Mambo ya pm Lowassa hayo, anatukumbusha enzi zile za pm sokoine.
Lowassa aendelea kuumbua vigogo
Ingawa Wahenga wana msemo usemao mgeni njoo mwenyeji apone kwa mabosi wa mkoa wa Kigoma hali imekuwa tofauti baada ya mgeni wao, Waziri Mkuu Bwana Edward Lowassa kuwaonjesha joto ya jiwe hadharani.
Miongoni mwa walioonja shubiri ya Waziri Lowassa ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Bw. John Mongella ambaye bila kutarajia alijikuta akikatizwa kusoma ripoti yake yenye kurasa zaidi ya 10 wakati ndiyo kwanza amefika ukurasa wa tatu.
Ripoti hiyo ilianza kumchafua Waziri Mkuu pale Mkuu huyo wa Wilaya aliposema kuwa chanzo cha kuzorota kwa kilimo cha kahawa ni ukosefu wa wataalam wa zao hilo.
Bw. Lowassa akasema hayo ni mambo ya zamani asiyotaka kuyasikia katika ziara yake na badala yake anahitaji kuona wakuu hao wa wilaya wakionyesha kwa vitendo uelewa wao baada ya kupigwa msasa wa nguvu na Rais Kikwete kwenye semina elekezi iliyomalizika hivi karibuni huko Arusha.
''John huna taarifa, afadhali twende kwenye ziara'', akasema Bw. Lowassa na kuinuka kuendelea na ziara.
Bosi mwingine aliyekumbwa na kasheshe hilo ni Mkuu wa wilaya ya Kibondo Luteni Kanari John Mzurikwao ambaye naye aliambiwa ripoti yake ni mbovu.
Waziri Mkuu akazidi kumuumbua mkuu huyo wa wilaya kwa kusema kuwa anashangazwa na utendaji wake wa kazi kwa vile ni tofauti kabisa na jinsi anavyomfahamu.
Akasema inaonekana wakuu hao wa wilaya hawakuambulia kitu katika semina elekezi iliyoendeshwa na Rais Kikwete hivi karibuni katika hoteli ya Ngurdoto iliyopo nje kidogo ya Jiji la Arusha.
''Inaonyesha kuwa semina ile haikueleweka wala hotuba ya Rais aliyoitoa mwishoni mwa mwezi uliopita haikusikilizwa, ndio maana mambo haya yanajitokeza'', akasema Bw. Lowassa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Lowassa pia akamuibukia Katibu Tawala wa wilaya ya Kigoma, Bw. Martin Mgongolwa na wakurugenzi wa wilaya hiyo kwa kushindwa kumsaidia mkuu wa wilaya na badala yake wakamuandalia hotuba iliyopitwa na wakati.
Akasema Mkuu wa wilaya hiyo bado ni mgeni na anahitaji msaada wa viongozi wengine wa wilaya ambao wana uzoefu na maeneo yao.
''Mnashindwa kuwasaidia vijana hawa na mnataka sisi tuwashambulie bure'', akacharuka Bw. Lowassa.
Waziri Mkuu yuko mkoani Kigoma kwa ziara ya siku tano akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo.
Lowassa aendelea kuumbua vigogo
Ingawa Wahenga wana msemo usemao mgeni njoo mwenyeji apone kwa mabosi wa mkoa wa Kigoma hali imekuwa tofauti baada ya mgeni wao, Waziri Mkuu Bwana Edward Lowassa kuwaonjesha joto ya jiwe hadharani.
Miongoni mwa walioonja shubiri ya Waziri Lowassa ni Mkuu wa Wilaya ya Kigoma, Bw. John Mongella ambaye bila kutarajia alijikuta akikatizwa kusoma ripoti yake yenye kurasa zaidi ya 10 wakati ndiyo kwanza amefika ukurasa wa tatu.
Ripoti hiyo ilianza kumchafua Waziri Mkuu pale Mkuu huyo wa Wilaya aliposema kuwa chanzo cha kuzorota kwa kilimo cha kahawa ni ukosefu wa wataalam wa zao hilo.
Bw. Lowassa akasema hayo ni mambo ya zamani asiyotaka kuyasikia katika ziara yake na badala yake anahitaji kuona wakuu hao wa wilaya wakionyesha kwa vitendo uelewa wao baada ya kupigwa msasa wa nguvu na Rais Kikwete kwenye semina elekezi iliyomalizika hivi karibuni huko Arusha.
''John huna taarifa, afadhali twende kwenye ziara'', akasema Bw. Lowassa na kuinuka kuendelea na ziara.
Bosi mwingine aliyekumbwa na kasheshe hilo ni Mkuu wa wilaya ya Kibondo Luteni Kanari John Mzurikwao ambaye naye aliambiwa ripoti yake ni mbovu.
Waziri Mkuu akazidi kumuumbua mkuu huyo wa wilaya kwa kusema kuwa anashangazwa na utendaji wake wa kazi kwa vile ni tofauti kabisa na jinsi anavyomfahamu.
Akasema inaonekana wakuu hao wa wilaya hawakuambulia kitu katika semina elekezi iliyoendeshwa na Rais Kikwete hivi karibuni katika hoteli ya Ngurdoto iliyopo nje kidogo ya Jiji la Arusha.
''Inaonyesha kuwa semina ile haikueleweka wala hotuba ya Rais aliyoitoa mwishoni mwa mwezi uliopita haikusikilizwa, ndio maana mambo haya yanajitokeza'', akasema Bw. Lowassa.
Kana kwamba hiyo haitoshi, Lowassa pia akamuibukia Katibu Tawala wa wilaya ya Kigoma, Bw. Martin Mgongolwa na wakurugenzi wa wilaya hiyo kwa kushindwa kumsaidia mkuu wa wilaya na badala yake wakamuandalia hotuba iliyopitwa na wakati.
Akasema Mkuu wa wilaya hiyo bado ni mgeni na anahitaji msaada wa viongozi wengine wa wilaya ambao wana uzoefu na maeneo yao.
''Mnashindwa kuwasaidia vijana hawa na mnataka sisi tuwashambulie bure'', akacharuka Bw. Lowassa.
Waziri Mkuu yuko mkoani Kigoma kwa ziara ya siku tano akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo.