Ummayed
JF-Expert Member
- May 21, 2019
- 6,156
- 2,573
YAH: FEDHA ZA DENI LA LIBYA
1.0. Libya ni moja kati ya nchi wafadhili wa Tanzania ambapo, kama ilivyo wafadhili wengine imekuwa ikiipa nchi yetu misaada na mikopo yenye masharti nafuu. Serikali yetu imekuwa ikifanya taratibu mbalimbali kulipa madeni ya nchi wafadhili kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kubadili madeni na kuyaingiza katika miradi n.k, yaani ‘Dept Swap’
2.0. Katika utaratibu huo wa ‘Dept Swap’, tarehe 20/7/2005, Serikali ya Tanzania na Libya zilitia sahihi mkataba wa Dept Swap (Dept Swap Agreement) ambao uliweka utaratibu wa matumizi na urejeshaji wa fedha za deni la Libya.
3.0. Tarehe 4/3/2009, Serikali ya Libya na Tanzania zilitia sahihi mkataba wa nyongeza (Addendum to the Dept Swap Agreement) ambao ulizungumzia, pamoja na mambo mengine, matumizi ya jumla ya dola za Kimarekani milioni 20 (20,000,000) ambazo zilikuwa zimehifadhiwa katika akaunti ya Libya No.004-200-0002216-01, Benki ya Rasilimali Tanzania (Tanzania Investment Bank).
4.0. Nyongeza hii ya mkataba ilitamka bayana katika kifungu No.4.02, kwamba, fedha zilizokuwa katika akaunti tajwa, zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua wao wenyewe, ambaye ni kampuni ya MEIS INDUSTRIES LIMITED kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha Saruji Lindi. Kwa mujibu wa nyongeza hii, mkopo ulipaswa kulipwa ndani ya miaka sita, na baada ya hapo, fedha hizo zirejeshwe na ziendelee kukopeshwa Watanzania kwa ajili ya miradi mingine ambayo Serikali za Libya na Tanzania zitakuwa zimeridhia.
5.0. Kumbukumbu zinaonyesha mambo mawili:-
5.1 Kwamba, kabla ya Serikali ya Libya kutia sahihi nyongeza hii ya mkataba iliyotaka fedha zikopeshwe kwa MEIS INDUSTRIES, upembuzi yakinifu wa mradi husika ulifanywa na serikali ya Libya kupitia vyombo vyake, na wao wenyewe walishajiridhisha juu ya ubora wa mradi huo (Viability of the Project)
5.2 Kwamba, baada ya kutia sahihi nyongeza ya mkataba, Serikali ya Libya kupitia Ubalozi wake hapa nchini iliendelea kusisitiza kwa maandishi kwamba Serikali ya Tanzania iharakishe mchakato wa kuwezesha fedha hizo zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua ili mradi huo muhimu usiendelee kuchelewa, na pia fedha ziingie katika mzunguko kwa manufaa ya Watanzania.
6.0. Katika kutekeleza mikataba hii miiwli, yaani Dept Swap Agreement ya tarehe 20/7/2005 na Addendum Dept Swap Agreement ya Tarehe 4/3/2009, na kwa kuzingatia umuhimu ambao serikali ya Libya iliuonyesha, Serikali ya Tanzania kupitia watalaamu wake wa Wizara ya Fedha, Benki ya Rasilimali (TIB) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, na Mwekezaji (Kampuni ya MEIS), walikutana chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na kuandaa hadidu za rejea ambazo zilipelekea kutengenezwa kwa mkataba wa uwekezaji (Investment Agreement) kati ya serikali ya Tanzania, TIB, Serikali ya Libya na Mwekezaji.
7.0. Serikali ya Tanzania, TIB na Mwekezaji walitia sahihi mkataba huu na kuupeleka Libya ili serikali ya Libya ipate kuweka sahihi. Kwa sababu ambazo hazikufahamika, serikali ya Libya haikutia sahihi mkataba huo.
8.0. Baada ya kufuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio, mwekezaji alimuandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania yenye kumbukumbu No. PC/MEIS/AG/2/10 ya tarehe 1/9/2010 akieleza kusudio la kuipeleka Serikali ya Libya Mahakamani kwa kitendo chake cha kutokutia sahihi mkataba.
9.0. Terehe 13/9/2010, Mwekezaji alifungua shauri Mahakama Kuu ya Tanzania, shauri la madai No. 124/2010 dhidi ya serikali ya Libya, akiiomba Mahakama Kuu itoe tamko kwamba kitendo cha serikali ya Libya kukataa kutia sahihi mkataba huu hakikuwa kitendo cha haki na kwamba mahakama itoe amri kwamba fedha hizo zitolewe kwa Mwekezaji ili kutekeleza mradi uliokusudiwa. Kumbukumbu zinaonyesha kwamba wito wa Mahakama (Summons) ulipelekwa Ubalozi wa Libya lakini hapakuwa na majibu wala mwakilishi aliyekuja mahakamani.
10.0. Mahakama Kuu, kwa kufuata taratibu zake, iliendelea na kusikiliza shauri na kutoa amri kama ambavyo mahakama yenyewe ilijiridhisha. Amri ya mahakama, pamoja na mambo mengine, iliagiza kwamba fedha hizo zitolewe kwa mwekezaji ili kutekeleza mradi husika.
11.0. Zilifanyika juhudi za Benki ya Rasilimali (TIB) pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupinga au kupata ufafanuzi zaidi juu ya amri hiyo ya utekelezaji wake. Mahakama Kuu pamoja na Mahakama ya Rufana, katika nyakati tofauti, zilishughulikia maombi hayo na kuyafikisha katika hatima yake kwa mujibu wa sheria. Kwa ajili ya kumbukumbu, mashauri yaliyofunguliwa ni kama ifuatavyo:-
11.1 TIB ilifungua maombi No. 126/2010 katika mahakama ya Rufaa kuiomba izuie na kufuta utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu. Maombi haya ya TIB yalifanyiwa uamuzi wa mwisho mnamo tarehe 7/11/2011, ambapo maombi hayo yaliondolewa mahakamani kwa kuwa, kwa mujibu wa Mah
SIKU NYINGINE MDOGO WANGU ULIZA UFUNDISHWE.
UNAROPOKA MPAKA UNATIA AIBUU
1.0. Libya ni moja kati ya nchi wafadhili wa Tanzania ambapo, kama ilivyo wafadhili wengine imekuwa ikiipa nchi yetu misaada na mikopo yenye masharti nafuu. Serikali yetu imekuwa ikifanya taratibu mbalimbali kulipa madeni ya nchi wafadhili kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na utaratibu wa kubadili madeni na kuyaingiza katika miradi n.k, yaani ‘Dept Swap’
2.0. Katika utaratibu huo wa ‘Dept Swap’, tarehe 20/7/2005, Serikali ya Tanzania na Libya zilitia sahihi mkataba wa Dept Swap (Dept Swap Agreement) ambao uliweka utaratibu wa matumizi na urejeshaji wa fedha za deni la Libya.
3.0. Tarehe 4/3/2009, Serikali ya Libya na Tanzania zilitia sahihi mkataba wa nyongeza (Addendum to the Dept Swap Agreement) ambao ulizungumzia, pamoja na mambo mengine, matumizi ya jumla ya dola za Kimarekani milioni 20 (20,000,000) ambazo zilikuwa zimehifadhiwa katika akaunti ya Libya No.004-200-0002216-01, Benki ya Rasilimali Tanzania (Tanzania Investment Bank).
4.0. Nyongeza hii ya mkataba ilitamka bayana katika kifungu No.4.02, kwamba, fedha zilizokuwa katika akaunti tajwa, zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua wao wenyewe, ambaye ni kampuni ya MEIS INDUSTRIES LIMITED kwa ajili ya mradi wa ujenzi wa kiwanda cha Saruji Lindi. Kwa mujibu wa nyongeza hii, mkopo ulipaswa kulipwa ndani ya miaka sita, na baada ya hapo, fedha hizo zirejeshwe na ziendelee kukopeshwa Watanzania kwa ajili ya miradi mingine ambayo Serikali za Libya na Tanzania zitakuwa zimeridhia.
5.0. Kumbukumbu zinaonyesha mambo mawili:-
5.1 Kwamba, kabla ya Serikali ya Libya kutia sahihi nyongeza hii ya mkataba iliyotaka fedha zikopeshwe kwa MEIS INDUSTRIES, upembuzi yakinifu wa mradi husika ulifanywa na serikali ya Libya kupitia vyombo vyake, na wao wenyewe walishajiridhisha juu ya ubora wa mradi huo (Viability of the Project)
5.2 Kwamba, baada ya kutia sahihi nyongeza ya mkataba, Serikali ya Libya kupitia Ubalozi wake hapa nchini iliendelea kusisitiza kwa maandishi kwamba Serikali ya Tanzania iharakishe mchakato wa kuwezesha fedha hizo zikopeshwe kwa mwekezaji waliyemteua ili mradi huo muhimu usiendelee kuchelewa, na pia fedha ziingie katika mzunguko kwa manufaa ya Watanzania.
