:welcome:Habari zenu wadau,
Napenda kuchukua nafasi hii, kutoa maoni yangu kuhusiana na pantoni zetu za Dar na hata za mikoani.
Wahusika mpatapo mawazo haya ni vema mkayafanyia kazi kwa yale mtakayoona yana tija.
Maoni
1. wahusika ni vyema kutoa elimu ya kuyatumia jaketi okovu(LIFE JACKET) na vifaa vingine vilivyopo ndani ya pantoni kwa ajili ya kujiokoa endapo kutatokea tatizo.
Maelezo:
pantoni zetu zina vifaa vingi tuu kwa ajili ya uokoaji endapo kutatokea tatizo pantoni ikiwa katikati ya bahari au ziwa. kwa hili nawapongeza sana wahusika ila JE MNAUHAKIKA KILA ANAYEINGIA NDANI YA CHOMBO HICHO ANAUELEWA WA KUTUMIA VIFAA HIVYO???? AU Tunangoja hadi litukie tukio ndipo muanze elekeza abiria jinsi ya kutumia????? Bila shaka kuna tatizo hapa.
Nini kifanyike
Ndani ya pantoni zetu hapa tanzania, nyingi zina radio au screen. napendekeza ziwepo picha zinazoonesha kwenye screen zikimuelekeza abiria jinsi ya kutumia vifaa vile, au kama hakuna screen basi mtangazaji awe anatangaza kila mara abiri aingiapo kwenye pantoni. kuliko kumlipa mtu kila siku anasema tuu karibu kwenye pantoni yetu, karibuni kwenye pantoni yetu. tena kwa shifti, tuwape kazi zaidi ya kutoa elimu kwa kuelekeza abiria. Mfano mzuri ndugu zangu, uingiapo ndani ya ndege lane:, kabla ya ndege kuondoka kuna muhudumu huwa anatoa maelekezo jinsi ya kutumia zile life jacket na nini cha kufanya endapo kunatatizo litajitokeza. vivyo hivyo natamani kwenye pantoni ifanyike.
Ni vizuri tunavyoweka matangazo mengine kwenye screen zile hata kama hizo screen zilitolewa na wanaoweka matangazo na imani hawataweza kukataa na hata hivyo haidhuru chochote tukiongeza matangazo au onyesho la jinsi ya utumiaji wa life jacket, boya etc.
2. Kuhusu kufanya service ya pantoni na vifaa hivyo vya uokoaji.
maelezo
Kuwepo na ratiba (schedule for service) ya kufanyia service pantoni yenyewe na siyo kusubiri hadi iaribike ndipo ifanyiwe matengenezo. ikiwepo ratiba inatangazwa inabandikwa na kutangazwa ili kukumbusha watu siku fulani pantoni haitafanya kazi kuanzia masaa fulani hadi fulani ili kuwafanya abiria nao wajipange kutokana na usumbufu utakaotokea. na ni matumaini yangu mda utakaopanga utazingatia huduma. namaanisha usiathiri kwa kiasi kikubwa
sana. kwa hapa kwa kweli mtaangalia jinsi ya kufanya.
Kuhusu service ya life jacket boyas, etc
Hivi ndugu zangu toka pantoni inunuliwe jamani kuna hata siku moja mlisha wahi kuangalia yale maboya, life jacket ziko katika hali gani??? Ni wazi mnajua kabisa kuna panya ndani ya pantoni na life jacket ikiliwa na panya, ina maana imeshatoboka. na hivyo haitaweza kutumika endapo kuna ajali imetokea. HIVI JAMANI TUNAKWENDA WAPI???
Okay nimekaa na kusema sina budi kuongea na kutoa maoni yangu. naomba jamani tusingojee litokee ndipo tuanze kusema yes maboya yalikuwa ya kutosha na hata life jacket zilikuwa za kutosha ila yalikuwa hayana upepo au yalikuwa yameliwa na panya. Mimi naangalia mbele sana, nikitafakari hata zile funguo zinazofunga yale makabati ya hivi vifaa sina uhakika kama wahusika wanajua zilipo. au tutaanza kuulizana funguo:A S-key: ziko wapi wakati wa ajali au hata kusema kofuli alifunguki kwa sababu ya kutu siku ya ajali. Mimi naamini tulikuwa tumelala na sasa kwa kutumia maoni yangu naomba tuamke. tufanye kazi kwa kufikiria endapo ikitokea hili tunaweza okoa abiria???? siyo kungoja itokee alafu ndipo tujifunze.
Kwa kifupi
Pantoni zifanyiwe service mara kwa mara na siyo kusubiri iharibike. ila ratiba ya service itangazwe kwa abiria siku mbili kabla.
Vifaa vya uokoaji vifanyiwe service(kujazwa upepo au kuzibwa kwa yale yaliyotoboka). makabati yawe yanafunguliwa na kuhakikisha funguo zipo sehemu rahisi kupatikana wakati wa ajali au tatizo
3. Kuwepo na sehemu ya kuweka maoni ndani ya pantoni au mtu wa kusikiliza abiria wakiwa ndani ya pantoni.
Maelezo
wahusika najua kuna watu wana kero nyingi sana kuhusu wahudumu wanaohudumu ndani ya pantoni. wale jamaa utafikiri hicho chombo tunapanda bure au tumeomba msaada kwa himaya yake.
ni hivi
- Nikianza kabisa na sehemu ya kukata tiketi
Mfano huu ni wa kweli na mimi binafsi ndiye mlengwa, imenikuta wikii hii na ndipo nikasema sina budi sasa kuongea.
nimetoa elfu mbili akaangalia akasema badilisha hiyo hela. mimi nikaiangalia nikifikiri nimetoa hela mfukoni ikachania au nini tatizo ila sikuona tatizo na wakati naiangalia waliokuwa nje waka guna, mmoja akaropoka kwa sauti akasema hela hii inatatizo gani au una gundu la nyumbani kwako. mwingine akasema hizi hela unaweka kwa nyumbani mwako au zinaenda benki. ila mimi sikuongea chochote nikaingiza mkono mfukoni nikatoa elfu tano. unajua akanijibu nini. sina chenji. kwa kweli nilijisikia vibaya nikamuuliza. dada nimekupa elfu mbili umesema nibadilishe hela, nimekupa elfu tano unasema sina chenji. unataka nifanyeje. akajibu kwa ubabe. Nimeshakuambia sina chenji unanilazimisha katafute huko kwa wengine. niliondoka nikaenda upande wa pili nikampa ile elfu mbili akapokea akanipa chenji.
natumai unaweza ona jinsi gani hawa tunaowaweka pale watuhudumie wanavyosahau wajibu wao na kujiona wamefika. nikasema laiti kungekuwa na mtu anasikiliza malalamiko ya abiria nikifikisha kwake ila hakuna na kama yupo hawekwi wazi kwa hiyo hatujui wapi kufikisha hivyo unakuta mtu analalamika tuu na kubaki na kero yake.
- Tuende kwenye pantoni yenyewe. (rubani na jopo lote linalokuwepo kule juu)
Unakuta pantoni umeshafunguliwa kuingia. ila pantoni inaweza chukua hata nusu saa inasubiri tuu. sasa ukiuliza inasubiri nini hujui. ila kwa vile abiria hata kama anauzika hawezi sema lolote basi utakuta kule juu wana piga story :lol: na mda watakao wao ndio wanaanza kuondoa. JAMANI WAHUSIKA KILA MTU HUWA ANA RATIBA YAKE MUHIMU SANA NA KASHAPANGIA MDA WAKE. WEWE UNAPOKUWA MZEMBE UNASABABISHA MADHARA MENGI SANA. SIJUI KAMA HUU NI UNGWANA.
ni kweli kuna wakati pantoni inasubiri meli ipite huwa wanatoa taarifa au watu wasogee watoke mlangoni, ila kuna wakati huwa tuu wameamua kukaa kimya, kama vile umeomba lift gari ya mtu. atasimama anapotaka na ataondoka katika mda anaotaka. huwa siyo ungwana. wengine ni wagonjwa, wengine wanawahi kazini, au hospitali. yapo mengi ila wenzangu hawajali. na si hawajali bali hakuna wa kuwakumbusha endapo kuna kitendo kama hichi kinatokea. siku ingine masikini, utakuta mtu kasimama chini pale pana jua au mvua anajua ni dakika 5 tuu navumilia nitakuwa nimeshavuka. kumbe tunasema mawazo yako siyo yao. wenzako wanachapa stori tuu.
