kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 8,839
- 17,437
Mayahudi wa Ethiopia waliorubuniwa kwenda Israel wapiga "takbir" waendelea kulalamikia unyanyasaji
Jul 06, 2019 10:58 UTC
Mayahudi wa Ethiopia maarufu kwa jina la Mafalasha, waliorubiniwa kwenda katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni, wanaendelea kufanya maandamano ya kalalamikia unyanyasaji na ubaguzi wanaofanyiwa na Wazayuni.
Kwa mujibu wa shirika la habari la IRNA, Waethiopia hao wamepiga mayowe na nara dhidi ya viongozi wa utawala wa Kizayuni, bali wengine hata wamepiga "takbir" katika maandamano hayo.
Jumapili iliyopita pia, maelfu ya Mayahudi wa Ethiopia walifanya maandamano ya kulaani kitendo cha polisi wa utawala wa Kizayuni kumuua kidhulma kijana mmoja wa Kifalasha aitwaye Solomon Teka.
Maandamano hayo makubwa yaliyoambatana na fujo yalifanyika katika miji ya Tel Aviv, Hayfa, Ashdod na Ashkelon. Watu 60 walitiwa mbaroni na maafisa usalama wa Israel wakati walipokandamiza kikatili maandamano hayo.
Wakati huo huo, gazeti la Kizayuni la Yedioth Ahronoth limeandika kuwa, Mayahudi wa Ethiopia wametishia kuwa leo Jumamosi pia watakusanyika katika medani kubwa zaidi ya mji wa Tel Aviv ili kutaka kisasi cha kuuliwa kijana huyo mwenye asili ya Ethiopia, na jeshi la polisi la Israel.
Mayahudi wa Ethiopia maarufu kwa jina la Mafalasha, ni miongoni mwa makundi maskini zaidi ndani ya utawala wa Kizayuni wa Israel. Mayahudi hao walirubuniwa kuacha makazi yao huko Ethiopia na kwenda kwenye ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu kwa tamaa ya kupata maisha mazuri. Hata hivyo wananyanyaswa na kubaguliwa sana na wanahesabiwa kuwa ni raia wa daraja la tatu wa utawala wa Kizayuni.
Tags
UTAWALA WA KIZAYUNI ETHIOPIA Kijana wa Kifalasha, Myahudi wa Ethiopia, Solomon Teka aliyeuliwa kikatili na polisi wa Israel
Kijana wa kike mwenye asili ya Ethiopia akiwa na picha ya kijana wa Ethiopia aliyeuliwa kikatili na polisi wa Israel. Maandishi yana maana isemayo, maisha yangu yana thamani
si kitu cha bure
Jul 06, 2019 10:58 UTC
Mayahudi wa Ethiopia maarufu kwa jina la Mafalasha, waliorubiniwa kwenda katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Wazayuni, wanaendelea kufanya maandamano ya kalalamikia unyanyasaji na ubaguzi wanaofanyiwa na Wazayuni.
Kwa mujibu wa shirika la habari la IRNA, Waethiopia hao wamepiga mayowe na nara dhidi ya viongozi wa utawala wa Kizayuni, bali wengine hata wamepiga "takbir" katika maandamano hayo.
Jumapili iliyopita pia, maelfu ya Mayahudi wa Ethiopia walifanya maandamano ya kulaani kitendo cha polisi wa utawala wa Kizayuni kumuua kidhulma kijana mmoja wa Kifalasha aitwaye Solomon Teka.
Maandamano hayo makubwa yaliyoambatana na fujo yalifanyika katika miji ya Tel Aviv, Hayfa, Ashdod na Ashkelon. Watu 60 walitiwa mbaroni na maafisa usalama wa Israel wakati walipokandamiza kikatili maandamano hayo.
Wakati huo huo, gazeti la Kizayuni la Yedioth Ahronoth limeandika kuwa, Mayahudi wa Ethiopia wametishia kuwa leo Jumamosi pia watakusanyika katika medani kubwa zaidi ya mji wa Tel Aviv ili kutaka kisasi cha kuuliwa kijana huyo mwenye asili ya Ethiopia, na jeshi la polisi la Israel.
Mayahudi wa Ethiopia maarufu kwa jina la Mafalasha, ni miongoni mwa makundi maskini zaidi ndani ya utawala wa Kizayuni wa Israel. Mayahudi hao walirubuniwa kuacha makazi yao huko Ethiopia na kwenda kwenye ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu kwa tamaa ya kupata maisha mazuri. Hata hivyo wananyanyaswa na kubaguliwa sana na wanahesabiwa kuwa ni raia wa daraja la tatu wa utawala wa Kizayuni.
Tags
UTAWALA WA KIZAYUNI ETHIOPIA Kijana wa Kifalasha, Myahudi wa Ethiopia, Solomon Teka aliyeuliwa kikatili na polisi wa Israel
Kijana wa kike mwenye asili ya Ethiopia akiwa na picha ya kijana wa Ethiopia aliyeuliwa kikatili na polisi wa Israel. Maandishi yana maana isemayo, maisha yangu yana thamani
si kitu cha bure