Kwa kweli tuache masihala mbilia beli amekwisha mpaka kuifikia kutumbuiza police mess mara Bukoba mwana mama ambaye alikuwa anatingisha barani afrika nakumbuka alipokuja hapa bongo na mzee Tabu rey sikuwa mdogo sana lakini balaa lake lilikuwa kubwa kama si daimon basi ilikuwa uwanja wa taifa mtu kibao lakini kosa lake ni kumtoroka mzee huyu na kwenda kwa kwenye bendi ya Mtoto wa Omar bongo kule gabon nakumbuka mzee Tabu rey iliripotiwa na vyombo vya habari kuwa alilazwa hospitali kwa mshituko!! kama ni duwa la kuku sasa limempata hebu fikiria toka katika makumbi mbalimbalitena makubwa huko paris france leo bukoba mara police mess bado kidogo tutasikia kimboka nighty pub buguruni jamani mi naomba mshaurini apumzike mziki atafute kazi nyingine iko siku atapelekwa mpanda halafu aachwe kama defao alivyopelekwa Rukwa halafu nauli ya kurudi ikawa shida hebu waige mfano wa wanamuziki wa amerika akichacha anachili home hii mipango ya kutumbuiza toka parisi mpaka Mtwara fedhea harafu kule unafikia Urimbo gest hausi bafu la jumuiya yaaaani jamani huruma akamwombe msamaa mzee Tabu rey wadau mnasemaje katika hili naomba maoni yenu!!