Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,144
Mbeya wamuuliza JK: Wafe wangapi ndipo hatua zichukuliwe?
Kituo cha Polisi Kyela chafananishwa na duka
Wasema Polisi hawawezi kujichunguza, iundwe tume huru
SI rahisi kuamini, lakini huo ndiyo ukweli wenyewe; kwamba wananchi katika Wilaya ya Kyela, mkoani Mbeya, wanakifananisha kituo cha polisi kilichopo mjini humo na duka. "Kile sio kituo cha polisi, ni duka lile. Ni kituo cha biashara. Wakati wanamkamata Lucas siku ile alikuwa na pesa nyingi, unajua Wapemba wengi wanaokuja kununua mchele huku walimwamini, walikuwa wanamwachia pesa awanunulie mchele.
"Alipokamatwa, ile pesa alimpa mwenzie ampelekee nyumbani na kusema hawa (polisi) nitamalizana nao," anasema mkazi mmoja wa Kyela aliyekuwa akifahamiana na Lucas kwa muda mrefu.
Inaaminika kuwa hatua ya marehemu kumwagiza mwenzake apeleke ile pesa nyumbani wakati akikamatwa; ndiyo iliyowaudhi wale askari polisi waliomkamata ambao pia wanadaiwa kumpiga; licha ya marehemu kuwatahadharisha kuwa alikuwa mgonjwa. Mtanzamo wa wananchi kadhaa waliohojiwa hivi karibuni na Raia Mwema, mjini Kyela, kuhusu kituo hicho cha polisi, ni kwamba ni sehemu ya kuendeshea 'biashara'.
Hisia hizo zipo pia kwa vituo vya polisi katika miji ya Tukuyu wilayani Rungwe na Tunduma wilayani Mbozi, ulipo mpakani mwa Tanzania na Zambia .
Sio kusudio la makala hii kuingia kwa undani kuhusu sakata la Kyela na Tunduma; kwa sababu tayari vyombo husika vinalishughulikia, lakini ni matukio yanayodhihirisha jambo moja la msingi. Jambo hilo ni kwamba wananchi sasa wamekosa imani na vituo vya polisi, na hali hii yawezekana ipo pia sehemu zingine nchini.
Hatua ya wananchi kukosa imani na baadhi ya vituo vya polisi nchini ndiyo inayoelezwa kuwa chanzo cha matukio ya vurugu hizo za hivi karibuni katika miji ya Tunduma na Kyela mkoani Mbeya kwa wananchi kupambana na askari polisi.
Katika toleo la Raia Mwema Na. 75 la Aprili 1-7, mwaka huu, kulikuwa na makala iliyokuwa na kichwa cha habari "Mbeya wamtahadharisha Kikwete," ambayo ilitokana na kauli za wananchi wa Kyela baada ya Jeshi la Polisi wilayani humo kuwazuia kufanya maandamano yao pasipo sababu za msingi. Mwananchi mmoja alinukuliwa kwenye makala ile akisema "Tunakoelekea ni kubaya na wa kulaumiwa ni Rais Jakaya Kikwete mwenyewe kwani ameigawa Kyela." Hatuhitaji tena tahadhari nyingine ya mdomo au maandishi; kwani matukio haya mawili ya hivi karibuni katika miji ya Kyela na Tunduma, ni tahadhari ya vitendo kwamba nchi inaelekea kubaya; kwani kuvurugika kwa amani katika sehemu moja ya nchi ni mwanzo wa taifa kuingia kwenye machafuko makubwa.
Mwandishi Wetu, Kyela
Julai 29, 2009SI rahisi kuamini, lakini huo ndiyo ukweli wenyewe; kwamba wananchi katika Wilaya ya Kyela, mkoani Mbeya, wanakifananisha kituo cha polisi kilichopo mjini humo na duka. "Kile sio kituo cha polisi, ni duka lile. Ni kituo cha biashara. Wakati wanamkamata Lucas siku ile alikuwa na pesa nyingi, unajua Wapemba wengi wanaokuja kununua mchele huku walimwamini, walikuwa wanamwachia pesa awanunulie mchele.
"Alipokamatwa, ile pesa alimpa mwenzie ampelekee nyumbani na kusema hawa (polisi) nitamalizana nao," anasema mkazi mmoja wa Kyela aliyekuwa akifahamiana na Lucas kwa muda mrefu.
Inaaminika kuwa hatua ya marehemu kumwagiza mwenzake apeleke ile pesa nyumbani wakati akikamatwa; ndiyo iliyowaudhi wale askari polisi waliomkamata ambao pia wanadaiwa kumpiga; licha ya marehemu kuwatahadharisha kuwa alikuwa mgonjwa. Mtanzamo wa wananchi kadhaa waliohojiwa hivi karibuni na Raia Mwema, mjini Kyela, kuhusu kituo hicho cha polisi, ni kwamba ni sehemu ya kuendeshea 'biashara'.
Hisia hizo zipo pia kwa vituo vya polisi katika miji ya Tukuyu wilayani Rungwe na Tunduma wilayani Mbozi, ulipo mpakani mwa Tanzania na Zambia .
Sio kusudio la makala hii kuingia kwa undani kuhusu sakata la Kyela na Tunduma; kwa sababu tayari vyombo husika vinalishughulikia, lakini ni matukio yanayodhihirisha jambo moja la msingi. Jambo hilo ni kwamba wananchi sasa wamekosa imani na vituo vya polisi, na hali hii yawezekana ipo pia sehemu zingine nchini.
Hatua ya wananchi kukosa imani na baadhi ya vituo vya polisi nchini ndiyo inayoelezwa kuwa chanzo cha matukio ya vurugu hizo za hivi karibuni katika miji ya Tunduma na Kyela mkoani Mbeya kwa wananchi kupambana na askari polisi.
Katika toleo la Raia Mwema Na. 75 la Aprili 1-7, mwaka huu, kulikuwa na makala iliyokuwa na kichwa cha habari "Mbeya wamtahadharisha Kikwete," ambayo ilitokana na kauli za wananchi wa Kyela baada ya Jeshi la Polisi wilayani humo kuwazuia kufanya maandamano yao pasipo sababu za msingi. Mwananchi mmoja alinukuliwa kwenye makala ile akisema "Tunakoelekea ni kubaya na wa kulaumiwa ni Rais Jakaya Kikwete mwenyewe kwani ameigawa Kyela." Hatuhitaji tena tahadhari nyingine ya mdomo au maandishi; kwani matukio haya mawili ya hivi karibuni katika miji ya Kyela na Tunduma, ni tahadhari ya vitendo kwamba nchi inaelekea kubaya; kwani kuvurugika kwa amani katika sehemu moja ya nchi ni mwanzo wa taifa kuingia kwenye machafuko makubwa.