Nini kifanyike
Kurekebisha hili natumai kungekuwepo na sehemu ya maoni, au muhusika atakaye unganisha baina ya abiria na chumba cha rubani juu nafikiri itasaidia au tubuni njia nyingine ilimradi hili tatizo tulitokemeze. mi nafikiri kuna siku UPOLE/UKIMYA :A S embarassed: WA MTANZANIA UTAFIKA MWISHO, Na watachoka kunyanyasika na siku moja wataamua kupanda wote juu na kuleta fujo. kuepusha hili tutumie UVUMILIVU wa mtanzia vizuri. acheni kunyanyasa abiria wa pantoni wapeni haki zao. sijaongelea lugha ya matusi huwa inatumika sana kwa pantoni hasa ukiwa kwenye pantoni ndogo. wadau wanaweza ongezea kwa hilo ila la msingi tuchukue hatua.
haya ni baadhi tu ya kero ebu ruhusu watu watoe maoni yao ndipo mtakapopata yanayojiri.:juggle:
yapo mengi ila hapa nitawachosha . tuzikatie haya na ndipo nitakuja na mengine kama la kuboresha sehemu za abiria kusubiria pantoni nakadhalika. :focus: WAHUSIKA MKIONA YAPO YANAYOWEZA KUFANYIWA KAZI NA MKIONA NI YANAUMUHIMU CHUKUENI HATUA. ILA SI KILA MAONI LAZIMA YATEKELEZWE. NI USHAURI TUU.
:closed_2:
Napenda kuchukua nafasi hii, kutoa maoni yangu kuhusiana na pantoni zetu za Dar na hata za mikoani.
Wahusika mpatapo mawazo haya ni vema mkayafanyia kazi kwa yale mtakayoona yana tija.
Maoni
1. wahusika ni vyema kutoa elimu ya kuyatumia jaketi okovu(LIFE JACKET) na vifaa vingine vilivyopo ndani ya pantoni kwa ajili ya kujiokoa endapo kutatokea tatizo.
Maelezo:
pantoni zetu zina vifaa vingi tuu kwa ajili ya uokoaji endapo kutatokea tatizo pantoni ikiwa katikati ya bahari au ziwa. kwa hili nawapongeza sana wahusika ila JE MNAUHAKIKA KILA ANAYEINGIA NDANI YA CHOMBO HICHO ANAUELEWA WA KUTUMIA VIFAA HIVYO???? AU Tunangoja hadi litukie tukio ndipo muanze elekeza abiria jinsi ya kutumia????? Bila shaka kuna tatizo hapa.
Nini kifanyike
Ndani ya pantoni zetu hapa tanzania, nyingi zina radio au screen. napendekeza ziwepo picha zinazoonesha kwenye screen zikimuelekeza abiria jinsi ya kutumia vifaa vile, au kama hakuna screen basi mtangazaji awe anatangaza kila mara abiri aingiapo kwenye pantoni. kuliko kumlipa mtu kila siku anasema tuu karibu kwenye pantoni yetu, karibuni kwenye pantoni yetu. tena kwa shifti, tuwape kazi zaidi ya kutoa elimu kwa kuelekeza abiria. Mfano mzuri ndugu zangu, uingiapo ndani ya ndege lane:, kabla ya ndege kuondoka kuna muhudumu huwa anatoa maelekezo jinsi ya kutumia zile life jacket na nini cha kufanya endapo kunatatizo litajitokeza. vivyo hivyo natamani kwenye pantoni ifanyike.
