Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Katika pita pita zangu na uzee huu nimekutana na mengi; yapo ya kusikitisha, kuchekesha na mengine ya kuudhi. Yapo mazuri na mabaya na mengine ya ukichaa kabisa. Lakini kati ya ambayo nimekutana nayo kwa muda na katika mazingira tofauti (bongo na nje) ni hili ambalo mwanamke anajikuta katika mazingira ambayo analazimika kumbambikizia mtu mimba. Na wengine huenda kaburini na siri hiyo kuu ambapo mtoto au watoto wanaweza kufikiri fulani ndiye baba yao kumbe ni mtu mwingine kabisa.
Lakini wengine wanajikuta wanalazimika kumbakizia mtu mtoto kwa sababu ukweli au mtu ambaye kweli anahusika wanajua asingepewa hadhi hiyo ya kuwa baba. Sasa najiluliza ni kweli kabisa mazingira kama hayo yapo kama inavyodaiwa au wakati mwingine ni woga labda kama wangeamua kumwambia mhusika ukweli labda angeelewa na kukubaliana nao. Lakini, kama mhusika hatoambiwa ukweli itakuwaje kama baadaye waje kukutana na kufall in love au watoto wao kukutana kumbe ni ndugu?
Maslahi ya mtoto katika mazingira hayo yanakuwa wapi?
Lakini wengine wanajikuta wanalazimika kumbakizia mtu mtoto kwa sababu ukweli au mtu ambaye kweli anahusika wanajua asingepewa hadhi hiyo ya kuwa baba. Sasa najiluliza ni kweli kabisa mazingira kama hayo yapo kama inavyodaiwa au wakati mwingine ni woga labda kama wangeamua kumwambia mhusika ukweli labda angeelewa na kukubaliana nao. Lakini, kama mhusika hatoambiwa ukweli itakuwaje kama baadaye waje kukutana na kufall in love au watoto wao kukutana kumbe ni ndugu?
Maslahi ya mtoto katika mazingira hayo yanakuwa wapi?