Maxence Melo: Changamoto za Vyombo vya Habari na kukosa Matangazo

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,861
Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums Maxence Melo amesema vyombo vingi vya habari hukubali matangazo kwa kuwa yana hela nyingi

Kwa JamiiForums amesema wana sera ambayo inawafanya wakatae matangazo ya Pombe na Matangazo ya Betting japo yana hela.

Aidha Chombo cha habari kutegemea matangazo ni suala la zamani sana ni lazima kukubali kubadilika

Amesema ni suala la ajabu kwa vyombo kulilia matangazo ya Serikali huku vikitaka kubaki kuwa 'watch dog' kwa Serikali.

Ameshauri Vyombo vya Habari kuwa na Mipango Shirikishi (wamiliki wawashirikishe wafanyakazi wao) katika kupanga hatma ya vyombo vyao ili kila mmoja awe sehemu ya safari kuliko mmiliki kuamini yeye anajua sana kuliko aliowaajiri.

Melo yuko mubashara StarTv muda huu
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom