Mbinguni sio salama, ni propaganda tu!

Umewaza kitulivu, lakini kuna maswali rahisi umeyafanya kuwa magumu kwa makusudi.

Mfano q#2! 'Ndani ya muda huo Adamu.....etc etc!

Jibu lake mbona ni rahisi tu, kwamba alikuwa hajabaleke, kwani binadamu kabla ya balekhe huwa ana uwezo wa kuyafanya hayo uliyouliza?

Maelezo yako ya hoja kuhusu uumbaji wa Mungu kuumba mwanadamu dume bila jike, wakati alikuwa na 'exposure' ya uumbaji huko nyuma kuumba viumbe kwa mfumo wa pair ya dume na jike ili vizaliane, ninayaunga mkono.

Katika maelezo ya vitabu vitakatifu kuna mkanganyiko, ni kama vile M/Mungu viumbe alioanza kuwaumba walikuwa ni binadamu, kumbe binadamu ndiye kiumbe wa mwisho kuumbwa na kuwekwa hapa duniani.

Binadamu kaletwa duniani kakuta viumbe wanaishi na wengine hakuwakuta, tayari walikuwa wametoweka (mf: dinosours), lakini viumbe wote hao walikuwa madume na majike.

Iweje kwa binadamu kuwe na mkwamo na kusua sua kwa uumbaji kiasi hicho?

Huwa inafika mahali maandishi yanajichanganya menyewe halafu waumini tunafokewa na kutishwa ili tusitafakari kiuyakinifu!

Sent using Jamii Forums mobile app
Niwazavyo mimi ninaona ipo siku wadamu wote watatoweka duniani na kuja viumbe wengine, jaribu kuona kwamba kwanini wanadamu wa kale walikua wakiishi miaka mingi ila kila siku na miaka inavyokwenda umri wa kuishi unapungua kutoka miaka 300 na kuendelea na kupungua hadi kufika miaka 95 kushuka chini adi dk 1.

Ona kwamba maisha yanavyobadilika mtoto uliemwacha kijijini bado ni mdogo ukionana nae after 5yrs tayar amebadilika kupita kiasi kwamba tayar mnalingan na hata yeye akaonekan ni mkubwa kwako, :
ni mfano:

Kwa mantiki hiyo kama zamani walikuepo viumbe wengine na sasa wametoweka kabisa, historia inatuambia kua MIJUSI ya kale ndio viumbe waliokua na akili na teknolojia ya juu kushinda hata mwanadamu.

Ila sasa walitoweka. Najaribu tu kuwaza
 
Dini na Sayansi haviendani
Dini na sayansi vinaendana. Dini inaelezea simple jambo ambalo kisayansi lina evolution kubwa mno.

Mf. Siku moja ya kwenye biblia (hasa za agano la kale ni kubwa na ndefu mno kuliko ya kisayansi au kisasa.)

The same, siku moja ya mbinguni ni sawa na miaka zaidi ya elfu ya duniani.

Upo uwezekano uumbaji wa Mungu kwa siku saba za kwenye kitabu cha dini, ni sawa na miaka mingi mno ambayo haielezeki kwenye Dunia yetu kisayansi

So, huenda ikawa kweli, kuna viumbe viliishi kabla ya mwanadamu, maana hata kisayansi, Dinosaurs na viumbe reptiles wa zamani walitokomeaga kwenye vilindi vya maji, kabla ya evolution of man.
 
Kwanini umeamua kuandika uongo, uongo ambao hata ukitafakari tu kwa akiki yako ndogo unauona ?

Kama wewe ni mkamilifu, inakuwaje una sahau ? Au kusahau ni ukamilifu ?

Kama umekamilika kwanini huwezi kusikia mazungumzo baina ya sisimizi ? Au kwanini huwezi kumuona sisimizi umbali wa mita tano kutoka wewe ulipo ?


Sasa hapa mbona unathibitisha kutokuamilika na muda huo huo unadai sisi tulimbwa tukiwa kamili ?
Mbna muumbaji nae alisahau Kumuumbia Adam jike ilhali tayari viumbe vingine viliumbiwa majike?
Na baadae ndo anahamaki kwamba haikupaswa awe pekeake ndo anamuumbia jike(Eva/Hawa)
 
Mbna muumbaji nae alisahau Kumuumbia Adam jike ilhali tayari viumbe vingine viliumbiwa majike?
Na baadae ndo anahamaki kwamba haikupaswa awe pekeake ndo anamuumbia jike(Eva/Hawa)
Thibitisha kama alisahau.
 
USALAMA WA MBINGUNI BADO NI MDOGO

Na, Robert Heriel

Wakati Mungu anaumba Mradi wake wa Dunia aliumba kila kitu kikiwa chema kabisa. Hakuna ambacho kilikuwa na kasoro, kila kitu kilikuwa kimekamilika. Hivyo yeyote unayemuona hapa duniani ujue amekamilika yaani yuko full completely. Hii Propaganda ya kusema mwanadamu hajakamilika ni hila, njama, ulaghai wa viumbe wasio na asili ya binadamu.

Kabla sijaenda mbali, nieleze kwa kifupi namna Mradi huu wa Dunia ilivyoumbwa na Mungu. Mungu aliiumba dunia kwa mfumo wa kutegemeana (Ecosytem) yaani viumbe vinategemeana. Kutegemeana huku ndio kunakamilisha mradi mzima wa dunia. Katika Mradi huu kuna aina nyingi za viumbe kulingana na asili yao walivyoumbwa. Mathaalani; Wapo viumbe walioumbwa kwa Hewa, wapo walioumbwa kwa maji, wapo walioumbwa kwa moto, wapo walioumbwa kwa Mwanga/ nuru wapo walioumbwa kwa udongo, wapo walioumbwa kwa mchanganyiko wa mada zaidi ya moja yaani labada maji na udongo, au hewa na mwanga.

Hivyo naweza kusema viumbe wapo aina zifuatazo kulingana na malighafi zilizotumiwa kuwaumba;
1. Viumbe wa umaji
2. Viumbe wa Umoto
3. Viumbe wa Uhewa
4. Viumbe wa Udongo/umadini
5. Viumbe wa Unuru/umwanga
6. Viumbe waliochanganya malighafi kama mwanadamu ambaye amechanganya umaji(ikiwemo damu), udongo na uhewa(Roho) chochote kikipungua katika mchanganyiko huo basi maisha ya mwanadamu aypo mashakani.

Kila kiumbe kimepewa Miliki au ufalme wake na watakaokitumikia. Mwanadamu amepewa dunia, na vyote vilivyopo duniani ni mali yake na vinamtumiikia.

Nikirejea kwenye Mada.

Adamu aliumbwa Duniani ambapo kiasili ndio kwake. Baadaye Mungu Akamchukua huyo Mtu akampeleka (Edeni) ambapo kiasili sio Duniani. Kumbuka Adamu akitolewa Duniani kupelekwa Edeni alikuwa pekeake kwa mujibu wa maandiko.

Baadaye Mungu akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wa Adamu. Hii ni kumaanisha Eva/Hawa aliumbiwa Edeni. Najaribu kufikiri na kugundua kuwa Eva ni matokeo ya mchangiko wa malighafi za dunia na Edeni. Kupitia Ubavu wa Adamu, Eva alijipatia malighafi za dunia(udongo) na kupitia malighafi zingine zilitoka pale pale Edeni. Nadhani mpaka sasa unaweza anza kupata picha ya kuelewa tofauti baina ya mwanaume na mwanamke kiasili.

