Mawimbi Ya Redio Ya Ajabu Kutoka Anga Za Juu Yagunduliwa

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
May 27, 2016
5,416
7,828
Mawimbi ya redio ya ajabu kutoka anga za juu yagunduliwa na darubini Canada

1547121780478.png

Picha: Mawimbi hayo huenda yanatoka kwa nyota ya nutroni - au pengine viumbe
wengine anga za juu. (Picha: Getty Images)


Wataalamu wa anga za juu wamefichua kwamba walinasa mawimbi ya redio ya ajabu ambayo yalikuwa yanatoka mbali sana katika anga za juu.

Mawimbi hayo yalinaswa na darubini ya kufuatilia mawimbi ya redio ambayo ipo Canada na yanaaminika kutoka kwenye mfumo wa nyota na sayari ulio mbali sana.

Chanzo halisi cha mawimbi hayo ya redio bado hakijabainika na wala wataalamu hao hawajafahamu sifa kamili za mawimbi hayo.

Miongoni mwa mawimbi hayo ya redio ya kasi sana (yanayofahamika pia kama FRBs kwa maana ya Fast Radio Bursts), ambayo yalinaswa mara 13, kulikuwa na mawimbi yasiyo ya kawaida yaliyokuwa yakijirudia tena na tena. Yanaaminika kutoka kwenye chanzo kimoja umbali wa takriban miaka 1.5 bilioni kwa miaka ya kasi ya mwanga.

Tukio kama hilo limewahi tu kuripotiwa mara moja tu awali, na darubini tofauti.

"Kufahamu kwamba kuna nyingine imepatikana ni jambo linalodokeza kwamba kunaweza kuwa hata na zaidi," amesema Ingrid Stairs, ambaye ni mtaalamu wa fizikia ya anga za juu katika Chuo Kikuu cha British Columbia (UBC).

"Na tukiwa na mitambo zaidi ya kuimarisha nguvu za mawimbi hayo na pia vyanzo vingi, basi tunaweza tukafahamu na kutanzua kitendawili hiki cha anga za juu - tujue mawimbi haya yanatokea wapi na nini chanzo chake."

Kituo cha kutafiti anga za juu cha CHIME, kinachopatikana katika Bonde la Okanagan katika eneo la British Columbia, kina antena nne (waya maalum za kupokelea mawimbi ya sauti) za urefu wa mita 100 ambazo hufuatilia anga ya kaskazini kila siku.

Darubini iliyotumiwa ilianza tu kufanya kazi mwaka jana, na iliyanasa mawimbi hayo 13 ya redio karibu mara moja, pamoja na mawimbi hay ya kujirudia.

1547121913033.png

Picha: Darubini mpya ya mawimbi ya redio ya CHIME, Canada.

Matokeo ya utafiti huo hamechapishwa katika jarida la Nature. "Tumegundua mawimbi ya pili yanayojirudia ambayo yanafanana na yale ya kwanza," Shriharsh Tendulkar wa Chuo Kikuu cha McGill, Canada amesema.

"Hili linatufahamisha zaidi kuhusu sifa za mawimbi haya ya kujirudia yakiwa kama kundi."

FRBs ni mawimbi mafupi, yenye nguvu sana ya redio ambayo yanaonekana kana kwamba yanatokea katikati ya mwendo nusu wa umbali wote wa vitu vyote vilivyopo (nyota na sayari na anga) kwa makadirio ya wanasayansi.

Kufikia sasa, wanasayansi wamegundua mawimbi takriban 60 ya redio ya pekee yanayokwenda kwa kasi sana, na mawimbi mara mbili yanayojirudia.

Wanaamini kwamba kunaweza kuwa na mawimbi ya redio ya FRBs maelfu yanayopita angani kila siku.

Mawimbi haya yanatolewa na viumbe wa anga za juu?

Kuna nadharia kadha kuhusu nini huenda kikawa chanzo cha mawimbi haya.

Moja ni kwamba huenda kukawa na nyota ya nutroni ambayo ina nguvu nyingi sana za sumaku na ambayo inazunguka yenyewe kwa kasi sana. Nyota za nutroni ni kitu kwenye anga za juu ambacho si kikubwa sana (nusu kipenyo chake ni kilomita 30 hivi) na kina uzani wa juu sana, na kimeundwa na nutroni (neutron) ambazo zimebanana sana).

1547122540850.png

Picha: Darubini ya VLA katika jimbo la New Mexico, Marekani ilikuwa ya kwanza
kunasa mawimbi ya redio yaendayo kasi kutoka anga za juu yanayojirudia.


Mawimbi haya ya redio yanaweza pia yakawa yanatokana na nyota mbili za nutroni kuungana.

Kuna baadhi ya watu, ingawa wachache, ambao wanasema kuna uwezekano mawimbi hayo yakawa yanatokana na chombo cha anga za juu pengine kutoka kwa viumbe wanaoishi anga za juu, au mawimbi yenyewe yawe ni chombo hicho cha anga za juu.

Chanzo: BBC Swahili
 
Toa sababu kwa nn wanakudanganya
Kha!! Huoni sababu hapo nimeweka!!? Mtu anakuambia eti source ya mawimbi hayo mpaka kuja kutufikia ni miaka 1.5billion. Huoni huu ni upuuzi na ujinga wa hali ya juu!? Hivi billion unaijua wewe kweli!?
Sekunde 1.5b ni sawa na miaka 1141.5525114.
Waache propaganda zao za kizamani.
 
Kha!! Huoni sababu hapo nimeweka!!? Mtu anakuambia eti source ya mawimbi hayo mpaka kuja kutufikia ni miaka 1.5billion. Huoni huu ni upuuzi na ujinga wa hali ya juu!? Hivi billion unaijua wewe kweli!?
Sekunde 1.5b ni sawa na miaka 1141.5525114.
Waache propaganda zao za kizamani.

Umeambiwa wamesema ili kutudanganya waafrika?
 
Hakuna sehemu nimetaja Africa.
But huu ni uongo wanataka kuueneza ili kutimiza matakwa yao. We are aware about their propaganda kuhusu Big bang and Cosmology.

Matakwa kwa kusema kuna mawimbi ya radio? Ni vingi tu wamefanya dunia hii. Labda na ww uweke ulichogundua dunia hii ili tuone kinachokupa jeuri ya kukataa huo ugunduzi wao.
 
Matakwa kwa kusema kuna mawimbi ya radio? Ni vingi tu wamefanya dunia hii. Labda na ww uweke ulichogundua dunia hii ili tuone kinachokupa jeuri ya kukataa huo ugunduzi wao.
Kha!!! Sasa kama wamefanya vingi ndio watuletee upuuzi kama huu tuukubali!!? Wakeup hivi unajua miaka 1.5b au tunachekeshana tu!? Kama hunielewi ni bora ukaacha ku quote comments zangu. Ni bora ukabaki na low thinking yako.

Unaambiwa 1.5b year kwa speed ya mwanga. Hivi unajua speed ya light!?
Speed ya light ni 300,000km/s.
Sasa zidisha kwa hiyo miaka 1.5b.
Kama siyo kutishana tu ni nini.
Mara wanakuambia Aliens mara Nibiru nk.
Huu ni uongo watu wenye akili tunajua.
 
Kha!! Huoni sababu hapo nimeweka!!? Mtu anakuambia eti source ya mawimbi hayo mpaka kuja kutufikia ni miaka 1.5billion. Huoni huu ni upuuzi na ujinga wa hali ya juu!? Hivi billion unaijua wewe kweli!?
Sekunde 1.5b ni sawa na miaka 1141.5525114.
Waache propaganda zao za kizamani.
"Yanaaminika kutoka kwenye chanzo kimoja umbali wa takriban miaka 1.5 bilioni kwa miaka ya kasi ya mwanga" Soma hapo kwa makini na ujue maanake
 
Kha!!! Sasa kama wamefanya vingi ndio watuletee upuuzi kama huu tuukubali!!? Wakeup hivi unajua miaka 1.5b au tunachekeshana tu!? Kama hunielewi ni bora ukaacha ku quote comments zangu. Ni bora ukabaki na low thinking yako.

Unaambiwa 1.5b year kwa speed ya mwanga. Hivi unajua speed ya light!?
Speed ya light ni 300,000km/s.
Sasa zidisha kwa hiyo miaka 1.5b.
Kama siyo kutishana tu ni nini.
Mara wanakuambia Aliens mara Nibiru nk.
Huu ni uongo watu wenye akili tunajua.

Mkuu weka hapa ulichowahi kugundua tupime hiyo akili yako. Nijuavyo mimi mtu anayekula ugali hana akili.
 
Hawa jamaa wanatudanganya sana. Eti miaka 1.5billion. Huu ni uongo wa hali ya juu.
Wasitutishe.
Yaani kutokana na jina unalotumia hapa Jf nikajua unayajua haya mambo lakini niliposoma changisho lako nimechoka lol. Kama kitu huna knowledge nacho ni vyema kuuliza ukaelekezwa kuliko kubisha. Kuna kitu kinaitwa light years; tunapima umbali wa nyota tokea tulipo ( duniani) kwa kasi ya mwanga. Utakapohitaji ufafanuzi zaidi uliza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani kutokana na jina unalotumia hapa Jf nikajua unayajua haya mambo lakini niliposoma changisho lako nimechoka lol. Kama kitu huna knowledge nacho ni vyema kuuliza ukaelekezwa kuliko kubisha. Kuna kitu kinaitwa light years; tunapima umbali wa nyota tokea tulipo ( duniani) kwa kasi ya mwanga. Utakapohitaji ufafanuzi zaidi uliza

Sent using Jamii Forums mobile app
mkuu naomba nielekeze kuhusu light stars

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom