Mawaziri wanapolalamikia fedha hazitoshi wasipuuzwe, wapo watu wanateseka

FakeID

Member
Feb 29, 2016
89
96
Kuna mijadala inaendelea kuhusu mawaziri wanaolalamika kwamba fedha za OC zinazopelekwa katika wizara zao ni ndogo, watu wengi wasiojua hali halisi wamekuwa wakishabikia wasichokijua hasa kuhusu malalamiko ya mawaziri hawa.

Ni miezi kadhaa sasa, tangu serikali ipunguze ghafla kiwango cha fedha za OC kwenda kwenye wizara, zipo wizara hupatiwa shilingi milioni tano kwa mwezi mmoja. Na imefanyika kwa miezi kadhaa sasa tangu kuingia kwa serikali ya hapa kazi tu.

Ikumbukwe fedha hizi za OC ndio hutumika kulipa stahiki za wakurugenzi, fedha za kujikimu kwa waajiriwa wapya, kulipa umeme, maji, kununua mafuta ya kuendeshea ofisi, kununua shajala na posho za mawaziri wanapokuwa safarini.

Hali hiyo inasababisha mpaka sasa kuna wafanyakazi wapya wengi hawajalipwa fedha zao za kujikimu huku wakiwa hawana mishahara, wanamaisha magumu mpaka inatia huzuni. Ipo wizara iliwarudisha nyumbani kwa muda na hata waliporudi bado wakakuta hali ni ile ile, hapa tunatarajia waziri waache kulalamika.

Sasa hivi yapo magari hayatembei sababu hakuna mafuta, kazi hazifanyiki kwa ufanisi sababu hata karatasi hakuna, wanashindwa kulipa umeme, wanashindwa kulipa maji, wanakatiwa hizi huduma muhimu kwenye maofisi wataacha kulalamika. Kuna ofisi ziko kwenye majengo ya kupanga, hawawezi kulipa pango na wengine wameshapewa notice, ni dhambi kusema fedha hazitoshi?

Ni kweli kwamba mawaziri na makatibu wakuu wanapaswa kujua kwamba wapo kwenye zama nyingine, lakini tunapofanya maamuzi tunapaswa kuwasikiliza kwa maana wao wanajukumu la kuhakikisha kazi zinafanyika kwa ufanisi.
 
Kuna mijadala inaendelea kuhusu mawaziri wanaolalamika kwamba fedha za OC zinazopelekwa katika wizara zao ni ndogo, watu wengi wasiojua hali halisi wamekuwa wakishabikia wasichokijua hasa kuhusu malalamiko ya mawaziri hawa.

Ni miezi kadhaa sasa, tangu serikali ipunguze ghafla kiwango cha fedha za OC kwenda kwenye wizara, zipo wizara hupatiwa shilingi milioni tano kwa mwezi mmoja. Na imefanyika kwa miezi kadhaa sasa tangu kuingia kwa serikali ya hapa kazi tu.

Ikumbukwe fedha hizi za OC ndio hutumika kulipa stahiki za wakurugenzi, fedha za kujikimu kwa waajiriwa wapya, kulipa umeme, maji, kununua mafuta ya kuendeshea ofisi, kununua shajala na posho za mawaziri wanapokuwa safarini.

Hali hiyo inasababisha mpaka sasa kuna wafanyakazi wapya wengi hawajalipwa fedha zao za kujikimu huku wakiwa hawana mishahara, wanamaisha magumu mpaka inatia huzuni. Ipo wizara iliwarudisha nyumbani kwa muda na hata waliporudi bado wakakuta hali ni ile ile, hapa tunatarajia waziri waache kulalamika.

Sasa hivi yapo magari hayatembei sababu hakuna mafuta, kazi hazifanyiki kwa ufanisi sababu hata karatasi hakuna, wanashindwa kulipa umeme, wanashindwa kulipa maji, wanakatiwa hizi huduma muhimu kwenye maofisi wataacha kulalamika. Kuna ofisi ziko kwenye majengo ya kupanga, hawawezi kulipa pango na wengine wameshapewa notice, ni dhambi kusema fedha hazitoshi?

Ni kweli kwamba mawaziri na makatibu wakuu wanapaswa kujua kwamba wapo kwenye zama nyingine, lakini tunapofanya maamuzi tunapaswa kuwasikiliza kwa maana wao wanajukumu la kuhakikisha kazi zinafanyika kwa ufanisi.

