Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,498
- 9,279
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia SALOME BUYA [23] Mkazi wa Mnazi kwa Ndomba wilayani Mbarali kwa tuhuma za kumjeruhi vibaya sehemu ya shingoni TABIA ABDALAH [38] Mkazi wa Msesule.
Tukio hili limetokea mnamo tarehe 06.10.2020 majira ya saa 18:00 jioni huko Kijiji cha Mnazi, Kata ya Imalilosongwe, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya ambapo mtuhumiwa SALOME BUYA alimjeruhi kwa kumchoma kisu sehemu ya shingoni upande wa kisogoni TABIA ABDALAH [38] Mkazi wa Msesule na kupelekea kupoteza fahamu.
Awali kabla ya tukio hilo, TABIA ABDALAH pamoja na wanawake wengine walimuita SALOME BUYA na kumtuhumu kuwatangazia wenzake kwa watu pindi wakichepuka nje ya ndoa zao. Chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliozuka baina yao baada ya kutuhumiana kutoleana nje siri za ndoa.
Aidha SALOME BUYA pia amepata majeraha kidogo sehemu ya puani. Majeruhi amelazwa Hospitali ya Wilaya ya Mbarali kwa matibabu hali yake sio nzuri. Upelelezi wa shauri hili unaendelea.
Tukio hili limetokea mnamo tarehe 06.10.2020 majira ya saa 18:00 jioni huko Kijiji cha Mnazi, Kata ya Imalilosongwe, Tarafa ya Ilongo, Wilaya ya Mbarali, Mkoa wa Mbeya ambapo mtuhumiwa SALOME BUYA alimjeruhi kwa kumchoma kisu sehemu ya shingoni upande wa kisogoni TABIA ABDALAH [38] Mkazi wa Msesule na kupelekea kupoteza fahamu.
Awali kabla ya tukio hilo, TABIA ABDALAH pamoja na wanawake wengine walimuita SALOME BUYA na kumtuhumu kuwatangazia wenzake kwa watu pindi wakichepuka nje ya ndoa zao. Chanzo cha tukio hilo ni ugomvi uliozuka baina yao baada ya kutuhumiana kutoleana nje siri za ndoa.
Aidha SALOME BUYA pia amepata majeraha kidogo sehemu ya puani. Majeruhi amelazwa Hospitali ya Wilaya ya Mbarali kwa matibabu hali yake sio nzuri. Upelelezi wa shauri hili unaendelea.