Maziko ya Bi. Safia bint Juma Makasara - Mama yake Balozi Dr. Dau

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,787
30,083
MAZIKO YA BI SAFIA BINT JUMA MAKASARA MAMA YAKE BALOZI DR. RAMADHANI KITWANA DAU YAMEVUNJA REKODI YA MAZIKO YOTE

Mji wa Dar es Salaam una historia ndefu ya mazishi makubwa yaliyopata kutokea.

Mimi nakua katika miaka ya 1960 nikiwasikia wazee wetu wakihadithia maziko ya Sheikh Idrissa bin Salad Khalifa wa Tariqa Askariyya.

Wanasema maziko yake hayakuwa na mfano.

Nimeanza na Sheikh Idrissa bin Saad kwa sababu wazee wakipenda kuanza historia hii na yeye.

Lakini historia hii ya maziko inakwenda nyuma kiasi cha zaidi ya miaka takriban 100 kabla yao kwa hesabu ya wakati ule.

Kwa ajili hii maziko makubwa ya kwanza ni ya Sheikh Mwinyikheri Akida, sheikh aliyeasisi Msikiti wa Mwinyikheri Akida ulioko Kisutu.

Kisha yanafuatia maziko ya Sheikh Idrissa bin Saad.

Yanafuatia maziko ya Sheikh Kaluta Amri Abeid mwaka wa 1963.

Halafu maziko ya Abdulwahid Kleist Sykes mwaka wa 1968.

Kisha maziko ya Sheikh Kassim bin Juma 1994.

Halafu maziko ya Prof. Kighoma Ali Malima mwaka wa 1995.

Maziko ya Prof. Malima yalikuwa ya aina yake kwani kwa mara ya kwanza sala ya jeneza ilisaliwa kwenye kiwanja cha wazi kwani hapakuwa na msikiti Dar es Salaam ambao ungeweza kuenea ule umma uliokuja mazikoni.

Watu wasingeweza.kuenea katika msikiti wowote. Jeneza la Prof. Malima lilisaliwa katika Viwanja Vya Mnazi Mmoja.

Yakaja maziko ya Mzee Kitwana Dau baba yake Balozi Dk. Ramadhani Dau.

Yakafuata maziko ya Sheikh Ilunga Hassan Kapungu.

Aliuliza muulizaji, ''Umma huu wote wa nani hapa mazikoni?

Umma huu wa Ramadhani au wa Mzee Kitwana?

Mtu akajibu, ''Umma huu wamegawana baba na mwananae kwani wote hawa ni watu wa watu.''

Wakati haya yakisemwa kulikuwa na kundi kubwa sana la masheikh na wote katika kanzu nyeupe kama vile wameaagana wanadhikiri.

Hawa walikuwa Qadiriyya.

Kwa miaka ile maziko kama haya ya Mzee Dau yalikuwa hayajapata kuonekana.

Ilikuwa jioni na mwili uikuwa bado haujawasili kutoka Uingereza.

Kila dakika zinavyosogea na ndivyo watu walivyokuwa wanamiminika nyumbani kwa Dr. Dau Kinondoni.

Maziko ya mama yetu Bi. Safia bint Juma Makasara hayajapata kutokea.

Alifariki siku ya Jumatano usiku nyumbani kwa mwanae Balozi Dau na kufikia Alkhamis mchana mahema yaliyokuwa yamefungwa nje ya nyumba yalimstaajabisha kila aliyefika msibani.

Mahema pembeni mwa barabara ubavu kwa ubavu nje ya lango kuu.

Hii si kawaida.

Ndani ya nyumba mahema mengine kwenye uwanja wa mbele na si mdogo.

Nyumba za jirani zote nje yameenea mahema.

Mama yetu kawakusanya watu hawajaonana miaka mingi sana wamekutanishwa na msiba wake.

Toka asubuhi ni visomo na nasaa kutoka kwa masheikh maarufu wa Dar es Salaam.

Sala ya adhuhuri imesaliwa hapo hapo nyumbani halikadhalika sala ya jeneza kwani msikiti wa jirani usingetosha kupokea umma wote ule.

Sala hii ya mama yetu ilinikumbusha sala ya jeneza ya Prof. Malima mwaka wa 1995 katika Viwanja Vya Mnazi Mmoja.

Safari ya kwenda kumzika mama yetu Mkuranga kijijini kwake Mbezi magari yalikuwa yamefunga ''convoy,'' gari moja nyuma ya lingine yalishangaza kila mtu katika vijiji tulivyopita Kilwa Road kimulimuli kikiwa mbele yetu kutusafisha njia.

Bi. Safia mimi ni mama yangu mara ya mwisho kumuona ni miaka mingi kidogo imepita.

Nilikuwa nyumbani kwa Balozi nikapita uani kwenda kumuamkia na nakumbuka nilikuwa nimefikwa na mtihani katika maisha mama akawa ananipa maneno ya kunifariji kisha akaniombea dua.

Zamani sana wakati huo yuko nyumbani kwake Mtaa wa Mvumi, Magomeni na baba yetu Mzee Dau yu hai.

Ilikuwa kila tukienda kumwamkia mimi na Dr. Dau pale nyumbani yeye bila ya kutuuliza tukikaa tu utaona mkeka unatandikwa tunatengewa chakula.

Wakati mwingine tuko katika suti zetu tumetoka katika mikutano ambayo tukihudhuria na mimi nikiwa afisa mdogo Idara ya Marketing Bandarini Ramadhani yeye akiwa Mkurugenzi wa Masoko.

Basi mama atatuangalia na ile misuti yatu tumekaa chini katika mkeka na atatabasamu tu hatiii neno labda kusema, ''Huyo samaki ndiyo kakushindeni?''

Ninachokumbuka ni kuwa kitoweo alichokuwa anatuwekea siku zote ni samaki tena samaki mwenye jina aliyeletwa nyumbani ndani ya kikapu kilichotakata.

Hii misemo ya ''samaki mwenye jina'' na ''samaki asiye na jina'' na ''kikapu kilichotaka,'' yote nimeipata kwa Balozi miaka mingi iliyopita.

Balozi kwao Mafia.
Mtu wa kisiwani.

Tabu kushidananae katika elimu ya bahari na misemo inayohusu samaki.

Wengi naamini watashangaa nikiwaambia kuwa Balozi ni mvuvi tena wa sifa.

Najua ni kwa kiasi gani ndugu yangu Ramadhani msiba huu ulivyompiga kwani natambua yale mapenzi aliyokuwanayo kwa mama yake.

Nakumbuka siku alipopokea simu kuwa bibi yake kafariki tulikuwa sote ndani ya gari yake usiku.

''Mohamed bibi yangu amefariki huyu ndiye aliyenilea mimi,'' Dr. Dau alinieleza akiwa na majonzi makubwa.

Niliongozana na Dr. Dau hijja mwaka wa 1998 na katika msafara wetu alikuwapo bibi yake wakati huo mtu mzima sana lakini alikuwa hataki kubebewa chochote chake kila kitu anataka afanye mwenyewe na Ramadhani muda wote akiwepo bibi yake yuko pembeni yake ingawa alikuwapo mama yetu mdogo kumtazama bibi.

Mume wa kweli mwenye mapenzi ya dhati na mkewe bibi yetu.

Mimi nikimuonea wivu sana Ramadhani.

Allah tunamuomba amrehemu mama yetu na amtie katika pepo Firdaus.

Amin.

Screenshot_20211122-171750_Facebook.jpg
 
Mzee hajielewi huyu ana udini sana. Sasa hapo kuna watu wengi kuzidi misiba ya Mzee Nyerere, Kanumba na Rais John Pombe Magufuli? Muda mwingine tuweni wa kweli na wawazi hii mitandao isitudanganye kwa faida yako au dini yako.
 
Mzee hajielewi huyu ana udini sana...sasa hapo kuna watu wengi kuzidi misiba ya Mzee Nyerere, Kanumba na Rais John Pombe Magufuli??Muda mwingine tuweni wa kweli na wawazi hii mitandao isitudanganye kwa faida yako au dini yako.
Mzee anajidanganya tu anatuona sote mazuzu, siki hizi namdharau sana, anazeeka vibaya, anaandika ujinga, udini unampofua.
 
Mzee anajidanganya tu anatuona sote mazuzu,siki hizi namdharau sana, anazeeka vibaya, anaandika ujinga, udini unampofua.
Hao walikufaga mwaka gani mbona ndio nawasikia leo..walipata kuishi Tanzania kweli au? Anyway wapumzike kwa amani.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nimeona udini tu ndo umekutawala badala ya uhalisia, yaani uko kwenye boxi moja la uislamu,na si boxi la waTanzania

Any way msiba wa Mwl JK Nyerere ndiyo msiba ulio wahi kutikisa zaidi hapo Dar es Salaam.

Nenda msikitini kaswali
 
Mzee hajielewi huyu ana udini sana...sasa hapo kuna watu wengi kuzidi misiba ya Mzee Nyerere, Kanumba na Rais John Pombe Magufuli??Muda mwingine tuweni wa kweli na wawazi hii mitandao isitudanganye kwa faida yako au dini yako
Kizeze,
Kila mwandishi anakuwa na watu wake anaowaandikia.

Mimi nimetokana na jamii ya mjini Dar es Salaam na ninaponyanyua kalamu hawa ndiyo ninaowaandikia.

Hii sikuanza leo.

Wengi hapa JF wamenifahamu kwa kuandika historia ya watu wa pwani na mfano wa hao katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Historia hii iligueza historia iliyokuwapo na kufunzwa shule za msingi hadi vyuo vikuu.

Niliamua kuandika historia hii kwa kuwa hakuna mtafiti aliyeiandika labda kwa kuwa si historia yao hivyo hawaijui au waliona haina umuhimu.

Wala mimi sikusema hawakuiandika kwa sababu ya udini.

Sikuona haja ya kukejeli wala kuandika maneno makali kwa sababu historia ya wazee wangu na jamii yangu haikuandikwa.

Wala sikughadhibika kuwa historia inayosomeshwa imetutupa nje.

Nilichofanya niliamua kufanya utafiti na kuandika.

Kilichonishangaza ni kuwa wako waliokujakunilaumu kuwa nimesukumwa kuandika kwa sababu za udini.

Hawa wote ni watu wa hapa nyumbani.

Nje ya mipaka ya Tanzania historia hii ilipokelewa vyema sana na nikaalikwa vyuo vingi kuzungumza.

Sasa ninapoandika historia ya maziko makubwa ninakusudia kueleza historia ya jamii yangu ifahamike ilikuwaje.

Hakuna anaekataa kuwa maziko ya Mwalimu Nyerere yalikuwa makubwa.

Lakini nitakuambia kitu.

Nyerere alipofika kwenye maziko ya Abdul Sykes hakuamini macho yake.

Alikuwa hajapata kushuhudia mazishi kama yale.

Sasa kama nisingeandika historia hii wewe ungeyajuaje haya?

Kuna mengi tungeweza kujadili kwa taratibu bahati mbaya historia hii inawapandisha hasira.

Ningeweza kuhadithia jinsi Mwalimu Nyerere na Mama Maria walivyopokelewa Dar es Salaam katika mitaa ya Kariakoo na wazee wetu na mapenzi yaliyokuwa baina yao.

Ningeweza kueleza maisha yalivyokuwa na mapenzi yaliyojengeka baina yao na kisa kilichomshtua Abdul Sykes siku ilipodhaniwa Nyerere kalishwa sumu katika chakula nyumbani kwake.

Mengi ninayo kwa kuwa ingawa mimi nilikuwa mtoto lakini ni sehemu ya historia hii na waliofanya haya ni wazazi wangu.
 
Kizeze,
Kila mwandishi anakuwa na watu wake anaowaandikia.

Mimi nimetokana na jamii ya mjini Dar es Salaam na ninaponyanyua kalamu hawa ndiyo ninaowaandikia.

Hii sikuanza leo.

Wengi hapa JF wamenifahamu kwa kuandika historia ya watu wa pwani na mfano wa hao katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Historia hii iligueza historia iliyokuwapo na kufunzwa shule za msingi hadi vyuo vikuu.

Niliamua kuandika historia hii kwa kuwa hakuna mtafiti aliyeiandika labda kwa kuwa si historia yao hivyo hawaijui au waliona haina umuhimu.

Wala mimi sikusema hawakuiandika kwa sababu ya udini.

Sikuona haja ya kukejeli wala kuandika maneno makali kwa sababu historia ya wazee wangu na jamii yangu haikuandikwa.

Wala sikughadhibika kuwa historia inayosomeshwa imetutupa nje.

Nilichofanya niliamua kufanya utafiti na kuandika.

Kilichonishangaza ni kuwa wako waliokujakunilaumu kuwa nimesukumwa kuandika kwa sababu za udini.

Hawa wote ni watu wa hapa nyumbani.

Nje ya mipaka ya Tanzania historia hii ilipokelewa vyema sana na nikaalikwa vyuo vingi kuzungumza.

Sasa ninapoandika historia ya maziko makubwa ninakusudia kueleza historia ya jamii yangu ifihamike ilikuwaje.

Hakuna anaekataa kuwa maziko ya Mwalimu Nyerere yalikuwa makubwa.

Lakini nitakuambia kitu.

Nyerere alipofika kwenye maziko ya Abdul Sykes hakuamini macho yake.

Alikuwa hajapata kushuhudia mazishi kama yale.

Sasa kama nisingeandika historia hii wewe ungeyajuaje haya?

Kuna mengi tungeweza kujadili kwa taratibu bahati mbaya historia hii inawapandisha hasira.

Ningeweza kuhadithia jinsi Mwalimu Nyerere na Mama Maria walivyopokelewa Dar es Salaam katika mitaa ya Kariakoo na wazee wetu na mapenzi yaliyokuwa baina yao.

Ningeweza kueleza maisha yalivyokuwa na mapenzi yaliyojengeka baina yao na kisa kilichomshtua Abdul Sykes siku ilipodhaniwa Nyerere kalishwa sumu katika chakula nyumbani kwa Bwana Abdul.

Mengi ninayo kwa kuwa ingawa mimi nilikuwa mtoto lakini ni sehemu ya historia hii na waliofanya haya ni wazazi wangu.

Mzee huwa naona pia una kama kijiba cha moyo kuona kundi la watu flani wa hapo Daressalaam wengi haswa wakiwa ndugu jamaa na marafiki zako (waislamu) hawajazungumziwa sana katika historia ya kudai uhuru wetu kitu ambacho siyo sahihi. Nisahihishe kama mtizamo wangu ni hasi
 
Mzee huwa naona pia una kama kijiba cha moyo kuona kundi la watu flani wa hapo Daressalaam wengi haswa wakiwa ndugu jamaa na marafiki zako (waislamu) hawajazungumziwa sana katika historia ya kudai uhuru wetu kitu ambacho siyo sahihi. Nisahihishe kama mtizamo wangu ni hasi
Mzee huwa naona pia una kama kijiba cha moyo kuona kundi la watu flani wa hapo Daressalaam wengi haswa wakiwa ndugu jamaa na marafiki zako (waislamu) hawajazungumziwa sana katika historia ya kudai uhuru wetu kitu ambacho siyo sahihi. Nisahihishe kama mtizamo wangu ni hasi
Vic...
Jibu lako limo post #12.
Ikiwa hujaelewa nifahamishe.
 
Mzee wa Gerezani Kariakoo!
Kipuyo,
Naam.

Dunia yangu ilikuwa hiyo.

Wala sikudhani kuwa iko siku nitaiona dunia na miguu yangu itakanyaga ardhi za mbali sana.

Kuwa nitasimama kwenye vyuo vikuu mbali na mitaa ya vumbi ya Gerezani ya 1950s na watu watakuja kunisikiliza nikizungumza.

Iko siku usiku nimesimama Broadway New York Manhattan naangalia magari yanavyopita mengi, mengi, mengi, nikajiuliza hivi huyu ni mie kweli?

Mtoto wa Gerezani na Kariakoo.

Sasa mimi niko katika uzee Gerezani ile haipo tena wala soko lile la Kariakoo Nyerere alipokuwa anakwenda ofisini kwa Market Master Abdulwahid Kleist Sykes halipo.

Nashukuru nimeweza kuihifadhi historia hii.
Kila mtafiti nikimfikisha pale sokoni ananiuliza, "Ilikuwaje hapa miaka hiyo?"

Wanashangaa wananiuliza mbona hatujaweka, "plaque," kueleza umuhimu wa sehemu hii?"
 
Hao walikufaga mwaka gani mbona ndio nawasikia leo..walipata kuishi Tanzania kweli au?..anyway wapumzike kwa amani.

#MaendeleoHayanaChama
Jiwe...
Usingeweza kuwafahamu watu hawa kwa kuwa historia zao hazikupata kuandikwa hadi kilipochapwa kitabu cha Abdul Sykes mwaka wa 1998.

Kwani wewe ulipata kujua kuwa kadi ya Abdul Sykes ni no. 3, Ally Sykes no. 2 na Julius Nyerere no. 1 na kadi yake Nyerere iliandikwa na Ally Sykes?

Au ulipata kusomeshwa kuwa jengo la ofisi ya TAA ilipoundwa TANU lilijengwa na Kleist Sykes na ni yeye katibu muasisi wa African Association 1929?

Ulilijua hili?

Ikiwa hii ndiyo historia ya TANU na historia ya Nyerere na uhuru wa Tanganyika hukuwa unaijua ndiyo utaijua historia ya Sheikh Idrissa bin Saad?

Naam hawa waliishi Tanganyika.
 

Similar Discussions

14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom