Mbatia aumbuka Arusha, wananchi aliowakusanya walalamikia malipo

nyamadoke75

Member
Apr 1, 2020
86
280
Mwenyekiti wa NCCR -Mageuzi Taifa, James Mbatia amejikuta kwenye wakati mgumu Mara baada ya kuishiwa fedha za kuwalipa waendesha pikipiki aliokuwa amewakusanya kuhudhulia mkutano wake kama wanachama wapya.

Mbatia alifika katika ukumbi wa hotel ya Corridor Spring jijini Arusha majira ya saa 6.30 mchana na baada ya salamu mbalimbali kutoka kwa wanachama aliodai wamehama kutoka vyama vingine vya upinzani, alianza kuhutubia na baadaye alitoa kadi kwa wanachama hao wapya wapatao 225.

Hata hivyo baada ya zoezi hilo kukamilika baadhi ya waendesha pikipiki walizingira gari la Mbatia na kuanza kumzonga wakitaka malipo yao ya sh, 10,000 hadi 20,000 waliokuwa wameahidiwa wakati wakikusanywa kutoka kwenye vijiwe vya pikipiki, hata hivyo hadi anaondoka.eneo hilo baadhi yao waliohudulia mkutano. Huo walikuwa bado wamekaa nje ya hoteli hiyo wakisubiri malipo yao huku wengine wakichana kadi kwa hasira walizokabidhiwa na kuzitupa.

Amani Mbise, Joshua Omari na Matayo Palangyo walisema kuwa wao wamefuatwa kwenye vijiwe vya boda boda na kuambiwa tuhudhulie mkutano wa Mbatia kwa muda WA masaa mawili tu tutapewa shilingo 10,000.

"Tumekaa ukumbini tangu SAA nne asubuhi hadi alipokuja SAA sita mchana, tumeshangaa akitugawia kadi za chama chake huku tukitambulishwa kuwa ni wanachama wapya" Alisema mmoja ya waendesha pikipiki Matayo Palangyo.

Watu hao walienda mbali zaidi wakidai kuwa mpango anaoufanya wa kununua wanachama kupitia waendesha pikipiki bila kuwalipa fedha alizoahidi ni kuwadhulumu muda wao wa kazi.

IMG-20200610-WA0014.jpeg
IMG_20200610_144117.jpeg
 

Attachments

  • IMG_20200610_144117.jpeg
    IMG_20200610_144117.jpeg
    90 KB · Views: 1
Huyu mama Tz anakwama wapi? Wenzake wako bungeni wanatoa mipasho kuhusu Mbowe yeye kaamua ajiongeze kununua watu bila malipo stahiki.!!
Tz ina shangaza kwa kweli.

Sio kwamba hataki kuwa bungeni, hayo ni maagizo ya waliomnunua, na vile fungu wameshampa wanampa muongozo nini cha kufanya. Huoni yeye anaribuni wanachama na wafuasi wa upinzani tu, lakini ni marufuku kusema kawapata wanaccm, maana mkataba wa manunuzi haruhusiwi hilo.
 
Hao ndio tunadhani ni think tank wa taifa hili kama system yenyewe ndo hawa kina mbatia na tuna ambiwa na senior kabisa basi kuna tatizo mahali, Utaifa umewekwa kando lakini uzuri ni kuwa hawa wanayo yapigania lazima yatawaumiza tu na wao Jana edo alikuwa analilia tume huru wakati juzi tu alikuwa hataki kusikia kuhusu hilo.

leo kamilus anasema aguswe anuke wakati ni jana tu mfumo ulikuwa upande wake, Sisi wafrica hatuangalii kesho yetu ndo mana tunajishibisha tu wenyewe, Ukisikiliza wabunge tena vijana unasikitika sana yani kama wanakufa kesho kumbe wana miaka mbele.
 
Mbatia anatia huruma sana na sijui ni kwanini hasomi alama za nyakati au kupitia kwa kina Lyatonga na Lipumba
Sio kwamba hataki kuwa bungeni, hayo ni maagizo ya waliomnunua, na vile fungu wameshampa wanampa muongozo nini cha kufanya. Huoni yeye anaribuni wanachama na wafuasi wa upinzani tu, lakini ni marufuku kusema kawapata wanaccm, maana mkataba wa manunuzi haruhusiwi hilo.
 
Tatizo kubwa linalo tukabili na kuangamiza ndoto zetu kama taifa ni kuendelea kuwepo kwa ccm
Hao ndio tunadhani ni think tank wa taifa hili kama system yenyewe ndo hawa kina mbatia na tuna ambiwa na senior kabisa basi kuna tatizo mahali, Utaifa umewekwa kando lakini uzuri ni kuwa hawa wanayo yapigania lazima yatawaumiza tu na wao Jana edo alikuwa analilia tume huru wakati juzi tu alikuwa hataki kusikia kuhusu hilo leo kamilus anasema aguswe anuke wakati ni jana tu mfumo ulikuwa upande wake, Sisi wafrica hatuangalii kesho yetu ndo mana tunajishibisha tu wenyewe, Ukisikiliza wabunge tena vijana unasikitika sana yani kama wanakufa kesho kumbe wana miaka mbele
 
Kikaragosi ni LAZIMA kifuate masharti vinginevyo itakula kwake viti 30 alivyoahidiwa ili awe chama FAKE kikuu cha upinzani VITAOTA MBAWA.

Sio kwamba hataki kuwa bungeni, hayo ni maagizo ya waliomnunua, na vile fungu wameshampa wanampa muongozo nini cha kufanya. Huoni yeye anaribuni wanachama na wafuasi wa upinzani tu, lakini ni marufuku kusema kawapata wanaccm, maana mkataba wa manunuzi haruhusiwi hilo.
 
Nilimdharau pale alipo kuwa analialia baada ya kubwagwa na mwana dada Halima Mdee pale kawe
Kikaragosi ni LAZIMA kifuate masharti vinginevyo itakula kwake viti 30 alivyoahidiwa ili awe chama FAKE kikuu cha upinzani VITAOTA MBAWA.
 
Kwanini hawa wakina Kawe Alumni, Yehodaya, JohnBaptist, na wengine msiende kumuongezea nguvu Mbatia?

Nyie mmempa pesa tu, halafu pesa zenyewe anazitoa kwa mawazo kama za kwake!.
 
Huyu mama Tz anakwama wapi? Wenzake wako bungeni wanatoa mipasho kuhusu Mbowe yeye kaamua ajiongeze kununua watu bila malipo stahiki.!!
Tz ina shangaza kwa kweli.
Hii nchi kupiga hatua inategemea kudra za mwenyezi Mungu
 
Back
Top Bottom