Lakini lazima tujiulize, wakati Mungu akiumba mradi wake mara zote alikuwa akikiri kuwa kila alichokifanya ni chema na hakika ilikuwa chema, lakini baada ya kumhamisha Adamu na kumpeleka Bustani ya Edeni ni kwa nini mawazo yake yalibadilika na kusema "Si vyema" "huyu mtu awe pekeake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye" na hapo ndipo akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wake. Hii ni kumaanisha Kwa duniani Adamu ilikuwa vyema kuwa pekeake wakati Edeni haikuwa Vyema.

Lakini hapa panaweza kuleta hitilafu kwenye kufikiri, je ni Mungu huyo huyo aliyesema kila kitu ni chema na sasa amebalisha mawazo? Mbona Mungu sio kigeugeu?

Akili yangu inaenda nisikokujua inafikiri hivi, huenda Aliyemuumba Adamu siye aliyemuumba Hawa. Kwa nini ninafikiri hivi? Pengine niseme sijui. Embu tuone.

Nafikiri Hawa aliumbwa kwa njama, hila, za Kumuangusha Adamu. Kumbuka Adamu kwake ni duniani, wala sio Edeni. Edeni ilikuwa inamwenyewe, je ni nani huyo?

Embu ona, Adamu analetwa tuu Edeni hapo hapo anapewa sheria ya kutokula Tunda la Mti wa Kati wa ujuzi wa mema na mabaya. Fikiria hapo! Punde anaumbwa Hawa/Eva kisha aliyeumbwa muda huo huo anakuwa wakwanza kula tunda. Bado hujashtuka. Akili yako inakuambia nini kuhusu aliyemwambia Adamu asile matunda ya mti wa kati wa ujuzi wa Mema na Mabaya kwani atakufa? Kisha aliyeumbwa Edeni anakula hilo tunda na anaenda kwa adamu akiwa hajafa, huoni adamu angeona aliyesema ukila utakufa angekuwa muongo? Kumbuka Mlengwa wa lile tunda kula hakuwa Hawa/Eva bali alikuwa adamu. Kama Adamu asingekula lile tunda ni wazi Eva asingepata madhara. Lakini hila za aliyemuumba Eva, na ndiye huyo huyo aliyemwambia ale ili ampe adamu amuaminishe kuwa hatakufa ili ale ndio zilimuingiza Adamu Mkenge, kula tunda la sumu, lenye kuua taratibu kizazi cha Adamu mpaka hivi leo. Bado hujaona kifo ni mradi wa viumbe fulani?

Baadaye tunapata habari za Nyoka akimdanganya Hawa/Eva ili akampe lile tunda Adamu. Lile Tunda lisingekuwa na madhara yoyote kwa Eva/Hawa kama Adamu asingelila. Mtihani ule ulikuwa unamhusu Eva/ Hawa. Hata hivyo Hawa/Eva hakudanganywa bali alifanya makusudi kwani tayari alikuwa anapewa oda na aliyemuumba(huyo aliyemwambia ampe mumewe lile tunda)

Nyoka(ambaye sio huyu atambaaye) ndiye alikuwa mmiliki wa ile Edeni. Kama Adamu alivyoambiwa atawale dunia.

Ili ujue Hawa/Eva alifanya kusudi kumuangamizA Adamu, angalia alivyoenda kumpa lile tunda Adamu ili alile, wala hakumpa maelezo yoyote kuhusu huko alikotoka zaidi ya kumwambia nimelila na lafaa kwa kula. Hakumwambia amekutana na nani. Habari hizo Adamu anakuja kuzifahamu baada ya Mungu kuja ambapo Eva/Hawa anasema kuwa amedanganywa na Nyoka, (Namuona Adamu akijiona mjinga akitumbua macho yake kama mtu asiyeamini kuwa kaangushwa bila kujua) Mungu akamwambia umeisikiliza sauti ya mke wako. Kumaanisha hakupaswa kumsikiliza bali yeye ndio asikilizwe.

Baadaye Adamu na Hawa wanatimuliwa Edeni, na kurudishwa Duniani tayari akiwa amekula tunda lenye sumu iuayo pole pole. Na Mmiliki wa Edeni anabaki kuwa mshindi.

Kilichokusudiwa kifanyike Edeni kimekamilika, Adamu hahitajiki tena Edeni hivyo kufukuzwa ndio suluhu.
Alifukuzwa, na hapo ndipo rasmi mwanadamu akaanza kukengeushwa na viumbe wa Mbinguni kwa kutumia mawakala zao waliopo huku duniani. Mara Mbinguni, mara peponi mara sijui Akhera.

Ati tutaishi na Mungu. Sirius!!! Kabla ya kuanguka hatukuishi na Mungu, hata sasa hatuishi na Mungu, na kamwe hatuishi na Mungu. Hata hao viumbe wengine hawajawahi kuishi na Mungu. Bali ni propaganda zao za kurubuni kizazi cha mwanadamu kzidi kuwa watumwa.

Nataka kusema Nini?

Dunia haijawahi kuwa mbaya, ubaya unatokea nje. Bila Edeni pasingekuwa na mabaya yote yanayoendelea duniani. Edeni ndio kulikuwa na tatizo wala sio dunani.

Mbinguni wanaishi malaika, Mungu haishi Mbinguni wala haishi duniani.Mungu hana Anuani, popote yupo kwa wakati wote. Mungu hana Kiti cha Enzi. Mungu hana Ulinzi. Malaika ni viumbe walioumbwa kwa Mwanga mkali, wenye mfano wa mwanadamu lakini hawana miili kama yetu. Malaika wapo wa aina nyingi kulingana na kazi, maumbile, na Sifa. Wapo malaika wenye mbawa kuanzia mbili, tatu, nne, sita, kumi na mbili na kuendelea.

Huko Mbinguni ndipo matatizo yalipoanzia, Falme za Malaika zimegawanyika. Kuihubiri mbinguni ni kuidhalilisha dunia. Kuwatukuza Malaika ni kuwatukana wanadamu.

Ipo tabia baadhi ya wanadamu wanawaabudu viumbe waishio mbinguni kwani viumbe hao wamewaahidi mambo mazuri, wengine wakiahidiwa kupewa uzima wa milele, wengine kwenda mbinguni, wengine wanaabudu kwa majina wakina Mikael, sijui Gabriel, na Yesu ambao kimsingi hao sio Mungu.

Bali wao wamekuja kuwafanya wanadamu kama mateka, kama vile huku duniani nchi moja inavyoenda kutawala nchi zingine, tunaita Ukoloni na sasa Ukoloni mamboleo. Ndivyo na viumbe wa Mbinguni walivyofanikiwa kuwatalawa viumbe wa duniani yaani sisi wanadamu.

Wanadamu wanawaona malaika ni bora kuliko binadamu. Wanapaona Mbinguni ni bora kuliko duniani.

Ninachotaka kusema ni kuwa, mwanadamu alikuwa mkamilifu kabisa kabla hajakutana na hila za viumbe wa mbinguni, si ajabu hata Edeni ilikuwa hila za hao viumbe kwani wamejaliwa nguvu, uweza, akili na mamlaka ya kusema kitu kikawa.

Matatizo ya duniani hayataisha leo lakini atakayeyamaliza ni mwanadamu mwenyewe. Pale Mwanadamu atakapoacha kuwatumikia Viumbe wa mbinguni iwe ni malaika au mashetani ndio siku hiyo hiyo dunia hii itakombolewa.

Naamini, miaka ya hivi karibuni mwanadamu ataweza kukikabili kifo. Watu hawatakufa tena kutokana na matokeo ya kisayansi na tekonolojia. Kifo kitadhibitiwa.

Nafahamu kuwa Kifo ilikuwa ni Mradi wa viumbe wa Mbinguni kumtawala mwanadamu. Lakini baada ya kifo kukidhibiti mamlaka ya mwanadamu itarejea kama ilivyomwanzo.

Kifo hakitadhibitiwa kwa kutamani kwenda Mbinguni. Watu wanachoshindwa kuelewa ni kuwa Kifo kimeletwa na viumbe hao hao wa mbinguni.

Sijajua Mungu yupo wapi kwa sasa, licha kuwa mahali popote yupo. Lakini hawezi ingilia mambo haya, mpaka siku ya hukumu.

Siku ya hukumu itafika pale ambapo Mwanadamu ataweza kukidhibiti Kifo.

Mbinguni sio salama kama watu wanavyofikiri.

Taikon nimemaliza, Leo sitaki maswali.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Unguja
Tamu sana
 
Nashukuru kwa uelewa wako Ila imeelezea Sana kutokana na historia ya biblia....

Kwenye Uislam. Ulivyoelezea kuumbwa Adam

Eden Garden

#NABII ADAM.
Allah, Kitu cha kwanza kukiumba ulimwenguni ni Qalam ambayo ameiumba kwa ajili ya kuandika mema na maovu ya viumbe.
.
Aliumba Lauhul-Mahfuudhna vyenginevyo.
.
Allah aliumba mbingu saba (7) Kwa Siku Sita (6) katika matabaka mbalimbali pamoja na mchanga (ardhi) siku ya Jumaamosi.
.
Aliumba majabali katika siku ya Jumaapili.
.
Miti siku ya Jumaatatu.
.
Vitu vyote vyenye kuchukiza aliviumba Allah katika siku ya Jumaanne.
.
Nuru siku ya Jumaatano.
.
Viumbe katika siku ya Alhamis.
.
Na mwisho alimuumba Adam katika siku ya Ijumaa nyakati za Alaasiri ndio siku ya mwisho ambayo wanaadamu wote wataondoka ulimwenguni.
.
Lakini kabla ya kuumbwa Nabii Adam, Allah alikuwa tayari amekwishawaumba majini ambao walifanya ufisadi katika ardhi na walimwaga damu za wengine.
.
Hatimae Allah aliwapelekea majini hao jeshi la malaika na wakateketezwa majini wote.
.
Mara tu baada ya Allah kuwateketeza majini hao, Malaika Jibriil alimbakisha mmoja katika kizazi cha majini aliyeitwa AZAAZIIL (Iblis) kwa vile jinni huyo alimuabudu sana Allah, hivyo Allah alimuweka pamoja na malaika peponi.
.
Iblis aliendelea kumwabudu Allah mpaka akafikia kuitwa Abaasijda, kutokana na wingi wa sijda zake kumsujudia Allah.
.
Hivyo ijapokuwa hakuumbwa kwa nuru (aliumbwa kwa moto), lakini Iblis alishirikiana na malaika katika ibada kumwabudia Allah.
.
Siku moja Allah aliwadokeza malaika kuwa anataka kuumba kiumbe mwengine duniani.
.
Malaika wakafikiri mambo yaliyowatokea kabla ya Adam, na jinsi wale majini walivyofanya ufisadi katika ardhi.
.
Hivyo malaika hao wakasema kwa kumuuliza katika quran tukufu;
“Ewe mola unataka kuweka katika ardhi anaetaka kufanya ufisadi na kumwaga damu, kama walivyomwaga damu waliopita.
Au unataka kuleta kiumbe atakaekuabudu kwa wingi?
Na je! Sisi tumepunguza kitu katika ibada yako? Na hali sisi tunakutukuza na tunakusabbihi kila usiku na mchana?”.
.
Nae Allah akawaambia katika qurani tukufu;
“Mimi ninajuwa vile msivyovijuwa nyinyi”.
.
Kutokana na uchamungu wao malaika wakasema;
”Basi aumbe Allah vile anavyovipenda katika viumbe.
Lakini hawatokua viumbe hao wabora na wajuzi kuliko Sisi"....

Hivyo Allah akauchukuwa mchanga inasemekana wa ufinyanzi na akaufinyanga kwa hatua mbalimbali mpaka ukafikia kwenye kiumbe mfano wa sanamu.
.
Hivyo Allah akasimamisha sanamu hiyo ya Adam kwa muda wa siku arubaini (40).
.
Na wakati ikiwa imesimama kila siku malaika walikuwa wakipita na kuiangalia sanamu hiyo iliyoweka uwanjani hapo.
.
Hivyo hapo sasa ikawa ni mwanzo wa fitna na kejeli kwa iblis kwani alihisi kiumbe huyo atakuja kupewa thamani kubwa kuliko wao, lakini mmoja wa malaika alipewa elimu ya kujuwa kitu cha baadae na Allah hivyo akawa anawatoa wasiwasi wenzake juu ya kiumbe hicho.
.
Katika siku ya arubaini Allah akaileta roho na kuanza kukipulizia kiwiliwili hicho.
.
Hapo Adam akapiga chafya na ndipo malaika wakamwambia Adam;
“EweAdam sema Alhamdulillah kwani Roho ndio kwanza imewasili”.
.
Adam hapo hapo kwa kushukuru akasema Alhamdulillah na Allah akamuitikia na ndipo Roho ikaingia machoni ambapo Adam akaona matunda ya aina kwa aina peponi.
.
Akaanza kuyatamani matunda yale ilhali roho haijafika hata tumboni, akataka pia kutembea wakati roho haijafika hata miguuni, na ndio maana mwanaadamu akawa ana tabia ya kuwa na pupa katika mambo yake siku zote.
.
Roho taratibu ikaingia kiungo kimoja baadaya chengine mpaka ikamalizia miguuni.
.
Hapo ndipo Allah akamuamrisha Adam apite mbele ya malaika na awatolee salam na hapo ikawa ni mwanzo wa salam katika Uislam.
.
Allah akasema, “Haya yatakuwa ni maamkizi kwa umma wako”.
.
Allah alimfundisha Adam majina ya vitu vyote duniani, pamoja na matumizi ya vitu hivyo.
.
Allah alivileta vitu hivyo mbele ya malaika na akawaambia;
”Nielezeni majina ya vitu hivyo ikiwa nyinyi ni wakweli”.
.
Malaika wakashindwa na wakajibu kumwambia Allah;
”Utakasifu ni wako Ewe mola, na sisi hatuvijui vitu hivyo ispokuwa vile ulivyotufundisha tu”.
.
Allah akamleta Adam na akamwambia avitaje vitu hivyo vyote, nae Adam hakusita akavitaja vitu hivyo vyote.
.
Hapo ndipo Allah akawaambia malaika;
“Ninayajuwa yale msiyoyajuwa, basi msujudieni Adam”.
.
Hapo malaika wote walisujudu ispokuwa Iblisi pekee akakataa na akafanya kiburi na akawa ni miongoni mwa waliokufuru..
Hizi story zimedumaza vichwa vya waumini wengi. Ni ujinga uliotukuka.
 
Mleta mada nimegundua vitu 2 vikuu kwako;
  1. Ulizaliwa ukiwa na akili sana na nahisi miaka yako ya awali ulikuwa mzuri sana class!
  2. Ulikuja kuingia magenge ya ujanani ukaanza bange ambayo inaonekana imekuvuruga kabisa! acha!
 
Mleta mada nimegundua vitu 2 vikuu kwako;
  1. Ulizaliwa ukiwa na akili sana na nahisi miaka yako ya awali ulikuwa mzuri sana class!
  2. Ulikuja kuingia magenge ya ujanani ukaanza bange ambayo inaonekana imekuvuruga kabisa! acha!

😄😄😄😄

Sijawahi kutumia kilevi waka madawa yoyote ya kulevya tangu nizaliwe na sina mpango huo Mkuu
 
USALAMA WA MBINGUNI BADO NI MDOGO

Na, Robert Heriel

Wakati Mungu anaumba Mradi wake wa Dunia aliumba kila kitu kikiwa chema kabisa. Hakuna ambacho kilikuwa na kasoro, kila kitu kilikuwa kimekamilika. Hivyo yeyote unayemuona hapa duniani ujue amekamilika yaani yuko full completely. Hii Propaganda ya kusema mwanadamu hajakamilika ni hila, njama, ulaghai wa viumbe wasio na asili ya binadamu.

Kabla sijaenda mbali, nieleze kwa kifupi namna Mradi huu wa Dunia ilivyoumbwa na Mungu. Mungu aliiumba dunia kwa mfumo wa kutegemeana (Ecosytem) yaani viumbe vinategemeana. Kutegemeana huku ndio kunakamilisha mradi mzima wa dunia. Katika Mradi huu kuna aina nyingi za viumbe kulingana na asili yao walivyoumbwa. Mathaalani; Wapo viumbe walioumbwa kwa Hewa, wapo walioumbwa kwa maji, wapo walioumbwa kwa moto, wapo walioumbwa kwa Mwanga/ nuru wapo walioumbwa kwa udongo, wapo walioumbwa kwa mchanganyiko wa mada zaidi ya moja yaani labada maji na udongo, au hewa na mwanga.

Hivyo naweza kusema viumbe wapo aina zifuatazo kulingana na malighafi zilizotumiwa kuwaumba;
1. Viumbe wa umaji
2. Viumbe wa Umoto
3. Viumbe wa Uhewa
4. Viumbe wa Udongo/umadini
5. Viumbe wa Unuru/umwanga
6. Viumbe waliochanganya malighafi kama mwanadamu ambaye amechanganya umaji(ikiwemo damu), udongo na uhewa(Roho) chochote kikipungua katika mchanganyiko huo basi maisha ya mwanadamu aypo mashakani.

Kila kiumbe kimepewa Miliki au ufalme wake na watakaokitumikia. Mwanadamu amepewa dunia, na vyote vilivyopo duniani ni mali yake na vinamtumiikia.

Nikirejea kwenye Mada.

Adamu aliumbwa Duniani ambapo kiasili ndio kwake. Baadaye Mungu Akamchukua huyo Mtu akampeleka (Edeni) ambapo kiasili sio Duniani. Kumbuka Adamu akitolewa Duniani kupelekwa Edeni alikuwa pekeake kwa mujibu wa maandiko.

Baadaye Mungu akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wa Adamu. Hii ni kumaanisha Eva/Hawa aliumbiwa Edeni. Najaribu kufikiri na kugundua kuwa Eva ni matokeo ya mchangiko wa malighafi za dunia na Edeni. Kupitia Ubavu wa Adamu, Eva alijipatia malighafi za dunia(udongo) na kupitia malighafi zingine zilitoka pale pale Edeni. Nadhani mpaka sasa unaweza anza kupata picha ya kuelewa tofauti baina ya mwanaume na mwanamke kiasili.

Lakini lazima tujiulize, wakati Mungu akiumba mradi wake mara zote alikuwa akikiri kuwa kila alichokifanya ni chema na hakika ilikuwa chema, lakini baada ya kumhamisha Adamu na kumpeleka Bustani ya Edeni ni kwa nini mawazo yake yalibadilika na kusema "Si vyema" "huyu mtu awe pekeake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye" na hapo ndipo akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wake. Hii ni kumaanisha Kwa duniani Adamu ilikuwa vyema kuwa pekeake wakati Edeni haikuwa Vyema.

Lakini hapa panaweza kuleta hitilafu kwenye kufikiri, je ni Mungu huyo huyo aliyesema kila kitu ni chema na sasa amebalisha mawazo? Mbona Mungu sio kigeugeu?

Akili yangu inaenda nisikokujua inafikiri hivi, huenda Aliyemuumba Adamu siye aliyemuumba Hawa. Kwa nini ninafikiri hivi? Pengine niseme sijui. Embu tuone.

Nafikiri Hawa aliumbwa kwa njama, hila, za Kumuangusha Adamu. Kumbuka Adamu kwake ni duniani, wala sio Edeni. Edeni ilikuwa inamwenyewe, je ni nani huyo?

Embu ona, Adamu analetwa tuu Edeni hapo hapo anapewa sheria ya kutokula Tunda la Mti wa Kati wa ujuzi wa mema na mabaya. Fikiria hapo! Punde anaumbwa Hawa/Eva kisha aliyeumbwa muda huo huo anakuwa wakwanza kula tunda. Bado hujashtuka. Akili yako inakuambia nini kuhusu aliyemwambia Adamu asile matunda ya mti wa kati wa ujuzi wa Mema na Mabaya kwani atakufa? Kisha aliyeumbwa Edeni anakula hilo tunda na anaenda kwa adamu akiwa hajafa, huoni adamu angeona aliyesema ukila utakufa angekuwa muongo? Kumbuka Mlengwa wa lile tunda kula hakuwa Hawa/Eva bali alikuwa adamu. Kama Adamu asingekula lile tunda ni wazi Eva asingepata madhara. Lakini hila za aliyemuumba Eva, na ndiye huyo huyo aliyemwambia ale ili ampe adamu amuaminishe kuwa hatakufa ili ale ndio zilimuingiza Adamu Mkenge, kula tunda la sumu, lenye kuua taratibu kizazi cha Adamu mpaka hivi leo. Bado hujaona kifo ni mradi wa viumbe fulani?

Baadaye tunapata habari za Nyoka akimdanganya Hawa/Eva ili akampe lile tunda Adamu. Lile Tunda lisingekuwa na madhara yoyote kwa Eva/Hawa kama Adamu asingelila. Mtihani ule ulikuwa unamhusu Eva/ Hawa. Hata hivyo Hawa/Eva hakudanganywa bali alifanya makusudi kwani tayari alikuwa anapewa oda na aliyemuumba(huyo aliyemwambia ampe mumewe lile tunda)

Nyoka(ambaye sio huyu atambaaye) ndiye alikuwa mmiliki wa ile Edeni. Kama Adamu alivyoambiwa atawale dunia.

Ili ujue Hawa/Eva alifanya kusudi kumuangamizA Adamu, angalia alivyoenda kumpa lile tunda Adamu ili alile, wala hakumpa maelezo yoyote kuhusu huko alikotoka zaidi ya kumwambia nimelila na lafaa kwa kula. Hakumwambia amekutana na nani. Habari hizo Adamu anakuja kuzifahamu baada ya Mungu kuja ambapo Eva/Hawa anasema kuwa amedanganywa na Nyoka, (Namuona Adamu akijiona mjinga akitumbua macho yake kama mtu asiyeamini kuwa kaangushwa bila kujua) Mungu akamwambia umeisikiliza sauti ya mke wako. Kumaanisha hakupaswa kumsikiliza bali yeye ndio asikilizwe.

Baadaye Adamu na Hawa wanatimuliwa Edeni, na kurudishwa Duniani tayari akiwa amekula tunda lenye sumu iuayo pole pole. Na Mmiliki wa Edeni anabaki kuwa mshindi.

Kilichokusudiwa kifanyike Edeni kimekamilika, Adamu hahitajiki tena Edeni hivyo kufukuzwa ndio suluhu.
Alifukuzwa, na hapo ndipo rasmi mwanadamu akaanza kukengeushwa na viumbe wa Mbinguni kwa kutumia mawakala zao waliopo huku duniani. Mara Mbinguni, mara peponi mara sijui Akhera.

Ati tutaishi na Mungu. Sirius!!! Kabla ya kuanguka hatukuishi na Mungu, hata sasa hatuishi na Mungu, na kamwe hatuishi na Mungu. Hata hao viumbe wengine hawajawahi kuishi na Mungu. Bali ni propaganda zao za kurubuni kizazi cha mwanadamu kzidi kuwa watumwa.

Nataka kusema Nini?

Dunia haijawahi kuwa mbaya, ubaya unatokea nje. Bila Edeni pasingekuwa na mabaya yote yanayoendelea duniani. Edeni ndio kulikuwa na tatizo wala sio dunani.

Mbinguni wanaishi malaika, Mungu haishi Mbinguni wala haishi duniani.Mungu hana Anuani, popote yupo kwa wakati wote. Mungu hana Kiti cha Enzi. Mungu hana Ulinzi. Malaika ni viumbe walioumbwa kwa Mwanga mkali, wenye mfano wa mwanadamu lakini hawana miili kama yetu. Malaika wapo wa aina nyingi kulingana na kazi, maumbile, na Sifa. Wapo malaika wenye mbawa kuanzia mbili, tatu, nne, sita, kumi na mbili na kuendelea.

Huko Mbinguni ndipo matatizo yalipoanzia, Falme za Malaika zimegawanyika. Kuihubiri mbinguni ni kuidhalilisha dunia. Kuwatukuza Malaika ni kuwatukana wanadamu.

Ipo tabia baadhi ya wanadamu wanawaabudu viumbe waishio mbinguni kwani viumbe hao wamewaahidi mambo mazuri, wengine wakiahidiwa kupewa uzima wa milele, wengine kwenda mbinguni, wengine wanaabudu kwa majina wakina Mikael, sijui Gabriel, na Yesu ambao kimsingi hao sio Mungu.

Bali wao wamekuja kuwafanya wanadamu kama mateka, kama vile huku duniani nchi moja inavyoenda kutawala nchi zingine, tunaita Ukoloni na sasa Ukoloni mamboleo. Ndivyo na viumbe wa Mbinguni walivyofanikiwa kuwatalawa viumbe wa duniani yaani sisi wanadamu.

Wanadamu wanawaona malaika ni bora kuliko binadamu. Wanapaona Mbinguni ni bora kuliko duniani.

Ninachotaka kusema ni kuwa, mwanadamu alikuwa mkamilifu kabisa kabla hajakutana na hila za viumbe wa mbinguni, si ajabu hata Edeni ilikuwa hila za hao viumbe kwani wamejaliwa nguvu, uweza, akili na mamlaka ya kusema kitu kikawa.

Matatizo ya duniani hayataisha leo lakini atakayeyamaliza ni mwanadamu mwenyewe. Pale Mwanadamu atakapoacha kuwatumikia Viumbe wa mbinguni iwe ni malaika au mashetani ndio siku hiyo hiyo dunia hii itakombolewa.

Naamini, miaka ya hivi karibuni mwanadamu ataweza kukikabili kifo. Watu hawatakufa tena kutokana na matokeo ya kisayansi na tekonolojia. Kifo kitadhibitiwa.

Nafahamu kuwa Kifo ilikuwa ni Mradi wa viumbe wa Mbinguni kumtawala mwanadamu. Lakini baada ya kifo kukidhibiti mamlaka ya mwanadamu itarejea kama ilivyomwanzo.

Kifo hakitadhibitiwa kwa kutamani kwenda Mbinguni. Watu wanachoshindwa kuelewa ni kuwa Kifo kimeletwa na viumbe hao hao wa mbinguni.

Sijajua Mungu yupo wapi kwa sasa, licha kuwa mahali popote yupo. Lakini hawezi ingilia mambo haya, mpaka siku ya hukumu.

Siku ya hukumu itafika pale ambapo Mwanadamu ataweza kukidhibiti Kifo.

Mbinguni sio salama kama watu wanavyofikiri.

Taikon nimemaliza, Leo sitaki maswali.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Ung
Uzi umetulia... Nimeukubali!
 
USALAMA WA MBINGUNI BADO NI MDOGO

Na, Robert Heriel

Wakati Mungu anaumba Mradi wake wa Dunia aliumba kila kitu kikiwa chema kabisa. Hakuna ambacho kilikuwa na kasoro, kila kitu kilikuwa kimekamilika. Hivyo yeyote unayemuona hapa duniani ujue amekamilika yaani yuko full completely. Hii Propaganda ya kusema mwanadamu hajakamilika ni hila, njama, ulaghai wa viumbe wasio na asili ya binadamu.

Kabla sijaenda mbali, nieleze kwa kifupi namna Mradi huu wa Dunia ilivyoumbwa na Mungu. Mungu aliiumba dunia kwa mfumo wa kutegemeana (Ecosytem) yaani viumbe vinategemeana. Kutegemeana huku ndio kunakamilisha mradi mzima wa dunia. Katika Mradi huu kuna aina nyingi za viumbe kulingana na asili yao walivyoumbwa. Mathaalani; Wapo viumbe walioumbwa kwa Hewa, wapo walioumbwa kwa maji, wapo walioumbwa kwa moto, wapo walioumbwa kwa Mwanga/ nuru wapo walioumbwa kwa udongo, wapo walioumbwa kwa mchanganyiko wa mada zaidi ya moja yaani labada maji na udongo, au hewa na mwanga.

Hivyo naweza kusema viumbe wapo aina zifuatazo kulingana na malighafi zilizotumiwa kuwaumba:

1. Viumbe wa umaji
2. Viumbe wa Umoto
3. Viumbe wa Uhewa
4. Viumbe wa Udongo/umadini
5. Viumbe wa Unuru/umwanga
6. Viumbe waliochanganya malighafi kama mwanadamu ambaye amechanganya umaji (ikiwemo damu), udongo na uhewa (Roho) chochote kikipungua katika mchanganyiko huo basi maisha ya mwanadamu aypo mashakani.

