Mbadala wa Samsung Note Edge ni upi?

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mambo zenu wakuu?

Nilikuwa natumia Samsung Note Edge imeniharibikia na nilipoenda kutafuta nyingine kwa lengo la kununua mpya nimeambiwa batch hii haikutoka tena hivyo ni out of stock.

Kiukweli niliizoea sana na sijui ipi ni mbadala wake.

Naombeni ushauri nihamie kwenye Samsung ipi? Binafsi ni mtumiaji sana wa simu kikazi na matumizi mengine ya kawaida hivyo nitashukuru nikipata ushauri mzuri ili nisije jutia.

Nipo hapa kupokea mapendekezo..
 
Asante sana mkuu Jose,
Hiyo S8 ikoje na ina sifa zipi? Nadhani ungenisaidia kufafanua zaidi kuliko kuniuliza tena swali.
Ikibidi weka na bei zake ili 'nipime'..
 
Chukua samsung kuanzia note 4-6 ni nzuri sana,hakuna simu nzuri kama samsung note series
 
Mimi nilikuwa na Samsung Note ikanizingua, ili crash halafu nikairudisha kwa matengenezo,ika crash upya.

Wakataka kunipa toleo jipya zaidi, mpya zikawa zinatoka hazina removable batteries au microsd card slots.

Bila hivyo vitu viwili simu siitaki hata kama imewekewa mavumba ya dhahabu.

Nikahamia LG ilipotoka LG G5.

Mpaka leo napeta nayo.
 
Mimi nilikuwa na Samsung Note ikanizingua, ili crash halafu nikairudisha kwa matengenezo,ika crash upya.

Wakataka kunipa toleo jipya zaidi, mpya zikawa zinatoka hazina removable batteries au microsd card slots.

Bila hivyo vitu viwili simu siitaki hata kama imewekewa mavumba ya dhahabu.

Nikahamia LG ilipotoka LG G5.

Mpaka leo napeta nayo.
Asante sana kwa kunipa mwanga kidogo.. Bado sijaziamini sana LG, what's so special with the brand?
 
Chukua samsung kuanzia note 4-6 ni nzuri sana,hakuna simu nzuri kama samsung note series
Asante sana mkuu. Latest hapo ni ipi na uwezo wake ukoje? Bei je? Nitashukuru ukiniweka sawa zaidi boss.
 
Mambo zenu wakuu?

Nilikuwa natumia Samsung Note Edge imeniharibikia na nilipoenda kutafuta nyingine kwa lengo la kununua mpya nimeambiwa batch hii haikutoka tena hivyo ni out of stock.

Kiukweli niliizoea sana na sijui ipi ni mbadala wake.

Naombeni ushauri nihamie kwenye Samsung ipi? Binafsi ni mtumiaji sana wa simu kikazi na matumizi mengine ya kawaida hivyo nitashukuru nikipata ushauri mzuri ili nisije jutia.

Nipo hapa kupokea mapendekezo..
Beth, nimetumia Note zote kasoro Note 6 ambayo haikutoka na 7 ambayo ilileta shida...
Achana S8 ni nzuri ila kama wewe ni mtu wa Note, s8 plus ni nzuri sana ila achana nayo...

Subiri mwezi wa kumi....unatoka mzigo mwingine hatari sana..Samsung Note 8...ikiwa na kalamu na iris scanner...hii itakua habari nyingine...andaa million 2 zako ufurahi...
 
Beth, nimetumia Note zote kasoro Note 6 ambayo haikutoka na 7 ambayo ilileta shida...
Achana S8 ni nzuri ila kama wewe ni mtu wa Note, s8 plus ni nzuri sana ila achana nayo...

Subiri mwezi wa kumi....unatoka mzigo mwingine hatari sana..Samsung Note 8...ikiwa na kalamu na iris scanner...hii itakua habari nyingine...andaa million 2 zako ufurahi...
Note series ndo simu bora kabisa kwa watu tunaotumia simu kama ofisi
 
Asante sana mkuu. Latest hapo ni ipi na uwezo wake ukoje? Bei je? Nitashukuru ukiniweka sawa zaidi boss.
Latest ni note 5,japo na note 4 ni nzuri pia,

Note 4,inauzwa laki 5-7,note 5 inauzwa laki 8-1m
 
Beth, nimetumia Note zote kasoro Note 6 ambayo haikutoka na 7 ambayo ilileta shida...
Achana S8 ni nzuri ila kama wewe ni mtu wa Note, s8 plus ni nzuri sana ila achana nayo...

Subiri mwezi wa kumi....unatoka mzigo mwingine hatari sana..Samsung Note 8...ikiwa na kalamu na iris scanner...hii itakua habari nyingine...andaa million 2 zako ufurahi...
S8 nimeona inapigiwa shangwe sana.. Ni toleo jipya bila shaka. Note Edge niliitumia nikaipenda sana ila hapo awali sikuwa mpenzi wa Note series kwa sababu ya vile vikalamu vyake na ubovu wa batteries zake..
 
Latest ni note 5,japo na note 4 ni nzuri pia,

Note 4,inauzwa laki 5-7,note 5 inauzwa laki 8-1m
Mkuu inaonyesha hizo ziko poa sana japo sijaelewa uzuri wake ni upi haswa.. Ni LTE?
Kuna hizi J Series nazo vipi?
 
Asante sana kwa kunipa mwanga kidogo.. Bado sijaziamini sana LG, what's so special with the brand?
I don't look so much at brands as features and reviews.At a certain level of course.

Kwangu mimi LG na Samsung wako level moja ya ushindani, so ni interchangeable.

Nilipenda LG walivyokuwa na features zangu ninazotaka za microsd card slot na removable battery (LG G5 ilikuja na concept ya simu unayochomeka vitu vingine zaidi kama camera na speakers etc, nikataka ku experiment).

Haijawahi kuniletea tatizo katika miezi kama 18 niliyokuwa nayo.

Ingawa sasa nafikiri nakaribia muda wa kubadilisha au angalau ku reset to factory settings nianze upya kwa sababu ya simu kuanza kujaa makorokoro.
 
Mkuu inaonyesha hizo ziko poa sana japo sijaelewa uzuri wake ni upi haswa.. Ni LTE?
Kuna hizi J Series nazo vipi?
kama umetoka note 4 j series yoyote una downgrade achana nazo,

path ya note 4 edge kwenye ku upgrade kuna
-samsung galaxy s6 edge plus
-samsung galaxy s7 edge plus
-samsung galaxy s8 plus

zote zina edge hizo sema ni pande zote mbili compare na upande mmoja wa note edge,

ila uangalie pia na utunzaji wako simu zote hapo juu zina glass mbele na nyuma zinahitaji utunzaji mzuri ila pia zina warranty ukiharibu bahati mbaya watatengeneza bure.
 
kama umetoka note 4 j series yoyote una downgrade achana nazo,

path ya note 4 edge kwenye ku upgrade kuna
-samsung galaxy s6 edge plus
-samsung galaxy s7 edge plus
-samsung galaxy s8 plus

zote zina edge hizo sema ni pande zote mbili compare na upande mmoja wa note edge,

ila uangalie pia na utunzaji wako simu zote hapo juu zina glass mbele na nyuma zinahitaji utunzaji mzuri ila pia zina warranty ukiharibu bahati mbaya watatengeneza bure.

Asante sana. Hakika umenifumbua macho. Kwa ushauri huu wa kitalaamu now naamini naelekea kupata mbadala niliokuwa nautaka. Just out of curiosity Chief, kinachofanya Samsung iwe 'edge' ni ule mdondoko wa screen?!
 
Asante sana. Hakika umenifumbua macho. Kwa ushauri huu wa kitalaamu now naamini naelekea kupata mbadala niliokuwa nautaka. Just out of curiosity Chief, kinachofanya Samsung iwe 'edge' ni ule mdondoko wa screen?!
yap huo huo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom