Maziwa kwa Mtoto

M

MegaPyne

Guest
WanaJF,

Natafuta maziwa kwajili ya mtoto wangu, ana miezi mitatu na mama yake anaishiwa maziwa siku zinavyozidi.

Hapa bongo mnanishauri nitumie maziwa gani?
 
Nakushauri tumia maziwa ya ng'ombe ya kopo hayaaminiki sana hope unakumbuka ishu ya MELAMINE
 
WanaJF,

Natafuta maziwa kwajili ya mtoto wangu, ana miezi mitatu na mama yake anaishiwa maziwa siku zinavyozidi. Hapa bongo mnanishauri nitumie maziwa gani?

Acha kucheza na afya ya mtoto wako. Miezi mitatu unafanya kuulizia ushauri wa maziwa humu!

Kumbuka lishe ya mtoto ndio ina-determine afya yake ya sasa na hata ukubwani, hivyo nenda kaonane na wataalamu wa afya mara moja (ma-daktari) kwa ajili ya uchunguzi wa mama na ushauri sahihi na mzuri zaidi.

Hii unayofanya sasa na kama matibabu kwa njia ya posta ya waganga wa jadi. Period.
 
Mkuu tafuta Maziwa ya S26, itasaidia, pole sana

Ni kati ya maziwa ya kopo ninayoyaamini, muulize na docta pia uone atakushauri utumie maziwa gani.

Tatizo la maziwa ya ng'ombe ni kwamba unanunua uwe unawafahamu na kuwaamini wauzaji maana wengine wanaweza kuchanganya na maji pia ng'ombe akawa na matatizo bado anakamuliwa maziwa.

Hivyo inakuwa siyo salama lakini kama unawafahamu unawaambia ni maziwa ya mtoto, maziwa ya ng'ombe ni mazuri kwa maana ni natural zaidi kuliko ya kopo.

Ila kama ya kopo S26 ni mazuri!
 
Ni kati ya maziwa ya kopo ninayoyaamini, muulize na docta pia uone atakushauri utumie maziwa gani.
Tatizo la maziwa ya ng'ombe ni kwamba unanunua uwe unawafahamu na kuwaamini wauzaji maana wengine wanaweza kuchanganya na maji pia ng'ombe akawa na matatizo bado anakamuliwa maziwa. Hivyo inakuwa siyo salama lakini kama unawafahamu unawaambia ni maziwa ya mtoto, maziwa ya ng'ombe ni mazuri kwa maana ni natural zaidi kuliko ya kopo.

Ila kama ya kopo S26 ni mazuri!

Yes, huyu mheshimiwa amtafutie S26......kama ulivyosema, maziwa ya ng'ombe tatizo lake kubwa ni wafugaji wetu na wazalishaji wa maziwa hayo siyo waaminifu na wanatamaa sana(huchanganya na maji).

Mwenyewe mtoto wangu alipokuwa mdogo, nilimwomba jamaa mmoja awe ananiletea maziwa ya ng'ombe but yule jamaa despite the fact nilimwambia ni ya mtoto aliendelea kuchanganya na maji so had to stop na kukimbilia S26....ni mazuri ila be careful, kuna S26 feki!
 
Pata ushauri wa daktari bingwa wa watoto kabla ya kuamua kumpa mtoto maziwa mbadala!

Pia kwa nini mama yake maziwa yamekoma. Kuna sababu pia kama afya yake ni fresh na anakula vizuri. Je mkeo hana stress yoyote???

Si kawaida sana mama kukosa maziwa kwa miezi mitatu!! Seek medical advice first!!! and do it soon ili mwanao asikose mlo maana inaathiri growth (child milestone development).
 
WanaJF,

Natafuta maziwa kwajili ya mtoto wangu, ana miezi mitatu na mama yake anaishiwa maziwa siku zinavyozidi. Hapa bongo mnanishauri nitumie maziwa gani?

Tafuta daktari wa watoto akupatie ushauri wa uhakika. Mama kuishiwa maziwa ni tatizo ambalo ni la kawaida.

Kwa sasa, mnaweza kujaribu uji mwepesi sana, na mtoto jinsi anavyokuwa ataendelea kunywa uji mzito zaidi na hadi kufikia vyakula vya kupondwa.

Maziwa ya kopo siyo ya kuamini sana...most likely ni zile fake/lead-tainted kutoka China.
 
Kwa sasa, mnaweza kujaribu uji mwepesi sana, na mtoto jinsi anavyokuwa ataendelea kunywa uji mzito zaidi na hadi kufikia vyakula vya kupondwa.
Uji ama vyakula vingine nje ya maziwa not recommended below age 4 months (UN, WHO, UNICEF, MoHSW-TZ)
 
Pole sana kaka, nenda hospitali ukapate ushauri wa kitaalamu kwa nini mkeo anakosa maziwa obvious there is somthing behind that.

S26 itasiaidia sana kwa mwanao but kwa mkeo bado tatizo liko pale pale.
 
Back
Top Bottom