek
Upo sahihi,lkn mimi huwa namchanganya pia kitaani,mfano huwa naenda nae mazoezin asubuh uwanjan ambapo ni mchangani na akifika hapo anacheza mpira na watoto wa shule za kata. Hii imenifanya kuona tofaut yake yeye na hao watoto, yeye anakosa ushapu lkn siku zinavyokwenda anabadilika. Nisichopenda kwa watoto wa kata ni tabia mbaya kama matusi nk, sasa nikiwepo wanaogopa kutoa hayo maneno ya ovyo.
 
81 Reactions
Reply
Back
Top Bottom