Mbezi Beach barabara zinatutesa, mbunge wetu na madiwani mpo likizo?

Lole Gwakisa

JF-Expert Member
Nov 5, 2008
4,728
2,259
Kwa muda mrefu sasa barabara za Mbezi Beach, tena eneo lote halipati matunzo yanayostahili eneo hili.

Barabara karibu zote ni mbovu kupundukia.
Ukiacha barabara mbili tu zilizojengwa zaidi ya miaka mitano iliyopita, hakuna chochote kinachofanyika, na barabara hizo ni Ally Sykes na ile ya Kawe-Africana.

Kuna barabara nyingi tu ambazo kuzitumia ni kero kubwa, na barabara hizo ni:
-Mbezi Garden hadi Baraza la mitihani
-Barabara ya kuelekea NSSF flats(inaungana na barabara ya Kawe/Africana)
-River rd kwenda shule ya St Marys
-Barabara ya kuunganisha Kunduchi na eneo la Kilongawima
-barabara ya Mbezi Jogoo

Pamoja na barabara hizo kuna ile barabara ambayo ni mfupa uliowashinda wengi, barabara ya Mbezi Samaki Wabichi hadi Goba.

Inabidi tuandike kwa masikitiko juu ya barabara hizi maana katika wilaya nyingine kama Ilala na Temeke kazi kubwa inafanyika, na mimi mwenyewe nimepita Temeke kwa kweli juhudi za wilaya hiyo kujenga hadi vichochoroni inatiamoyo-hongera Mbunge wa eneo hilo.

Kule Oysterbay lami inatandikwa hadi barabara ndogo kabisa zenye kuhudumia watu si zaidi ya kumi!

Na hapo ndio nawageukia wawakilishi wetu, mnatuteteaje kwenye vikao vyenu?
Mbona wala hatusikii kuwa barabara nillizotaja ziko kwenye mpango wa kujengwa?
Msituangushe wawakilishi wetu
 
Hapo mchangia mada umegusa penyewe kabisa, mi ni mkazi ninayeishi mbezi juu, ninatumia moja ya barabara uliyoitaja (Mbezi garden-Baraza la mitihani). Barabara hii haijawahi kufanyiwa hata marekebisho madogo tu kwa muda mrefu sana. Ukitoka makonde baada ya kuacha junction ya St Marys na baraza la mitihani ukiingia kulia hali ni mbaya zaidi. Njia hii ina mahandaki makubwa ambayo mbuzi wanaweza kujificha na hali inakuwa mbaya zaidi kwa sababu kuna mto Ndumbwi ambao hauna daraja. Mvua zikinyesha sehemu hiyo haipitiki kwa muda na inabidi kusubiri hadi maji yapite au kuzunguka umbali mrefu (kupitia Afrikana)

Tunaomba wahusika (madiwani na mh mbunge) waangalie hali hii kwani inatukatisha tamaa wakazi wa maeneo haya.
 
Wamechaguliwa wanajaza kwanza matumbo yao watatukumbuka 2015 kwenye uchaguzi mkuu
 
huko viwanja si ndiyo mil 800 sasa hata barabara inawashinda

Mkuu tunatakiwa vilevile kujua kuwa barabara ni zetu si za wabunge, kwanini watu wa Mbezi ambao wanadiriki kununua kiwanja shili milioni 800, hawakubali kutoa milioni 100 kila mmjoja na kusimamia kujenga barabara zao. Hapa unaweza kusema kuwa kuna wakati tunawaonea wabunge.

Sidhani kama Halima Mdee ana uwezo wa kutengeneza barabara zaidi ya kukodisha Grader kukwangua barabara, kitu kinachofanya barabara iwe mbaya zaidi pale mvua inaponyesha.
 
Aliyekuiambia barabara zinajengwa na wabunge na madiwani ni nani?
Kwa muda mrefu sasa barabara za Mbezi Beach, tena eneo lote halipati matunzo yanayostahili eneo hili.

