Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Siku chache Mara baada ya serikali wilayani Hai kusitisha uhamisho wenye utata wa Mkuu wa shule ya sekondari Lyamungo, Adriano Mushi Mazito yameibuka huku chanzo kikielezwa ni fedha zilizotolewa na Rais Magufuli Tshs milioni 800 kwa ajili ukarabati wa shule hiyo.
Sakata la kuhamishwa ghafla kwa Mkuu huyo wa shule iliamuliwa na katibu tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro (RAS), kwa madai kwamba hana mahusiano mazuri na walimu wenzake na kutakiwa kuhamia Shule ya Sekondari Lemira iliyopo wilayani humo.
Kwa mujibu wa barua ya Tar 23 mach, 2020 iliyoandikwa na Shukuru Maleo ambaye ni fundi ujenzi kwenda kwa Mkuu wa shule ya sekondari Lyamongo akiomba kibarua cha ujenzi katika shule hiyo, inaonyesha kwamba Flugence Mponji ambaye ni msimamizi wa miradi ya elimu mkoani humo ndiye aliyemdhamini fundi huyo aweze kupata kibarua.
Baada ya fundi huyo kuwasilisha barua yake ya maombi ya ujenzi April mosi mwaka huu, bodi ya shule hiyo iliketi na kufanya maamuzi ya kupitia maombi ya kazi ambapo kati ya majina yaliyopitishwa jina la Shukuru Maleo aliyetambulishwa na Mponji kwa mkuu wa shule halikuwepo hapo ndipo kimbembe kilipoanzia.
Hatua hiyo iliibua mtafaruku na chuki baina ya Mkuu wa shule hiyo na baadhi ya wajumbe wa sekretarieti ya mkoa na kwamba mnamo tar 9, April mwaka huu Mkuu huyo wa shule alipokea barua ya uhamisho.
Kutokana na uhamisho huo wa ghafla wa Mkuu huyo wa shule baadhi ya walimu,wazazi na wananchi mbalimbali walihoji sababu ya uhamisho huo hasa Katika kipindi ambacho shule ilipokea sh, milioni 800 zilizotolewa na serikali kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo Kongwe wilayani humo.
Hata hivyo wakati sekeseke hilo likiendelea kuliibuka tetesi kwamba kuna kamati iliundwa kwa ajili ya kufuatilia mahusiano ya Mkuu huyo na walimu wenzake na kwamba taarifa ya kamati hiyo ilidai kwamba mwalimu huyo hakuwa na mahusiano na walimu wenzake.
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo ambaye kwa mujibu wa taratibu ndiye mwajiri wa Mkuu huyo wa shule hakushirikishwa suala hilo na kwamba hata Mkuu huyo pia hakuhojiwa na kamati hiyo.
Jambo hilo limeonyesha wazi kwamba kunampango wa maksudi ili kumwondoa Mkuu huyo wa shule kwa lengo la upigaji wa fedha hizo kutokana na kwamba Mkuu huyo alikuwa akisimamia utaratibu wa matumizi sahihi ya fedha za umma suala ambalo liliwachukiza baadhi ya wakuu wake wa kazi na kuamua kumhamisha ili kupata mianya ya kuchomeka watu wao katika mradi huo ili kujipatia maslahi binafsi.
Suala hilo linaibua dhana mbaya ya matumizi mabaya ya madaraka na uonevu iliyofanywa na ofisi ya katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro na ni mwendelezo wa ukandamizaji wa watumishi wa kada za chini na kati hali ambayo imekuwa ikikemewa na rais John Pombe Magufuli.
Bila shaka vyombo vya dola ikiwemo Takukuru vitafuatilia kwa undani suala hili na kuibua yanayofanywa katika ofisi ya RAS na itakuwa mwanzo mzuri wa kulindwa kwa haki za wanyonge wanaonyanyasika mahala pa kazi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sakata la kuhamishwa ghafla kwa Mkuu huyo wa shule iliamuliwa na katibu tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro (RAS), kwa madai kwamba hana mahusiano mazuri na walimu wenzake na kutakiwa kuhamia Shule ya Sekondari Lemira iliyopo wilayani humo.
Kwa mujibu wa barua ya Tar 23 mach, 2020 iliyoandikwa na Shukuru Maleo ambaye ni fundi ujenzi kwenda kwa Mkuu wa shule ya sekondari Lyamongo akiomba kibarua cha ujenzi katika shule hiyo, inaonyesha kwamba Flugence Mponji ambaye ni msimamizi wa miradi ya elimu mkoani humo ndiye aliyemdhamini fundi huyo aweze kupata kibarua.
Baada ya fundi huyo kuwasilisha barua yake ya maombi ya ujenzi April mosi mwaka huu, bodi ya shule hiyo iliketi na kufanya maamuzi ya kupitia maombi ya kazi ambapo kati ya majina yaliyopitishwa jina la Shukuru Maleo aliyetambulishwa na Mponji kwa mkuu wa shule halikuwepo hapo ndipo kimbembe kilipoanzia.
Hatua hiyo iliibua mtafaruku na chuki baina ya Mkuu wa shule hiyo na baadhi ya wajumbe wa sekretarieti ya mkoa na kwamba mnamo tar 9, April mwaka huu Mkuu huyo wa shule alipokea barua ya uhamisho.
Kutokana na uhamisho huo wa ghafla wa Mkuu huyo wa shule baadhi ya walimu,wazazi na wananchi mbalimbali walihoji sababu ya uhamisho huo hasa Katika kipindi ambacho shule ilipokea sh, milioni 800 zilizotolewa na serikali kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo Kongwe wilayani humo.
Hata hivyo wakati sekeseke hilo likiendelea kuliibuka tetesi kwamba kuna kamati iliundwa kwa ajili ya kufuatilia mahusiano ya Mkuu huyo na walimu wenzake na kwamba taarifa ya kamati hiyo ilidai kwamba mwalimu huyo hakuwa na mahusiano na walimu wenzake.
Taarifa zaidi zimeeleza kuwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo ambaye kwa mujibu wa taratibu ndiye mwajiri wa Mkuu huyo wa shule hakushirikishwa suala hilo na kwamba hata Mkuu huyo pia hakuhojiwa na kamati hiyo.
Jambo hilo limeonyesha wazi kwamba kunampango wa maksudi ili kumwondoa Mkuu huyo wa shule kwa lengo la upigaji wa fedha hizo kutokana na kwamba Mkuu huyo alikuwa akisimamia utaratibu wa matumizi sahihi ya fedha za umma suala ambalo liliwachukiza baadhi ya wakuu wake wa kazi na kuamua kumhamisha ili kupata mianya ya kuchomeka watu wao katika mradi huo ili kujipatia maslahi binafsi.
Suala hilo linaibua dhana mbaya ya matumizi mabaya ya madaraka na uonevu iliyofanywa na ofisi ya katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro na ni mwendelezo wa ukandamizaji wa watumishi wa kada za chini na kati hali ambayo imekuwa ikikemewa na rais John Pombe Magufuli.
Bila shaka vyombo vya dola ikiwemo Takukuru vitafuatilia kwa undani suala hili na kuibua yanayofanywa katika ofisi ya RAS na itakuwa mwanzo mzuri wa kulindwa kwa haki za wanyonge wanaonyanyasika mahala pa kazi.
Sent using Jamii Forums mobile app