Ni vizuri tunavyoweka matangazo mengine kwenye screen zile hata kama hizo screen zilitolewa na wanaoweka matangazo na imani hawataweza kukataa na hata hivyo haidhuru chochote tukiongeza matangazo au onyesho la jinsi ya utumiaji wa life jacket, boya etc.
2. Kuhusu kufanya service ya pantoni na vifaa hivyo vya uokoaji.
maelezo
Kuwepo na ratiba (schedule for service) ya kufanyia service pantoni yenyewe na siyo kusubiri hadi iaribike ndipo ifanyiwe matengenezo. ikiwepo ratiba inatangazwa inabandikwa na kutangazwa ili kukumbusha watu siku fulani pantoni haitafanya kazi kuanzia masaa fulani hadi fulani ili kuwafanya abiria nao wajipange kutokana na usumbufu utakaotokea. na ni matumaini yangu mda utakaopanga utazingatia huduma. namaanisha usiathiri kwa kiasi kikubwa
sana. kwa hapa kwa kweli mtaangalia jinsi ya kufanya.
Kuhusu service ya life jacket boyas, etc
Hivi ndugu zangu toka pantoni inunuliwe jamani kuna hata siku moja mlisha wahi kuangalia yale maboya, life jacket ziko katika hali gani??? Ni wazi mnajua kabisa kuna panya ndani ya pantoni na life jacket ikiliwa na panya, ina maana imeshatoboka. na hivyo haitaweza kutumika endapo kuna ajali imetokea. HIVI JAMANI TUNAKWENDA WAPI???
Okay nimekaa na kusema sina budi kuongea na kutoa maoni yangu. naomba jamani tusingojee litokee ndipo tuanze kusema yes maboya yalikuwa ya kutosha na hata life jacket zilikuwa za kutosha ila yalikuwa hayana upepo au yalikuwa yameliwa na panya. Mimi naangalia mbele sana, nikitafakari hata zile funguo zinazofunga yale makabati ya hivi vifaa sina uhakika kama wahusika wanajua zilipo. au tutaanza kuulizana funguo:A S-key: ziko wapi wakati wa ajali au hata kusema kofuli alifunguki kwa sababu ya kutu siku ya ajali. Mimi naamini tulikuwa tumelala na sasa kwa kutumia maoni yangu naomba tuamke. tufanye kazi kwa kufikiria endapo ikitokea hili tunaweza okoa abiria???? siyo kungoja itokee alafu ndipo tujifunze.
Kwa kifupi
Pantoni zifanyiwe service mara kwa mara na siyo kusubiri iharibike. ila ratiba ya service itangazwe kwa abiria siku mbili kabla.
Vifaa vya uokoaji vifanyiwe service(kujazwa upepo au kuzibwa kwa yale yaliyotoboka). makabati yawe yanafunguliwa na kuhakikisha funguo zipo sehemu rahisi kupatikana wakati wa ajali au tatizo
3. Kuwepo na sehemu ya kuweka maoni ndani ya pantoni au mtu wa kusikiliza abiria wakiwa ndani ya pantoni.
Maelezo
wahusika najua kuna watu wana kero nyingi sana kuhusu wahudumu wanaohudumu ndani ya pantoni. wale jamaa utafikiri hicho chombo tunapanda bure au tumeomba msaada kwa himaya yake.
ni hivi
- Nikianza kabisa na sehemu ya kukata tiketi
Mfano huu ni wa kweli na mimi binafsi ndiye mlengwa, imenikuta wikii hii na ndipo nikasema sina budi sasa kuongea.
