Mazishi ya Mapadri watatu wa kanisa katoliki jimbo la Same ambao vifo vyao vilipishana kwa siku moja moja yanafanyika katika Seminari ya Chanjare wilayani Mwanga muda huu.
Viongozi wa waandamizi wamehudhuria akiwemo mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira
Historia ya vifo vyao
Akizungumza na waandishi wa habari ofisa mawasiliano wa Kanisa Katoliki Jimbo la Same, Padri Joseph Mlacha, alisema mmoja alifariki akiwa katika mafungo; mwingine akiwa katika uchunguzi wa matibabu na wa tatu ni baada ya kupata taarifa za vifo vya wenzake wawili.
“Kwanza, Padri Michael Kiraghanja alifariki dunia Aprili 11 usiku, Maua Kilema akiwa kwenye mafungo. Habari za kifo chake zikawafikia watu mbalimbali wakiwamo maaskofu, mapadri na waamini kwa jumla,” alisema.
Alisema Padri Kiraghanja alikuwa katika hali ya kawaida lakini ghafla alijihisi vibaya na alitumia dawa za kupunguza maumivu na kwenda kupumzika ambapo alifariki dunia akiwa usingizini.
Padri Mlacha alisema uchunguzi wa awali unaonyesha alifariki dunia kwa maradhi ya kisukari.
“Wakati tukiwa katika maandalizi ya mazishi ya Padri Kiraghanja tukapata taarifa ya kifo cha mwingine Arobogasti Mndeme wa Parokia ya Kirangare aliyefariki Aprili 12 katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyoko mjini Moshi alikokuwa amelazwa,” alisema.
Alisema Padri Mndeme alilazwa hospitalini hapo kwa uchunguzi wa kawaida baada ya kufanyiwa upasuaji akiwa na maradhi ya saratani ya utumbo mpana.
Alisema Padri Ulbadius Kindavari wa Parokia ya Bwambo, kifo chake kilitokea Temeke jijini Dar es Salaam.
“Huyu hatuwezi kutoa taarifa kamili kuhusu kifo chake, ila habari tulizopata ni kuwa alifariki baada kupata mshtuko kutokana na taarifa za vifo vya mapadri wenzake wawili,” alisema.
Pia soma > Mapadri watatu wa Kanisa Katoliki jimbo la Same, wamefariki dunia ndani ya saa 72
Viongozi wa waandamizi wamehudhuria akiwemo mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira
Historia ya vifo vyao
Akizungumza na waandishi wa habari ofisa mawasiliano wa Kanisa Katoliki Jimbo la Same, Padri Joseph Mlacha, alisema mmoja alifariki akiwa katika mafungo; mwingine akiwa katika uchunguzi wa matibabu na wa tatu ni baada ya kupata taarifa za vifo vya wenzake wawili.
“Kwanza, Padri Michael Kiraghanja alifariki dunia Aprili 11 usiku, Maua Kilema akiwa kwenye mafungo. Habari za kifo chake zikawafikia watu mbalimbali wakiwamo maaskofu, mapadri na waamini kwa jumla,” alisema.
Alisema Padri Kiraghanja alikuwa katika hali ya kawaida lakini ghafla alijihisi vibaya na alitumia dawa za kupunguza maumivu na kwenda kupumzika ambapo alifariki dunia akiwa usingizini.
Padri Mlacha alisema uchunguzi wa awali unaonyesha alifariki dunia kwa maradhi ya kisukari.
“Wakati tukiwa katika maandalizi ya mazishi ya Padri Kiraghanja tukapata taarifa ya kifo cha mwingine Arobogasti Mndeme wa Parokia ya Kirangare aliyefariki Aprili 12 katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC iliyoko mjini Moshi alikokuwa amelazwa,” alisema.
Alisema Padri Mndeme alilazwa hospitalini hapo kwa uchunguzi wa kawaida baada ya kufanyiwa upasuaji akiwa na maradhi ya saratani ya utumbo mpana.
Alisema Padri Ulbadius Kindavari wa Parokia ya Bwambo, kifo chake kilitokea Temeke jijini Dar es Salaam.
“Huyu hatuwezi kutoa taarifa kamili kuhusu kifo chake, ila habari tulizopata ni kuwa alifariki baada kupata mshtuko kutokana na taarifa za vifo vya mapadri wenzake wawili,” alisema.
Pia soma > Mapadri watatu wa Kanisa Katoliki jimbo la Same, wamefariki dunia ndani ya saa 72