figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,491
- 54,884
Junior Bakari Siame mwanafunzi wa Darasa la tatu shuke ya Msingi ya Hanga, ametekwa na kunyongwa hadi kufa
Baba mzazi alipigiwa simu na mtekaji kwamba atume hela ya kumkomboa mtoto, Mzee Bakari anasema alijitahidi kumtumia elfu 30 ili asimdhuru mtoto. Akaambiwa hela haitoshi utume nyingine.
Watekaji walitaka mzazi auze nyumba. Simu ya mwisho juzi alipigiwa na kuulizwa kati ya mtoto na nyumba kipi muhimu?. Akatata simu na kuishia hapo.
Naye Mkuu wa mkoa wa Mbeya, amekemea vikali tukio hilo.
Amesema huyo mtu asiyejulikana alitaka hela zaidi ya Milioni 10, alimchukua mtoto na kumpeleka mlima nyoka, mtoto alipoona yupo na mtu asiye sahihi, alianza kupiga kelele. Yule mtekaji alimbeba na kumziba mdomo na kumpeleka mashambani. Alimziba mdomo ili asiweze kukmatwa, muda si muda yule mtoto alidondoka. Mtekaji akaanza kumpepea akijua amezimia tu kumbe ameshafariki.
Baada ya kufanya tukio hilo, aliondoka na kuelekea yule akachukua Magari ya Makambako hadi Iringa ambapo Jeshi la Polisi kupitia Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, waliweza kumkamata na kumrudisha mpaka Mbeya na akaonesha mtoto alipo.
Na alikiri akiwa huko huko kwamba mtoto nlikwisha muua
Pamoja na kumuua mtoto, aliendelea kudai mil 10 ili aoneshe mtoto alipo.
Chelamila amesema Mauaji haya haya mahusiano na migogoro yoyote ya kidini, ya kiukoo wala ya kikabila.
Mtekaji aliaema alifanya hivyo kutokana na uchu wa hela sababu alipokuwa gerezani kafungwa alisikia watu wakipiga stori kwamba walikuwa wanatumia mbinu hizo kupata fedha ndipo naye akafanya, bahati mbaya mtoto akawa amefariki.
Mkuu wa mkoa amewata wananchi kuendelea kuwa wamoja kuamini jeshi la Polisi na vyombo vyote vya ulinzi na Usalama.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Ulrich Matei amsema, Tarehe 9/04/2019 Majira ya saa kumi na mbili huko mtaa wa shinga Igalilo tarafa ya Iyunga jijini Mbeya, Junior Bakari Siame wa miaka 8 Mnyamwanga na mwanafunzi wa darasa la tatu. Aliuawa na mtu asiyejulikana katika shamba moja la mahindi lililopo Mlima nyoka.
Mtuhumiwa alipokutana na marehemu alimuuliza kwenu kuna mali gani? akaambiwa nyumba na gari na baba anataka kuliuza hilo gsri. Wakaenda wote hadi nyumbani ili mtoto akabadilishe nguo na kwenda kutafuta mteja wa gari..
Walitembea kwa mguu hadi nane nane na wakapanda gari nanenane na kwenda hadi Saraga. Walipofika saraga ndo mzazi alianza kupigiwa simu ili atoe Milioni 10.
Na mnamo tarehe 14/04/2019 Majira ya saa saba, mtuhumiwa alikamatwa Iringa katika stand ya Ipogoro na kurudishwa Mbeya.
Mtuhumiwa anaonesha alishawahi kuwa na kesi ya kubaka kule Mwanza Criminal case namba 44 ya mwaka 2017 ambapo alifungwa mika 30. Na alitoka kwa rufaa tarehe 22 mwezi wa Pili mwaka huu kule mwanza.
Baba mzazi alipigiwa simu na mtekaji kwamba atume hela ya kumkomboa mtoto, Mzee Bakari anasema alijitahidi kumtumia elfu 30 ili asimdhuru mtoto. Akaambiwa hela haitoshi utume nyingine.
Watekaji walitaka mzazi auze nyumba. Simu ya mwisho juzi alipigiwa na kuulizwa kati ya mtoto na nyumba kipi muhimu?. Akatata simu na kuishia hapo.
Naye Mkuu wa mkoa wa Mbeya, amekemea vikali tukio hilo.
Amesema huyo mtu asiyejulikana alitaka hela zaidi ya Milioni 10, alimchukua mtoto na kumpeleka mlima nyoka, mtoto alipoona yupo na mtu asiye sahihi, alianza kupiga kelele. Yule mtekaji alimbeba na kumziba mdomo na kumpeleka mashambani. Alimziba mdomo ili asiweze kukmatwa, muda si muda yule mtoto alidondoka. Mtekaji akaanza kumpepea akijua amezimia tu kumbe ameshafariki.
Baada ya kufanya tukio hilo, aliondoka na kuelekea yule akachukua Magari ya Makambako hadi Iringa ambapo Jeshi la Polisi kupitia Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, waliweza kumkamata na kumrudisha mpaka Mbeya na akaonesha mtoto alipo.
Na alikiri akiwa huko huko kwamba mtoto nlikwisha muua
Pamoja na kumuua mtoto, aliendelea kudai mil 10 ili aoneshe mtoto alipo.
Chelamila amesema Mauaji haya haya mahusiano na migogoro yoyote ya kidini, ya kiukoo wala ya kikabila.
Mtekaji aliaema alifanya hivyo kutokana na uchu wa hela sababu alipokuwa gerezani kafungwa alisikia watu wakipiga stori kwamba walikuwa wanatumia mbinu hizo kupata fedha ndipo naye akafanya, bahati mbaya mtoto akawa amefariki.
Mkuu wa mkoa amewata wananchi kuendelea kuwa wamoja kuamini jeshi la Polisi na vyombo vyote vya ulinzi na Usalama.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya Ulrich Matei amsema, Tarehe 9/04/2019 Majira ya saa kumi na mbili huko mtaa wa shinga Igalilo tarafa ya Iyunga jijini Mbeya, Junior Bakari Siame wa miaka 8 Mnyamwanga na mwanafunzi wa darasa la tatu. Aliuawa na mtu asiyejulikana katika shamba moja la mahindi lililopo Mlima nyoka.
Mtuhumiwa alipokutana na marehemu alimuuliza kwenu kuna mali gani? akaambiwa nyumba na gari na baba anataka kuliuza hilo gsri. Wakaenda wote hadi nyumbani ili mtoto akabadilishe nguo na kwenda kutafuta mteja wa gari..
Walitembea kwa mguu hadi nane nane na wakapanda gari nanenane na kwenda hadi Saraga. Walipofika saraga ndo mzazi alianza kupigiwa simu ili atoe Milioni 10.
Na mnamo tarehe 14/04/2019 Majira ya saa saba, mtuhumiwa alikamatwa Iringa katika stand ya Ipogoro na kurudishwa Mbeya.
Mtuhumiwa anaonesha alishawahi kuwa na kesi ya kubaka kule Mwanza Criminal case namba 44 ya mwaka 2017 ambapo alifungwa mika 30. Na alitoka kwa rufaa tarehe 22 mwezi wa Pili mwaka huu kule mwanza.