nimetoa elfu mbili akaangalia akasema badilisha hiyo hela. mimi nikaiangalia nikifikiri nimetoa hela mfukoni ikachania au nini tatizo ila sikuona tatizo na wakati naiangalia waliokuwa nje waka guna, mmoja akaropoka kwa sauti akasema hela hii inatatizo gani au una gundu la nyumbani kwako. mwingine akasema hizi hela unaweka kwa nyumbani mwako au zinaenda benki. ila mimi sikuongea chochote nikaingiza mkono mfukoni nikatoa elfu tano. unajua akanijibu nini. sina chenji. kwa kweli nilijisikia vibaya nikamuuliza. dada nimekupa elfu mbili umesema nibadilishe hela, nimekupa elfu tano unasema sina chenji. unataka nifanyeje. akajibu kwa ubabe. Nimeshakuambia sina chenji unanilazimisha katafute huko kwa wengine. niliondoka nikaenda upande wa pili nikampa ile elfu mbili akapokea akanipa chenji.
natumai unaweza ona jinsi gani hawa tunaowaweka pale watuhudumie wanavyosahau wajibu wao na kujiona wamefika. nikasema laiti kungekuwa na mtu anasikiliza malalamiko ya abiria nikifikisha kwake ila hakuna na kama yupo hawekwi wazi kwa hiyo hatujui wapi kufikisha hivyo unakuta mtu analalamika tuu na kubaki na kero yake.
- Tuende kwenye pantoni yenyewe. (rubani na jopo lote linalokuwepo kule juu)
Unakuta pantoni umeshafunguliwa kuingia. ila pantoni inaweza chukua hata nusu saa inasubiri tuu. sasa ukiuliza inasubiri nini hujui. ila kwa vile abiria hata kama anauzika hawezi sema lolote basi utakuta kule juu wana piga story :lol: na mda watakao wao ndio wanaanza kuondoa. JAMANI WAHUSIKA KILA MTU HUWA ANA RATIBA YAKE MUHIMU SANA NA KASHAPANGIA MDA WAKE. WEWE UNAPOKUWA MZEMBE UNASABABISHA MADHARA MENGI SANA. SIJUI KAMA HUU NI UNGWANA.
ni kweli kuna wakati pantoni inasubiri meli ipite huwa wanatoa taarifa au watu wasogee watoke mlangoni, ila kuna wakati huwa tuu wameamua kukaa kimya, kama vile umeomba lift gari ya mtu. atasimama anapotaka na ataondoka katika mda anaotaka. huwa siyo ungwana. wengine ni wagonjwa, wengine wanawahi kazini, au hospitali. yapo mengi ila wenzangu hawajali. na si hawajali bali hakuna wa kuwakumbusha endapo kuna kitendo kama hichi kinatokea. siku ingine masikini, utakuta mtu kasimama chini pale pana jua au mvua anajua ni dakika 5 tuu navumilia nitakuwa nimeshavuka. kumbe tunasema mawazo yako siyo yao. wenzako wanachapa stori tuu.
Nini kifanyike
Kurekebisha hili natumai kungekuwepo na sehemu ya maoni, au muhusika atakaye unganisha baina ya abiria na chumba cha rubani juu nafikiri itasaidia au tubuni njia nyingine ilimradi hili tatizo tulitokemeze. mi nafikiri kuna siku UPOLE/UKIMYA :A S embarassed: WA MTANZANIA UTAFIKA MWISHO, Na watachoka kunyanyasika na siku moja wataamua kupanda wote juu na kuleta fujo. kuepusha hili tutumie UVUMILIVU wa mtanzia vizuri. acheni kunyanyasa abiria wa pantoni wapeni haki zao. sijaongelea lugha ya matusi huwa inatumika sana kwa pantoni hasa ukiwa kwenye pantoni ndogo. wadau wanaweza ongezea kwa hilo ila la msingi tuchukue hatua.
haya ni baadhi tu ya kero ebu ruhusu watu watoe maoni yao ndipo mtakapopata yanayojiri.:juggle:
yapo mengi ila hapa nitawachosha . tuzikatie haya na ndipo nitakuja na mengine kama la kuboresha sehemu za abiria kusubiria pantoni nakadhalika. :focus: WAHUSIKA MKIONA YAPO YANAYOWEZA KUFANYIWA KAZI NA MKIONA NI YANAUMUHIMU CHUKUENI HATUA. ILA SI KILA MAONI LAZIMA YATEKELEZWE. NI USHAURI TUU.
:closed_2: