Mbeya waichezesha kwata CCM - Mawaziri wazomewa

Mbunge wa jimbo la Kilombero Mh Castor Ligallama Juzi alipata joto la jiwe baada ya wananchi kususia mkutano wake wa hadhara maeneo ya Kiugani hapa mjini Ifakara. Maandalizi ya kualika watu wakamsikilize mbuge huyo yalifanyika kwa juhudi za aina yake, matangazo yalitolewa kanisani baada ya Ibada za misa, Kwenye misikiti na magari yaliyokuwa na vipaza sauti na matangazo lukuki. Cha kushangaza ni watu wachache sana walioweza kufika pale kwenye viwanja vya kiungani, na hao waliofika walikuwa wakimzomea sana bw Ligalama kwa maneno ya wala rushwa nyie, mafisadi, sumu, mara Buzwagi na mara nyingi walikuwa wamwita Zitto Kabwe. Hali hii ilimfadhaisha sana mbuge, polisi walijitahidi sana kuzuia fujo, Bwana Ligallama hakuweza kuhutubia wananchi ndipo alipoamua kwenda kuhutubia kwenye soko la mjini Ifakara ambako pia alizomewa sana, alisisikika akiwaambia wananchi jamani mimi ni mbuge wenu natoka kwenye chama kilichopo madarakani, naomba mnisikilize nina majibu ya kero zenu. Wananchi walijaa jazba na hakuweza kuwahutumbia. Cha ajabu Ifakara kuna waandishi wengi wa habari wa vyombo mbali mbali habari hii wala haikutangazwa!! Nafikiri wakati umefika wananchi wameanza kujua kweli na wapo tayari kutafuta haki zao, zile kauli mbiu za maisha bora wamepata tafsiri ya kuwekewa mchanga wa macho wakistuka mafisadi wamechukua nchi na umasikini uliokubuhu kwa wananchi waliwaji ukiendelea. Aluta continua ipo siku watarusha mawe na kuingia msituni kutafuta wanachokitaka. zile nyimbo za kijinga nchi yetu ni kisiwa cha amani na ujinga zitapotea iwe historia.
 
Kuna Haja ya wana JF kuhamasisha marafiki zetu popote walipo huko nyumbani kujiunga na JF ili kama habari haikuripotiwa na media zetu basi wenzetu watupe habari tujue kinachoondelea.

Kwa kuanza nimeshashawishi vijana watatu kijini kwangu wajiunge na mtandao maana siku moja moja wanaweza kupata nafasi kuingia cyber cafe watupe yanayojiri huko.
 
bwana huna hata digital camera jamani ya kutuletea hata kaushaidi. wakina mtu wa pwani, kili time na kada watasema huo ni uzushi we utasikia tu

Tehetehe,,,

Demokrasi inakuwa jambo jema kwa taifa, sasa wale wa ushabiki ni jambo jema kuendelea,,, lakini kuna jambo zuri kwa upande wa chama tawala, waendelee kukubali kuulizwa maswali ili wajue jamii imebadilika,,, miaka iliyopita kiongozi anahutubia alafu anaondoka zake, siku hizi maswali yanaulizwa tena magumu, which is good for the nation!

Ingawa sio jambo la kujivunia kujenga utamaduni wa kuzomea, lakini wa ku-express ideas is a GREAT thing,

Tuzame mambo kwa mbali zaidi, katika uhai wa taifa hili kutakuwa na vyama tawala na chama pinzani, today may be CCM, tomorrow CHADEMA, the other year CUF, la muhimu ni kujenga jamii ambayo inavumiliana katika utoaji wa hoja....
 
Kilitime. it is true, leo ccm, kesho chadema n.k wananchi wanachotaka ni hoja sio bla bla. hata chadema nao wakikosa hoja, uzomeaji hautakoma. maana wananchi wanataka maendeleo bila kujali nani anayaleta.

Rafiki yangu mmoja leo kaniuliza, uchumi wa Nchi yako unategemea nini? nikamjibu kwa kifupi.

Tunayo madini (Dhahabu, Almasi na vito vya tahmani)
Tunayo Misitu karibu pande zote za nchi
Tunayo Maziwa makuu matatu
Tunayo bahari
Tunanyo Ardhi nzuri na kila aina ya mazao ulimwenguni yanastawi
Tunazo hifadhi za wanyama wa kila aina.
Tuna watu wa kutosha
Tuna Amani

Huyu rafiki akahamaki, akaniuliza tena, kwa hiyo Watanzania mna maisha mazuri sana, sasa kwa nini uko huku na mbona Tanzania Haijulikani kimataifa wakati ina utajiri mkubwa? nami nikamuuliza why?

Akaniambia chanzo kikuu cha uchumi ktk nchi yake (Algeria) ni mafuta na kidogo kilimo na zaidi matunda. sikuwa na jibu maana nilipata aibu.

Watu wetu Maskini wa kutupwa, hakuna miundo mbinu kama barabara, umeme n.k hakuna huduma nzuri za afya na pale ambapo zipo hakuna madawa. gharama za maisha zimepanda n.k

Yeyote asiyeweza kuboresha maisha yetu ni lazima azomewe ili akiondoka ainamishe kichwa chini au ajifanye kupokea simu kwa kuogopa aibu.
 
Kilitime. it is true, leo ccm, kesho chadema n.k wananchi wanachotaka ni hoja sio bla bla. hata chadema nao wakikosa hoja, uzomeaji hautakoma. maana wananchi wanataka maendeleo bila kujali nani anayaleta.

Rafiki yangu mmoja leo kaniuliza, uchumi wa Nchi yako unategemea nini? nikamjibu kwa kifupi.

Tunayo madini (Dhahabu, Almasi na vito vya tahmani)
Tunayo Misitu karibu pande zote za nchi
Tunayo Maziwa makuu matatu
Tunayo bahari
Tunanyo Ardhi nzuri na kila aina ya mazao ulimwenguni yanastawi
Tunazo hifadhi za wanyama wa kila aina.
Tuna watu wa kutosha
Tuna Amani

Huyu rafiki akahamaki, akaniuliza tena, kwa hiyo Watanzania mna maisha mazuri sana, sasa kwa nini uko huku na mbona Tanzania Haijulikani kimataifa wakati ina utajiri mkubwa? nami nikamuuliza why?

Akaniambia chanzo kikuu cha uchumi ktk nchi yake (Algeria) ni mafuta na kidogo kilimo na zaidi matunda. sikuwa na jibu maana nilipata aibu.

Watu wetu Maskini wa kutupwa, hakuna miundo mbinu kama barabara, umeme n.k hakuna huduma nzuri za afya na pale ambapo zipo hakuna madawa. gharama za maisha zimepanda n.k

Yeyote asiyeweza kuboresha maisha yetu ni lazima azomewe ili akiondoka ainamishe kichwa chini au ajifanye kupokea simu kwa kuogopa aibu.


Nikumbushe tu kama uliondoka nchini muda mrefu!

Bado nchi yetu watu hawafanyi kazi, waiting for government kuleta maisha bora!

Ikifika saa kumi na moja, nchi nzima usingizi, viwanda vinavyofanya kazi 24hrs vinahesabika,,, kwa hiyo hata tuwe na raslimali vipi kama ikifika saa kumi na moja tunasheherekea mafanikio kwenye grocery/pubs/baa na vichochoro vyote vinavyouza vinjwaji hatutaenda popote...

Ndio maana naihurumia hii nchi kwa kuwa sioni mwanasiasa anayesimama imara kusema pamoja na mambo mengine soluhisho la uchumi wetu ni pamoja na kuchapa kazi....

Mzee Mkapa alisema lakini wengine wemepuuza, mzee huyu alirudia kwamba mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, sasa serikali ya awamu ya nne badala ya kubuild on that foundation, wao wanasema watawaletea wananchi maendeleo, wapi na taifa gani linagawa maendeleo...

nikupe mfano,,, Tanzania ukitaka kufanya kazi kwenye mkoa mwingine kazi ya dakika tano,,, unalazimika kuharibu siku tatu za uzalishaji,..., siku ya kwenda,,, siku ya kazi, na siku ya kurudi,,, tatizo,,, ati mabasi yasisafiri usiku ni mchana tu...haya... amri ya Tangu mzee Malechela akiwa waziri mkuu mpaka sasa nobody revisited and challenged it... ati mpaka rais aseme... we have serious problem watanzania, sio la CCM au Rais na Baraza lake la mawaziri ... mindset zetu zimeganda....

Mh. mmoja anasema... ati mtu mwenye uwezo aliyesoma Academy school anaambia achangine 300,000/- university na yeye alazimisha serikali impe mkopo 100%, maana yake anazuia maskini mwingine kama mimi kupata nafasi ya kusoma... this is our country
 
Nakuunga mkono kilitime,

Mimi sijazamia huku, mara kwa mara hufika nyumbani, walau mara mbili kwa mwaka. hali ya nyumbani ninaijua vizuri. Arusha - Dodoma ni kama 460km hivi. lakini ukitaka kufika dodoma lazima uzunguke Chalinze - morogoro, zaidi ya 800km. tumelaaniwa sana.

Pamoja na uvivu wetu, bado kuna watu wenye nia ya dhati ya kufanya kazi. nina proposal yangu hadi leo inaozea kwenye kabati, kisa natakiwa nianze kwanza project ndipo nipewe mkopo. ukiomba serikali ikudhamini danadana kibao.

Foreigners wakija, wanapewa hata muda wa kutokulipa kodi. ndiyo maana watu wamekata tamaa. badala ya kufikiri miradi gani wafanye, wanaamua kuishia kwenye mitungi na hata utapeli usio na maana.

Bado hatuna viongozi waelekazaji kuelekea maendeleo ya kweli. hawajui kufundisha. na hata wakifundisha hafanyi kile wanachokifundisha. Mbona Baba wa Taifa watu walimwelewa na siasa ni kilimo na watu waliitikia kwa nguvu zao zote? kwa nini wao washindwe. kwa nini watu wakae vijiweni? je yatosha tu kusema ni wavivu? hivi kuna wavivu duniani kama jamii ya kiarabu? mbona kuanzia asubuhi hadi jioni wanashinda kunywa kahawa? mbona nchi zao zina maendeleo makubwa kuliko yetu? tukae tujiulize, lazima ipo sababu. Je sera zetu zinatekelezeka au ni za kuombea kura?
 
.......................Hivi huwa naona watu wengi wakimfagilia na kumpa 'u mr clean' Mwandosya, kama kweli yuko clean kwanini asijiengue kutoka kwa hao mafisadi? Na usomi wake wote, na kama yuko makini kwanini asisimame kidete kupinga kuburuzwa na PM kwa mwamvuli wa nidhamu ya chama?

PM na Mwandosya ni washikaji kwa saana saana...........just for your information!!
 
Zomeazomea yazidi

na Mwandishi Wetu


WAKATI Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, akikanusha taarifa zilizoandikwa na gazeti hili jana na jingine la kila siku, zinazoeleza kuhusu kuzomewa na wananchi wa Mbeya wakati wa mkutano wao wa hadhara uliofanyika juzi, waziri mwingine katika serikali ya Rais Jakaya Kikwete, alikutwa na zahama kama hiyo huko Mpanda, mkoani Rukwa.