6.0. Katika kutekeleza mikataba hii miiwli, yaani Dept Swap Agreement ya tarehe 20/7/2005 na Addendum Dept Swap Agreement ya Tarehe 4/3/2009, na kwa kuzingatia umuhimu ambao serikali ya Libya iliuonyesha, Serikali ya Tanzania kupitia watalaamu wake wa Wizara ya Fedha, Benki ya Rasilimali (TIB) na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, na Mwekezaji (Kampuni ya MEIS), walikutana chini ya usimamizi wa Wizara ya Fedha na kuandaa hadidu za rejea ambazo zilipelekea kutengenezwa kwa mkataba wa uwekezaji (Investment Agreement) kati ya serikali ya Tanzania, TIB, Serikali ya Libya na Mwekezaji.
7.0. Serikali ya Tanzania, TIB na Mwekezaji walitia sahihi mkataba huu na kuupeleka Libya ili serikali ya Libya ipate kuweka sahihi. Kwa sababu ambazo hazikufahamika, serikali ya Libya haikutia sahihi mkataba huo.
8.0. Baada ya kufuatilia kwa muda mrefu bila mafanikio, mwekezaji alimuandikia barua Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Tanzania yenye kumbukumbu No. PC/MEIS/AG/2/10 ya tarehe 1/9/2010 akieleza kusudio la kuipeleka Serikali ya Libya Mahakamani kwa kitendo chake cha kutokutia sahihi mkataba.
9.0. Terehe 13/9/2010, Mwekezaji alifungua shauri Mahakama Kuu ya Tanzania, shauri la madai No. 124/2010 dhidi ya serikali ya Libya, akiiomba Mahakama Kuu itoe tamko kwamba kitendo cha serikali ya Libya kukataa kutia sahihi mkataba huu hakikuwa kitendo cha haki na kwamba mahakama itoe amri kwamba fedha hizo zitolewe kwa Mwekezaji ili kutekeleza mradi uliokusudiwa. Kumbukumbu zinaonyesha kwamba wito wa Mahakama (Summons) ulipelekwa Ubalozi wa Libya lakini hapakuwa na majibu wala mwakilishi aliyekuja mahakamani.
10.0. Mahakama Kuu, kwa kufuata taratibu zake, iliendelea na kusikiliza shauri na kutoa amri kama ambavyo mahakama yenyewe ilijiridhisha. Amri ya mahakama, pamoja na mambo mengine, iliagiza kwamba fedha hizo zitolewe kwa mwekezaji ili kutekeleza mradi husika.
11.0. Zilifanyika juhudi za Benki ya Rasilimali (TIB) pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupinga au kupata ufafanuzi zaidi juu ya amri hiyo ya utekelezaji wake. Mahakama Kuu pamoja na Mahakama ya Rufana, katika nyakati tofauti, zilishughulikia maombi hayo na kuyafikisha katika hatima yake kwa mujibu wa sheria. Kwa ajili ya kumbukumbu, mashauri yaliyofunguliwa ni kama ifuatavyo:-
11.1 TIB ilifungua maombi No. 126/2010 katika mahakama ya Rufaa kuiomba izuie na kufuta utekelezaji wa amri ya Mahakama Kuu. Maombi haya ya TIB yalifanyiwa uamuzi wa mwisho mnamo tarehe 7/11/2011, ambapo maombi hayo yaliondolewa mahakamani kwa kuwa, kwa mujibu wa Mah
SIKU NYINGINE MDOGO WANGU ULIZA UFUNDISHWE.
UNAROPOKA MPAKA UNATIA AIBUU
Natokea milima ya Ulugulu.
Arab hana cha kuisadia Tanzania kujenga msikiti siyo msaada, alimuhonga Mungu wao ile misikiti ambaye alimsaliti tena vibaya, kapigwa na kafir mpaka leo wanaokota takataka.
hiyo misikiti alijenga baada ya kafir kumuachia mateka wa vita ya kagera