Barabara karibu zote ni mbovu kupundukia.
Ukiacha barabara mbili tu zilizojengwa zaidi ya miaka mitano iliyopita, hakuna chochote kinachofanyika, na barabara hizo ni Ally Sykes na ile ya Kawe-Africana.

Kuna barabara nyingi tu ambazo kuzitumia ni kero kubwa, na barabara hizo ni:
-Mbezi Garden hadi Baraza la mitihani
-Barabara ya kuelekea NSSF flats(inaungana na barabara ya Kawe/Africana)
-River rd kwenda shule ya St Marys
-Barabara ya kuunganisha Kunduchi na eneo la Kilongawima
-barabara ya Mbezi Jogoo

Pamoja na barabara hizo kuna ile barabara ambayo ni mfupa uliowashinda wengi, barabara ya Mbezi Samaki Wabichi hadi Goba.

Inabidi tuandike kwa masikitiko juu ya barabara hizi maana katika wilaya nyingine kama Ilala na Temeke kazi kubwa inafanyika, na mimi mwenyewe nimepita Temeke kwa kweli juhudi za wilaya hiyo kujenga hadi vichochoroni inatiamoyo-hongera Mbunge wa eneo hilo.

Kule Oysterbay lami inatandikwa hadi barabara ndogo kabisa zenye kuhudumia watu si zaidi ya kumi!

Na hapo ndio nawageukia wawakilishi wetu, mnatuteteaje kwenye vikao vyenu?
Mbona wala hatusikii kuwa barabara nillizotaja ziko kwenye mpango wa kujengwa?
Msituangushe wawakilishi wetu
 
Mkuu tunatakiwa vilevile kujua kuwa barabara ni zetu si za wabunge, kwanini watu wa Mbezi ambao wanadiriki kununua kiwanja shili milioni 800, hawakubali kutoa milioni 100 kila mmjoja na kusimamia kujenga barabara zao. Hapa unaweza kusema kuwa kuna wakati tunawaonea wabunge.

Sidhani kama Halima Mdee ana uwezo wa kutengeneza barabara zaidi ya kukodisha Grader kukwangua barabara, kitu kinachofanya barabara iwe mbaya zaidi pale mvua inaponyesha.

Pale Mbezi namfahamu jamaa ambaye kwa zaidi ya miaka kumi amekuwa akitengeneza barabara ya Mbezi Garden kwenda juu, na hata ili ya Mbezi Jogoo akiwasirikisha wakazi wengine.

Sehemu nyingine wananchi vile vile wamekuwa wakijitilea kukarabati mitaro ya maji ya mvua.

Hata hivyo susla si hilo, suala ni ushiriko wa halmashauri yetu kujenga upya barabara hizo kwa kiwango cha lami.
 
Aliyekuiambia barabara zinajengwa na wabunge na madiwani ni nani?

Katika nchi ya demokrasia kama yetu, wawakilishi wana jukumu kubwa ya kuhakikisha keki ya maendeleo inawafikia wananchi wote, na si sehemu moja tu.

Nimeandika thread hii baada ya kutembelea wilaya zote tatu za DSM na kuona maendeleo huko yanavyopamba moto katika ujenzi wa barabara.

Wilaya ya Temeke pitia mitaa ya Tandika, sehemu za Sterio utaona barabara zilvyo karabtiwa na kutiwa lami vizuri.
Achilia mbali barabara ya Yombo ambayo imefungua Jiji kwa sehemu hiyo.

Huko Oysterbay na Masaki barabara zinawekwa lami hadi mitaa ya kuhudumia si zaidi ya nyumba kumi mfano mtaa wa Mzinga, na mitaa yote ya karibu, mitaa ya Yatch Club na Slipway, Lincoln st na Mkadini. hizi zote ni barabara ndogo lakini zemewekwa lami.

Ndio maana tunauliza sisi haya mapot holes mpaka lini?
Sote tunalipa kodi au siyo.

Nampongeza sana Mb Mtemvu wa Temeke maana niliona wakati mmoja akitetea kwa uchungu barabara za wilaya yake, matokeo tunayaona.

