Mathias Byabato
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,020
- 691
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Lawrence Masha na Mbunge wa Jimbo la Busega Raphael Chegeni pamoja na vijana 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya wakituhumiwa kuvunja nyumba ya muwekezaji wa zao la Parachichi Peter Cruise kinyume cha taratibu.
Masha na wenzake wanadaiwa kufanya fujo hizo wakidai wana amri halali ya Mahakama Kuu ya kuwatoa nje mke wa Peter aitwaye Petra na mwanasheria wake Robyin Kennedy wakati mmiliki akiwa amesafiri.
Pia wanadaiwa kuwajeruhi kwa kuwapiga watu hao ambao baada ya kupigwa waliripoti tukio hilo kituo cha polisi Tukuyu na kisha kutibiwa katika hospital ya wilaya ya Makandana.
Masha na wenzake wanadaiwa kufanya fujo hizo wakidai wana amri halali ya Mahakama Kuu ya kuwatoa nje mke wa Peter aitwaye Petra na mwanasheria wake Robyin Kennedy wakati mmiliki akiwa amesafiri.
Pia wanadaiwa kuwajeruhi kwa kuwapiga watu hao ambao baada ya kupigwa waliripoti tukio hilo kituo cha polisi Tukuyu na kisha kutibiwa katika hospital ya wilaya ya Makandana.