Nadhani hawajanyimwa kusema kwamba fedha hazitoshi! Alichogomba Magufuli, ni tabia ya kulalamika na kunung'unika ki-majungu kunakofanywa na baadhi ya mawaziri! Mahitaji uliyoyainisha yanaeleweka na yangepaswa kuakisiwa kwenye bajeti na sio OC. Na hata pale upungufu wa kweli unapojitokeza kwenye OC kuna proper channels za kuwasilisha madai na sio kulalamika!
 
Nadhani hawajanyimwa kusema kwamba fedha hazitoshi! Alichogomba Magufuli, ni tabia ya kulalamika na kunung'unika ki-majungu kunakofanywa na baadhi ya mawaziri! Mahitaji uliyoyainisha yanaeleweka na yangepaswa kuakisiwa kwenye bajeti na sio OC. Na hata pale upungufu wa kweli unapojitokeza kwenye OC kuna proper channels za kuwasilisha madai na sio kulalamika!
Watu wanaolalamika maana yake wanaogopa kusema, mzee apunguze ukali aisee khaaaa
 
Kuna mijadala inaendelea kuhusu mawaziri wanaolalamika kwamba fedha za OC zinazopelekwa katika wizara zao ni ndogo, watu wengi wasiojua hali halisi wamekuwa wakishabikia wasichokijua hasa kuhusu malalamiko ya mawaziri hawa.
Kama hela hazitoshi waachie nafasi zao upesi tena haraka.
Kuna mtu aliniambia kuwa Rwanda ukipewa bajeti unaulizwa unadhani kwa bajeti hii utaweza kutimiza majukumu yako? ukisema kwa bajeti hii siwezi,unaambiwa ondoka Kagame anatafuta mtu mwingine atakayeweza.
Ukisema mimi nitaweza basi bajeti ikipita unapewa bajeti unaenda kusimama mbele ya jaji wa mahakama kuu na kuapa mbele yake kuwa utatekeleza hizo kazi kwa hiyo bajeti iliyopo na kusainishwa performance contract na jaji.Ukishindwa wakati wa utekelezaji utakiona cha mtema kuni.

Sasa kama bajeti ndogo mtu anashupalia kubaki kazini kwa ajili ya nini ondoka andika barua ya kuacha.Mwambie wazi raisi kwa resources hizi siwezi tekeleza majukumu mpe kazi hii mtu mwingine.

Bajeti ikiwa ndogo rekebisha matumizi.Badala ya mkuu wa idara kuja na shangingi kazini kapande daladala.Huwezi kubaki na matumizi yale yale uliyozoea wakati pesa ni ndogo.Hivi MAGUFULI akisema anabana matumizi huko kwingine wanaelewa au hawaelewi?
wao pia wanatakiwa wabane matumizi

HAPA KAZI TU
 
Nakuunga mkono, napendekeza waongezewe fungu baada ya kutengeneza kanuni ilandane na hii hapa:-

Posho na marupurupu ya mtumishi wa umma kwa ujumla wake haitapita 18% ya mshahara wake.

Lengo ni kuwa hela zikafanye kazi zenye tija kwa taifa.

Naamini mishahara inatosha ndio maana hata pale wagombea walipokataa kuahidi kupandisha mishahara, wafanyakazi ambao ndio wanatoka kada ya wasomi nchini waliwamiminia kura nyiiingi kabisa hao wanasiasa.

Twende kazini.
 
Kama hela hazitoshi waachie nafasi zao upesi tena haraka.
Kuna mtu aliniambia kuwa Rwanda ukipewa bajeti unaulizwa unadhani kwa bajeti hii utaweza kutimiza majukumu yako? ukisema kwa bajeti hii siwezi,unaambiwa ondoka Kagame anatafuta mtu mwingine atakayeweza.
Ukisema mimi nitaweza basi bajeti ikipita unapewa bajeti unaenda kusimama mbele ya jaji wa mahakama kuu na kuapa mbele yake kuwa utatekeleza hizo kazi kwa hiyo bajeti iliyopo na kusainishwa performance contract na jaji.Ukishindwa wakati wa utekelezaji utakiona cha mtema kuni.

Sasa kama bajeti ndogo mtu anashupalia kubaki kazini kwa ajili ya nini ondoka andika barua ya kuacha.Mwambie wazi raisi kwa resources hizi siwezi tekeleza majukumu mpe kazi hii mtu mwingine.

Bajeti ikiwa ndogo rekebisha matumizi.Badala ya mkuu wa idara kuja na shangingi kazini kapande daladala.Huwezi kubaki na matumizi yale yale uliyozoea wakati pesa ni ndogo.Hivi MAGUFULI akisema anabana matumizi huko kwingine wanaelewa au hawaelewi?
Hao wanaolalamika wamefikia hatua ya kukosa hata mahitaji muhimu, mfano fedha ya kujikimu ya mtumishi unaibanaje? Karatasi za ream unabanaje matumizi?
 
Hao wanaolalamika wamefikia hatua ya kukosa hata mahitaji muhimu, mfano fedha ya kujikimu ya mtumishi unaibanaje? Karatasi za ream unabanaje matumizi?

Weka mfano hai tusiongelee vitu vya kufikirika.Ni nani kapewa bajeti ipi ,matumizi yake yapi weka hapa vitu halisia.
 
Kuna mijadala inaendelea kuhusu mawaziri wanaolalamika kwamba fedha za OC zinazopelekwa katika wizara zao ni ndogo, watu wengi wasiojua hali halisi wamekuwa wakishabikia wasichokijua hasa kuhusu malalamiko ya mawaziri hawa.

Ni miezi kadhaa sasa, tangu serikali ipunguze ghafla kiwango cha fedha za OC kwenda kwenye wizara, zipo wizara hupatiwa shilingi milioni tano kwa mwezi mmoja. Na imefanyika kwa miezi kadhaa sasa tangu kuingia kwa serikali ya hapa kazi tu.

Ikumbukwe fedha hizi za OC ndio hutumika kulipa stahiki za wakurugenzi, fedha za kujikimu kwa waajiriwa wapya, kulipa umeme, maji, kununua mafuta ya kuendeshea ofisi, kununua shajala na posho za mawaziri wanapokuwa safarini.

Hali hiyo inasababisha mpaka sasa kuna wafanyakazi wapya wengi hawajalipwa fedha zao za kujikimu huku wakiwa hawana mishahara, wanamaisha magumu mpaka inatia huzuni. Ipo wizara iliwarudisha nyumbani kwa muda na hata waliporudi bado wakakuta hali ni ile ile, hapa tunatarajia waziri waache kulalamika.

Sasa hivi yapo magari hayatembei sababu hakuna mafuta, kazi hazifanyiki kwa ufanisi sababu hata karatasi hakuna, wanashindwa kulipa umeme, wanashindwa kulipa maji, wanakatiwa hizi huduma muhimu kwenye maofisi wataacha kulalamika. Kuna ofisi ziko kwenye majengo ya kupanga, hawawezi kulipa pango na wengine wameshapewa notice, ni dhambi kusema fedha hazitoshi?

Ni kweli kwamba mawaziri na makatibu wakuu wanapaswa kujua kwamba wapo kwenye zama nyingine, lakini tunapofanya maamuzi tunapaswa kuwasikiliza kwa maana wao wanajukumu la kuhakikisha kazi zinafanyika kwa ufanisi.

....Ikumbukwe fedha hizi za OC ndio hutumika kulipa stahiki za wakurugenzi, fedha za kujikimu kwa waajiriwa wapya, kulipa umeme, maji, kununua mafuta ya kuendeshea ofisi, kununua shajala na posho za mawaziri wanapokuwa safarini...

Miaka yote wizara hazijui wanatumia kiasi gani kwenye umeme? Kwa nini wasichukue matumizi ya mwaka wa fedha uliopita na kuongeza asilimia fulani ili kiwango hicho kiingie kwenye budget badala ya OC?

Wizara hazina mipango ya ajira au wanakurupuka tu kila wakati? Kwa nini wasijue mwakani wataajiri watu wangapi na hela ikaingia kwenye budget?

Wizara kwa miaka yote bado hawajui wanatumia kiasi gani kwenye mafuta na matengenezo ya magari ili waingize kwenye budget?

Hayo matumizi yapo kila mwaka na hayaji kama ajali. Ujanja wa kuweka OC kubwa upo miaka mingi na ni chaka la kukwapulia pesa tu.

Huo ndiyo ujumbe JPM anajaribu kufikisha kwenye wizara na idara za serikali!
 
Kati ya pesa inatafunwa serikalini basi ni OC, wenyewe wanakuambia hii hela haina kazi maalumu si unaona hata jina lake other charges
 
Wasiliana na wahasibu wa wizara na halmashauri yoyote usikie wanavyolia

Wewe una matatizo.Wewe ndio umeleta mada ukijidai kuwa wapo wenye hayo matatizo nakwambia wataje unanisukumia kwingine.Acha kuleta umbeya jamiiforums.

Na uelewe kwenye kutengeneza mabajeti ya nchi hicho kipengele cha OTHER CHARGES nchi nyingi huwa hawataki hata kukiona.CHARGES LAZIMA ZIJULIKANE ni za nini.Huwezi kusema sizijui zinaweza jitokeza zitajulikana mbele kwa mbele.

Magufuli OTHER CHARGES nalo ni jipu la kutumbua ziondoe kabisa kusiwe na kifungu kinachojulikana kama OTHER CHARGES.
 
Dah mbaya saana lakini si huwa wanataja bidget yao?

Ama wanapewa tu OC bila kutaja bidget zao
 
Kweli watu mitaani hawajui umuhimu wa fedha za OC kwa ustawi wa watumishi na huduma kwa wananchi. Ni vizuri check and Balance ktk hili ili taasisi ziweze kumudu uendeshaji wa ofisi wanazosimamia
 
Oc ifutwe kabisa, ni sawa na bajeti ya dharura kwenye harusi, baada ya harusi ile pesa ya dharura huwa hakuna maelezo ilifanya kazi gani, huu ni wizi tu na ubatili mtupu. Futa kabisa OC.
 
Mleta mada sio kweli kwamba kazi ya fedha hizi sio kulipa posho za safari mawaziri wanaposafiri! Acha kuchapia! najua jiwe limekupata gizani! Pole na kuwa mpole
 
... Kuna ofisi ziko kwenye majengo ya kupanga, hawawezi kulipa pango na wengine wameshapewa notice, ni dhambi kusema fedha hazitoshi?...

''DHAMBI yao'' ipo kwenye njia wanayotumia kufikisha vilio vyao. If we have to go by Magufuri's word, hawa watu wanalalamika chinichini - kwenye corridors. Kwa nini? kwa kuwa labda hawana ujasiri kwa kujustify OC kubwa kubwa walizokuwa wanapiga miaka yote ile.
 
''DHAMBI yao'' ipo kwenye njia wanayotumia kufikisha vilio vyao. If we have to go by Magufuri's word, hawa watu wanalalamika chinichini - kwenye corridors. Kwa nini? kwa kuwa labda hawana ujasiri kwa kujustify OC kubwa kubwa walizokuwa wanapiga miaka yote ile.
Naungana na wewe, kulalamika kwenye corridor sio jambo jema kwa watu wa hadhi ya mawaziri.
 
Nadhani hawajanyimwa kusema kwamba fedha hazitoshi! Alichogomba Magufuli, ni tabia ya kulalamika na kunung'unika ki-majungu kunakofanywa na baadhi ya mawaziri! Mahitaji uliyoyainisha yanaeleweka na yangepaswa kuakisiwa kwenye bajeti na sio OC. Na hata pale upungufu wa kweli unapojitokeza kwenye OC kuna proper channels za kuwasilisha madai na sio kulalamika!
Proper channel ni ipi sasa? Wizara zina bajeti zake zilizoidhinshwa na serikali (Approved budget). Bunge lilishapitisha mswada wa makadirio na matumizi kwa mwaka husika (financial bill na baada ya kupitishwa ni financial act). Maana yake hiyo ni sheria. Sasa serikali isipotoa hizo pesa kupeleka kwenye wizara husika ni kuvunja sheria. Hupaswi kusema mawaziri wasilalamike. Wasilalamike vipi wakati serikali haitimizi wajibu wa kisheria inaopaswa kutekeleza.

Kuna wagonjwa mahospitalini, katika hospitali ambazo hazikusanyi fedha zozote za kuchangia gharama kwa kuwa kuna sera inayosema wagonjwa aina hiyo wasamehewe kama vile Mirembe. Utamwambia mgonjwa wa akili achangie gharama atakuelewa. Wagonjwa hawa wanahitaji kula kulala, dawa maji na umeme halafu serikali haipeleki hela. Watendaji wasilalamike, kweli? Wazabuni wanakataa kuleta chakla Msd hakuna dawa, TEMESA wanazuia gari la hospitali, unataka wauguzi wabebe wagonjwa mgongoni. Unataka wasilalamike, are you serious?

Anachojua Magufuli ni kukusanya hela kupelka kupanua barabara, kununua madawati na kulipa stahili za viongozi. Hivyo ndiyo vipaumbele vyake, kwa kuwa amewahi kuwa elimu na ujenzi wizara zingine hajui umuhimu wake bora basi angekuwa na masikio asikie mawazo ya washauri wake, hana, hadi madaktari wanapigwa na ndugu za wagonjwa kama ilivyotokea Mtwara. Hajui wakulima wanashida gani.

Serikali haiwezi kuwa ni viongozi wa kisiasa, elimu, mahakama na barabara peke yake ni zaidi ya hapo. Kulalamika mahali pasipotakiwa kunasababishwa na ubabe wa rais kutotaka kushauriwa aliloamua ndilo linakuwa anakuwa ni zaidi hata ya Mungu maana Muungu huwasikiliza watu wake: hawa wakitaka mvua huwapa wakitaka jua huwapa wakitaka baridi huwapa hata wakitaka joto huwapa pia, lakini siyo kwa Magufuli anataka apewe yeye sifa pasipo kutekeleza matakwa ya watu wake. Anataka kupiga simu bila kuweka salio. Kwa mwendo huu hatufiki mbali, ngoma ikilia sana hupasuka hima
 
Kuna mijadala inaendelea kuhusu mawaziri wanaolalamika kwamba fedha za OC zinazopelekwa katika wizara zao ni ndogo, watu wengi wasiojua hali halisi wamekuwa wakishabikia wasichokijua hasa kuhusu malalamiko ya mawaziri hawa.

Ni miezi kadhaa sasa, tangu serikali ipunguze ghafla kiwango cha fedha za OC kwenda kwenye wizara, zipo wizara hupatiwa shilingi milioni tano kwa mwezi mmoja. Na imefanyika kwa miezi kadhaa sasa tangu kuingia kwa serikali ya hapa kazi tu.

Ikumbukwe fedha hizi za OC ndio hutumika kulipa stahiki za wakurugenzi, fedha za kujikimu kwa waajiriwa wapya, kulipa umeme, maji, kununua mafuta ya kuendeshea ofisi, kununua shajala na posho za mawaziri wanapokuwa safarini.

Hali hiyo inasababisha mpaka sasa kuna wafanyakazi wapya wengi hawajalipwa fedha zao za kujikimu huku wakiwa hawana mishahara, wanamaisha magumu mpaka inatia huzuni. Ipo wizara iliwarudisha nyumbani kwa muda na hata waliporudi bado wakakuta hali ni ile ile, hapa tunatarajia waziri waache kulalamika.

Sasa hivi yapo magari hayatembei sababu hakuna mafuta, kazi hazifanyiki kwa ufanisi sababu hata karatasi hakuna, wanashindwa kulipa umeme, wanashindwa kulipa maji, wanakatiwa hizi huduma muhimu kwenye maofisi wataacha kulalamika. Kuna ofisi ziko kwenye majengo ya kupanga, hawawezi kulipa pango na wengine wameshapewa notice, ni dhambi kusema fedha hazitoshi?

Ni kweli kwamba mawaziri na makatibu wakuu wanapaswa kujua kwamba wapo kwenye zama nyingine, lakini tunapofanya maamuzi tunapaswa kuwasikiliza kwa maana wao wanajukumu la kuhakikisha kazi zinafanyika kwa ufanisi.
Mkuu unajua maana ya oc. Ni other charges. Katika upangaji wa bajet hakunaga kitu inaitwa oc. Kama kuna posho au hela ya mafuta vyote hupangiwa bajet. Kila kitu lazima kiwe kwenye bajet. Huwezi kuweka tu hela pale bilion kumi et oc. Hakunaga bajet ya aina hiyo.
Ni mbinu tu ilibuniwa kuweka hela nyingi kwenye kitu inaitwa oc ili wakizitumia wasiulizwe.

Mm hata sielewi kwann Mawaziri wazima wanasema oc haitoshi. Wakat hela ya mafuta, ya chai, ya nauli, ya kujikimu, ya perfum, sijui air fresh et, yaani kila kikorombwezo inapaswa kuwemo kwenye bajet. Yaani inajulikana chai kwa mwezi ni tsh ngapi. Usafiri kwa mwezi ni tsh ngapi na mafuta kwa mwezi ni tsh ngapi. Sasa oc ya nn.

Kama hawajui kuandaa bajet za wizara zao ni issue ya kuomba training zaid kuhusu namna ya kuandaa bajet. Waende un au us embasy au organization yoyote ya kimataifa watapewa semima ya namna ya kuandaa bajet tena bure.
Sasa ukitaka hela zikae tu pale et oc ili ww uamue tu kutumia bila mpango mwisho wa siku utaona haitoshi kwa sabb haina mpango au utaratibu wowote.
Hata mtu mwingine akitumia ovyo huwezi kumbana kwa sabb ni oc.

Kiuhalisia oc haipaswi kuwepo. Ni uwizi tu. Mwisho utataka bajet yote ya wizara iwe oc ili wenyewe watumie wanavotaka. Wabunge wana mfuko wa jimbo na mawaziri nao wakitaka wawe na mfuko special kwa ajili ya mambo wanayoona kuwa yanapaswa kutengewa bajet. Lakini sio kila kitu et oc..

Hapa kweli panaonyesha upungufu mkubwa wa ujuzi wa masuala ya bajet..
Wizara ya fedha ifanyike mpango wa kuandaa semina kwa mawaziri na makatibu wakuu na wakurugenz wa wizara na taasisi za serikali haraka iwezekanavyo
 
Mkuu unajua maana ya oc. Ni other charges. Katika upangaji wa bajet hakunaga kitu inaitwa oc. Kama kuna posho au hela ya mafuta vyote hupangiwa bajet. Kila kitu lazima kiwe kwenye bajet. Huwezi kuweka tu hela pale bilion kumi et oc. Hakunaga bajet ya aina hiyo.
Ni mbinu tu ilibuniwa kuweka hela nyingi kwenye kitu inaitwa oc ili wakizitumia wasiulizwe.

Mm hata sielewi kwann Mawaziri wazima wanasema oc haitoshi. Wakat hela ya mafuta, ya chai, ya nauli, ya kujikimu, ya perfum, sijui air fresh et, yaani kila kikorombwezo inapaswa kuwemo kwenye bajet. Yaani inajulikana chai kwa mwezi ni tsh ngapi. Usafiri kwa mwezi ni tsh ngapi na mafuta kwa mwezi ni tsh ngapi. Sasa oc ya nn.

Kama hawajui kuandaa bajet za wizara zao ni issue ya kuomba training zaid kuhusu namna ya kuandaa bajet. Waende un au us embasy au organization yoyote ya kimataifa watapewa semima ya namna ya kuandaa bajet tena bure.
Sasa ukitaka hela zikae tu pale et oc ili ww uamue tu kutumia bila mpango mwisho wa siku utaona haitoshi kwa sabb haina mpango au utaratibu wowote.
Hata mtu mwingine akitumia ovyo huwezi kumbana kwa sabb ni oc.

Kiuhalisia oc haipaswi kuwepo. Ni uwizi tu. Mwisho utataka bajet yote ya wizara iwe oc ili wenyewe watumie wanavotaka. Wabunge wana mfuko wa jimbo na mawaziri nao wakitaka wawe na mfuko special kwa ajili ya mambo wanayoona kuwa yanapaswa kutengewa bajet. Lakini sio kila kitu et oc..

Hapa kweli panaonyesha upungufu mkubwa wa ujuzi wa masuala ya bajet..
Wizara ya fedha ifanyike mpango wa kuandaa semina kwa mawaziri na makatibu wakuu na wakurugenz wa wizara na taasisi za serikali haraka iwezekanavyo
Hivi leo mnataka kuniaminisha kwamba hakuna items ambazo zina fall kwenye OC? mnadhani walioweka OC walikurupuka? Hata Ikulu Ina OC bwana
 
Back
Top Bottom