Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya sekondari Sinde jijini Mbeya, Faraja Kasole (16), ameuawa kwa kukatwa na shoka shingoni na mwanafunzi mwenzie aitwaye Humphrey Ngogo (17) mwanafunzi wa kidato cha tano shule ya sekondari Iduda, baada ya kushindwa kumbaka.
Chanzo cha mauaji hayo kimedaiwa kuwa ni tamaa za kimwili ambapo mtuhumiwa Ngogo alifanya jaribio la kumbaka marehemu, lakini baada ya kuzidiwa nguvu akachukua shoka na kumpiga nalo kichwani.
East Africa Radio
============
MWANAFUNZI wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari Sinde jijini Mbeya, Faraja Kasole ( 16) ameuawa kwa kukatwa na shoka shingoni na mwanafunzi mwenzie aitwaye Humphrey Ngogo ( 17) mwanafunzi wa kidato cha tano Shule ya Sekondari Iduda.
Chanzo cha mauaji hayo kimedaiwa kuwa ni tamaa za kimwili ambapo mtuhumiwa Ngogo alifanya jaribio la kumbaka marehemu lakini baada ya kuzidiwa nguvu akachukua shoka na kumpiga nalo kichwani.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Jeshi la Polisi, Mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ulrich Matei, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba kabla ya tukio hilo, mtuhumiwa alifika nyumbani kwa marehemu ambaye kwa muda huo alikuwa peke yake na kisha kumvamia chumbani kwake kwa nia ya kumbaka na alipozidiwa nguvu ndipo alimua kuchukua shoka na kumpiga nalo.
Kamanda Matei alisema baada ya upelelezi wa jarada hilo unaendelea na mara baada ya kukamilika atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua nyingine za kisheria ikiwamo mtuhumiwa kuchukuliwa hatua.
“ Jeshi la Polisi linalaani tukio hili kikatili na linatoa pole kwa wazazi na familia ya marehemu, hata hivyo tunatoa rai kwa wazazi au walezi kujenga tabia ya kuzungumza na watoto wao kuhusu masuala ya makuzi huku wakisisitiza kujikitiza zaidi kwenye masomo na kuachana na tama za kimapenzi wangali masomoni ili kujiepusha na matukio kama hayo,” alisema Kamanda Matei.
Katika hatua nyingine Kamanda Matei alisema wanamshikilia, mfanyabiashara Mabula Mabhembe (35) mkazi wa kijiji cha Ifumbo wilayani Chunya kwa tuhuma za kuuza dawa za kulevya aina ya bangi katika duka lake la kuuza bidhaa za nyumbani.
Alisema mtuhumiwa huyo alikamatwa Septemba 5 mwaka huu majira ya saa 11 jioni akiwa na magunia matatu yenye ujazo wa kilogramu 20 , misokoto 3500 pamoja rizla boksi mbili ndani ya duka lake.
Aliongeza kuwa mtuhumiwa alikiri kufanya biashara ya kuuza dawa hizo za kulevya kwa kushirikiana na mtuhumiwa mwingine aitwaye Hamis Shauritanga ambaye anaendelea kutafutwa na Jeshi la Polisi.
“Tayari tumemkamata mtuhumiwa mmoja kuhusiana na tukio hilo bado mwingine ambaye tunamtaka popote alipo ajisalimishe kituo cha Polisi, lakini natoa rai kwa wananchi kwa yeyote mwenye taarifa za mahali alipo asisite kuzitoa ili akamatwe na kushughulikiwa kwa mujibu wa sheria,”
Kwa mujibu wa maelezo ya Mjomba wa marehemu, Sauli Mwaisenye alisema maziko yalifanyika Septemba 4 mwaka huu katika makaburi ya Iyela jijini Mbeya na kwamba familia inaomba vyombo vya maamuzi kutenda haki.