Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,883
Naye Nyerere alisema anawasikitikia wananchi wa Njombe, kwani licha ya kulima miti ya nguzo za umeme, wanalazimishwa kuuza kwa Sh. 5,000, huku Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) likiuza nguzo hizo kuanzia Sh. 800,000 hadi Sh. milioni moja.
"Makinda hawatetei bungeni, kwa sababu hazungumzi. Hakuna wakati aliwahi kuwatetea wananchi wa Njombe Kusini bungeni kwamba wana barabara mbovu. Hivyo, tunataka kubadilisha Katiba ili Spika awe Spika na mbunge awe mbunge," alisema Nyerere.
Alisema kutokana na wananchi wengi wa mkoa wa Iringa kunyimwa elimu, wengi wao wamebaki kuwa wafanyakazi za ndani na walinzi na kusema kuwa Chadema inataka mkoa huo utoe madaktari bingwa na wataalamu wengine na kuwa anayetaka mfanyakazi wa ndani aende nchini India.
IPPMedia