Mazishi ya Wapigania Uhuru wa TZ huko Arusha waliouawa kidhalimu 5 January 2011

mwenye taarifa kamili tafadhali atujuze ni watu wangapi wamafariki huko Arusha na hali ikoje sasa
 
Hivi sheria za Polisi Tanzania zaruhusu kuua raia? Kimbari yanukia
aafu police wenyewe hawana hata haaaya jana usiku baaada ya taaarifa ya habari ya arusha ilifuata taaarifa ya habari kuhusu makazi yao yaaani wanaishi nyuumba zina ufa hadi mtoto mdogo anaweeza pita.shime shiime wana jf.
 
Jamani, hata picha za waliojeruhiwa hampost?
Ina maana hakuna mwana JF yeyote aliyetembelea majeruhi hospitali?
 
Natamani leo nikaiangalie ile Kanda ya SARAFINA, wale vijana wenzetu wa Bondeni enzi za kudai UHURU kutoka utawala wa Makaburu(The Boers regime) miaka ile ya 1960s. "FREEDOM IS COMING TOMORROW!
Hakika hawa waliokufa kwa kupigwa risasi na Polisi wa Utawala wa Kimabavu wa CCM kule Arusha ni mashujaa wa Taifa letu.
Tunajua kabisa nchi hii ilipewa Uhuru kwenye kisahani baada ya Hekima na Busara za Mwalimu kuwalainisha Wakoloni. Ni kweli kuna vita kama vya Majimaji vilivopiganwa na kina Chief Mkwawa na kina Mirambo kupinga utawala wa Mkoloni lakini havikufua dafu. Mpaka Mwalimu alipoingia ulingoni baada ya kupita kama karne moja hivi.

Madhara ya kupata Uhuru kwa kupewa kwenye kisahani ni haya tunayoyashuhudia kwa sasa. Kwamba watawala hawajui gharama ya Kumwaga damu kwa umma ukidai Uhuru na Haki za Wananchi. Utawala wa CCM zamani TANU haujawahi kuona vuguvugu la Wananchi wakidai Haki zao za msingi kwa njia ya mapambano.(Peoples Power).

Kwa maana hiyo Watanzania hatujapata Uhuru wetu kikamilifu. Uhuru tulionao ni wa Uhuru wa Bandia au Uhuru wa Bendera. Bado hatujajikomboa Kikatiba,Kisiasa,Kiuchumi,Kifikra na Kimawazo. CCM kwa kujua hili wameamua kutumia udhaifu huu wa Watanzania kutugandamiza na KUTUTAWALA WATANZANIA KWA MABAVU. Kwa lugha nyepesi ni kuwa WHETHER WE LIKE IT OR NOT LAZIMA TUBURUZWE NA CCM KAMA INAVYOTAKA.

Lakini sasa WATANZANIA wameamua kusema SASA BASI. LIWALO NA LIWE TUMECHOKA KUBURUZWA NA CCM. MWISHO WA CCM KUACHIA NGAZI UNANUKIA NA SAA UKUTANI INAONYESHA NI MASAA KADHAA TU KABLA YA ANGUKO.CCM WANATAPATAPA KAMA MFA MAJI.CCM WAMECHANGANYIKIWA NGUVU YA UMMA INAWATIA KIWEWE,WAMEBANWA KILA KONA. WANAJUA WAMELAZIMISHA USHINDI WA URAIS ILHALI WANAJUA WALISHINDWA. BAADA YA KUBANWA KUHUSU KATIBA MPYA NA CHADEMA WAMEONA HAWANA JINSI ISIPOKUWA KUSALIMU AMRI! HAKIKA SIKU ZA CCM ZINAHESABIKA!!!

Makaburu wa Afrika Kusini walikuwa wakiamini kuwa SA haiwezi kutawaliwa na mtu mwingine yeyote hasa Mwafrika. Lakini wako wapi sasa???

CCM msifikiri mna hati miliki ya kuitawala TZ milele, one of these days you will be dead,buried and forgotten forever. Hakuna atakaye walilia wala kuwakumbuka kwa jema lolote mliloifanyia nchi hii zaidi ya KUENDEKEZA UFISAIDI,UBAKAJI WA DEMOKRASIA,WIZI WA MALI YA UMMA NA KUWANYIMA WATU KUTOA MAWAZO YAO KWA UHURU NA MAUAJI YASIYO YA LAZIMA.

SHAME ON YOU CHAMA CHA MAJAMBAZI/MAFISADI(CCM).

Naunga mkono hoja kwa asilimia 100.
 
NAunga Mkono hoja....Tunaomba ndugu zetu wa Arusha watusaidie kupata Taarifa za Waliofia Uhuru na majeruhi pia...
 
Mkuu tutafuatilia ili kupata data kamili za watu waliokufa ila kwa vyovyote lazima wapewe heshima yao kwani walijitoa mhanga kwa mustakabali wa nchi yetu. Nafikiri wana JF watapata taarifa kabla ya saa 12 kwamba wamekufa wangapi. Tatizo lililopo ni kwamba Kamanda wa polisi Andengenye hataki kuonana na waandishi wa habari na pia hospitalini hakuna ushirikiano.
 
Ndugu wananchi wenzangu tunaopigania uhuru wa kweli wa nchi yetu ya Tanganyika, poleni sana. Serikali haramu ya CCM katika jiji la Arusha imeua waajiri wake (wananchi), imewajeruhi, kuwadhalilisha, kuwatesa, kuwapiga mabomu ya machozi, kuwarushia maji washawasha, kuwakera, kuwakimbiza hovyohovyo, kuwafarakanisha na familia na ndugu zao, kuwasababisha wasiendelee na kazi zao za kujipatia kipato, na kuwadharau. Imewaweka korokoroni viongozi halali wa wananch, na leo nasikia itawafikisha mahakamani.

Wakati kwenye thread nyingine tunahabarishana kinachojiri na kujieleza hisia zetu, nimeona nianzishe hii thread kuomba na kuelekeza yafuatayo;

1. Tuoneshe heshima yetu ya dhati kwa kuwaenzi wale waliokufa katika harakati hizi za siku ya kwanza ya kudai uhuru na ukombozi wa kweli wa nchi yetu Tanganyika (hata kama ni polisi alikufa). Ndugu, jamaa na marafiki zao watafarijika sana kuona kwamba wamepoteza ndugu zao ambao wanathaminiwa na wananchi wote. Kwanza walio arusha wafuatilie kwa kina details za waliokufa watupatie. Pili, watutangazie tarehe za mazishi kwa kila mmoja wao na eneo/mkoa ambapo maziko yatafanyika. Tatu, chadema wafungue bank account ili tupitishe michango yetu humo kuwafariji waliofiwa. Hii ina maana kama aliyekufa ni bread earner wa familia basi watoto wake wapelekwe shule na mambo kama hayo.

2. Waliojeruhiwa na kulazwa hospitali watambuliwe na kuorodheshwa kwenye tovuti maalumu ya uhuru wa kweli wa Tanganyika (ianzishwe). Kisha walio arusha na wale wanaoweza kusafiri kuelekea huko wawatembelee hawa majeruhi na kuwafariji. Michango yetu pia itumike kugharamia matibabu yao. Wapewe cheti maalumu cha kutambua mchango wao katika kudai uhuru wa kweli ya nchi yetu Tanganyika, ili hata vitukuu vyao viwe na ushahidi wa kujivunia.

3. Kwenye picha za jana, niliona baadhi ya wakina mama wachache sana pale uwanjani. Nilisisimka! Naomba watafutwe nao waorodheshwe na kutambuliwa kwa namna ya pekee. Hawa ndio wanawake wanaojua uwezo wao, siyo wale wanaosubiri kuwezeshwa ndipo waweze. Pia kwenye picha niliona wabunge wanawake wa Chadema na Mke wa Rais wa Ukweli wa Tanganyika, itafurahisha kama watatambuliwa kwa namna ya pekee pia

4. Wapinganaji wenzetu wamekamatwa na polisi na watafikishwa katika mahakama. Tunaomba pia tuchangie gharama za kesi na kujikimu kwao na wale wanaoshuhulikia hili tatizo

5. Tuanzishe kalenda ya ukombozi na kudai uhuru wa Tanganyika, ikianzia tarehe 5 January 2011. Chadema waanzishe kitengo cha kurekodi kumbukumbu za matukio na vitendo vyote kila siku ili vije kutumika kuandika historia ya kweli ya ukombozi wa nchi yetu. Taarifa hizi ziwe wazi kwenye tovuti ili kuepusha kuchakachuliwa kama ccm walivyochakachua histori ya tanzania

6. Kila mmoja wetu katika eneo alilopo, achangie na kugharamia harakati za wananchi wanaounga mkono mapambano ya kuikomboa nchi yetu kutoka kwenye mikono ya hawa makuwadi, matapeli, majambazi, na wauaji. Eneza habari mtaani kwako, kazini kwako na hata mahali popote unapotembelea. Watu wengi bado wana imani kwamba serikali yetu ni tukufu na hawajui matatizo makubwa ya utawala huu uliopo madarakani sasa hivi.

Sina mamlaka wala wadhifa wa kutoa tamko, bali ni mawazo yangu tu

Naunga mkono jitihada zozote zile za kuonesha heshima na masikitiko yetu kwa wale wote waliuwawa, walioumizwa na wale waliopotelewa na ndugu zao na wale wanaouguza ndugu zao. Tupo tayari kushirikiana nao kwa hali zote. Mawazo uliyoyatoa ni mazuri sana, CHADEMA wayatengenezee utaratibu ili kabla vumbi halijatulia, tuanze kulitekeleza hili.
 
Mkuu tutafuatilia ili kupata data kamili za watu waliokufa ila kwa vyovyote lazima wapewe heshima yao kwani walijitoa mhanga kwa mustakabali wa nchi yetu. Nafikiri wana JF watapata taarifa kabla ya saa 12 kwamba wamekufa wangapi. Tatizo lililopo ni kwamba Kamanda wa polisi Andengenye hataki kuonana na waandishi wa habari na pia hospitalini hakuna ushirikiano.

nashukuru sana kwa taarifa zako, poleni pia kwa kunyimwa ushirikiano na huyo Ande*&^%$nzi na hospitali. Watabana lakini lazima wataachia tu. Huyo Ande*&^%$nzi alidhani ni jambo la mchezo tu, sasa kokote aliko lazima ana tumbo la kuhara kwani he has misled the so called police Inteli and the image of the current government has become so ugly and sour, internationally.

tunakusubiri mkuu utupatie updates pindi upatapo
 
Nami naunga mkono jitahadi za kuujulisha umma kwa yote haya yaliyotokea.
Picha na video zichukuliwe na kusambazwa vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi.
Huu ni unyama mkubwa na ukandamizaji wa haki za binadam. Watawala wa taifa hili wanalipeleka kubaya
 
Haya sasa tumeambiwa na Ande*&^%$nzi kwamba watu wawili waliuawa. Sikuweza kunukuu majina yao kamili naomba aliyemsikia vizuri aweke majina hapa. Pia ni vizuri chadema wakathibitisha kama kweli ni hao wawili tu

Vipi hali ya majeruhi? First lady wa ukweli anaendeleaje?
 
Wana wa nchi; topic nzuri na inakubalika. Hii ni muhimu. Viongozi wengine wa cdm watuambie kinachoendelea polisi Arusha. wapelekewe hii post na wajichague ni nani atafuatilia majeruhi na hata wafiwa na waliokufa. watuelekeze tuchangie kupitia njia ipi. Hili litaonyesha uzalendo na pia majitoleo kama hao waliofikwa na maafa jana walivyojitolea. Hayo maandamano yanayodaiwa na hao mapolisi walieleze Taifa na wananchi wote kilichokuwa kinafanyika kwenye maandamano hayo. Kama watu walikuwa wanatembea kuelekea NMC au krokoni kwenye mitumba wote walipigwa mabomu. Its unfair kwa mapolisi watanzania kuwalpiga watanzania wenzao ambao wote tuna dhiki moja. Aibu kuua / kujeruhi ndugu yako ambaye anatetea haki ya wadhulumiwa walio wengi. Ukiona mwenzio akinyolewa nawe tia zako maji. Mungu anaona yote yaliyo sirini na anachunguza mioyo ya watu. Siku ipo yote yatakuwa bayana.
 
Kwani Chadema hawatembelei hapa janvini leo? Mbona hatupati majibu wala maelekezo?
 
Poleni wafiwa wote na Mungu azilaze pema roho za marehemu. Naowaombea afya njema wote waliojeruhiwa. Mungu akipenda Tanganyika huru itakuwepo muda si mrefu. Aluta continua
 
BBC Swahili wanasema watu 10, AFP 2, hlafu sijui wapi tena 4, jamani ni vigumu kufuatilia na kwa jinsi navyojua serikali yetu wanaweza kuwa wamekufa hata zaidi ya hapo na mkaambiwa ni wawili ama mmoja
 
BBC Swahili wanasema watu 10, AFP 2, hlafu sijui wapi tena 4, jamani ni vigumu kufuatilia na kwa jinsi navyojua serikali yetu wanaweza kuwa wamekufa hata zaidi ya hapo na mkaambiwa ni wawili ama mmoja

Lazima wachakachue idadi ya waliokufa, siyo aibu ndogo ati
 
Maoni yangu nitayaelekeza kwako Gurudumu. Itambue talanta yako ya uongozi na kuiboresha kwa manufaa yako na ya wengine. Watu wenye fikra za mfano wako ni nadra kuwapata. Shukrani za dhati kwako kwa kuanzisha mwendo. I salute you!

Lazydog
 
Back
Top Bottom