Mb Mtemvu anaishi Mbezi karibu na babara moja mbovu niliyoitaja, hebu tunaomba awasiliane na mbunge mwenziwe ampe mbinu.
 
Kwa muda mrefu sasa barabara za Mbezi Beach, tena eneo lote halipati matunzo yanayostahili eneo hili.

Barabara karibu zote ni mbovu kupundukia.
Ukiacha barabara mbili tu zilizojengwa zaidi ya miaka mitano iliyopita, hakuna chochote kinachofanyika, na barabara hizo ni Ally Sykes na ile ya Kawe-Africana.

Kuna barabara nyingi tu ambazo kuzitumia ni kero kubwa, na barabara hizo ni:
-Mbezi Garden hadi Baraza la mitihani
-Barabara ya kuelekea NSSF flats(inaungana na barabara ya Kawe/Africana)
-River rd kwenda shule ya St Marys
-Barabara ya kuunganisha Kunduchi na eneo la Kilongawima
-barabara ya Mbezi Jogoo

Pamoja na barabara hizo kuna ile barabara ambayo ni mfupa uliowashinda wengi, barabara ya Mbezi Samaki Wabichi hadi Goba.

Inabidi tuandike kwa masikitiko juu ya barabara hizi maana katika wilaya nyingine kama Ilala na Temeke kazi kubwa inafanyika, na mimi mwenyewe nimepita Temeke kwa kweli juhudi za wilaya hiyo kujenga hadi vichochoroni inatiamoyo-hongera Mbunge wa eneo hilo.

Kule Oysterbay lami inatandikwa hadi barabara ndogo kabisa zenye kuhudumia watu si zaidi ya kumi!

Na hapo ndio nawageukia wawakilishi wetu, mnatuteteaje kwenye vikao vyenu?
Mbona wala hatusikii kuwa barabara nillizotaja ziko kwenye mpango wa kujengwa?
Msituangushe wawakilishi wetu

Mbezi beach si ile mbezi beach ya ukweli, hainatofauti na sinza kumbe za harusi kila kona, makanisa uchwara kila kona(jumapili hata kulala ndani issue ni mapambio kwa kwenda mbele), vi pub ndio usiseme

Hizo barabara nani aje akutengeneze kama matatizo hayo hapo juu hawayaoni?
 
Hapo mchangia mada umegusa penyewe kabisa, mi ni mkazi ninayeishi mbezi juu, ninatumia moja ya barabara uliyoitaja (Mbezi garden-Baraza la mitihani). Barabara hii haijawahi kufanyiwa hata marekebisho madogo tu kwa muda mrefu sana. Ukitoka makonde baada ya kuacha junction ya St Marys na baraza la mitihani ukiingia kulia hali ni mbaya zaidi. Njia hii ina mahandaki makubwa ambayo mbuzi wanaweza kujificha na hali inakuwa mbaya zaidi kwa sababu kuna mto Ndumbwi ambao hauna daraja. Mvua zikinyesha sehemu hiyo haipitiki kwa muda na inabidi kusubiri hadi maji yapite au kuzunguka umbali mrefu (kupitia Afrikana)

Tunaomba wahusika (madiwani na mh mbunge) waangalie hali hii kwani inatukatisha tamaa wakazi wa maeneo haya.
GREGORY J

Nimejikuta nacheka! ... waswahili kwa kukuza mambo! ... hawajambo! ...

Yaani mpaka Mbuzi wanajificha kwenye mashimo ya barabarani!
 
Mbezi beach si ile mbezi beach ya ukweli, hainatofauti na sinza kumbe za harusi kila kona, makanisa uchwara kila kona(jumapili hata kulala ndani issue ni mapambio kwa kwenda mbele), vi pub ndio usiseme

Hizo barabara nani aje akutengeneze kama matatizo hayo hapo juu hawayaoni?
Acha madharau bwana, huko wanaishi watu wa hali zote, naona jina la Beach linakupa matatizo yanayoibua inferiority complex kwako.

Kwa taarifa yako kuna watu wa kila aina Mbezi Beach , mtajiri, wa kati na wa hali ya chini kabisa.

Kama wananchi wanahitaji huduma bora kama wenzao wa sehemu zingine za mji wa DSm.

Hilo la maknisa uchwara ni la kwako mdhambi maana sitegemei hilo kutoka kwenye mtu mwenye akili ya kumwogopa Mungu.

Kuna kumbi nyingi za starehe na harusi , hilo tu linaifanya sehemu hii iwe na umuhimu pekee wa huduma za miundombinu kama barabara.

Wewe Watu, inaelekea una moyo unaitwa wa korosho, moyo ambao una kijocho, moyo usiopendelea maendeleo ya wengine.
Sitashangaa kama wewe mwenyewe huna maisha ya kuigwa.
 
Hata kama watu wa mbezi beach wangekuwa na uwezo bado viongozi walikuwa na jukumu la kuwaunganisha kuchangia maendeleo yao. Labda viongozi hawapo, wako huko makwao labda nje ya Kawe
 
Hapo mchangia mada umegusa penyewe kabisa, mi ni mkazi ninayeishi mbezi juu, ninatumia moja ya barabara uliyoitaja (Mbezi garden-Baraza la mitihani). Barabara hii haijawahi kufanyiwa hata marekebisho madogo tu kwa muda mrefu sana. Ukitoka makonde baada ya kuacha junction ya St Marys na baraza la mitihani ukiingia kulia hali ni mbaya zaidi. Njia hii ina mahandaki makubwa ambayo mbuzi wanaweza kujificha na hali inakuwa mbaya zaidi kwa sababu kuna mto Ndumbwi ambao hauna daraja. Mvua zikinyesha sehemu hiyo haipitiki kwa muda na inabidi kusubiri hadi maji yapite au kuzunguka umbali mrefu (kupitia Afrikana)

Tunaomba wahusika (madiwani na mh mbunge) waangalie hali hii kwani inatukatisha tamaa wakazi wa maeneo haya.

Ni bora mpige kelele la sivyo mtaambulia mahandaki tu el nino yaja. Barabara ya samaki-Goba- Mbezi Louis ilikuwa ianze kujengwa baada ya ile ya Ally sykes kutoka BP kwenda baharini kujengwa. Hii ilitolewa na mbunge Rita Mlaki na Massawe (mkuu wa Wilaya) enzi hizo. Mpaka leo hakuna dalili. Mbunge, madiwani mko wapi? Kura hamzitaki 2015? Kufanikiwa mahali popote duniani ni lazima upige kelele upigani upande wako mpaka kieleweke.
 
Mkuu tunatakiwa vilevile kujua kuwa barabara ni zetu si za wabunge, kwanini watu wa Mbezi ambao wanadiriki kununua kiwanja shili milioni 800, hawakubali kutoa milioni 100 kila mmjoja na kusimamia kujenga barabara zao. Hapa unaweza kusema kuwa kuna wakati tunawaonea wabunge.

Sidhani kama Halima Mdee ana uwezo wa kutengeneza barabara zaidi ya kukodisha Grader kukwangua barabara, kitu kinachofanya barabara iwe mbaya zaidi pale mvua inaponyesha.

Barabara ya Samaki mpaka Mbezi Mwisho (Loius) ni muhimu sana sana kuwekwa lami. Ni kiungo kizuri sana cha kupunguza foleni ya Ubungo kwa watu wa Mbezi beach na Tegeta!
 
Hivi nafasi ya meya katika masuala hayo ni ipi?

Na meya wa Kinondoni ni nani? Na ameshafanya nini?

Nijuavyo mimi hata meya ni mtu wa kuchaguliwa na watu, kwanza kama diwani, kisha anachaguliwa na madiwani kuwa meya. Nijuavyo pia Meya ndiye msimamizi mkuu wa miradi ya ujenzi wa barabara katika eneo la mji wake na ana bajeti inayotumwa kwa halmashauri yake toka kwenye kodi zetu.

Mbona tunazunguka na meya yupo?
 
Back
Top Bottom