Aliyefikwa na mkasa huo hiyo hiyo juzi jioni alikuwa ni Naibu Waziri wa Usalama wa Raia, Mohammed Aboud, ambaye alijikuta akizomewa na wananchi waliofika katika mkutano aliouhutubia, baada ya kutoa ahadi kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa kikikusudia kulirejesha Jimbo la Mpanda Kati.

Aboud alipata wakati mgumu na kujikuta akizomewa pale alipotangaza mkakati wa CCM kulikomboa Jimbo la Mpanda Kati linaloongozwa na Mbunge wa CHADEMA, Said Alfi.

Awali Aboud aliwaambia wananchi wa Mpanda kuwa malengo ya ziara yake hapo yalikuwa ni kutaka kujua kero zao na hususan zinazohusiana na usalama wa raia na pia kufafanua Bajeti ya Serikali ya mwaka 2007/2008.

Baada ya kuwasalimia wananchi, aliwataka watoe kero zao, maoni na ushauri ndipo apate mwelekeo wa hotuba yake kwa kujibu hoja kwa njia ya hotuba, jambo lililowafurahisha mno wananchi.

Huku wakiwa na matumaini ya ufumbuzi wa tatizo la watu kupigwa nondo na mapanga kwa muda mrefu sasa, wananchi wengi walihoji ubia uliopo kati ya baadhi ya polisi wilayani Mpanda na wahalifu wanaofahamika kwa polisi, ingawa hawachukuliwi hatua zozote za kisheria.

Mambo mengine aliyoulizwa Naibu Waziri Abood ni pamoja na kesi za madai wilayani Mpanda kuamuliwa na polisi badala ya mahakama, baadhi ya polisi kudai fedha za kufuta kesi pale wanaoshitakiana wanaporidhiana, ukosefu wa magari kwa ajili ya usafiri kwa Jeshi la Polisi na kutokuwepo kwa vituo vya polisi mjini Mpanda.

Miguno ilianza pale naibu waziri huyo alipoziponda kauli alizoziita za wapinzani, waliodai kuwa maisha ya Watanzania ni magumu mno katika awamu hii na wananchi lazima wafunge mikanda na kudai mipango ya serikali inalenga maisha bora kwa kila Mtanzania.

"Hawa wanataka kuwakosanisha wananchi na serikali yao, hatutawasikiliza na tunaendelea kuchapa kazi kuwaletea maendeleo, waache gere zao," alisema Aboud huku akizomewa badala ya kushangiliwa na watu waliosikika wakisema; "umeishiwa, huna la kutudanganya, kodi zetuuu," na maneno mengi mengine.

Hali ya kuguna ilizidi zaidi pale alipotoa takwimu za kupungua kwa uhalifu nchini kwa asilimia 45, badala ya kujibu hoja za msingi za kwa nini polisi wilayani Mpanda wameshindwa kuzuia vitendo vya watu kukatwa mapanga na kupigwa nondo.

"Tunataka ufumbuzi wa tatizo la ujambazi si kututaka tutoe ushirikiano kwa polisi wanaoshirikiana na majambazi," alisikika akisema kijana mmoja kwa jazba.

Wakati hayo yakimfika Aboud, Waziri Wasira aliyepiga simu chumba cha habari cha gazeti hili jana asubuhi na akazungumza na Mhariri Mkuu, alizielezea taarifa za wao kuzomewa Mbeya kuwa ni za uzushi na zisizo na ukweli wowote.

"Nimepigiwa simu nyingi na watu wakiniuliza kuhusu kuwapo kwa taarifa za kuzomewa, na mimi nikasema hayo ni mambo ya magazeti. Nilikuwapo pale uwanjani na nilikuwa mtu wa mwisho kuondoka," alisema Wasira aliyeeleza kuwa alikuwa akizungumza wakati akiwa safarini kutoka Mbeya kurejea Dar es Salaam.

Wakati Wasira akikanusha taarifa hizo, habari nyingine kutoka mkoani Mbeya zinaeleza kuwa, muda mfupi baada ya mkutano huo wa hadhara kumalizika, katibu wa mmoja wa mawaziri waliokuwapo katika mkutano huo, aliwakusanya waandishi wa habari waliokuwapo hapo na akawataka waandike maneno ya viongozi na waachane na matukio ya kuzomea zomea.

"Hawa viongozi walifanya kila waliloweza kuzuia taarifa za wao kuzomewa. Katibu wa waziri (anamtaja jina waziri), aliwaita waandishi na kuwapa shilingi 10, 000 kila mmoja na akawataka kutoandika kuhusu kuzomea kulikotokea na badala yake kuzingatia hoja zilizotolewa," alisema mwandishi wa habari wa gazeti hili aliyekuwapo katika mkutano huo.

Kwa upande wake Waziri Wasira alipoulizwa jana na Mhariri Mkuu wa gazeti hili ni kwa sababu gani basi, kiongozi wa kikundi cha Sanaa cha Tanzania One Theatre (TOT), John Komba aliyekuwapo katika mkutano huo wa juzi, alilazimika kuwataka wale wote waliokuwa hawataki kukishangilia chama hicho kwa kupunga mikono waondoke uwanjani, iwapo kulikuwa hakuna zomeazomea, alijibu kwa maneno machache bila kufafanua; "Komba yule ni msanii."

Malalamiko hayo ya Wasira yalimfanya Mhariri Mkuu wa gazeti hili, Absalom Kibanda, awasiliane na watu kadhaa wa Mbeya waliokuwapo katika mkutano ule, wakiwamo waandishi wa habari wa vyombo kadhaa (si wa Tanzania Daima) wanaofanya kazi Mbeya ili kupata uhakika wa kile kilichotokea.

