Baija Bolobi
JF-Expert Member
- Feb 25, 2009
- 1,093
- 1,726
Serikali ya awamu ya tano mpaka sasa inalaumiwa kwa kutopenda kukosolewa. Inapenda kupongezwa, kushangiliwa au kuikalia kimya. Watu wamenyamazishwa. Wanaoruhusiwa kutukana mitandaoni na hadharani ni CCM tu. Wanaoruhusiwa kuandamana na kufanya mikutano ya ndani na nje ni CCM tu. Hii haijatosha kuzima kiu ya kunyamazisha wakosoaji. Kuna mbinu mpya zimekuja:
-Ukiikosoa serikali, unatumiwa na Maafisa Uhamiaji ili kuhakiki uraia wako. Baadhi ya viongozi wa dini na asasi za kiraia wamepelekewa barua wathibitishe uraia wao haraka iwezekanavyo. Wamo maaskofu wa TEC, CCT na asasi za kiraia kama ile ya Mama Bisimba.
-Ukithibitisha wewe ni raia, unatumiwa "Msamaria mwema" wa kukujulisha mipango ya kukumiminia risasi au kukupoteza kama waliopotea. Unahakikishiwa kuwa ukifanyiwa hivyo hakuna lolote litakalotokea na watakaofanya hivyo watapandishwa vyeo. Baadhi ya wabunge na wanasiasa wameishakutana na msamaria mwema huyo. Utitiri wa wanaohama vyama uko katika kundi hili.
-Matumizi ya TRA na ile taasisi ya kudhibiti madawa ya kulevya ni jambo la kawaida kwa wakosoaji wenye ukwasi wa fedha mali nyinginezo.
Lakini katikati ya zoezi hili, watekelezaji wanadai fedha nyingi. Kiwango cha rushwa hapa nchini kimepanda bei. Hakuna afisa wa kitengo anayehongwa laki tano tena!
Siamini kama wakubwa wanajua haya yanayoendelea ndani ya nchi.
-Ukiikosoa serikali, unatumiwa na Maafisa Uhamiaji ili kuhakiki uraia wako. Baadhi ya viongozi wa dini na asasi za kiraia wamepelekewa barua wathibitishe uraia wao haraka iwezekanavyo. Wamo maaskofu wa TEC, CCT na asasi za kiraia kama ile ya Mama Bisimba.
-Ukithibitisha wewe ni raia, unatumiwa "Msamaria mwema" wa kukujulisha mipango ya kukumiminia risasi au kukupoteza kama waliopotea. Unahakikishiwa kuwa ukifanyiwa hivyo hakuna lolote litakalotokea na watakaofanya hivyo watapandishwa vyeo. Baadhi ya wabunge na wanasiasa wameishakutana na msamaria mwema huyo. Utitiri wa wanaohama vyama uko katika kundi hili.
-Matumizi ya TRA na ile taasisi ya kudhibiti madawa ya kulevya ni jambo la kawaida kwa wakosoaji wenye ukwasi wa fedha mali nyinginezo.
Lakini katikati ya zoezi hili, watekelezaji wanadai fedha nyingi. Kiwango cha rushwa hapa nchini kimepanda bei. Hakuna afisa wa kitengo anayehongwa laki tano tena!
Siamini kama wakubwa wanajua haya yanayoendelea ndani ya nchi.