Mawazo yangu juu ya mchakato wa katiba mpya!

Dijovisonjn

JF-Expert Member
Nov 14, 2011
466
125
Naamin katiba mpya siyo tiba yaumaskini wa watanzania bali itakuwa nyenzo mojawapo ya kututoa sehemu moja na kutupeleka sehemu nyingne ambayo naamin itakuwa bora zaidi.
Ninachooka katika mchakato huu wa awali wa kupata katiba mpya ni nia ya uongo na ya kinafiki walionayo viongozi wetu haswa wa vyama vya siasa!
Binafsi sioni nia ya kweli na dhati walionayo viongozi wa CCM, CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI na hata TLP ktk kuwasaidia watanzania kutengeneza njia nzuri ya kuondokana na umaskini kupitiakatiba! Wote ni wanafiki.
Binafsi naiona nia ya CCM ya kutaka kuendelea kubaki madarakan kwa kuitumia katiba mpya itakayotungwa! Nia hyo ipo kwny huu mswada uliopo bungeni ambao wenyewe wamejipa nguvu ya kutosha ya kuweka na kupitisha matakwa yao bila matatzo!
Binafsi pia naiona nia ya CHADEMA ya kutaka kuutumia mchakato huu kujitengenezea njia ya kuingia ikulu! CHADEMA wao wanataka wapate uwanja sawa wa kiushndan kisiasa!
CUF na TLP wao mafanikio ya CCM ndo mafanikio yao huku mafanikio ya CHADEMA ndo mafanikio ya NCCR MAGEUZI japo c kwa zaidi 80%
Binafsi naona wananchi tumekubali kutekwa na kutumiwa na hawa wanasiasa bila cc wenyewe kujitambua! Wananchi wengi tumekuwa tukiunga na kupinga mambo bila kujiuliza! Wananchi wengi tumewaruhu watu fulani wawaze kwa niaba yetu!
HEBU WANANCHI WENZANGU TUKAE CHINI NA KUUTAFAKARI HUU MCHAKATO NA KUAMUA LA KUFANYA SISI KAMA SISI NA SIO KUWARUHUSU WATU WAPLAY PART YETU!
BINAFSI NAYAUNGA MKONO MAWAZO YA CCM,CUF NA TLP KWA 25% NA KWA UPANDE WA PILI MAWAZO YA CHADEMA NA NCCR MAGEUZI NAYO NAYAUNGA MKONO KWA 25% JUMLA NAYAUNGA MKONO MAWAZO YA WANASIASA KWA 50%
NAAMINI 50% ZIPO KWA WANANCHI AMBAO NI MIMI NA WEWE!
 
Back
Top Bottom