Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,001
- 9,866
Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imemhukumu mkazi wa Kata Mjele, Wilaya ya Mbeya, Mateso Wilson (34) kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya kumuua na kunyofoa viungo vya mkewe.
Mateso alidaiwa kumuua mkewe Zaina Mela na kunyofoa viungo vyake yakiwemo maziwa na masikio.
Hakimu Mkazi Mfawidhi, Zawadi Laizer ametoa hukumu leo Jumatano Oktoba 20, 2021 baada ya mahakama kuridhika kuwa ushahidi wa upande wa Jamhuri haukuacha shaka yoyote.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa mnamo April 22 , mwaka 2017 mshtakiwa Wilson alishirikiana kufanya mauaji hayo na wenzake wawili kwa lengo la kupeleka kwa mganga wa kienyeji ili wapate utajiri wa kudumu. Wenzake walioshirikiana nao katika mauaji hayo hawajakatwa.
Hakimu Laizer amesema mahakama imezingatia maelezo ya pande mbili na ushauri wazee wa mahakama kabla ya kufikia uamuzi huo.
Mshtakiwa ambaye alikuwa akiwakilishwa na wakili wa kujitegemea, Hilda Mbele aliiomba mahakama kumpunguzie adhabu.
Hata hivyo, upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Davice Msanga aliomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine.
Hakimu Laizer ameeleza mahakama hiyo kuwa mshtakiwa anahukumiwa kunyogwa hadi kufa ili iwe fundisho kwa watu wengine ambao wanatafuta mali kinyume cha utaratibu.
MWANANCHI
Mateso alidaiwa kumuua mkewe Zaina Mela na kunyofoa viungo vyake yakiwemo maziwa na masikio.
Hakimu Mkazi Mfawidhi, Zawadi Laizer ametoa hukumu leo Jumatano Oktoba 20, 2021 baada ya mahakama kuridhika kuwa ushahidi wa upande wa Jamhuri haukuacha shaka yoyote.
Ilielezwa mahakamani hapo kuwa mnamo April 22 , mwaka 2017 mshtakiwa Wilson alishirikiana kufanya mauaji hayo na wenzake wawili kwa lengo la kupeleka kwa mganga wa kienyeji ili wapate utajiri wa kudumu. Wenzake walioshirikiana nao katika mauaji hayo hawajakatwa.
Hakimu Laizer amesema mahakama imezingatia maelezo ya pande mbili na ushauri wazee wa mahakama kabla ya kufikia uamuzi huo.
Mshtakiwa ambaye alikuwa akiwakilishwa na wakili wa kujitegemea, Hilda Mbele aliiomba mahakama kumpunguzie adhabu.
Hata hivyo, upande wa Jamhuri ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Davice Msanga aliomba mahakama kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa wengine.
Hakimu Laizer ameeleza mahakama hiyo kuwa mshtakiwa anahukumiwa kunyogwa hadi kufa ili iwe fundisho kwa watu wengine ambao wanatafuta mali kinyume cha utaratibu.
MWANANCHI