sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
Leo tarehe 13 June,2012 ni siku ambayo wanachadema na wakazi wa mkoa wa shinyanga hawatoisahau, siku ya mazishi ya kipenzi chao hayati Mohamed Ally Nyanga Makani.Ni siku ambayo ilikutanisha kada mbalimbali kwa itikadi tofauti na misimamo ya kichama tofauti.Ni siku ambayo siasa iliwekwa kando na watu wote kuzungumza umoja wa kitaifa.
Bob Makani amekwenda,hatutamuona tena lakini maneno,falsafa na vitendo vyake vitaendelea kubaki kwenye mioyo ya wapenda amani wa Tanzania, ikiwa ni kudumisha mshikamano na umoja wa kitaifa kwa falsafa yake ya nawapenda.
Hotuba mbalimbali kutoka pande zote zilielezea wasifu wake kama kiongozi aliyewapenda na kuwatumikia watu wote bila kujali rangi,dini na itikadi za kichama.Mbali na hotuba hizo,hotuba iliyowagusa sana watu na kuwaacha watu wakiitafakari kwa kina ni hotuba iliyotolewa na mh. Mbowe mwenyekiti wa CDM taifa na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni.Maneno yake ya majonzi yalibeba ujumbe mzito juu ya amani na mshikamano kwa taifa letu.
Kamanda huyu alifika mbali sana kiasi cha kusema mshikamano ulionyeshwa leo usiishie hapa,na kesho yake mnyukano ukachukua mkondo wake katika harakati za kisiasa kuelekea kushika dola.Amani ya Watanzania ni muhimu kuliko CCM na CDM,CDM na CCM vitapita lakini Tanzania itabaki pale pale.
Maneno haya ya mh. Mbowe yawe changamoto kwa mustakabali wa amani ya nchi yetu,maneno haya mara nyingi yamekuwa yanasisitizwa na hayati Bob Makani,Watanzania tusikubali kugawanywa kwa minajili ya kidini,kikabila na kikanda kama propaganda chafu zinazojaribu kupandikizwa na watu waliochoka siasa za kistaarabu.Kwa mantiki hii msiba huu uwe changamoto na mtaji wa rasilimali amani ambayo wengi wanaililia.
Mwisho,tujifunze mengi mema aliyoyafanya mzee wetu huyu,tuwe wazalendo wa kweli na kuipigania nchi yetu mama Tanzania katika kudumisha amani ,ndio njia pekee itakayo weza kuimarisha uchumi,lakini tunda hili la amani likidondoka na uchumi wetu pia utaangamia.Upendo na uzalendo iwe ndiyo mhimili mkubwa katika ujenzi na maendeleo ya taifa hili.Mungu ibariki Afrika ,Mungu ibariki Tanzania.
Bob Makani amekwenda,hatutamuona tena lakini maneno,falsafa na vitendo vyake vitaendelea kubaki kwenye mioyo ya wapenda amani wa Tanzania, ikiwa ni kudumisha mshikamano na umoja wa kitaifa kwa falsafa yake ya nawapenda.
Hotuba mbalimbali kutoka pande zote zilielezea wasifu wake kama kiongozi aliyewapenda na kuwatumikia watu wote bila kujali rangi,dini na itikadi za kichama.Mbali na hotuba hizo,hotuba iliyowagusa sana watu na kuwaacha watu wakiitafakari kwa kina ni hotuba iliyotolewa na mh. Mbowe mwenyekiti wa CDM taifa na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni.Maneno yake ya majonzi yalibeba ujumbe mzito juu ya amani na mshikamano kwa taifa letu.
Kamanda huyu alifika mbali sana kiasi cha kusema mshikamano ulionyeshwa leo usiishie hapa,na kesho yake mnyukano ukachukua mkondo wake katika harakati za kisiasa kuelekea kushika dola.Amani ya Watanzania ni muhimu kuliko CCM na CDM,CDM na CCM vitapita lakini Tanzania itabaki pale pale.
Maneno haya ya mh. Mbowe yawe changamoto kwa mustakabali wa amani ya nchi yetu,maneno haya mara nyingi yamekuwa yanasisitizwa na hayati Bob Makani,Watanzania tusikubali kugawanywa kwa minajili ya kidini,kikabila na kikanda kama propaganda chafu zinazojaribu kupandikizwa na watu waliochoka siasa za kistaarabu.Kwa mantiki hii msiba huu uwe changamoto na mtaji wa rasilimali amani ambayo wengi wanaililia.
Mwisho,tujifunze mengi mema aliyoyafanya mzee wetu huyu,tuwe wazalendo wa kweli na kuipigania nchi yetu mama Tanzania katika kudumisha amani ,ndio njia pekee itakayo weza kuimarisha uchumi,lakini tunda hili la amani likidondoka na uchumi wetu pia utaangamia.Upendo na uzalendo iwe ndiyo mhimili mkubwa katika ujenzi na maendeleo ya taifa hili.Mungu ibariki Afrika ,Mungu ibariki Tanzania.