BM X6
JF-Expert Member
- Nov 24, 2020
- 1,360
- 4,149
Hii Dunia ni Mungu pekee ndio anajua sisi viumbe wake namna tunavyoishi, Inawezekana mm ndio nimechelewa kujua haya mambo, pengine yapogo na watu wanavuna pesa kwa mtindo huu, ila kwa upande wangu hii ni Mara ya kwanza kushuhudia hii kitu tena kutoka kwa ndugu.
Anyways, nina ndugu yangu anaishi Dar es salaam ila kwao ni Mtwara, ni Mama mtu mzima anakaribia 42 hivi na ana mtoto mmoja, mwanae anafanya kazi za ndani hapo hapo Dar.
Sasa kilichokuja kutokea, huyu Mama kwanza ni mtu wa Dini sana (Mkristo) halafu ni mtaratibu sana, kuna kanisa moja wanajiita 'waaminio' na kuna Nabii wao anaitwa WILLIAM BRANHAM (Pichani). Ukiacha Jumapili pia wanafanya ibada Jumatano na Ijumaa kuanzia saa kumi jioni, ijumaa hii liyopita huyu mama alienda ibada kama kawaida yake ambapo alipofika alimfuata mmoja wa viongozi aliyekuwepo siku hiyo nakumjuza taarifa za msiba wa Mama yake mzazi (Mama yake anaumwa kwa muda sasa Mtwara) basi bila kupoteza muda yule Kiongozi aliwajuza na watu waliohudhuria ibaya siku hiyo ile taarifa ya msiba huku akimpatia elfu 50 ya nauli yule mama na kumuahidi nauli ya kurudi toka msibani
Huyu mgonjwa anayedaiwa amekufa mimi namuita Bibi ila sio Bibi yangu mzaa Mama wala Baba, na hizi taarifa za msiba zilinifikia nilijuzwa na jirani yake Mama mkubwa (wote wanasali kanisa moja) sasa ukipata taarifa ya msiba kikawaida ni lazima uwajuze wengine, ndio hapo nilipo staajabishwa baada ya kumpigia Dogo flani kule mtwara kama amepata taarifa hizi za msiba, akaniuliza "wewe nani kakupa hizo taarifa kwasababu nimetoka muda si mrefu huko kwa mgonjwa ni mzima lakini hali yake si nzuri" nikamwambia taarifa nimezipata Dar ila huyu Dogo alivyonambia tu hali ya mgonjwa sio nzuri, mm moja kwa moja nikaiwekea tiki ile taarifa kwamba huenda dogo wakati anaondoka kwa mgonjwa na muda huo huo ndio mgonjwa alikuwa anakata roho.
Dogo ilibidi arudi kule hospital kwa mgonjwa baada ya mm kumpa taarifa zile alipofika akanipigia akanambia "ni vile tu hali yake sio nzuri ila ningekupa uongee nae" akarudia kuniuliza tena "kwani wewe nani alikupa taarifa hizo" nikamwambia ni jirani yake na Mama mkubwa hivyo taarifa imetoka kwa Mama mkubwa japokuwa mimi hajanambia yeye moja moja na kanisani wamembariki kwa nauli kuja kuzika huko Mtwara. Dogo alishangaa sana na hatimaye taarifa zilifika kwa ndugu wote ila wengi tulijua Mama mkubwa atakuwa kachanganyikiwa tu au alichanganya taarifa wakati anaulizia taarifa za mgonjwa....cha ajabu imekuja kugundulia kwamba huyu mama alikusudia kufanya hivi kwasababu
1: Jirani yake ambaye anasali naye kamziba mdomo, kamwambia asiongee chochote kanisani ila yeye atasafiri kwenda Mtwara, hivyo kanisani wabaki na taarifa za msiba kama zilivyotolewa mwanzo
2: Kawaida ya kanisani hapo inapotokea msiba ni lazima mfiwa asindikizwe na mtu hata mmoja ila huyu Mama unaambiwa hakutaka alimuomba Kiongozi wake aende mwenyewe....na kumbuka hiyo ilikuwa Ijumaa
Jana Jumapili sasa, unaambiwa baada ya ibada Pastor akatangaza taarifa ile ya msiba upya ili taarifa iwafikie wengi zaidi na rambirambi zikakusanywa, wakati huo huyu Mama kashasafiri kwenda Mtwara na anayeshuhudia yote haya ni jirani yake ambaye ndiye aliyenipa taarifa hizi za msiba ambazo hazikuwa za kweli, Jirani anasema alijisikia vibaya sana kuona Pastor anatangaza taarifa za msiba ambao haujatokea, alitamani kwenda kumwambia ukweli lakini ameshindwa, na ukweli huu unaujua yeye tu hapo Kanisani kwao, jambo hili limebaki kichwani kwake anawaza namna ya kufanya
Akae kimya au amwambie ukweli Pastor?
Anyways, nina ndugu yangu anaishi Dar es salaam ila kwao ni Mtwara, ni Mama mtu mzima anakaribia 42 hivi na ana mtoto mmoja, mwanae anafanya kazi za ndani hapo hapo Dar.
Sasa kilichokuja kutokea, huyu Mama kwanza ni mtu wa Dini sana (Mkristo) halafu ni mtaratibu sana, kuna kanisa moja wanajiita 'waaminio' na kuna Nabii wao anaitwa WILLIAM BRANHAM (Pichani). Ukiacha Jumapili pia wanafanya ibada Jumatano na Ijumaa kuanzia saa kumi jioni, ijumaa hii liyopita huyu mama alienda ibada kama kawaida yake ambapo alipofika alimfuata mmoja wa viongozi aliyekuwepo siku hiyo nakumjuza taarifa za msiba wa Mama yake mzazi (Mama yake anaumwa kwa muda sasa Mtwara) basi bila kupoteza muda yule Kiongozi aliwajuza na watu waliohudhuria ibaya siku hiyo ile taarifa ya msiba huku akimpatia elfu 50 ya nauli yule mama na kumuahidi nauli ya kurudi toka msibani
Huyu mgonjwa anayedaiwa amekufa mimi namuita Bibi ila sio Bibi yangu mzaa Mama wala Baba, na hizi taarifa za msiba zilinifikia nilijuzwa na jirani yake Mama mkubwa (wote wanasali kanisa moja) sasa ukipata taarifa ya msiba kikawaida ni lazima uwajuze wengine, ndio hapo nilipo staajabishwa baada ya kumpigia Dogo flani kule mtwara kama amepata taarifa hizi za msiba, akaniuliza "wewe nani kakupa hizo taarifa kwasababu nimetoka muda si mrefu huko kwa mgonjwa ni mzima lakini hali yake si nzuri" nikamwambia taarifa nimezipata Dar ila huyu Dogo alivyonambia tu hali ya mgonjwa sio nzuri, mm moja kwa moja nikaiwekea tiki ile taarifa kwamba huenda dogo wakati anaondoka kwa mgonjwa na muda huo huo ndio mgonjwa alikuwa anakata roho.
Dogo ilibidi arudi kule hospital kwa mgonjwa baada ya mm kumpa taarifa zile alipofika akanipigia akanambia "ni vile tu hali yake sio nzuri ila ningekupa uongee nae" akarudia kuniuliza tena "kwani wewe nani alikupa taarifa hizo" nikamwambia ni jirani yake na Mama mkubwa hivyo taarifa imetoka kwa Mama mkubwa japokuwa mimi hajanambia yeye moja moja na kanisani wamembariki kwa nauli kuja kuzika huko Mtwara. Dogo alishangaa sana na hatimaye taarifa zilifika kwa ndugu wote ila wengi tulijua Mama mkubwa atakuwa kachanganyikiwa tu au alichanganya taarifa wakati anaulizia taarifa za mgonjwa....cha ajabu imekuja kugundulia kwamba huyu mama alikusudia kufanya hivi kwasababu
1: Jirani yake ambaye anasali naye kamziba mdomo, kamwambia asiongee chochote kanisani ila yeye atasafiri kwenda Mtwara, hivyo kanisani wabaki na taarifa za msiba kama zilivyotolewa mwanzo
2: Kawaida ya kanisani hapo inapotokea msiba ni lazima mfiwa asindikizwe na mtu hata mmoja ila huyu Mama unaambiwa hakutaka alimuomba Kiongozi wake aende mwenyewe....na kumbuka hiyo ilikuwa Ijumaa
Jana Jumapili sasa, unaambiwa baada ya ibada Pastor akatangaza taarifa ile ya msiba upya ili taarifa iwafikie wengi zaidi na rambirambi zikakusanywa, wakati huo huyu Mama kashasafiri kwenda Mtwara na anayeshuhudia yote haya ni jirani yake ambaye ndiye aliyenipa taarifa hizi za msiba ambazo hazikuwa za kweli, Jirani anasema alijisikia vibaya sana kuona Pastor anatangaza taarifa za msiba ambao haujatokea, alitamani kwenda kumwambia ukweli lakini ameshindwa, na ukweli huu unaujua yeye tu hapo Kanisani kwao, jambo hili limebaki kichwani kwake anawaza namna ya kufanya
Akae kimya au amwambie ukweli Pastor?