Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,552
Inauma sana. Inauma kweli!
Kwanza kabisa naomba nichukue nafasi hii kuwapa pole nyingi sana wale wote ambao wamewahi kukumbwa na hii mikasa ya either kukamatwa na kufichwa or ndugu /jamaa/wapendwa wao kukumbwa na hiyo kadhia.Poleni sana!
Imekuwa ikiripotiwa mara nyingi sana kuwa watu wamepotea katika mazingira ya kutatanisha ama wameteswa na watu wasiojulikana na kufichwa huko kusikojulikana. Matukio mengi sana yamekuwa yakitokea hapa Tanzania. Hapa tusiwagusie wale watoto wadogo wanaopotea na kutangazwa ITV ama misikitini.
Hapa tunazungumzia watu wazima ambao wanakuwa wanaonekana kutetea vitu fulani katika nafasi walizo nazo kwenye taasisi zao.
Katika hao kuna ambao hurudi uraiani na wengine hupotezwa mazima na kuacha familia zao zikiteseka kwa shida.Huwaacha wajane wakihangaika na watoto wao hapa duniani.
Jamani hao 'wataalam' hufanyeje fanyeje mpaka kumweka mtu kwenye 18 na kumpeleka kusikojulikana bila watu kujua?
Wanatumia chambo gani kumvuta mtu? Na huko ambako hupeleka watu ni hapahapa Tanzania au nje ya nchi?
Hivi ni kweli mtu aliwahi kupotea zaidi ya wiki moja akaja kuonekana akiwa hai?
Pengine hapa kuna wataalam wa hayo maswala na wengine walishawahi kukumbwa na kadhia hii.Tunaombeni mawazo yenu
Alamsiki!
Kwanza kabisa naomba nichukue nafasi hii kuwapa pole nyingi sana wale wote ambao wamewahi kukumbwa na hii mikasa ya either kukamatwa na kufichwa or ndugu /jamaa/wapendwa wao kukumbwa na hiyo kadhia.Poleni sana!
Imekuwa ikiripotiwa mara nyingi sana kuwa watu wamepotea katika mazingira ya kutatanisha ama wameteswa na watu wasiojulikana na kufichwa huko kusikojulikana. Matukio mengi sana yamekuwa yakitokea hapa Tanzania. Hapa tusiwagusie wale watoto wadogo wanaopotea na kutangazwa ITV ama misikitini.
Hapa tunazungumzia watu wazima ambao wanakuwa wanaonekana kutetea vitu fulani katika nafasi walizo nazo kwenye taasisi zao.
Katika hao kuna ambao hurudi uraiani na wengine hupotezwa mazima na kuacha familia zao zikiteseka kwa shida.Huwaacha wajane wakihangaika na watoto wao hapa duniani.
Jamani hao 'wataalam' hufanyeje fanyeje mpaka kumweka mtu kwenye 18 na kumpeleka kusikojulikana bila watu kujua?
Wanatumia chambo gani kumvuta mtu? Na huko ambako hupeleka watu ni hapahapa Tanzania au nje ya nchi?
Hivi ni kweli mtu aliwahi kupotea zaidi ya wiki moja akaja kuonekana akiwa hai?
Pengine hapa kuna wataalam wa hayo maswala na wengine walishawahi kukumbwa na kadhia hii.Tunaombeni mawazo yenu
Alamsiki!