Kila kiumbe kimepewa Miliki au ufalme wake na watakaokitumikia. Mwanadamu amepewa dunia, na vyote vilivyopo duniani ni mali yake na vinamtumiikia.

Nikirejea kwenye Mada.

Adamu aliumbwa Duniani ambapo kiasili ndio kwake. Baadaye Mungu Akamchukua huyo Mtu akampeleka (Edeni) ambapo kiasili sio Duniani. Kumbuka Adamu akitolewa Duniani kupelekwa Edeni alikuwa pekeake kwa mujibu wa maandiko.

Baadaye Mungu akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wa Adamu. Hii ni kumaanisha Eva/Hawa aliumbiwa Edeni. Najaribu kufikiri na kugundua kuwa Eva ni matokeo ya mchangiko wa malighafi za dunia na Edeni. Kupitia Ubavu wa Adamu, Eva alijipatia malighafi za dunia(udongo) na kupitia malighafi zingine zilitoka pale pale Edeni. Nadhani mpaka sasa unaweza anza kupata picha ya kuelewa tofauti baina ya mwanaume na mwanamke kiasili.

Lakini lazima tujiulize, wakati Mungu akiumba mradi wake mara zote alikuwa akikiri kuwa kila alichokifanya ni chema na hakika ilikuwa chema, lakini baada ya kumhamisha Adamu na kumpeleka Bustani ya Edeni ni kwa nini mawazo yake yalibadilika na kusema "Si vyema" "huyu mtu awe pekeake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye" na hapo ndipo akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wake. Hii ni kumaanisha Kwa duniani Adamu ilikuwa vyema kuwa pekeake wakati Edeni haikuwa Vyema.

Lakini hapa panaweza kuleta hitilafu kwenye kufikiri, je ni Mungu huyo huyo aliyesema kila kitu ni chema na sasa amebalisha mawazo? Mbona Mungu sio kigeugeu?

Akili yangu inaenda nisikokujua inafikiri hivi, huenda Aliyemuumba Adamu siye aliyemuumba Hawa. Kwanini ninafikiri hivi? Pengine niseme sijui. Embu tuone.

Nafikiri Hawa aliumbwa kwa njama, hila, za Kumuangusha Adamu. Kumbuka Adamu kwake ni duniani, wala sio Edeni. Edeni ilikuwa inamwenyewe, je ni nani huyo?

Embu ona, Adamu analetwa tuu Edeni hapo hapo anapewa sheria ya kutokula Tunda la Mti wa Kati wa ujuzi wa mema na mabaya. Fikiria hapo! Punde anaumbwa Hawa/Eva kisha aliyeumbwa muda huo huo anakuwa wakwanza kula tunda. Bado hujashtuka. Akili yako inakuambia nini kuhusu aliyemwambia Adamu asile matunda ya mti wa kati wa ujuzi wa Mema na Mabaya kwani atakufa? Kisha aliyeumbwa Edeni anakula hilo tunda na anaenda kwa adamu akiwa hajafa, huoni adamu angeona aliyesema ukila utakufa angekuwa muongo? Kumbuka Mlengwa wa lile tunda kula hakuwa Hawa/Eva bali alikuwa adamu. Kama Adamu asingekula lile tunda ni wazi Eva asingepata madhara. Lakini hila za aliyemuumba Eva, na ndiye huyo huyo aliyemwambia ale ili ampe adamu amuaminishe kuwa hatakufa ili ale ndio zilimuingiza Adamu Mkenge, kula tunda la sumu, lenye kuua taratibu kizazi cha Adamu mpaka hivi leo. Bado hujaona kifo ni mradi wa viumbe fulani?

Baadaye tunapata habari za Nyoka akimdanganya Hawa/Eva ili akampe lile tunda Adamu. Lile Tunda lisingekuwa na madhara yoyote kwa Eva/Hawa kama Adamu asingelila. Mtihani ule ulikuwa unamhusu Eva/ Hawa. Hata hivyo Hawa/Eva hakudanganywa bali alifanya makusudi kwani tayari alikuwa anapewa oda na aliyemuumba(huyo aliyemwambia ampe mumewe lile tunda)

Nyoka(ambaye sio huyu atambaaye) ndiye alikuwa mmiliki wa ile Edeni. Kama Adamu alivyoambiwa atawale dunia.

Ili ujue Hawa/Eva alifanya kusudi kumuangamizA Adamu, angalia alivyoenda kumpa lile tunda Adamu ili alile, wala hakumpa maelezo yoyote kuhusu huko alikotoka zaidi ya kumwambia nimelila na lafaa kwa kula. Hakumwambia amekutana na nani. Habari hizo Adamu anakuja kuzifahamu baada ya Mungu kuja ambapo Eva/Hawa anasema kuwa amedanganywa na Nyoka, (Namuona Adamu akijiona mjinga akitumbua macho yake kama mtu asiyeamini kuwa kaangushwa bila kujua) Mungu akamwambia umeisikiliza sauti ya mke wako. Kumaanisha hakupaswa kumsikiliza bali yeye ndio asikilizwe.

Baadaye Adamu na Hawa wanatimuliwa Edeni, na kurudishwa Duniani tayari akiwa amekula tunda lenye sumu iuayo pole pole. Na Mmiliki wa Edeni anabaki kuwa mshindi.

Kilichokusudiwa kifanyike Edeni kimekamilika, Adamu hahitajiki tena Edeni hivyo kufukuzwa ndio suluhu.

Alifukuzwa, na hapo ndipo rasmi mwanadamu akaanza kukengeushwa na viumbe wa Mbinguni kwa kutumia mawakala zao waliopo huku duniani. Mara Mbinguni, mara peponi mara sijui Akhera.

Ati tutaishi na Mungu. Sirius! Kabla ya kuanguka hatukuishi na Mungu, hata sasa hatuishi na Mungu, na kamwe hatuishi na Mungu. Hata hao viumbe wengine hawajawahi kuishi na Mungu. Bali ni propaganda zao za kurubuni kizazi cha mwanadamu kzidi kuwa watumwa.

Nataka kusema nini?

Dunia haijawahi kuwa mbaya, ubaya unatokea nje. Bila Edeni pasingekuwa na mabaya yote yanayoendelea duniani. Edeni ndio kulikuwa na tatizo wala sio dunani.

Mbinguni wanaishi malaika, Mungu haishi Mbinguni wala haishi duniani.Mungu hana Anuani, popote yupo kwa wakati wote. Mungu hana Kiti cha Enzi. Mungu hana Ulinzi. Malaika ni viumbe walioumbwa kwa Mwanga mkali, wenye mfano wa mwanadamu lakini hawana miili kama yetu. Malaika wapo wa aina nyingi kulingana na kazi, maumbile, na Sifa. Wapo malaika wenye mbawa kuanzia mbili, tatu, nne, sita, kumi na mbili na kuendelea.

Huko Mbinguni ndipo matatizo yalipoanzia, Falme za Malaika zimegawanyika. Kuihubiri mbinguni ni kuidhalilisha dunia. Kuwatukuza Malaika ni kuwatukana wanadamu.

Ipo tabia baadhi ya wanadamu wanawaabudu viumbe waishio mbinguni kwani viumbe hao wamewaahidi mambo mazuri, wengine wakiahidiwa kupewa uzima wa milele, wengine kwenda mbinguni, wengine wanaabudu kwa majina wakina Mikael, sijui Gabriel, na Yesu ambao kimsingi hao sio Mungu.

