Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,991
Kasi ya Rais Magufuli ya kufyatua vimbwanga inaendelea, Na inafika mahali mtu unajiuliza maswali ya msingi. Wakati anaendesha zoezi la Bomoa Bomoa bila fidia katika maeneo ya Kimara na kuendelea, Rais Magufuli alikuwa mkali kama pilipili, akinukuu sheria ya miaka karibu mia iliyopita. Sheria msumeno. Kabla ya hapo aliendesha bomoa bomoa katika maeneo ya mabondeni, pia akinukuu sheria. vilio vilitawala. Leo anasema amesimamisha bomoa bomoa, siyo makosa ya wananchi. busara itumike.
Hapo nyuma tumeshuhudia watu wakibomolewa nyumba zao kwa sheria ya mita 60 toka mtoni. Kilimo katika maeneo yaliyokatazwa, vyanzo vya maji, ilipelekea kuharibiwa kwa shamba la Mh. Mbowe. Leo tunaambiwa busara itumike.
Inawezekana pia kuna watu walilengwa, na sasa wameshashughulikiwa, "busara ndiyo inatumika"? maana kulilkuwa na operesheni ya kukusanya madeni ya nyumba za NHC. Tulishuhudia jengo ilipokuwepo Bilicanas, iliyomilikiwa na Mh. Mbowe, ndilo pekee lililoshughulikiwa. Mbowe akatimuliwa na baada ya hapo kimya.
Hapo nyuma, Rais Magufuli alitumia sheria zilizotungwa "na wakoloni" kuhusu upana wa barabara ya Morogoro, akabomoa maelfu ya nyumba bila huruma na bila fidia, leo anasema kwamba "hizi sheria tulirithi kutoka kwa wakoloni, zimepitwa na wakati, tuangalie rialite ya watanzania".
Inaeonekana wazi Magufuli ameshatosheka na kisasi chake kwa watu au makundi ya watu, na sasa anaangalia 2020. Amesababisha maumivu makubwa yasiyosemekana kwa watu wengi, amewatia wengi sana umasikini, wengi wamefariki, leo anasema "busara itumike".
Lakini pia kuna baadhi ya maamuzi ambayo anayatoa, mfano kuruhusu wamachinga, halafu baadaye atakauja rais mwingine katili kama yeye au hata kumzidi yeye, naye atasema "sheria msumeno", na kuwafurusha. magufuli atakuwa ametimiza mahitaji yake ya kisiasa kwa sasa lakini hatakuwa ametoa ufumbuzi wa matatizo ya watanzania.
Na hii ndiyo athari ya kuwa na Rais ambaye hatumii wala kufuata "sera" inayoeleweka. leo atasema hivi, kesho atasema vile. Ila burudani kubwa zaidi ni kwamba daima watu watampongeza. akivunja nyumba leo watampongeza kwa kuwa "imara" na mwenye msimamo katika "kuwaletea watanzania maendeleo". kesho akisema "busara itumike" watampongeza kwamba ni Rais "msikivu" na "anayejali maisha ya watanzania".
Hapo nyuma tumeshuhudia watu wakibomolewa nyumba zao kwa sheria ya mita 60 toka mtoni. Kilimo katika maeneo yaliyokatazwa, vyanzo vya maji, ilipelekea kuharibiwa kwa shamba la Mh. Mbowe. Leo tunaambiwa busara itumike.
Inawezekana pia kuna watu walilengwa, na sasa wameshashughulikiwa, "busara ndiyo inatumika"? maana kulilkuwa na operesheni ya kukusanya madeni ya nyumba za NHC. Tulishuhudia jengo ilipokuwepo Bilicanas, iliyomilikiwa na Mh. Mbowe, ndilo pekee lililoshughulikiwa. Mbowe akatimuliwa na baada ya hapo kimya.
Hapo nyuma, Rais Magufuli alitumia sheria zilizotungwa "na wakoloni" kuhusu upana wa barabara ya Morogoro, akabomoa maelfu ya nyumba bila huruma na bila fidia, leo anasema kwamba "hizi sheria tulirithi kutoka kwa wakoloni, zimepitwa na wakati, tuangalie rialite ya watanzania".
Inaeonekana wazi Magufuli ameshatosheka na kisasi chake kwa watu au makundi ya watu, na sasa anaangalia 2020. Amesababisha maumivu makubwa yasiyosemekana kwa watu wengi, amewatia wengi sana umasikini, wengi wamefariki, leo anasema "busara itumike".
Lakini pia kuna baadhi ya maamuzi ambayo anayatoa, mfano kuruhusu wamachinga, halafu baadaye atakauja rais mwingine katili kama yeye au hata kumzidi yeye, naye atasema "sheria msumeno", na kuwafurusha. magufuli atakuwa ametimiza mahitaji yake ya kisiasa kwa sasa lakini hatakuwa ametoa ufumbuzi wa matatizo ya watanzania.
Na hii ndiyo athari ya kuwa na Rais ambaye hatumii wala kufuata "sera" inayoeleweka. leo atasema hivi, kesho atasema vile. Ila burudani kubwa zaidi ni kwamba daima watu watampongeza. akivunja nyumba leo watampongeza kwa kuwa "imara" na mwenye msimamo katika "kuwaletea watanzania maendeleo". kesho akisema "busara itumike" watampongeza kwamba ni Rais "msikivu" na "anayejali maisha ya watanzania".