Mazishi ya Mandela kuvunja rekodiyanalinganishwa na yale ya Papa John Paul II m

Kibo10

JF-Expert Member
Aug 20, 2013
11,277
8,840
Afrika na dunia inatarajiwa kushuhudia kitu kipya katika maziko ya Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela (95) aliyefariki dunia juzi, baada ya kuugua kwa zaidi ya miezi sita.

Serikali ya Afrika Kusini imesema kiongozi huyo ambaye atazikwa Desemba 15, imeandaa mazishi ya kihistoria yanayosemekana yatazidi yale ya Papa John 11.

Matukio ya shughuli mbalimbali zinazohusu mipango ya maziko ya kiongozi huyo maarufu yanatarajiwa kushuhudiwa sehemu mbalimbali duniani, tofauti na tukio jingine lililowahi kutokea barani Afrika mbali na kombe la dunia.

Rais Jacob Zuma alisema jana kwamba “Mpendwa wetu Madiba atazikwa kwa heshima zote za Serikali. Nimeagiza bendera zote za Afrika Kusini zipepee nusu mlingoti na hiyo itaendelea hivyo hadi tutakapokamilisha mazishi yake.

Mazishi ya Mandela yanalinganishwa na yale ya Papa John Paul II mwaka 2005, ambayo yalihudhuriwa na wafalme watano, malkia sita wa falme mbalimbali na marais wapatao 70 na mawaziri kadhaa, wakiwamo wafuasi wake zaidi ya milioni mbili. Yanakadiriwa pia kulingana na maziko ya Winston Churchil aliyekuwa Waziri Mkuu wa Uingereza mwaka 1965.

Marais wote wa Marekani walio hai wanatarajiwa kuhudhuria mazishi hayo iwapo afya zao zitawaruhusu kusafiri, pamoja na Prince Charles wa Uingereza na hata Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe. Pia watu maarufu wenye urafiki wa karibu na Mandela akiwamo msanii Oprah Winfrey wameshathibitisha kuhudhuria.

Kutokana na idadi kubwa ya wakuu wa nchi na watu maarufu duniani wanaotarajiwa kufika Afrika Kusini, suala la usalama limeelezewa kuwa changamoto mpya kwa vyombo vya usalama nchini humo.

Afrika Kusini imekuwa moja ya nchi zinazokabiliwa na matukio ya uporaji na mauaji yanayotokana na idadi kubwa ya wahalifu, wengi wao wakidaiwa kuwa wahamiaji haramu.

“Huyu ni shujaa wa dunia. Tutafanya mipango ya mazishi makubwa ambayo hayajawahi kushuhudiwa. Nadhani kila nchi itakuwa imeandaa utaratibu wake wa namna ya kushiriki,” alisema mmoja wa wanadiplomasia wa Afrika Kusini ambaye hakutaka kutajwa jina lake.

Serikali ya Afrika Kusini, kwa mujibu wa gazeti la The Guardian tayari imeweka wazi ratiba ya siku 11 za maombolezo tangu alipofariki dunia juzi jioni. Japokuwa ratiba hiyo ilishaandaliwa karibu mwaka mmoja uliopita na kupitiwa na kufanyiwa maboresho katika baadhi ya maeneo, inaonyesha namna maofisa wa Serikali ya Afrika Kusini walivyolipa uzito suala hilo na kulifanya kuwa tukio la kukumbukwa katika historia. ImageUploadedByJamiiForums1386407157.658519.jpg
 
anastahili kila aina ya heshima

RIP Mzee Tata N. M. Mandela

The real son of Africa
 
Anastahili! Na mwenyenzi MUNGU mwingi wa Rehema na ampe pumziko la Milele katika shamba lake BWANA WETU sasa na hata Milele!
 
Mandela anastahili kuzikwa kwa heshima zote kwa hakika atakumbukwa na vizazi vya sasa na hata baadae kwa watakao kuwepo.nashauri vijana wadogo wa sasa muisome historia vizuri kumfahamu huyu bwana Mandela ili kujua alichokuwa akipigania. Si jambo rahisi ambalo kila binadamu anaweza kufanya kwa ajili ya kutetea haki ya wake. Rest in peace Madiba
 
Back
Top Bottom