Mbegu hii mlipanda CCM, leo msilalamike. Tusitiane ujinga wa uzalendo na utu

chawa wa mama

JF-Expert Member
Jun 8, 2020
292
1,083
Wakati Mh. Tundu Antipas Lissu anapigania uhai wake hospitali kwa kupigwa risasi kadhaa sisi tulitaka kumfanyia maombi.

Tulitaka kukusanyika na kumwombea kama taifa, mkakataa!

Hadi Wabunge wenzake waliotaka kwenda kumwona mliwazuia, mkamtenga, mkamnyima haki zake.

Watu walipotaka kuja msiba wa Mkapa mkawazuia, tena kibabe tu.

Siku hizi za karibuni mmeanza kusikika eti watu sio wazalendo na utu, wanaombea wenzao na kuzushia vifo.

Lini nyie mlikuwa na upendo na wenzenu? Lini mlikuwa na utu? Lini mlikuwa na uzalendo?

Mliyaanzisha wenyewe, na kuna mbegu nyingi mlipanda, naona miti yote imekuwa na maua yameanza, mtavuna hivi punde?
 
Tunaomba huyu bwana afe kweli ili basi huu unaoitwa uzushi usiwe uzushi, sijui kwa nini anakuwa mgumu hivi kukata moto, mbona wenzake wa Zambia na Tunisia walikata mioto na mambo yanakwenda kama kawaida
Hahahahahaa you made my day. Watu wenye roho mbaya mara nyingi wanachelewaga kufa..wale wenye roho nzur wanakata moto mapema
 
CCM kitovu cha madhila, chuki na uhasama miongoni mwetu watanzania

1. Chaguzi wanalazimisha ushindi pasipo kushinda

2. Nyakati za majanga na matatizo kwa wapinzani hawaheshimu, hawana huruma, na huzuwia mambo muhimu ya kijamii.... kuombeana kwa Mungu, kusaidiana nk

3. CCM wazushi na wanyanyasaji sana

Ukweli ccm wamebomoa kabisa msingi wa waasisi wa Taifa letu.

Tuliitana ndugu bila kujali niwakanda gani, dini gani nk. Sasa hivi tumehasimishwa nakugombanishwa

Ccm ya sasa nitatizo kwetu watanzania
 
Wakati mh. Tundu Antipas Lissu anapigania uhai wake hospitali kwa kupigwa risasi kadhaa sisi tulitaka kumfanyia maombi.....
Yote uliyozungumza ni kweli kabisa.
Kuna kosa moja kubwa linafanywa na uongozi na wanachama Chadema na ni hili la kushabikia wakati mwingine bila kutafakari.

Wilbroad Slaa akiwa katika peak aliingizwa chaka kuhusu kura feki zilizotokea Zambia.Wakati ule angalau palikuwa na uwazi kiasi na kilichogundulika ni kontena la vipodozi.

Mwaka juzi katika ziara ya kusini kikatokea kilichotokea na Kigogo2014 akiwa ametangulia mbele tukalishwa matango pori mpaka tukavimbiwa na mwisho wa siku ikawa ni aibu.

Siku nne hizi taharuki imetanda na wengi wameshabikia bila kutafakari na leo kauli ya Waziri Mkuu (Kama ni ya kweli) itakuwa imefunga mjadala.

Katiba yetu haitupi ufafanuzi wa muda mabao kiongozi akiwa haonekani tuulize na wote tunajua hasa katika kipindi cha uchaguzi Rais anaomba kura lakini akishaapishwa hamumpangii kitu tena.Hata kama hatumpendi lakini tuvute subra na tuache muda uwe muamuzi mzuri.

Kuna hili la kitengo cha propaganda cha CCM nacho kikiongozwa na magazeti Tanzanite na mwenzio;hawa hata ile kutafakari kuwa ndio chama tawala wamesahau. Wamemzushia Mrema na Mbowe kifo na mawaziri husika wameshindwa kulikemea hilo, hii tayari ni rejea ya kutosha siku zijazo.

Tupende tusipende umoja na mshikamano wetu umepigwa ufa!
 
'
20210312_194832.jpg
 
Yote uliyozungumza ni kweli kabisa.
Kuna kosa moja kubwa linafanywa na uongozi na wanachama Chadema na ni hili la kushabikia wakati mwingine bila kutafakari...

1. Unataka kutuambia CCM ilishinda viti vyote popote CHADEMA ilipogombea kihalali?

2. Je, kupiga marufuku wote waliotaka kufunga na kumuombea Lissu alipopigwa risasi ni akili?

3. Ni kwa vipi iwe maumivu CCM wanapopata maumivu ila Mawazo isiwe maumivu kiasi kwamba hata maziko yalizuiliwa?
 
1. Unataka kutuambia ccm ilishinda viti vyote popote cdm ilipogombea kihalali?

2. Je, kupiga marufuku wote waliotaka kufunga na kumuombea Lisu alipopigwa risasi ni akili?

3. Nikwavipi iwe maumivu ccm wanapopata maumivu ila Mawazo isiwe maumivu kiasi kwamba hata maziko yalizuiliwa?
Hukunielewa, kinyume chake ndicho nilichodhamiria.
 
Back
Top Bottom