Bali wao wamekuja kuwafanya wanadamu kama mateka, kama vile huku duniani nchi moja inavyoenda kutawala nchi zingine, tunaita Ukoloni na sasa Ukoloni mamboleo. Ndivyo na viumbe wa Mbinguni walivyofanikiwa kuwatalawa viumbe wa duniani yaani sisi wanadamu.

Wanadamu wanawaona malaika ni bora kuliko binadamu. Wanapaona Mbinguni ni bora kuliko duniani.

Ninachotaka kusema ni kuwa, mwanadamu alikuwa mkamilifu kabisa kabla hajakutana na hila za viumbe wa mbinguni, si ajabu hata Edeni ilikuwa hila za hao viumbe kwani wamejaliwa nguvu, uweza, akili na mamlaka ya kusema kitu kikawa.

Matatizo ya duniani hayataisha leo lakini atakayeyamaliza ni mwanadamu mwenyewe. Pale Mwanadamu atakapoacha kuwatumikia Viumbe wa mbinguni iwe ni malaika au mashetani ndio siku hiyo hiyo dunia hii itakombolewa.

Naamini, miaka ya hivi karibuni mwanadamu ataweza kukikabili kifo. Watu hawatakufa tena kutokana na matokeo ya kisayansi na tekonolojia. Kifo kitadhibitiwa.

Nafahamu kuwa kifo ilikuwa ni Mradi wa viumbe wa Mbinguni kumtawala mwanadamu. Lakini baada ya kifo kukidhibiti mamlaka ya mwanadamu itarejea kama ilivyomwanzo.

Kifo hakitadhibitiwa kwa kutamani kwenda Mbinguni. Watu wanachoshindwa kuelewa ni kuwa Kifo kimeletwa na viumbe hao hao wa mbinguni.

Sijajua Mungu yupo wapi kwa sasa, licha kuwa mahali popote yupo. Lakini hawezi ingilia mambo haya, mpaka siku ya hukumu.

Siku ya hukumu itafika pale ambapo Mwanadamu ataweza kukidhibiti Kifo.

Mbinguni sio salama kama watu wanavyofikiri.

Taikon nimemaliza, Leo sitaki maswali.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Unguja
Kusema tu Adam alitolewa duniani kupelekwa Edeni umechemka. Leta vithibitisho. Edeni ni duniani mkuu
 
USALAMA WA MBINGUNI BADO NI MDOGO

Na, Robert Heriel

Wakati Mungu anaumba Mradi wake wa Dunia aliumba kila kitu kikiwa chema kabisa. Hakuna ambacho kilikuwa na kasoro, kila kitu kilikuwa kimekamilika. Hivyo yeyote unayemuona hapa duniani ujue amekamilika yaani yuko full completely. Hii Propaganda ya kusema mwanadamu hajakamilika ni hila, njama, ulaghai wa viumbe wasio na asili ya binadamu.

Kabla sijaenda mbali, nieleze kwa kifupi namna Mradi huu wa Dunia ilivyoumbwa na Mungu. Mungu aliiumba dunia kwa mfumo wa kutegemeana (Ecosytem) yaani viumbe vinategemeana. Kutegemeana huku ndio kunakamilisha mradi mzima wa dunia. Katika Mradi huu kuna aina nyingi za viumbe kulingana na asili yao walivyoumbwa. Mathaalani; Wapo viumbe walioumbwa kwa Hewa, wapo walioumbwa kwa maji, wapo walioumbwa kwa moto, wapo walioumbwa kwa Mwanga/ nuru wapo walioumbwa kwa udongo, wapo walioumbwa kwa mchanganyiko wa mada zaidi ya moja yaani labada maji na udongo, au hewa na mwanga.

Hivyo naweza kusema viumbe wapo aina zifuatazo kulingana na malighafi zilizotumiwa kuwaumba:

1. Viumbe wa umaji
2. Viumbe wa Umoto
3. Viumbe wa Uhewa
4. Viumbe wa Udongo/umadini
5. Viumbe wa Unuru/umwanga
6. Viumbe waliochanganya malighafi kama mwanadamu ambaye amechanganya umaji (ikiwemo damu), udongo na uhewa (Roho) chochote kikipungua katika mchanganyiko huo basi maisha ya mwanadamu aypo mashakani.

Kila kiumbe kimepewa Miliki au ufalme wake na watakaokitumikia. Mwanadamu amepewa dunia, na vyote vilivyopo duniani ni mali yake na vinamtumiikia.

Nikirejea kwenye Mada.

Adamu aliumbwa Duniani ambapo kiasili ndio kwake. Baadaye Mungu Akamchukua huyo Mtu akampeleka (Edeni) ambapo kiasili sio Duniani. Kumbuka Adamu akitolewa Duniani kupelekwa Edeni alikuwa pekeake kwa mujibu wa maandiko.

Baadaye Mungu akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wa Adamu. Hii ni kumaanisha Eva/Hawa aliumbiwa Edeni. Najaribu kufikiri na kugundua kuwa Eva ni matokeo ya mchangiko wa malighafi za dunia na Edeni. Kupitia Ubavu wa Adamu, Eva alijipatia malighafi za dunia(udongo) na kupitia malighafi zingine zilitoka pale pale Edeni. Nadhani mpaka sasa unaweza anza kupata picha ya kuelewa tofauti baina ya mwanaume na mwanamke kiasili.

Lakini lazima tujiulize, wakati Mungu akiumba mradi wake mara zote alikuwa akikiri kuwa kila alichokifanya ni chema na hakika ilikuwa chema, lakini baada ya kumhamisha Adamu na kumpeleka Bustani ya Edeni ni kwa nini mawazo yake yalibadilika na kusema "Si vyema" "huyu mtu awe pekeake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye" na hapo ndipo akamuumba Hawa/Eva kupitia ubavu wake. Hii ni kumaanisha Kwa duniani Adamu ilikuwa vyema kuwa pekeake wakati Edeni haikuwa Vyema.

Lakini hapa panaweza kuleta hitilafu kwenye kufikiri, je ni Mungu huyo huyo aliyesema kila kitu ni chema na sasa amebalisha mawazo? Mbona Mungu sio kigeugeu?

Akili yangu inaenda nisikokujua inafikiri hivi, huenda Aliyemuumba Adamu siye aliyemuumba Hawa. Kwanini ninafikiri hivi? Pengine niseme sijui. Embu tuone.

Nafikiri Hawa aliumbwa kwa njama, hila, za Kumuangusha Adamu. Kumbuka Adamu kwake ni duniani, wala sio Edeni. Edeni ilikuwa inamwenyewe, je ni nani huyo?

Embu ona, Adamu analetwa tuu Edeni hapo hapo anapewa sheria ya kutokula Tunda la Mti wa Kati wa ujuzi wa mema na mabaya. Fikiria hapo! Punde anaumbwa Hawa/Eva kisha aliyeumbwa muda huo huo anakuwa wakwanza kula tunda. Bado hujashtuka. Akili yako inakuambia nini kuhusu aliyemwambia Adamu asile matunda ya mti wa kati wa ujuzi wa Mema na Mabaya kwani atakufa? Kisha aliyeumbwa Edeni anakula hilo tunda na anaenda kwa adamu akiwa hajafa, huoni adamu angeona aliyesema ukila utakufa angekuwa muongo? Kumbuka Mlengwa wa lile tunda kula hakuwa Hawa/Eva bali alikuwa adamu. Kama Adamu asingekula lile tunda ni wazi Eva asingepata madhara. Lakini hila za aliyemuumba Eva, na ndiye huyo huyo aliyemwambia ale ili ampe adamu amuaminishe kuwa hatakufa ili ale ndio zilimuingiza Adamu Mkenge, kula tunda la sumu, lenye kuua taratibu kizazi cha Adamu mpaka hivi leo. Bado hujaona kifo ni mradi wa viumbe fulani?

Baadaye tunapata habari za Nyoka akimdanganya Hawa/Eva ili akampe lile tunda Adamu. Lile Tunda lisingekuwa na madhara yoyote kwa Eva/Hawa kama Adamu asingelila. Mtihani ule ulikuwa unamhusu Eva/ Hawa. Hata hivyo Hawa/Eva hakudanganywa bali alifanya makusudi kwani tayari alikuwa anapewa oda na aliyemuumba(huyo aliyemwambia ampe mumewe lile tunda)

Nyoka(ambaye sio huyu atambaaye) ndiye alikuwa mmiliki wa ile Edeni. Kama Adamu alivyoambiwa atawale dunia.

Ili ujue Hawa/Eva alifanya kusudi kumuangamizA Adamu, angalia alivyoenda kumpa lile tunda Adamu ili alile, wala hakumpa maelezo yoyote kuhusu huko alikotoka zaidi ya kumwambia nimelila na lafaa kwa kula. Hakumwambia amekutana na nani. Habari hizo Adamu anakuja kuzifahamu baada ya Mungu kuja ambapo Eva/Hawa anasema kuwa amedanganywa na Nyoka, (Namuona Adamu akijiona mjinga akitumbua macho yake kama mtu asiyeamini kuwa kaangushwa bila kujua) Mungu akamwambia umeisikiliza sauti ya mke wako. Kumaanisha hakupaswa kumsikiliza bali yeye ndio asikilizwe.

Baadaye Adamu na Hawa wanatimuliwa Edeni, na kurudishwa Duniani tayari akiwa amekula tunda lenye sumu iuayo pole pole. Na Mmiliki wa Edeni anabaki kuwa mshindi.

Kilichokusudiwa kifanyike Edeni kimekamilika, Adamu hahitajiki tena Edeni hivyo kufukuzwa ndio suluhu.

Alifukuzwa, na hapo ndipo rasmi mwanadamu akaanza kukengeushwa na viumbe wa Mbinguni kwa kutumia mawakala zao waliopo huku duniani. Mara Mbinguni, mara peponi mara sijui Akhera.

Ati tutaishi na Mungu. Sirius! Kabla ya kuanguka hatukuishi na Mungu, hata sasa hatuishi na Mungu, na kamwe hatuishi na Mungu. Hata hao viumbe wengine hawajawahi kuishi na Mungu. Bali ni propaganda zao za kurubuni kizazi cha mwanadamu kzidi kuwa watumwa.

Nataka kusema nini?

Dunia haijawahi kuwa mbaya, ubaya unatokea nje. Bila Edeni pasingekuwa na mabaya yote yanayoendelea duniani. Edeni ndio kulikuwa na tatizo wala sio dunani.

Mbinguni wanaishi malaika, Mungu haishi Mbinguni wala haishi duniani.Mungu hana Anuani, popote yupo kwa wakati wote. Mungu hana Kiti cha Enzi. Mungu hana Ulinzi. Malaika ni viumbe walioumbwa kwa Mwanga mkali, wenye mfano wa mwanadamu lakini hawana miili kama yetu. Malaika wapo wa aina nyingi kulingana na kazi, maumbile, na Sifa. Wapo malaika wenye mbawa kuanzia mbili, tatu, nne, sita, kumi na mbili na kuendelea.

Huko Mbinguni ndipo matatizo yalipoanzia, Falme za Malaika zimegawanyika. Kuihubiri mbinguni ni kuidhalilisha dunia. Kuwatukuza Malaika ni kuwatukana wanadamu.

Ipo tabia baadhi ya wanadamu wanawaabudu viumbe waishio mbinguni kwani viumbe hao wamewaahidi mambo mazuri, wengine wakiahidiwa kupewa uzima wa milele, wengine kwenda mbinguni, wengine wanaabudu kwa majina wakina Mikael, sijui Gabriel, na Yesu ambao kimsingi hao sio Mungu.

Bali wao wamekuja kuwafanya wanadamu kama mateka, kama vile huku duniani nchi moja inavyoenda kutawala nchi zingine, tunaita Ukoloni na sasa Ukoloni mamboleo. Ndivyo na viumbe wa Mbinguni walivyofanikiwa kuwatalawa viumbe wa duniani yaani sisi wanadamu.

Wanadamu wanawaona malaika ni bora kuliko binadamu. Wanapaona Mbinguni ni bora kuliko duniani.

Ninachotaka kusema ni kuwa, mwanadamu alikuwa mkamilifu kabisa kabla hajakutana na hila za viumbe wa mbinguni, si ajabu hata Edeni ilikuwa hila za hao viumbe kwani wamejaliwa nguvu, uweza, akili na mamlaka ya kusema kitu kikawa.

Matatizo ya duniani hayataisha leo lakini atakayeyamaliza ni mwanadamu mwenyewe. Pale Mwanadamu atakapoacha kuwatumikia Viumbe wa mbinguni iwe ni malaika au mashetani ndio siku hiyo hiyo dunia hii itakombolewa.

Naamini, miaka ya hivi karibuni mwanadamu ataweza kukikabili kifo. Watu hawatakufa tena kutokana na matokeo ya kisayansi na tekonolojia. Kifo kitadhibitiwa.

Nafahamu kuwa kifo ilikuwa ni Mradi wa viumbe wa Mbinguni kumtawala mwanadamu. Lakini baada ya kifo kukidhibiti mamlaka ya mwanadamu itarejea kama ilivyomwanzo.

Kifo hakitadhibitiwa kwa kutamani kwenda Mbinguni. Watu wanachoshindwa kuelewa ni kuwa Kifo kimeletwa na viumbe hao hao wa mbinguni.

Sijajua Mungu yupo wapi kwa sasa, licha kuwa mahali popote yupo. Lakini hawezi ingilia mambo haya, mpaka siku ya hukumu.

Siku ya hukumu itafika pale ambapo Mwanadamu ataweza kukidhibiti Kifo.

Mbinguni sio salama kama watu wanavyofikiri.

Taikon nimemaliza, Leo sitaki maswali.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa Unguja
Robert, I wish ningekuona tukakaa nikakupa elimu sahihi ya Biblia.You have some knowledge of the Bible,lakini kuna gaps nyingi na heresy.You also seem to have a lot of interest in knowing the Bible,but you lack the Holy Spirit, who leads believers to all truth.

What are you supposed to do?Receive Jesus Christ as your personal saviour.By doing that ,you will receive the Holy Spirit,who will then guide you to all truth, including assuring you that Heaven is our real home and indeed the safest and most beautiful place to be.Mkuu ukisema Mbinguni sio salama,hata Shetani anakucheka,because he was there and he knows it.
 
Back
Top Bottom