Maziwa ya Ng'ombe hayashauriwi kupewa Mtoto mwenye chini ya Mwaka mmoja

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Maziwa ya ng’ombe ni mojawapo ya chakula kilicho na virutubisho vingi vinavyofaa kwa afya ya binadamu. Pamoja na ubora wake huu, aina hii ya maziwa haifai kwa mtoto mwenye umri chini ya mwaka mmoja kutokana na sababu kuu tatu.

Moja, huwa na kiasi kidogo sana cha madini ya chuma ambayo hayawezi kukidhi mahitaji ya mtoto ambaye hukua kwa kasi wakati huo, hivyo kuyategemea sana kunaweza kusababisha mtoto apatwe na changamoto ya upungufu mara kwa mara wa damu.

Pili, miongozo mbalimbali ya WHO , CDC pamoja na utafiti maarufu sana wa Ekhard E Ziegler et al (2007) vinaelezea kuwa wastani wa asilimia 40 ya watoto chini ya mwaka mmoja wanaopatiwa maziwa ya ng’ombe hupatwa na tatizo la kuvujia kwa damu kwenye utumbo hivyo kuwafanya wapoteze damu nyingi kupitia choo.

Tatu, huwa na kiasi kikubwa sana cha protini pamoja na madini ambavyo kwa umri wake huwa ni ngumu sana kuvitunza mwilini. Kiasi cha ziada hupaswa kutolewa kupitia mkojo, hivyo ni lazima mwili wa mtoto upoteze pia maji mengi katika kutoa nje uchafu huu. Kuna taarifa za uhakika kuwa watoto wanaopatiwa maziwa ya ng’ombe kwenye umri huu hukabiliwa mara kwa mara na tatizo la upungufu mkubwa wa maji mwilini.

Maziwa haya ni mazuri kwa afya. Yanapaswa kutolewa kwa mtoto baada ya kufikia mwaka mmoja na siyo chini ya hapo.

Chanzo: AfyaInfo
 
Mama hana maziwa ya kutosha ana mtto wa miezi 4 anataka amuanzishie maziwa ya kopo yapi ninmazuri kwa umri wa mtto huyu
 
Maziwa ya ng’ombe ni mojawapo ya chakula kilicho na virutubisho vingi vinavyofaa kwa afya ya binadamu. Pamoja na ubora wake huu, aina hii ya maziwa haifai kwa mtoto mwenye umri chini ya mwaka mmoja kutokana na sababu kuu tatu.

Moja, huwa na kiasi kidogo sana cha madini ya chuma ambayo hayawezi kukidhi mahitaji ya mtoto ambaye hukua kwa kasi wakati huo, hivyo kuyategemea sana kunaweza kusababisha mtoto apatwe na changamoto ya upungufu mara kwa mara wa damu.

Pili, miongozo mbalimbali ya WHO , CDC pamoja na utafiti maarufu sana wa Ekhard E Ziegler et al (2007) vinaelezea kuwa wastani wa asilimia 40 ya watoto chini ya mwaka mmoja wanaopatiwa maziwa ya ng’ombe hupatwa na tatizo la kuvujia kwa damu kwenye utumbo hivyo kuwafanya wapoteze damu nyingi kupitia choo.

Tatu, huwa na kiasi kikubwa sana cha protini pamoja na madini ambavyo kwa umri wake huwa ni ngumu sana kuvitunza mwilini. Kiasi cha ziada hupaswa kutolewa kupitia mkojo, hivyo ni lazima mwili wa mtoto upoteze pia maji mengi katika kutoa nje uchafu huu. Kuna taarifa za uhakika kuwa watoto wanaopatiwa maziwa ya ng’ombe kwenye umri huu hukabiliwa mara kwa mara na tatizo la upungufu mkubwa wa maji mwilini.

Maziwa haya ni mazuri kwa afya. Yanapaswa kutolewa kwa mtoto baada ya kufikia mwaka mmoja na siyo chini ya hapo.

Chanzo: AfyaInfo
Bandiko swaaafi kabisa. Hongera sana.
To add on that, kwa jamii nyingi za kiafrika most people hawawez kuafford kununua formula a.k.a maziwa ya makopo, therefore kuna jinsi ya kuchanganya maziwa ya ngombe na maji ili kusaidia mtoto kuweza kuya digest vizuri with minimal side effects
 
Mama hana maziwa ya kutosha ana mtto wa miezi 4 anataka amuanzishie maziwa ya kopo yapi ninmazuri kwa umri wa mtto huyu
Maziwa ya kopo yapo aina tofauti kutokana na umri wa mtoto. Ni vyema kwenda maduka makubwa ya dawa ili kupata the right formula. But angalizo ni kwamba in many cases maziwa haya hua yanaleta risk ya mtoto kupata allergies, so ni kuwa makini.
Also, at 4 months, mtoto anaweza kuanzishiwa complimentary feeding kama ya maziwa ya ng'ombe au uji mwepesi wakat at the same time akiendelea na kunyonya
 
Maziwa ya ng’ombe ni mojawapo ya chakula kilicho na virutubisho vingi vinavyofaa kwa afya ya binadamu. Pamoja na ubora wake huu, aina hii ya maziwa haifai kwa mtoto mwenye umri chini ya mwaka mmoja kutokana na sababu kuu tatu.

Moja, huwa na kiasi kidogo sana cha madini ya chuma ambayo hayawezi kukidhi mahitaji ya mtoto ambaye hukua kwa kasi wakati huo, hivyo kuyategemea sana kunaweza kusababisha mtoto apatwe na changamoto ya upungufu mara kwa mara wa damu.

Pili, miongozo mbalimbali ya WHO , CDC pamoja na utafiti maarufu sana wa Ekhard E Ziegler et al (2007) vinaelezea kuwa wastani wa asilimia 40 ya watoto chini ya mwaka mmoja wanaopatiwa maziwa ya ng’ombe hupatwa na tatizo la kuvujia kwa damu kwenye utumbo hivyo kuwafanya wapoteze damu nyingi kupitia choo.

Tatu, huwa na kiasi kikubwa sana cha protini pamoja na madini ambavyo kwa umri wake huwa ni ngumu sana kuvitunza mwilini. Kiasi cha ziada hupaswa kutolewa kupitia mkojo, hivyo ni lazima mwili wa mtoto upoteze pia maji mengi katika kutoa nje uchafu huu. Kuna taarifa za uhakika kuwa watoto wanaopatiwa maziwa ya ng’ombe kwenye umri huu hukabiliwa mara kwa mara na tatizo la upungufu mkubwa wa maji mwilini.

Maziwa haya ni mazuri kwa afya. Yanapaswa kutolewa kwa mtoto baada ya kufikia mwaka mmoja na siyo chini ya hapo.

Chanzo: AfyaInfo
Huu uzi hauna wachangiaji kabisa kama huku JF watu hawana watoto au hawajapitia changamoto za wenza au kina mama kukosa maziwa.

Mimi nimeshujudia mtoto wa kaka yangu ambaye kwa muda mrefu mama yake kakosa maziwa tangia hapo awali yalibahatika kupatikana kidogo ndani ya miezi mitatu tuu ila wakaanza kumpa ya kopo na baadae kidogo akaendele na ya ng'ombe na sasa ameshatimiza miaka miwili.
Hivyo wakati mwingine haya pia ni msaada sana hasa kama watu kipato kinayumba.

Ila kikubwa ni kuzingatia huu ushauri uliotolewa na wataalamu.
 
Back
Top Bottom