Mkazi mmoja wa Mbeya aliyejitambulisha kwa jina moja la Hiriza, aliyezungumza na gazeti hili jana, alieleza kushangaa baada ya kuelezwa na mhariri mkuu kuwa Waziri Wasira alikuwa akikanusha kuwapo kwa tukio la wao kuzomewa.

"Ni muongo. Tukio lilikuwa ni la wazi kabisa, mimi ni shuhuda, nilikuwa pale na kila mtu aliyekuwapo pale aliliona. Kila aliyepanda jukwaani alipokuwa akizungumza kulikuwa na kuguna, na hali ilizidi wakati msafara ukiondoka, ndipo watu walipoanza kuzomea huku wengine wakirusha mchanga hewani," alisema Hiriza.

Mwandishi mmoja mwandamizi wa habari wa gazeti moja la kila siku (si wa Tanzania Daima), alipoulizwa kuhusu kile kilichotokea wakati wa mkutano huo wa juzi alikuwa na haya ya kusema:

"Ndugu yangu mkutano wa jana (juzi) ulimalizika kwa aibu. Kwanza walijitokeza watu wachache sana kulinganisha na wale waliojitokeza wakati wapinzani walipokuwa hapa wiki chache tu zilizopita.

"Pili, baada ya baadhi ya viongozi wa CCM mkoani hapa kubaini kuwa walikuwa wakishangiliwa na kikundi kidogo tu cha wanachama wao waliokuwa mbele huku wale waliokuwa nyuma wakiwa kimya, walitoroka mkutanoni mapema, na hali ya kuzomea iliongezeka wakati viongozi hao walipokuwa wakiondoka mkutanoni," alisema mwandishi huyo mwandamizi wa habari.

Kutokana na majibu hayo, mhariri mkuu alilazimika kumweleza mwandishi huyo wa habari kuwa Waziri Wasira alikuwa amepiga simu chumba cha habari cha gazeti hili akikanusha kuwapo kwa tukio lolote la kuzomea.

"Wasira hasemi kweli. Hapa mjini hivi sasa hiyo ndiyo habari kubwa, kila mtu aliyekuwapo uwanjani jana (juzi) aliiona hali hiyo ya kuzomea iliyokuwa kubwa hasa wakati msafara wa viongozi na makada wa CCM ulipokuwa ukiondoka," alisema mwandishi huyo wa habari.

Mwandishi mwingine wa gazeti la Mwananchi aliyekuwapo Mbeya wakati wa tukio hilo, alipoelezwa kuhusu taarifa za Wasira kukanusha taarifa hizo alisisitiza kutokea kwa tukio hilo.

"Kilichotokea kwenye ule mkutano ni cha wazi kabisa. Watu walizomea, tena sana. Wasira mwenyewe alizomewa alipoongelea mbolea," alisema mwandishi huyo wa habari.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari huyo, hali ya kuzomea ilizidi wakati Akwilombe, kada wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) aliposimama na kukiponda chama chake hicho cha zamani akisema ni cha kifamilia.

Kwa mujibu wa mwandishi huyo, kauli hiyo ya Akwilombe ilisababisha watu waliokuwa wakimsikiliza kumzomea na kuanza kuimba ‘Mbowe, Mbowe, Mbowe, CHADEMA CHADEMA CHADEMA'.

Hali kama hiyo ilitokea pia wakati Tambwe Hizza na Salum Msabah, makada wawili wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF) walipopanda jukwaani kwa nyakati tofauti na kuviponda vyama vya upinzani.

Viongozi na makada wa CCM waliokuwapo katika mkutano huo wa juzi mbali ya Wasira, Akwilombe, Hizza na Msabah, ni Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, John Chiligati na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Aggrey Mwanri, aliyekuwa kiongozi wa msafara.

Tukio hili linakuja siku chache tu tangu mawaziri na makada wengine wa CCM watumwe kwenda mikoani kufafanua kuhusu bajeti na kukanusha tuhuma za vyama vinne vya upinzani dhidi ya serikali na viongozi wake wa juu na wa chama tawala, wanaotuhumiwa kwa vitendo mbalimbali ya ufisadi.


Tanzania Daima.
 
Mbunge wa jimbo la Kilombero Mh Castor Ligallama Juzi alipata joto la jiwe baada ya wananchi kususia mkutano wake wa hadhara maeneo ya Kiugani hapa mjini Ifakara. Maandalizi ya kualika watu wakamsikilize mbuge huyo yalifanyika kwa juhudi za aina yake, matangazo yalitolewa kanisani baada ya Ibada za misa, Kwenye misikiti na magari yaliyokuwa na vipaza sauti na matangazo lukuki. Cha kushangaza ni watu wachache sana walioweza kufika pale kwenye viwanja vya kiungani, na hao waliofika walikuwa wakimzomea sana bw Ligalama kwa maneno ya wala rushwa nyie, mafisadi, sumu, mara Buzwagi na mara nyingi walikuwa wamwita Zitto Kabwe. Hali hii ilimfadhaisha sana mbuge, polisi walijitahidi sana kuzuia fujo, Bwana Ligallama hakuweza kuhutubia wananchi ndipo alipoamua kwenda kuhutubia kwenye soko la mjini Ifakara ambako pia alizomewa sana, alisisikika akiwaambia wananchi jamani mimi ni mbuge wenu natoka kwenye chama kilichopo madarakani, naomba mnisikilize nina majibu ya kero zenu. Wananchi walijaa jazba na hakuweza kuwahutumbia. Cha ajabu Ifakara kuna waandishi wengi wa habari wa vyombo mbali mbali habari hii wala haikutangazwa!! Nafikiri wakati umefika wananchi wameanza kujua kweli na wapo tayari kutafuta haki zao, zile kauli mbiu za maisha bora wamepata tafsiri ya kuwekewa mchanga wa macho wakistuka mafisadi wamechukua nchi na umasikini uliokubuhu kwa wananchi waliwaji ukiendelea. Aluta continua ipo siku watarusha mawe na kuingia msituni kutafuta wanachokitaka. zile nyimbo za kijinga nchi yetu ni kisiwa cha amani na ujinga zitapotea iwe historia.


Hii inanikumbusha ule wimbo wa pili wa mwanamziki Prof J. wananchi wanapomkataa mh. walio mchagua. This is gud sign naamini 2010 wananchi wa Tanzania wataimplement hiyo zomea kwenye uchaguzi. Hata kama wapinzanihawatashinda japo tuwe tuu na wabunge wengi wa upinzani ili kubalance power bngeni. Chonde chonde wananchi msikubali kuhongwa kwa Khanga, Kofia na pilau.
 
Zomeazomea yazidi

Na Mwandishi Wetu
Chanzo: Tanzania Daima

WAKATI Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wasira, akikanusha taarifa zilizoandikwa na gazeti hili jana na jingine la kila siku, zinazoeleza kuhusu kuzomewa na wananchi wa Mbeya wakati wa mkutano wao wa hadhara uliofanyika juzi, waziri mwingine katika serikali ya Rais Jakaya Kikwete, alikutwa na zahama kama hiyo huko Mpanda, mkoani Rukwa.

Aliyefikwa na mkasa huo hiyo hiyo juzi jioni alikuwa ni Naibu Waziri wa Usalama wa Raia, Mohammed Aboud, ambaye alijikuta akizomewa na wananchi waliofika katika mkutano aliouhutubia, baada ya kutoa ahadi kwamba Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa kikikusudia kulirejesha Jimbo la Mpanda Kati.

Aboud alipata wakati mgumu na kujikuta akizomewa pale alipotangaza mkakati wa CCM kulikomboa Jimbo la Mpanda Kati linaloongozwa na Mbunge wa CHADEMA, Said Alfi.

Awali Aboud aliwaambia wananchi wa Mpanda kuwa malengo ya ziara yake hapo yalikuwa ni kutaka kujua kero zao na hususan zinazohusiana na usalama wa raia na pia kufafanua Bajeti ya Serikali ya mwaka 2007/2008.

Baada ya kuwasalimia wananchi, aliwataka watoe kero zao, maoni na ushauri ndipo apate mwelekeo wa hotuba yake kwa kujibu hoja kwa njia ya hotuba, jambo lililowafurahisha mno wananchi.

Huku wakiwa na matumaini ya ufumbuzi wa tatizo la watu kupigwa nondo na mapanga kwa muda mrefu sasa, wananchi wengi walihoji ubia uliopo kati ya baadhi ya polisi wilayani Mpanda na wahalifu wanaofahamika kwa polisi, ingawa hawachukuliwi hatua zozote za kisheria.

Mambo mengine aliyoulizwa Naibu Waziri Abood ni pamoja na kesi za madai wilayani Mpanda kuamuliwa na polisi badala ya mahakama, baadhi ya polisi kudai fedha za kufuta kesi pale wanaoshitakiana wanaporidhiana, ukosefu wa magari kwa ajili ya usafiri kwa Jeshi la Polisi na kutokuwepo kwa vituo vya polisi mjini Mpanda.

Miguno ilianza pale naibu waziri huyo alipoziponda kauli alizoziita za wapinzani, waliodai kuwa maisha ya Watanzania ni magumu mno katika awamu hii na wananchi lazima wafunge mikanda na kudai mipango ya serikali inalenga maisha bora kwa kila Mtanzania.

“Hawa wanataka kuwakosanisha wananchi na serikali yao, hatutawasikiliza na tunaendelea kuchapa kazi kuwaletea maendeleo, waache gere zao,” alisema Aboud huku akizomewa badala ya kushangiliwa na watu waliosikika wakisema; “umeishiwa, huna la kutudanganya, kodi zetuuu,” na maneno mengi mengine.

Hali ya kuguna ilizidi zaidi pale alipotoa takwimu za kupungua kwa uhalifu nchini kwa asilimia 45, badala ya kujibu hoja za msingi za kwa nini polisi wilayani Mpanda wameshindwa kuzuia vitendo vya watu kukatwa mapanga na kupigwa nondo.

“Tunataka ufumbuzi wa tatizo la ujambazi si kututaka tutoe ushirikiano kwa polisi wanaoshirikiana na majambazi,” alisikika akisema kijana mmoja kwa jazba.

Wakati hayo yakimfika Aboud, Waziri Wasira aliyepiga simu chumba cha habari cha gazeti hili jana asubuhi na akazungumza na Mhariri Mkuu, alizielezea taarifa za wao kuzomewa Mbeya kuwa ni za uzushi na zisizo na ukweli wowote.

“Nimepigiwa simu nyingi na watu wakiniuliza kuhusu kuwapo kwa taarifa za kuzomewa, na mimi nikasema hayo ni mambo ya magazeti. Nilikuwapo pale uwanjani na nilikuwa mtu wa mwisho kuondoka,” alisema Wasira aliyeeleza kuwa alikuwa akizungumza wakati akiwa safarini kutoka Mbeya kurejea Dar es Salaam.

Wakati Wasira akikanusha taarifa hizo, habari nyingine kutoka mkoani Mbeya zinaeleza kuwa, muda mfupi baada ya mkutano huo wa hadhara kumalizika, katibu wa mmoja wa mawaziri waliokuwapo katika mkutano huo, aliwakusanya waandishi wa habari waliokuwapo hapo na akawataka waandike maneno ya viongozi na waachane na matukio ya kuzomea zomea.

“Hawa viongozi walifanya kila waliloweza kuzuia taarifa za wao kuzomewa. Katibu wa waziri (anamtaja jina waziri), aliwaita waandishi na kuwapa shilingi 10, 000 kila mmoja na akawataka kutoandika kuhusu kuzomea kulikotokea na badala yake kuzingatia hoja zilizotolewa,” alisema mwandishi wa habari wa gazeti hili aliyekuwapo katika mkutano huo.

Kwa upande wake Waziri Wasira alipoulizwa jana na Mhariri Mkuu wa gazeti hili ni kwa sababu gani basi, kiongozi wa kikundi cha Sanaa cha Tanzania One Theatre (TOT), John Komba aliyekuwapo katika mkutano huo wa juzi, alilazimika kuwataka wale wote waliokuwa hawataki kukishangilia chama hicho kwa kupunga mikono waondoke uwanjani, iwapo kulikuwa hakuna zomeazomea, alijibu kwa maneno machache bila kufafanua; “Komba yule ni msanii.”

Malalamiko hayo ya Wasira yalimfanya Mhariri Mkuu wa gazeti hili, Absalom Kibanda, awasiliane na watu kadhaa wa Mbeya waliokuwapo katika mkutano ule, wakiwamo waandishi wa habari wa vyombo kadhaa (si wa Tanzania Daima) wanaofanya kazi Mbeya ili kupata uhakika wa kile kilichotokea.

Mkazi mmoja wa Mbeya aliyejitambulisha kwa jina moja la Hiriza, aliyezungumza na gazeti hili jana, alieleza kushangaa baada ya kuelezwa na mhariri mkuu kuwa Waziri Wasira alikuwa akikanusha kuwapo kwa tukio la wao kuzomewa.

“Ni muongo. Tukio lilikuwa ni la wazi kabisa, mimi ni shuhuda, nilikuwa pale na kila mtu aliyekuwapo pale aliliona. Kila aliyepanda jukwaani alipokuwa akizungumza kulikuwa na kuguna, na hali ilizidi wakati msafara ukiondoka, ndipo watu walipoanza kuzomea huku wengine wakirusha mchanga hewani,” alisema Hiriza.

Mwandishi mmoja mwandamizi wa habari wa gazeti moja la kila siku (si wa Tanzania Daima), alipoulizwa kuhusu kile kilichotokea wakati wa mkutano huo wa juzi alikuwa na haya ya kusema:

“Ndugu yangu mkutano wa jana (juzi) ulimalizika kwa aibu. Kwanza walijitokeza watu wachache sana kulinganisha na wale waliojitokeza wakati wapinzani walipokuwa hapa wiki chache tu zilizopita.

“Pili, baada ya baadhi ya viongozi wa CCM mkoani hapa kubaini kuwa walikuwa wakishangiliwa na kikundi kidogo tu cha wanachama wao waliokuwa mbele huku wale waliokuwa nyuma wakiwa kimya, walitoroka mkutanoni mapema, na hali ya kuzomea iliongezeka wakati viongozi hao walipokuwa wakiondoka mkutanoni,” alisema mwandishi huyo mwandamizi wa habari.

Kutokana na majibu hayo, mhariri mkuu alilazimika kumweleza mwandishi huyo wa habari kuwa Waziri Wasira alikuwa amepiga simu chumba cha habari cha gazeti hili akikanusha kuwapo kwa tukio lolote la kuzomea.

“Wasira hasemi kweli. Hapa mjini hivi sasa hiyo ndiyo habari kubwa, kila mtu aliyekuwapo uwanjani jana (juzi) aliiona hali hiyo ya kuzomea iliyokuwa kubwa hasa wakati msafara wa viongozi na makada wa CCM ulipokuwa ukiondoka,” alisema mwandishi huyo wa habari.

Mwandishi mwingine wa gazeti la Mwananchi aliyekuwapo Mbeya wakati wa tukio hilo, alipoelezwa kuhusu taarifa za Wasira kukanusha taarifa hizo alisisitiza kutokea kwa tukio hilo.

“Kilichotokea kwenye ule mkutano ni cha wazi kabisa. Watu walizomea, tena sana. Wasira mwenyewe alizomewa alipoongelea mbolea,” alisema mwandishi huyo wa habari.

Kwa mujibu wa mwandishi wa habari huyo, hali ya kuzomea ilizidi wakati Akwilombe, kada wa zamani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) aliposimama na kukiponda chama chake hicho cha zamani akisema ni cha kifamilia.

Kwa mujibu wa mwandishi huyo, kauli hiyo ya Akwilombe ilisababisha watu waliokuwa wakimsikiliza kumzomea na kuanza kuimba ‘Mbowe, Mbowe, Mbowe, CHADEMA CHADEMA CHADEMA’.

Hali kama hiyo ilitokea pia wakati Tambwe Hizza na Salum Msabah, makada wawili wa zamani wa Chama cha Wananchi (CUF) walipopanda jukwaani kwa nyakati tofauti na kuviponda vyama vya upinzani.

Viongozi na makada wa CCM waliokuwapo katika mkutano huo wa juzi mbali ya Wasira, Akwilombe, Hizza na Msabah, ni Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, John Chiligati na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Aggrey Mwanri, aliyekuwa kiongozi wa msafara.

Tukio hili linakuja siku chache tu tangu mawaziri na makada wengine wa CCM watumwe kwenda mikoani kufafanua kuhusu bajeti na kukanusha tuhuma za vyama vinne vya upinzani dhidi ya serikali na viongozi wake wa juu na wa chama tawala, wanaotuhumiwa kwa vitendo mbalimbali ya ufisadi.
 
Nikumbushe tu kama uliondoka nchini muda mrefu!

Bado nchi yetu watu hawafanyi kazi, waiting for government kuleta maisha bora!

Ikifika saa kumi na moja, nchi nzima usingizi, viwanda vinavyofanya kazi 24hrs vinahesabika,,, kwa hiyo hata tuwe na raslimali vipi kama ikifika saa kumi na moja tunasheherekea mafanikio kwenye grocery/pubs/baa na vichochoro vyote vinavyouza vinjwaji hatutaenda popote...

Ndio maana naihurumia hii nchi kwa kuwa sioni mwanasiasa anayesimama imara kusema pamoja na mambo mengine soluhisho la uchumi wetu ni pamoja na kuchapa kazi....

Mzee Mkapa alisema lakini wengine wemepuuza, mzee huyu alirudia kwamba mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, sasa serikali ya awamu ya nne badala ya kubuild on that foundation, wao wanasema watawaletea wananchi maendeleo, wapi na taifa gani linagawa maendeleo...

nikupe mfano,,, Tanzania ukitaka kufanya kazi kwenye mkoa mwingine kazi ya dakika tano,,, unalazimika kuharibu siku tatu za uzalishaji,..., siku ya kwenda,,, siku ya kazi, na siku ya kurudi,,, tatizo,,, ati mabasi yasisafiri usiku ni mchana tu...haya... amri ya Tangu mzee Malechela akiwa waziri mkuu mpaka sasa nobody revisited and challenged it... ati mpaka rais aseme... we have serious problem watanzania, sio la CCM au Rais na Baraza lake la mawaziri ... mindset zetu zimeganda....

Mh. mmoja anasema... ati mtu mwenye uwezo aliyesoma Academy school anaambia achangine 300,000/- university na yeye alazimisha serikali impe mkopo 100%, maana yake anazuia maskini mwingine kama mimi kupata nafasi ya kusoma... this is our country

Interesting..
Unamejitahidi kuweka points zako ila naomba kukuuliza ni kitu gani ambacho kinachowafanya watu ambao wengi wao hawajawahi kufanya kazi hata siku moja Tanzania wakienda nchi kama US wanafanya kazi kama hawana akili nzuri. Kama ni kweli "mindset zimeganda" ni nini kinazifanya ziyeyuke.
Kuhusu mikopo kwa mawazo yangu "mkopo" siyo sadaka au grant au scholarship. Ni kivipi hela ambayo itarudi ikuzuie wewe kupata elimu? Kwa kuwa uwezo wa watanzania wengi ni mdogo kujisomesha na serikali haina uwezo wa kusomesha nadhani kila mtu anatakiwa apewe mkopo kiasi ambacho anahitaji. Jambo ya kuzungumzia hapa je kuna utaratibu wa kuakikisha kuwa kila aliyekopa atapata kazi na kurudisha hizo hela. If education is the key why don't they give key to everyone? Kwa umasikini uliopo Tanzania elimu ilitakiwa iwe bure. Hatuwezi kuendelea hata siku moja kama hatuta wekeza kwenye elimu. I will come for this one later on.
Kuhusu hali ya kisiasa na position ya CCM katika uringo wa siasa nadhani hili nitaliongelea kwa undani baada ya mkutano mkuu wa CCM mwezi ujao. Nilishawahi kuongea kwenye hizi forum kwamba JK alikuwa na nafasi ya kuleta maenedeleo kwa sababu moja kubwa ya kupendwa na kusikilizwa na wananchi nadhani hakulitambua hilo na sasa yamemkuta yaliyomkuta. Mtu pekee kwa sasa ambaye anaweza kuiokoa CCM mahali ilipo ni yeye. It is time now to act siyo kuendeleza usanii huyu EL amewaahidi wamasai viwanda 10 vya kusindika nyama ndani ya miaka mitatu nadhani mjifunze kufanya kazi tofauti jengeni viwanda halafu wafuateni na kuwaeleza wananchi kuwa kuna viwanda siyo kuahidi mambo ambayo baadaye yatawatokeeni puani.
Mimi siwezi kwenda na stats za watu hapa JF na kusema CCM imeanguka. Stats mara nyingi hazisemi ukweli. Kwa mfano stats zinaonyesha kuwa LOVE ni kitu kizuri sana lakini nikikuuliza ni watu wangapi LOVE hurts them utajiuliza mara mbili kama kweli kupenda ni kitu kizuri.
Nimeongea hapa na watu mbalimbali wengi wao wanasema wamechoka na mafisadi blah blah lakini ukiwauliza ni nani wanataka awe rais au chama gani kitawale hawana majibu. Nadhani tutaongelea ili kwa undani huko mbeleni.
Mkandara vipi, ufuturishi mwaka huu?
 
CCM walikuwa likizo kwa muda mrefu, nadhani sasa wanatamani dunia ipasuke. wamekuwa kama waumini wakati wa nuhu, wanaanza kulia oooh nuhu tufungulie safina. This is the end of Nazi's politcs, and CCM will remain as hostory. Hope 2010 alot of combine forces from each side of the world will be in Tanzania, to be part of the history.
 
Nakuunga mkono kilitime,

Mimi sijazamia huku, mara kwa mara hufika nyumbani, walau mara mbili kwa mwaka. hali ya nyumbani ninaijua vizuri. Arusha - Dodoma ni kama 460km hivi. lakini ukitaka kufika dodoma lazima uzunguke Chalinze - morogoro, zaidi ya 800km. tumelaaniwa sana.

Pamoja na uvivu wetu, bado kuna watu wenye nia ya dhati ya kufanya kazi. nina proposal yangu hadi leo inaozea kwenye kabati, kisa natakiwa nianze kwanza project ndipo nipewe mkopo. ukiomba serikali ikudhamini danadana kibao.

Foreigners wakija, wanapewa hata muda wa kutokulipa kodi. ndiyo maana watu wamekata tamaa. badala ya kufikiri miradi gani wafanye, wanaamua kuishia kwenye mitungi na hata utapeli usio na maana.

Bado hatuna viongozi waelekazaji kuelekea maendeleo ya kweli. hawajui kufundisha. na hata wakifundisha hafanyi kile wanachokifundisha. Mbona Baba wa Taifa watu walimwelewa na siasa ni kilimo na watu waliitikia kwa nguvu zao zote? kwa nini wao washindwe. kwa nini watu wakae vijiweni? je yatosha tu kusema ni wavivu? hivi kuna wavivu duniani kama jamii ya kiarabu? mbona kuanzia asubuhi hadi jioni wanashinda kunywa kahawa? mbona nchi zao zina maendeleo makubwa kuliko yetu? tukae tujiulize, lazima ipo sababu. Je sera zetu zinatekelezeka au ni za kuombea kura?

Saharavoice, Kilitime you both have good points. Now lets take these great points further! Mie naona we need action- and that action should come from me, and you and everybody else who is asking the questions/issues you have both raised. Viongozi wetu hawana mawazo mapya- they have used all they have and we really have to releave them now so we get on the drawing boards- change the policies, change people's attitudes, remotivete Tanzanians to wake up and work for our lives/prosperity. For All Tanzanians to wake up from the deep sleep we are all sleeping. Tusilalamike tu jamani na worse tusiendelee kujilaani. MANENO HUUMBA!- lets each do something from now, however small and wherever we are- with a clear vision of where we wanna take our beautiful TANZANIA. and off-course last but not least, LETS SHARE THIS FORUM TOO, it is a great way to inform and waken people up. HAKUNA KULALA!!
 
..tuwapige nje hawa CCM ili wawe upande wa upinzani labda waatabadilika na kuanza kupigana na rushwa kwa sababu wanajua deal zote za kula rushwa na hawatakubali jamaa wengine wale.
 
..tuwapige nje hawa CCM ili wawe upande wa upinzani labda waatabadilika na kuanza kupigana na rushwa kwa sababu wanajua deal zote za kula rushwa na hawatakubali jamaa wengine wale.

Watahama chama na kujiunga na upinzani "mvingyo ule ule kwa kibuyu kipya" Any way CCM sasa tumeichoka walau ibadili jina sasa (kiding)
 
cheers Mshobozi, Na bado; Nimecheka sana kusikia JK anaitwa Kingwendu, Anyway fanya kila linalowezekana ututumie habari za mikutano ya leo,
 
[QUOTE
=kilitime;80471],,, lakini kuna jambo zuri kwa upande wa chama tawala, waendelee kukubali kuulizwa maswali ili wajue jamii imebadilika,,, miaka iliyopita kiongozi anahutubia alafu anaondoka zake, siku hizi maswali yanaulizwa tena magumu, which is good for the nation!

Basi walau wajibu maswali. Waziri Mkuu kaulizwa swali na Mwanafunzi kule Ukerewe kashindwa kujibu, matokeo yake Usalama wa Taifa wanaanza kumsukasuka yule mtoto. Sasa demokrasia ganui hiyo unayoisema hapa?


Ingawa sio jambo la kujivunia kujenga utamaduni wa kuzomea, lakini wa ku-express ideas is a GREAT thing,

Sasa tufanyeje? Huo ndiyo uwezo wetu na nguvu yetu. Kuwapiga mawe ni kosa na uvunjifu mkubwa wa amani. Hii ndiyo njia rahisi na mwafaka ya kuwafikishia ujumbe kuwa TUMEWACHOKA!

Tuzame mambo kwa mbali zaidi, katika uhai wa taifa hili kutakuwa na vyama tawala na chama pinzani, today may be CCM, tomorrow CHADEMA, the other year CUF, la muhimu ni kujenga jamii ambayo inavumiliana katika utoaji wa hoja...


Hakuna uvumilivu usokuwa na kikomo; kama tumechoka hiyo ndiyo njia sahihi kwa wakti huu. Tena ni jambo la kumshukuru Mungu, msipobadilika mtakuja kupigwa kwa mawe na Polisi wataangalia tu kama ilivyofanyika Yugoslavi hadi Milosevic akaikimbia Ikulu!
 
Binti Haki shukrani kwa ushauri wako, nilichojaribu kukisema ni kwamba, Watu tunao, ardhi safi yenye kila aina ya utajiri tunayo. tunachokosa ni uongozi bora na siasa safi.

Kwa hiyo mimi kama mwananchi na wengine wengi tumejaribu kujitahidi sana kwa kadri tunavyoweza. kama kungekuwa na uongozi bora na siasa safi nadhani tungekwenda mbali sana. ndio maana tunasema enough is enough, waliopo hawatufai lazima waondoke. wataondokaje? tutawaondoa kwa kuwakoromea sana wabadhirifu wa mali yetu, tutawazomea kila kona waendako, kwa kutumia mitandao, wanaharakati na vyama vya upinzani tutawaelimisha watanzania juu ya haki zao na hatimaye kufanya mabadiliko ya serikali kupitia kura.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom